Kufukuzwa Membe CCM: Hakika siasa ni Mchezo kama ilivyo Karata na Draft

Kufukuzwa Membe CCM: Hakika siasa ni Mchezo kama ilivyo Karata na Draft

Bado hujajua mkuu?. Ccm ya sasa ni ya mtu mmoja tu. Hata waliopita wanamuogopa. Membe hakuwa na kosa hata kidogo,hata ile kamati iliyomhoji aliigaragaza.

Hicho kitu kikamuudhi sana. Maana pale ndipo alipokuwa anatafutiwa achinjiwe kwenye kamati pale,lakini bahati mbaya ndio hiyo akaigaragaza.

Kwa hiyo kilichobaki baada ya hapo ni achinjwe mzima mzima sasa. “maana hakuna namna sasa”

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unafikiri ni sahihi kwa TISS kufanya siasa tena ikiegemea upande wa Chama fulani?
Unafikiri kuna haja ya kuwa na vyama vingi kama taasisi nyeti za usalama zina chama?
Tunaweza kupima umahiri wa TISS kwa kuisaidia CCM kuushinda upinzani?
TISS inafahamu tofauti ya Tanzania na CCM?

Nafikiri kazi ya vyombo nyeti vya usalama ni kuwa neutral organs zinazocontrol hali zote katika nchi kuanzia siasa mpaka uchumi, Taasisi zote za usalama hazipaswi kuwa na upande baadala yake zinatakiwa ziwe sehemu ya kuwalinda wananchi juu ya ujinga wa wanasiasa na mwisho wa siku pawepo siasa safi.
 
Huu ni mchezo tu. Kafukuzwa ili aende upinzani na baada ya uchaguzi atarudi chamani. Utaona.

Sent using Jamii Forums mobile app
Membe ni kiherehere chake tu sababu ya ukwasi wake. Alipendelewa na kaka mkubwa kwa kiasi kikubwa sana na bado NEC ikampiga chini.

Alipotangaza kutimiza ndoto yake alijisahau kuwa nguvu za kaka mkubwa zimeisha fika ukingoni.

Baada ya Kufukuzwa katika CCM hana kinga tena akiendelea kupiga kelele sitashangaa kusikia yupo lupango.
 
Hii ndio CCM niliyoifahamu yenye maamuzi yasiyomuangalia mtu usoni.

Haijalishi wewe ni maarufu kiasi gani unapokengeuka lazima hatua zichukuliwe dhidi yako.

Hii ndio CCM aliyotuachia Nyerere na Kawawa

Maendeleio hayana vyama!
[/QUOTE
Afukuzwe na godfather wake Wa awamu ya NNE.
 
Najua ni ukweli unaouma sana ila Membe ana hoja za msingi kuhusu utawala katili na hatari kuwai kutokea Tanzania ila ukweli ni kwamba Membe ni mchafu kama ilivyokuwa kwa Lowassa 2015. Hana jipya, hana cha ku-ofa Watanzania.

Membe kashiriki ufisadi wa kila aina kwenye utawala wa Kikwete.

Membe kashiriki mara kibao kutaka kukiua CHADEMA akiwa na wakina Zitto, Mwigulu na January Makamba.

Mtu wa namna hii siwezi kumtetea. Hapishani na Lowassa ambaye alikataa katiba akaja CHADEMA kutaka mabadiliko.

Membe ndiye alishiriki kuzuia Katiba ya wananchi kwenye utawala wa Kikwete.

Kiufupi Membe ni moja ya waasisi wa mfumo mbovu wa kiutawala uliopo. Ashugulikiwe kwelikweli, avune alichokipanda.
 
Hii habari ya membe mara lowasa mchafu uzushi wa kisengele nyuma, nani anatuma kusema fulani mchafu wakati wewe ni mchambawima tu
 
Ni uamuzi makini sana kusafisha nyumba mapema, kwani hawa mngewaacha mwishoni kabisa karibia na uchaguzi wangewaletea yale ya mwaka 2015, na matokeo yake wanachama wangegawanyika na kupunguza ushindi wa CCM halikadhalika CCM kujipa tabu kuisaka dola.

Ndio maana wapinzani wamelaani sana Kinana, hasa Membe kutolewa mapema, kwani turufu yao ilikua ajikatae uchaguzi ukikaribia.

Sasa Membe kabla hajafanya hivyo amewahiwa. Kiukweli CCM muendelee kuhakikisha masalia yote ya 2015 ya makundi yanakwisha au kumalizwa nguvu kabisa.

Nidhamu ndani ya chama kuelekea Uchaguzi Mkuu mwaka huu ni muhimu sana.

Mwisho kabisa CCM hongereni kwa kuonyesha kwamba ni taasisi imara haiyumbishwi na majina ya wale wanaojifanya bila wao CCM haipo.
 
Back
Top Bottom