Kuhani Musa Richard Mwacha ni nani?

Kuhani Musa Richard Mwacha ni nani?

Uthibitisho kwamba nyie ni matapeli uko kwenye maandiko matakatifu. Yote mnayoyaeneza huko yako nje ya maandiko. Hayo mashuhuda mnayowadanya watu hata kwa waganga wa kienyeji yanapatikana!

Yataje yale yanayofanyika ambayo yako nje ya maandiko

Halafu nikuulize swali, unaposema mashuhuda yanayofanyika huko hata kwa waganga yanafanyika ulishawahi kusoma biblia walau ujue ya waganga wa kienyeji hayawahi shinda ya Mungu? Kabla ya kuleta blahblah nenda kamuulize Farao atakueleza yaliyomkuta

Kutoka 7: 8 - 12
Bwana akanena na Musa na Haruni, akawaambia, Farao atakaponena nanyi, na kuwaambia, Jifanyieni miujiza; ndipo utakapomwambia Haruni, Shika fimbo yako, uibwage chini mbele ya Farao, ili iwe nyoka.
Basi Musa na Haruni wakaingia kwa Farao, wakafanya vivyo kama Bwana alivyowaambia; Haruni akaibwaga fimbo yake chini mbele ya Farao, mbele ya watumishi wake, ikawa nyoka.
Ndipo Farao naye akawaita wenye akili na wachawi; na hao waganga wa Misri wakafanya vivyo kwa uganga wao. Wakabwaga chini kila mtu fimbo yake, nazo zikawa nyoka; lakini fimbo ya Haruni ikazimeza fimbo zao.

Kama hujui usijitie aibu, tulia ujifunze ndio uongee.
 
Kuzuia huo udanganyifu ni pamoja na kukuambia ukweli wewe uliyertumwa na ibilisi kupigia debe mafundisho ya kuuawa watu kiroho. Injili ya Yesu iko wazi kwenye maandiko matakatifu. Hiyo injili yenu unayoieneza hapa wala sio injili ya ufalme, ni ile injili nyingine ya kupeleka watu upotevuni! Msaada hauwezi kutolewa kupitia injili isiyo yenyewe. Mnapoteza watu kama waganga wa kienyeji wanavyopoteza watu!

Shetani ni roho iliyo ndani ya mtu na huyo mtu atajulikana kwa matendo yake ya kumtukuza aliye ndani yake kama wewe unavyomtukuza shetani wako

Vinginevyo niambie hiyo injili inayohubiriwa kupeleka watu upotevuni ni ipi

Sio unaongeaongea tuu kama Chawa wa Ibilisi😅😅😅😅
 
Sijaona Tatizo, Hiyo ni Biashara kama Biashara nyingine halali, mteja anaenda kupata huduma anakuwa huru mwenyewe as long as halazimishwi. Hivyo ni muhimu kila mteja apime mwenyewe kabla ya kupata huduma kama ambavyo anaweza kuchagua Shule ya watoto wake, Hospitali ya Tiba ya familia yake, Kampuni ya Ndege anayoipenda etc
 
Ukigeuka huku mungu chini ya jua, ukigeuka huku nabii sijui nani, ukirudi huku kuhani, ukizunguka hapa mtume, yani naona mdogo mdogo tunarudi zama za akina Elia.
 
Musa Richard ni mganga (mchawi ) mpya pale kimara temboni
Hiyo ni kweli,
Haiwezekani mfanyabiashara maji ya nusu lita anafanya production na yuko profit oriented lakini anayauza TSh. 300/= halafu yeye ujazo huohuo wa maji ya upako eti kisa kayaombea anauza TaSh .2500/= yaani ni jizi kabisa , bora hata lingeuza buku japo bado ni faida kubwa sana,
 
Uthibitisho kwamba nyie ni matapeli uko kwenye maandiko matakatifu. Yote mnayoyaeneza huko yako nje ya maandiko. Hayo mashuhuda mnayowadanya watu hata kwa waganga wa kienyeji yanapatikana!
Lile jamaa hata ukilitazsms sura lake unaona ni jizi, chawi na lina roho mbaya ya kishetani.
Wala huoni nuru ya Upendo wa YESU KRISTO usoni mwake.
 
Hiyo ni kweli,
Haiwezekani mfanyabiashara maji ya nusu lita anafanya production na yuko profit oriented lakini anayauza TSh. 300/= halafu yeye ujazo huohuo wa maji ya upako eti kisa kayaombea anauza TaSh .2500/= yaani ni jizi kabisa , bora hata lingeuza buku japo bado ni faida kubwa sana,

Kama unafikiri ni rahisi hivyo kuuza maji na wewe tengeneza maji yako uuze!

Vinginevyo tulia uwasikilize wanaoyatumia wanasemaje

Cc mama kubwa
 
Yaani mwanamke hata vakiwa Profesa kwanye hii mambo ananaswa kirahisi....yaani hao mashuhuda hasa huyo sijui malkia wa freemason unaona kabisa amekaririshwa hayo anayoongea....hata mtoto wa chekechea hawezi kukubali

Thibitisha
 
Kama unafikiri ni rahisi hivyo kuuza maji na wewe tengeneza maji yako uuze!

Vinginevyo tulia uwasikilize wanaoyatumia wanasemaje

Cc mama kubwa
Hovyoo..! eti uwasikilize wanaoyatumia wanasemaje? Huu ni ujinga uliopitiliza. Kwanza, hakuna mahali Yesu alifanya ujinga wa namna hii. Na biblia inatuambia watu walipomkimbilia wakitaka miujiza dizaini kama hiyo ya kwenu, aliwapotezea! Nyie mnaona deal watu wanapojazana kwenu kusaka miujiza feki badala ya kusaka neno la Mungu. No doubt, hakuna injili huko mnakokusifia, hata huyo mtu wenu halijui neno la Mungu!, neno la Mungu huhubiriwa hadharani, hivyo ni rahisi kupimwa kwa mujibu wa maandiko matakatifu.. Pili, hao wanaoshuhudia wengi miongoni mwao wanapita au waliishapita kwa mitume na manabii wengine kushuhudia yale yale wanayoshuhudia huko kwenu leo. kwahiyo, wanakusanyana Nabii wa Uongo na makristo wa uongo kila mmoja kutetea tumbo lake!
 
Tuachane na miujiza anayofanya YESU wa Ngomeni kwa Kuhani Musa ambayo na mimi nimeiona maishani mwangu ila Kuhani Musa ni mwalimu mzuri wa Biblia, na hili ndio lililonivutia kwenda ktk ibada zake, maana napenda kusikia neno.

Mimi nilikuwa mbishi kama wabishi wengine, ila kunawakati maji yalifika shingoni, niseme tu toka nimehudhuria ibada niliona mabadiliko na pia nilipotumia VIFAA VYA KIROHO VYA NGOME YA YESU kwa Kuhani, Mwalimu na Mwonaji Musa Richard Mwacha vilinisaidia.

Pia IMANI yangu ndio iliyochangia mimi kusaidiwa, kwakuwa niliweka Imani kuwa natumia kwa jina la YESU nikapokea.

Tatizo watu wengi wanaamini watumishi zaidi ya kumwamini YESU/MUNGU.

BWANA YESU KRISTO ATUKUZWE

mama D
 
Tuachane na miujiza anayofanya YESU wa Ngomeni kwa Kuhani Musa ambayo na mimi nimeiona maishani mwangu ila Kuhani Musa ni mwalimu mzuri wa Biblia, na hili ndio lililonivutia kwenda ktk ibada zake, maana napenda kusikia neno.

Mimi nilikuwa mbishi kama wabishi wengine, ila kunawakati maji yalifika shingoni, niseme tu toka nimehudhuria ibada niliona mabadiliko na pia nilipotumia VIFAA VYA KIROHO VYA NGOME YA YESU kwa Kuhani, Mwalimu na Mwonaji Musa Richard Mwacha vilinisaidia.

Pia IMANI yangu ndio iliyochangia mimi kusaidiwa, kwakuwa niliweka Imani kuwa natumia kwa jina la YESU nikapokea.

Tatizo watu wengi wanaamini watumishi zaidi ya kumwamini YESU/MUNGU.

BWANA YESU KRISTO ATUKUZWE

mama D


Ubarikiwe Donatila
Maelezo makini sana haya

Tatizo ni watu wengi tunajiita wakristo na hata waislamu ila hatuujui huo ukristo hatulijui neno wala hatuna pa kusimama tukijaribiwa au tunapohitaji nguvu za Mungu...... mbaya zaidi tumezibeba dini na madhehebu yetu tukifikiri ndio za kutupatia msaada

Humjui Mungu unayemuabudu, huzijui sheria na maagizo yake amini hata yeye hakuoni kwenye nafasi yake

Mungu ambariki sana Kuhani na mwalimu Musa Richard Mwacha kwa mafundisho yake

Mungu atusaidie sana
 
Uthibitisho kwamba nyie ni matapeli uko kwenye maandiko matakatifu. Yote mnayoyaeneza huko yako nje ya maandiko. Hayo mashuhuda mnayowadanya watu hata kwa waganga wa kienyeji yanapatikana!
Mkuu kwa kuhan Musa hakunaga habari njema, yaan kuwahubiria watu waokoke, kwa kupitia jina la Yesu Kristo? namaanisha huwa haiti watu kuokoka? siku zote ni habari za miujiza tu?
 
Mkuu kwa kuhan Musa hakunaga habari njema, yaan kuwahubiria watu waokoke, kwa kupitia jina la Yesu Kristo? namaanisha huwa haiti watu kuokoka? siku zote ni habari za miujiza tu?

Akikujibu nitag please
 
Sijaona Tatizo, Hiyo ni Biashara kama Biashara nyingine halali, mteja anaenda kupata huduma anakuwa huru mwenyewe as long as halazimishwi. Hivyo ni muhimu kila mteja apime mwenyewe kabla ya kupata huduma kama ambavyo anaweza kuchagua Shule ya watoto wake, Hospitali ya Tiba ya familia yake, Kampuni ya Ndege anayoipenda etc
Isingekuwa tatizo kama ingebaki hivyo.

Ila tatizo ni kudanganya na kupotosha Watu...kuaminisha Watu kuwa Mtu anaweza kufufuka ni utapeli kama tu ule unaofanywa na Waganga wa kinyeji wa kubambikia Watu Mtu asiye ao na kuwaambia wamemleta ili hali Wali walishamzika Marehemu wao.

Ugomvi wangu na hawa Watu ni hapo tu, "uongo".
 
Back
Top Bottom