Kuhusu Katiba Mpya: Hoja ya Rais Samia haina mashiko
Nchi ina mfumo wa vyama vingi tangu 1992 kwanini maccm waendelee kufanya uhuni wao kwa miaka 30 sasa kukumbatia katiba ya mfumo wa chama kimoja? Kwanini Butiku na Warioba ambao ni maccm damu damu wanaunga hoja ya kuwa na Katiba mpya. Kwanini Bashiru kabla ya kuwa Katibu Mkuu wa maccm aliona umuhimu mkubwa wa kuwa na Katiba mpya?

Je katiba mpya ni takwa la wanasiasa au la wananchi......??
 
Nani amekwambia tunatafuta perfection ya 100%?
Tunachosema ni kuwa katiba ya siasa siyo muafaka wa kitaifa wa nmna tunavyotaka nchi yetu iongozwe.
The only reason CCM na Rais hawataki katiba mpya ni kwa sababu wanaitumia katiba hii kupora chaguzi za wananchi, kutapanya resources za Taifa kupitia mikataba ya kifisadi bila consequences.
Hakuna reason ya msingi ya wao kukataa katiba mpya!
Ni maoni yako. Kuna ambao wanapata maisha bora kupitia katiba hii hii. Kuna watendaji wanaongeza pato la taifa kupitia katiba hii hii.

Rwanda hana katiba nzuri lakini nchi yao inapaa kiuchumi.
 
Mkuu kuna dikteta mwingine Ikulu anayedhani ana haki ya kutuamulia Watanzania vile atakavyo yeye kinyume na Katiba ya Nchi.
Sema kimeumana..hahahahhahaha..nmefurah sana..mama anaupiga ule ule wa mzee baba sema kwa saut ya kinyonge sana.saf mama samia

Mnaohis hamwez ish bila siasa imekula kwenu
 
Nani anataka kupiga kura yake ya kuchagua Rais, Mbunge au diwani kisha kura hiyo ikaibiwa kwa mtutu wa bunduki? Chama kiko madarakani kwa miaka 60 sasa kimefanya lipi katika kuboresha uchumi wa nchi katika hiyo miaka 60? Ajira hakuna graduates wanasaga lami, elimu yetu ni ya hovyo sana, matibabu pia ni hovyo sana, usafiri pia ni hovyo sana. Mishahara ya wenye ajira ni ya chini mno miaka sita sasa bila nyongeza. Hebu tia akili kichwani japo KIDUCHU badala ya KUKURUPUKA.
Unafikiri katiba mpya itasababisha mshinde uchaguzi? kwa nini usiamini katika kujenga vyema chama chenu? Je unafahamu kwamba Vyama vingi vya upinzani hapa nchini ni vya hovyo hovyo tena bado hawajitambua? Je malengo yenu ya katiba mpya yanalenga nini zaidi ya kutaka kushinda uchaguzi? Nitajie katiba mpya ya nchi yoyote ilivyosaidia graduate wote wa nchi hiyo kupata ajira,
Mwisho naungana na wewe ukitaka katiba mpya ingawa malengo yako hayajaangalia masilahi ya walio wengi.
 
Kuiheshimu katiba iliyowekwa kwa mujibu wa sheria ni kiapo chake, hilo halina mjadala, wala hahitaji kuomba ushauri kwetu

Ila tunachomwambia ni kuwa kuna sheria ya mabadiliko ya katiba, inabidi aitekeleze hiyo wananchi tupate katiba mpya, hilo nalo siyo hiari yake

Mkuu, nini kimebadilika?

Alisema Samia = JPM watu wakamshangilia na wengine huku wakanuna.

Nini alifanya? Leo hii kina Nigrastratatract wanapanga kuunda chama kipya.

Anachosema acha aseme. Tujikite kwenye anafanya nini. Hilo la kwanza. Ila la msingi zaidi ni kuwa tumtake kuheshimu katiba kwa kuendelea na shughuli zetu kwa mujibu wa katiba. Huo ndiyo msingi wa hoja kwenye uzi huu:


Kwa nini kelele za chura tusinywe maji?
 
Ni maoni yako. Kuna ambao wanapata maisha bora kupitia katiba hii hii. Kuna watendaji wanaongeza pato la taifa kupitia katiba hii hii.

Rwanda hana katiba nzuri lakini nchi yao inapaa kiuchumi.
Hii katiba ipo toka mwaka 1977 ingekuwa nzuri basi CCM wasingeiweka kwenye ilani ya uchaguzi mwaka 2015 ibadilishwe. Ofcourse tunajua kuwa Serikali ya Magufuli na Samia akiwa makamu wake ilifanya uhuni na kukataa kutekeleza suala hilo!

Haiwezekani mtu aliyeomba kazi ya kuwa makamu mwenyekiti wa bunge la kubadili katiba aone eti katiba mpya siyo kipaumbele chake. Kwa hii flipflop ambayo rais anaifanya anaonyesha kuwa naye kanogewa na katiba hii ya kidikteta
 
Wapi nilipoandika kwamba Katiba mpya itasababisha Chadema ishinde uchaguzi? Unajua chochote kuhusu uchaguzi huru na wa haki ambao vyama na Watanzania wanashiriki bila ya hofu ya kupigwa mabomu ya machozi, risasi na kuibiwa kura zao?

Mbona maccm Butiku na Warioba nao wanaipigia debe Katiba mpya? Mbona Mkapa kabla ya kufariki alitaka uchaguzi wa 2020 usimamiwe na Tume huru!?

Huwezi kusema eti hatuhitaji katiba mpya Kwa sababu vyama vingi nchini havijitambui na vya hovyo hovyo.

Katiba mpya na Tume huru ya uchaguzi ni haki yetu Watanzania bila kujali uwepo wake utabadili vipi matokeo ya uchaguzi nchini.

Unafikiri katiba mpya itasababisha mshinde uchaguzi? kwa nini usiamini katika kujenga vyema chama chenu? Je unafahamu kwamba Vyama vingi vya upinzani hapa nchini ni vya hovyo hovyo tena bado hawajitambua? Je malengo yenu ya katiba mpya yanalenga nini zaidi ya kutaka kushinda uchaguzi? Nitajie katiba mpya ya nchi yoyote ilivyosaidia graduate wote wa nchi hiyo kupata ajira,
Mwisho naungana na wewe ukitaka katiba mpya ingawa malengo yako hayajaangalia masilahi ya walio wengi.
 
Rais Samia anasema eti suala la kipaumbele kwake ni uchumi kwanza halafu mambo ya katiba mpya ni ya baadae huko mbeleni.

Ningependa kumkumbusha rais Samia kuwa, hoja ya katiba mpya ni hoja nyeti, ni suala muhimu sana na haliwezi kuwa option ya pili katika mambo yanayopaswa kufanyika nchini kwa sasa. Na hii ni kwa sababu zifuatazo

1. Katiba mpya haizuii kujenga uchumi
Rais anaposema eti tumpe muda ajenge uchumi kwanza ndo afikirie katiba mpya, tungependa kumueleza rais kuwa kuwa na katiba mpya hakumzuii yeye au serikali yake kukjenga uchumi, Labda Rais atueleze, je katiba bora iliyo nzuri inazuiaje yeye kuvutia wawekezaji, inazuiaje kuboresha utalii, inazuiaje kujenga miundo mbinu?. Hapa kimsingi rais hana hoja yenye mashiko kabisa juu ya kukataa kuwapa wananchi aina ya katiba wanayoitaka.

2. Mchakato wa katiba mpya si hisani ya rais bali ni hitajio la kisheria
Ipo sheria ya mwaka 2012 inayogovern mchakato wa mabadiliko ya katiba mpya, Sisi wananchi tunamtaka rais atekeleze sheria hiyo, asifanye hili suala kama hisani yake binafsi, hili ni hitajio la wananchi wengi.

3. Hofu ya rais ni ya kisiasa na si kimaslahi ya kitaifa
Kauli ya rais ya kukataa kuipa katiba kipaumbele ilianza kwenye awamu ya tano ambayo yeye alikuwa makamu wa rais, rais wa wakati huo na yeye alisema hoja hizohizo za kujenga uchumi kwanza kabla ya kuleta katiba mpya, leo hii tuna miaka mitano bado tunapigwa kalenda hizohizo za ngoja tujenge uchumi. Huhitaji kuwa genius kuona kwamba hofu ya viongozi hawa ni hofu za kisiasa tu, za kuhofia hatma zao na vyama vyao kisiasa iwapo Taifa litapata katiba mpya, ni dhahiri wahafidhina ndani ya CCM hawataki. katiba mpya, lakini kama alivyowahi kusema katibu mkuu mstaafu wa CCM, Hoja ya katiba mpya haitakufa mpaka ipatikane.

4. Kujenga uchumi bila kuwa na katiba ya kuulinda ni kazi bure
Hii katiba tuliyonayo inampa rais mpya power za kuvunjilia mbali mafanikio ya serikali zilizopita, anaweza kusitisha mradi wa kimkakati, anaweza kuingia mikataba ya siri isiyo na faida, anaweza kutapanya rasilimali zetu na asishtakiwe. Kwa hiyo ni dhahiri hata ujenge uchumi mzuri kivipi, bila katiba nzuri huwezi kuulinda uchumi huo, ndiyo maana hitajio letu la katiba mpya ni muhimu sana

5. Watanzania hatuko tayari kurudi katika utawala wa kidikteta aina ya awamu ya tano
Ktk utawala wa awamu ya tano tuliona matendo ya kinyama na kiuonevu yaliyofanyika, sababu mojawapo ya matendo hayo ni kuwa na katiba inayotoa mwanya mtawala kuvunja sheria bila consequences ikiwemo kushtakiwa, Katiba hii imetoa mamlaka makubwa kwa rais, na kiukweli ni katiba ya kidikteta, Hatuwezi kuruhusu scenario ya kupata aina ya uongozi wa awamu iliyopita, na guarantee bora ya kutofika huko ni katiba mpya na si maneno matamu tu ya rais Samia
Samia ni mccm tu, Katiba Mpya na Tume huru ni kitanzi kwa CCM.
 
Mimi nilisema Mkuu Maza sina imani naye sasa maneno yangu yametimia Mkuu.

Wakuu BAK na bwana Missile of the Nation sioni penye lolote jipya. Kumbukeni huyu mama alishatamka:

Samia = JPM

Kuna iliyo more serious leo kuliko hiyo? Kwani hata aliyosema hivyo alifanya nini?

Jamani tuwe watulivu hakuna lolote jipya.

Kufahamu haki haitakuja kwa kupewa ni suala la msingi sana. Tulipofika hata angekuwa jiwe angesalimu amri.

Vita hivi ni vita vya watu wanaotegemea kusikia habari mbaya zaidi kuliko kila mbaya tunazopata.

Ni kwa njia hiyo tu ambayo kwayo tutashinda.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Ni vema Rais Samia akaruhusu mchakato wa katiba mpya kufanyika kuliko akasubiri alazimishwe.

Rais hajui kuwa hawezi kupata wawekezaji makini bila kuwa na sheria nzuri ja zinazoheshimika na kila mtu. Huwezi kupata sheria nzuri kama huja katiba nzuri.
 
Kwanini mnataka kuchukua nafasi kama wasemaji wa wananchi? chadema ndo waongeaji wakuu wa katiba?
 
Mumewauliza wananchi kama wanataka Katiba mpya au wanataka uchumi?.Wananchi wengi,tunataka uchumi,tupate mkate wetu wa leo na kesho,mambo ya Katiba ni yenu nyinyi wanasiasa,sisi wananchi bora mkono uwende kinywani.Hebu anzeni nyinyi wanasiasa muwaulize wananchi,hata kwa kupiga kura,kwenye maeneo yenu.
Hiyo ni sawa na kumwuliza mtu kama anataka usingizi mzuri au godoro zuri.
 
Ccm ni ileile, hata kama Rais ni mama lazima muisome namba kina faru John & Co.
 
Ni ngumu sana nchi hii kupata katiba nzuri kwasababu agenda yenyewe imetekwa na wanasiasa, tena uchwara.

Wananchi wamewekwa pembeni.
Hao wanasiasa wanapigania katiba mpya kwa maslahi ya nani.....??
 
Nchi ina mfumo wa vyama vingi tangu 1992 kwanini maccm waendelee kufanya uhuni wao kwa miaka 30 sasa kukumbatia katiba ya mfumo wa chama kimoja? Kwanini Butiku na Warioba ambao ni maccm damu damu wanaunga hoja ya kuwa na Katiba mpya. Kwanini Bashiru kabla ya kuwa Katibu Mkuu wa maccm aliona umuhimu mkubwa wa kuwa na Katiba mpya?

Je unadhani wananchi wana uelewa wa umuhimu wa katiba na faida za moja kwa moja zitokanazo na mabadiliko ya katiba mpya.......na kipi ni kipimo cha wananchi cha uelewa wao juu ya katiba mpya......??
 
Back
Top Bottom