Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 15,101
- 56,054
Rais Samia anasema eti suala la kipaumbele kwake ni uchumi kwanza halafu mambo ya katiba mpya ni ya baadae huko mbeleni.
Ningependa kumkumbusha Rais Samia kuwa, hoja ya Katiba Mpya ni hoja nyeti, ni suala muhimu sana na haliwezi kuwa option ya pili katika mambo yanayopaswa kufanyika nchini kwa sasa. Na hii ni kwa sababu zifuatazo:
1. Katiba mpya haizuii kujenga uchumi
Rais anaposema eti tumpe muda ajenge uchumi kwanza ndo afikirie Katiba Mpya, tungependa kumueleza Rais kuwa kuwa na katiba mpya hakumzuii yeye au Serikali yake kujenga Uchumi, Labda Rais atueleze, je Katiba bora iliyo nzuri inazuiaje yeye kuvutia wawekezaji, inazuiaje kuboresha utalii, inazuiaje kujenga miundo mbinu? Hapa kimsingi Rais hana hoja yenye mashiko kabisa juu ya kukataa kuwapa wananchi aina ya Katiba wanayoitaka.
2. Mchakato wa Katiba Mpya si hisani ya Rais bali ni hitaji la kisheria
Ipo sheria ya mwaka 2012 inayo-govern Mchakato wa Mabadiliko ya Katiba Mpya, Sisi wananchi tunamtaka Rais atekeleze Sheria hiyo, asifanye hili suala kama hisani yake binafsi, hili ni hitajio la wananchi wengi.
3. Hofu ya Rais ni ya kisiasa na si kimaslahi ya kitaifa
Kauli ya Rais ya kukataa kuipa Katiba kipaumbele ilianza kwenye awamu ya tano ambayo yeye alikuwa Makamu wa Rais, Rais wa wakati huo na yeye alisema hoja hizohizo za kujenga uchumi kwanza kabla ya kuleta Katiba Mpya, leo hii tuna miaka mitano bado tunapigwa kalenda hizohizo za ngoja tujenge uchumi. Huhitaji kuwa genius kuona kwamba hofu ya viongozi hawa ni hofu za kisiasa tu, za kuhofia hatma zao na vyama vyao kisiasa iwapo Taifa litapata Katiba Mpya, ni dhahiri wahafidhina ndani ya CCM hawataki Katiba Mpya, lakini kama alivyowahi kusema Katibu Mkuu mstaafu wa CCM, Hoja ya Katiba Mpya haitakufa mpaka ipatikane.
4. Kujenga Uchumi bila kuwa na Katiba ya kuulinda ni kazi bure
Hii katiba tuliyonayo inampa Rais Mpya power za kuvunjilia mbali mafanikio ya Serikali zilizopita, anaweza kusitisha mradi wa kimkakati, anaweza kuingia mikataba ya siri isiyo na faida, anaweza kutapanya rasilimali zetu na asishtakiwe. Kwa hiyo ni dhahiri hata ujenge uchumi mzuri kivipi, bila Katiba nzuri huwezi kuulinda Uchumi huo, ndiyo maana hitajio letu la Katiba Mpya ni muhimu sana.
5. Watanzania hatuko tayari kurudi katika utawala wa kidikteta aina ya awamu ya tano
Ktk utawala wa awamu ya tano tuliona matendo ya kinyama na kiuonevu yaliyofanyika, sababu mojawapo ya matendo hayo ni kuwa na Katiba inayotoa mwanya mtawala kuvunja sheria bila consequences ikiwemo kushtakiwa, Katiba hii imetoa mamlaka makubwa kwa Rais, na kiukweli ni Katiba ya kidikteta, Hatuwezi kuruhusu scenario ya kupata aina ya uongozi wa awamu iliyopita, na guarantee bora ya kutofika huko ni Katiba Mpya na si maneno matamu tu ya Rais Samia.
Ningependa kumkumbusha Rais Samia kuwa, hoja ya Katiba Mpya ni hoja nyeti, ni suala muhimu sana na haliwezi kuwa option ya pili katika mambo yanayopaswa kufanyika nchini kwa sasa. Na hii ni kwa sababu zifuatazo:
1. Katiba mpya haizuii kujenga uchumi
Rais anaposema eti tumpe muda ajenge uchumi kwanza ndo afikirie Katiba Mpya, tungependa kumueleza Rais kuwa kuwa na katiba mpya hakumzuii yeye au Serikali yake kujenga Uchumi, Labda Rais atueleze, je Katiba bora iliyo nzuri inazuiaje yeye kuvutia wawekezaji, inazuiaje kuboresha utalii, inazuiaje kujenga miundo mbinu? Hapa kimsingi Rais hana hoja yenye mashiko kabisa juu ya kukataa kuwapa wananchi aina ya Katiba wanayoitaka.
2. Mchakato wa Katiba Mpya si hisani ya Rais bali ni hitaji la kisheria
Ipo sheria ya mwaka 2012 inayo-govern Mchakato wa Mabadiliko ya Katiba Mpya, Sisi wananchi tunamtaka Rais atekeleze Sheria hiyo, asifanye hili suala kama hisani yake binafsi, hili ni hitajio la wananchi wengi.
3. Hofu ya Rais ni ya kisiasa na si kimaslahi ya kitaifa
Kauli ya Rais ya kukataa kuipa Katiba kipaumbele ilianza kwenye awamu ya tano ambayo yeye alikuwa Makamu wa Rais, Rais wa wakati huo na yeye alisema hoja hizohizo za kujenga uchumi kwanza kabla ya kuleta Katiba Mpya, leo hii tuna miaka mitano bado tunapigwa kalenda hizohizo za ngoja tujenge uchumi. Huhitaji kuwa genius kuona kwamba hofu ya viongozi hawa ni hofu za kisiasa tu, za kuhofia hatma zao na vyama vyao kisiasa iwapo Taifa litapata Katiba Mpya, ni dhahiri wahafidhina ndani ya CCM hawataki Katiba Mpya, lakini kama alivyowahi kusema Katibu Mkuu mstaafu wa CCM, Hoja ya Katiba Mpya haitakufa mpaka ipatikane.
4. Kujenga Uchumi bila kuwa na Katiba ya kuulinda ni kazi bure
Hii katiba tuliyonayo inampa Rais Mpya power za kuvunjilia mbali mafanikio ya Serikali zilizopita, anaweza kusitisha mradi wa kimkakati, anaweza kuingia mikataba ya siri isiyo na faida, anaweza kutapanya rasilimali zetu na asishtakiwe. Kwa hiyo ni dhahiri hata ujenge uchumi mzuri kivipi, bila Katiba nzuri huwezi kuulinda Uchumi huo, ndiyo maana hitajio letu la Katiba Mpya ni muhimu sana.
5. Watanzania hatuko tayari kurudi katika utawala wa kidikteta aina ya awamu ya tano
Ktk utawala wa awamu ya tano tuliona matendo ya kinyama na kiuonevu yaliyofanyika, sababu mojawapo ya matendo hayo ni kuwa na Katiba inayotoa mwanya mtawala kuvunja sheria bila consequences ikiwemo kushtakiwa, Katiba hii imetoa mamlaka makubwa kwa Rais, na kiukweli ni Katiba ya kidikteta, Hatuwezi kuruhusu scenario ya kupata aina ya uongozi wa awamu iliyopita, na guarantee bora ya kutofika huko ni Katiba Mpya na si maneno matamu tu ya Rais Samia.