Kufukuzwa Membe CCM: Hakika siasa ni Mchezo kama ilivyo Karata na Draft

Kufukuzwa Membe CCM: Hakika siasa ni Mchezo kama ilivyo Karata na Draft

Wazungu wanapenda kusema "Political Chess Game". Maana katika mchezo wa chess, kete ikisogegezwa inaweza kukuvusha au kukuangusha. CCM imemwaga maji, mara nyingi maji yakimwagika lazima yatafute mkondo.

Ni wazi kuwa Lissu alishaweka hadharani nia ya kugombea urais, na Zitto naye hakuchelewa akaweka nia yake pia wazi. Kama Membe akienda kulia hawezi kumkosa Lissu anamsubiri, akienda kushoto yupo Zitto.

Kijana Zitto alishasema, kadi namba 2 ameiweka kabatini kwa ajili ya mtu mzito kutoka CCM. Kauli hiyo ya Zitto ya kumsubiri nguli wa CCM, inawezakana imeshabadilika kutokana dynamics ya mchezo wa kisiasa unaoendelea hivi sasa.

Wakati huo huo wale waliobanwa Zanzibar kina Maalim Seif na kundi lake dogo watampa mkono? Nyalandu je, yeye anaingia kundi gani? Hapa bila VAR [V] uamuzi utakuwa mgumu sana.
 
Bado tunasafari ndefu kuelekea Demokrasia ya kweli.

Tulipofikia ni hapa ambapo, wanasiasa wanagombea nafasi za uongozi ili kutimiza ndoto zao.
 
Binafsi nampongeza jpm kwa kuwafukuza wapinzani wake ndani ya chama. Maana kwa sasa ccm ndo jpm
 
Wamepigwa Red card wakiwa vyumba vya kubadilishia nguo

Kidumu chama cha Mapinduzi

Kumyumbisha Rais ni sawa na kumyumbisha Nahodha akiongoza chombo, unakuwa Adui wa Safar nzima sio Adui wa Nahodha peke yake

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naunga mkono hoja, ni vyema vyama kusisitiza nidhamu, tena CCM imefuata utaratibu na kanuni, ila ushahidi uliotumika ni ushahidi uliopatikana kijinai!, hivyo hawaku hukumiwa kwa haki.
Membe, Japo Umeonewa, Usifanye Kosa la Lowassa!, Ila CCM ya Ajabu!, Uamuzi based on Illegal Evidence ni Void Ab Initial!.

Sasa CCM isipotenda haki, nani atatenda haki?.
P
Sio kweli ushahidi umepatikana kijinai wala maamuzi hayakulalia kwenye huo ushahidi usio halali.

Hiyo aliyofanya Musiba ni kupiga kig'ora (whistle blowing) kuwa kuna jambo ovu linaendelea. Sasa CCM kupitia intelijensia unit yake ikalifanyia kazi na kupata legal evidences na ndio uliwawajibisha hawa. Tambua mpaka wanaitwa kamati ya usalama na maadili wenzao walishaenda kutubu na kuomba msamaha. Tambua unapotubu unaelezea mchoro wote wa uovu. Hii nayo ilikuwa ni sehemu ya ushahidi.

Kwa hiyo msijidanganye kuwa CCM imefanya maamuzi based on illegal evidence.
 
technically,
Yaani uko sahihi kwa asilimia mia moja kuwa Membe ni mchafu na nitashangaa sana iwapo wapinzani sana sana cdm watampokea, hasa baada ya wale wahuni wengine Lowassa na Sumaye kuleta siasa za kusaka madaraka, wakati hawana habari zozote. Ila hata huyo aliyeshinikiza afukuzwe huko ccm ni mchafu mwenzake lakini ndio aliyeshika mpini.
 
Mbowe akiamua hakuna kamanda wa kupinga! CCM will continue fixing upinzani kwa miongo mingi sana.

Sent using Jamii Forums mobile app

Ni kweli, Mbowe anaweza kuamua na hakuna kamanda wa kupinga ndani ya chama chake, lakini sisi mashabiki tulio wengi hatutamuunga mkono na tutashiriki humu mitandaoni kupinga wazi wazi iwapo uhuni huo wa kumpokea utafanyika. Na madhara ya sisi kupinga wazi wazi iwapo uhuni huo utafanyika yatakuwa wazi peupe.
 
Naunga mkono hoja
Sio kweli ushahidi umepatikana kijinai wala maamuzi hayakulalia keenye huo ushahidi usio halali.

Hiyo aliyofanya Musiba ni kupiga kigora (whistle blowing) kuwa kina jambo ovu linaendelea. Sasa CCM kupitia intelijensia unit yake ikalifanyia kazi na kupata legal evidence na ndio iliwawajibisha hawa. Tambua mpaka wanaitwa kamati ya usalama na maadili wenzao walishaenda kutubu na kuom a msamaha. Tambua unapotubu unaelezea mchoro wote wa uovu. Hii nayo ilikuwa ni sehemu ya ushahidi.

Kwa hiyo msijidanganye kuwa CCM imefanya maamuzi based on illegal evidence.
 
Binafsi Natamani Nyalandu agombee kupitia Chadema tatizo sio maarufu sana na tatizo lingine alitoka CCM sijui itakuwaje lakini ana mtaji pia anaweza ukija kwa Lissu matatizo aliyopata ni changamoto kwenye physical appearance,Zitto ni kete tatizo Chama chake hakiaminiki wakati Benard nje ya CCM si kitu japo Nasikia wana CCM kibao watajitokeza 2020 kuchukua form

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom