Kuishi kwingi kuona mengi: Soma kisa nilichokiona Kawe

Kuishi kwingi kuona mengi: Soma kisa nilichokiona Kawe

Mkuuu.... Sikwenda kufanya research ya Watu kuanguka .. Ndugu Yangu aliniona hali Yangu..akanishauri niende huko... Imani Yangu ilikua haba Kama SI hamna.

Tena nishawai kwenda na kanisa Moja pale posta PSSF TOWER sijui saiv linaitwaje....wale hawakuanguka ..Ila miss ilikua ya kiingereza SIKUELEWA KITU.
Omba sana upate imani, maana
 
"E="Jasmoni Tegga, post: 37314175, member: 614149"]
Mkuu,

Kuanguka ishara ya kufunguliwa ("maombi ni ya deliverance"), ile nguvu ya mauzauza ambayo siyo halisi inayokutesa inakuwa imekemewa kwa mamlaka na inaondoka.
[/QUOTE]
unahisi nguvu za uponyaji zinatoka kwa shetani au mungu?!
 
Huu ulimwengu hatujauumba sisi tumezaliwa tumeukuta. Kama unatambua uwepo wa uchawi naamini utaamini kuna Mungu. Wewe jiulize tu maswali rahisi tu kwanini hakuna siti namba 13 kwenye Ndege, Wewe jiuliza tu unaambiwa mtu kafa hivi nini kinaondoka mwilini maana kila kitu ukikagua vipo mwilini lakini hapumui. Jiulize vijiswali vyepesi tu inakuaje Mtu anatoa kafara familia yake kisha anakuwa Tajiri,Hivi nini kinamkuta mtu tunayeambiwa anayo Mapepo unakuta Mtu anapiga kelele anapiga ukuta vichwa, anazama kwenye maji masaa mpaka mawili akiwa Hana mtungi wa gesi pamoja na yote akiombewa na Sheikh au Mchungaji anapona na anaendelea na Shughuli zake, Jiulize nini dhumuni la wewe kuwepo duniani, Natakua kujua kwanini haujiulizi Dunia imetengenezwa na nani na ni Fundi wa aina gani.Jichunguze mwenyewe kisha jiulize tu kwanini Daktari wa Macho kwanini hawezi kutibu moyo halafu jiulize ni nani anaweza kutibu vyote. Umewahi kufikiri kwanini Madaktari nguli lakini bado wanakwenda Ibadan. Umewahi kuona watu wanapasua Nazi njia panda? Au kuchinja Mbuzi njia panda, Leo fikiria kwa upana zaidi Hivi walioandika vitabu vitKatifu walikuwa na upeo gani wa kufikiri?. Jiulize vijiswali vidogo hivyo kisha njoo utujibu..
Kwa hiyo maswali yote hayo jibu lake moja??
 
Picha linaanza napokea simu kwa ndugu zangu upande wa mama watoto wangu wanasema, samahani tunakuja kwenye maombezi kwa Mwamposa wewe kama mwenyeji tunaomba utupokee ili utupeleke kwa Mwamposa tukaombewe.

Nikasema ok poa nitawapeleka nyie njooni. Ijumaa wakaingia ndani ya jiji la Dsm nikawapokea, Jumamosi chapu nikawapeleka Kawe kuombewa, mimi nikaamsha kwenye mishe zangu za hapa jijini.

Kesho yake Jumapili waakambiwa warudi tena kweli Jumapili tena nikawarudisha kwenye ibada kama kawaida nikasema ibada ikiisha mtanistua nije kuwachukua.

Mida ya saa nane ibada ikaiisha wakanishitua nikawachukuwe nilipofika kwa Mwamposa mmoja wao akasema kuwa kuna mfanyakazi mwenzake walishawahi kufanya naye kazi miaka ya nyuma kwenye kampuni kampigia simu waonane maeneo ya PICOLO HOTEL kuna maombezi pia.

Basi bwana tukaenda pale Picolo hotel kufika pale wakatupandisha juu kuna ukumbi kule wanasali.

Nilichokikuta kule kinashangaza sana kwa kuwa ilibidi niwasubiri basi nikasema hebu ngoja nikae nisikilizie hapahapo ukumbini.

Kanisa lina waumini 13 tu, wanawake 10 na wanaume 3. Maombi yakaanza nguvu ya upako sijui nini inawashukia wakawa wanadondoka waumini wote hadi ndugu zangu nao wanadondoka.

Nikajisemea moyoni mbona haya majanga. Ikawa kama mchezo sasa wanaombewa watano waliobaki wanasimama nyuma yao kuwashikilia ili wasijibamize sakafuni. Wakizinduka wengine tena wanaombewa halafu waliodondoka wanaamka tena kuwashikilia wenzao.

Nikachoka kuangalia movie ya kitoto nikawambia oya nyie si mnadondoka humu hebu niwaache mkipona mtanishitua nije niwachukue twende nyumbani. Nimeshangaa hivi kipi kinamfanya mtu anadondoka hovyo wakati wa maombezi au ni michezo ya kuigiza?​
 
[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji38][emoji38][emoji38]
Nina dada yangu humwambii kitu kuhusu Mwamposa, kila akija kunitembelea lazima aje na mafuta kwenye kichupa huwa akinipa nachukua akiondoka natupa, nahisi amegundua, jana nilipita nyumbani kwake kumsalimia akanivizia akanipaka kichwani
 
hahahaha apo ndo uamini mjini shule kijijini tuition na ndio staili yao iyo yakukusanya watu af wengine wasio jua wana amini kuna upako kumbe n ujanja wakutengeneza mazingiri ya sadaka…………...
 
Nikweli..wanaume wamesimama nyuma ya wanawake eti wanawadaka na kuwabeba wakianguka..

Kuna Muda wa maombi Huyu Ndugu Yangu alikua TU anaapiga kelele anaanguka ...wanakuja vijana wanambeba wanampleka mbele ya kanisa..

Sijajua kwa undani sababu ya kuanguka..Rashid Gwajima anaweza kuwa na jibu.
Hahahahahaha..eti Rashid gwajima...mpaka Sasa hv porn video ya Gwaji boy limenitenga na rafiki yg kipenzi,akibisha lile sio Gwaji boy....tulibishana tukashindwa kuelewana ..akanichukua kuwa mm ni balozi wa shetani..
 
Hahahahahaha..eti Rashid gwajima...mpaka Sasa hv porn video ya Gwaji boy limenitenga na rafiki yg kipenzi,akibisha lile sio Gwaji boy....tulibishana tukashindwa kuelewana ..akanichukua kuwa mm ni balozi wa shetani..
Mimi sikuiona hiyo video kwa kwakweli....ila.mbunge Askofu Ustadhi Rashid Gwajima....sidhani Kama anafimbo sahihi ya kuongoza kondoo.
 
Au itakuwa hukumwelewa? But miujiza ipo sana
NI kweli miujiza ipo ila shaka yangu kubwa inatokana na mambo makuu mawili, kama umenisoma vizuri hapo juu. Ni kwamba huyu mtumishi baada ya kuwa amekaribishwa na kusimama kwenye madhabahu:

MOJA: Hakutoa hata ile sala fupi tu ya maombi, kuombea program iliypokuwa mbele yake

PILI: Kipindi chote alichokuwa amesimama madhabahuni, hakuwahi kusoma hata fungu moja fupi tu kutoka kwenye maandiko matakatifu.

Hoja yake kubwa ilikuwa ni kwamba apewe hela kwa ajili ya kwenda kufanya uinjilisti, ndiyo topic aliyoongelea mwanzo mpaka mwisho

Sasa haya yote ndiyo yanayonifanya niwe na mashaka makubwa sana kwamba mtumishi wa aina hii anaweza kweli akaambatana na muujiza wa kiwango cha juu kwa kiasi hicho tajwa, wakati hata kule kutoa sala fupi anapokuwa kwenye ibada kwaker ni shida, achilia mbali kusoma fungu fupi kutoka kwenye maandiko matakatifu. Tukio hili lilkitokea mwaka 2014 mwezi Septemba au Oktoba

Halafu kama wewe ni muumini kanisani, naktahadharisha uwe mwangalifu sana na mtumishi yeyote wa Mungu anayesimama madhabahuni halafu akawa anafanya mojawapo ya mambo haya matatu au yote kwa kwa pamoja

MOJA: Mtumishi kukaribishwa madhabahuni halafu akaanza kufundisha somo la maandiko matakatifu bila kuwa limetanguliwa na sala. Hata hivyo hii ina-apply tu kwa haya makanisa yetu ambayo huwa yanaendesha Ibada ambazo usomaji wake wa maandiko hauko guided sana.

MBILI: Mtumishi wa Mungu kusimama madhabahuni akifundisha maandiko matakatifu, bila yeye kuwa anasoma maandiko hayo, badala yake anakuwa amechagua mtu aqu watu miongoni mwa waumini kuwa wanasoma mafungu ya maandiko hayo badala yake yeye ila yeye anakuwa hasomi kabisa. Kwenye ulimwengu wa roho, kuna tofauti kati ya maandiko matakatifu kusomwa kutokea madhabahuni na kutokea sehemu nyingine yoyote ile ndani ya nyumba ya Ibada. Ndiyo maana watumishi huwa wanapanda juu madhabahuni wakiwa na Bibila. Neno linalosomwa na mtumishi kutokea mbele ya waumini au madhabahuni lina nguvu kuliko lile linalosomwa na muumini mwingine yoyote aliyekaa sehemu yoyote ile katikati ya waumini wengine, ndani ya nyuma ya Ibada. Kwa hiyo ukimuona mtumishi ambaye hasomi neno kutokea mbele ya waumini au madhabahuni, uwezekano mkubwa ni kuwa kuna kitu hakiko sawa na kwamba anaweza kuwa anafanya uchakachuaji wa hali ya juu sana.

TATU: Mtumishi wa Mungu kusimama mbele ya madhabahu na kuanza kufundisha maandiko matakaitu kutokea mdomoni kwake. Yaani anakuwa hasomi maandiko na sana sana ikibidi llabda anafaribu kutaja taja mafungu tu. Huyu anayeangukia kwenye kundi hili la mwisho ndiyo hatari zaidi na ni wa kuogopa kama ukoma!
 
Of course kuna fake pastor amini usiamimi, ila pia kuna jamaa alikata moto kwasababu ya kuanguka, aliangukia sehemu mbaya
 
Niliombewa na bibi yangu mzaa mama' alitumia jina la yesu kukemea ugonjwa huo.. bibi yangu ni nurse ila nilikataa dawa zake kwani hazikunisaidia na hali ilikua mbaya' nilimwambia nipeleke kwa mchungaji.. nadhani hii imani ndiyo iliniponya

hiyo imenifanya ni amini ukiwa na IMANI hakuna haja ya wachungaji

Nb.sisali kanisa lolote!
Wengi wetu imani ndio tatizo, tunaweka imani yetu kwa mchungaji kuliko kuweka kwa Mungu.


Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Of course kuna fake pastor amini usiamimi, ila pia kuna jamaa alikata moto kwasababu ya kuanguka, aliangukia sehemu mbaya
Na yule.paster anaembeba mwanaume mtu mzima na kumtupia kwenye viti...kweli hii style ya maombi ndo Yesu aliombea Watu hivyo...

Au kila nabiii anapata ufunuo wake.mwenyewe...?
 
Hili limenikumbusha miaka kadhaa iliyopita niliudhuria maombi katika kanisa moja liko boko maarufu kwa mzee*** basi bwana ilikua zamu yangu kuombewa nikawekwa mtu kati maombi yakaanza baada ya mda nikawa nimewekewa mikono sehemu mbalimbali ya mwili wangu,kutokana na kuomba kwao kwa kutumia nguvu wakawa wanasababisha maumivi mwilini mwangu especially mikono waliyokua wananivuta na kuniminya kwa nguvu,sasa nilishindwa kuvumilia nikawa nawatoa waniache wenyewe ndowanasema pepo linawajibu nikawa nawaambia mnaniumiza hawaniskii wanasema pepo linawajibu aisee nilipata tabu ambayo siwezi isahau mpaka nilipopata akili ya kwamba nitulie wajue pepo limeondoka nilikua na maumivu mwili mzima yaliyosababisha niumwe wiki nzima nyumbani ukijumlisha na yale mafuta tuliyokua tunapakwa machoni yanawasha kama pilipili...dah


Kingsmann
 
Na yule.paster anaembeba mwanaume mtu mzima na kumtupia kwenye viti...kweli hii style ya maombi ndo Yesu aliombea Watu hivyo...

Au kila nabiii anapata ufunuo wake.mwenyewe...?
[emoji1787] [emoji1787] [emoji1787] [emoji1787] [emoji1787] [emoji1787] [emoji1787] Nahisi ili pepo litoke unatakiwa upigwe wrestling [emoji2247] kwanza ukiumia basi pepo linaumia pia [emoji12][emoji12] linatoka nduki
 
Na yule.paster anaembeba mwanaume mtu mzima na kumtupia kwenye viti...kweli hii style ya maombi ndo Yesu aliombea Watu hivyo...

Au kila nabiii anapata ufunuo wake.mwenyewe...?
Kuna yule pastor anawatoa wadada chupi zao mbele ya kadamnasi ili wadada hao wapate watoto
 
Mimi sikuiona hiyo video kwa kwakweli....ila.mbunge Askofu Ustadhi Rashid Gwajima....sidhani Kama anafimbo sahihi ya kuongoza kondoo.
Hukuiona video ya gwajiboy? Usiangalie hana mazuri zaidi ya uchafu
 
Back
Top Bottom