Kulikuwa na uhalali gani kwa Chief Mkwawa kutambulika kama 'Shujaa?

Kulikuwa na uhalali gani kwa Chief Mkwawa kutambulika kama 'Shujaa?

Mpaka sasa bado dunia haijui Hitler alitowekaje duniani. Kuna wanaodai aidha USA au USSR kuna mmoja aliwahi kumkamata kisha akamficha...
Kaka tafadhali anza kusoma vitabu vya historia! Hitler alijiua. Taarifa ya askari waliokuwepo ziko.
Alijiua mnamo 30 Aprili 1945 saa tisa na nusu alasiri; alikaa kwenye handaki iliyoimarishwa chini ya ikulu yake mjini Berlin. Wakati ule jeshi jekundi (Warusi) waliwahi kuingia Berlin tayari walikuwa takriban mita 200-300 ilhali mapigano yaliendelea. Asubuhi ya 30 Aprili aliwaruhusu wote ambao bado walikuwa naye kwenye handaki waweze kuondoka. Yeye alijifunga ndani ya chumba kimoja pamoja na Eva Braun (aliyemwoa tar 29 Aprili). Baada ya kusikia mlio wa bastola askari 3 waliingia katika chumba wakakuta maiti za Hitler na Braun ; Braun alikuwa amemeza sumu, Hitler alijiua kwa bastola yake ya modeli Walther PPK 7.65. Afisa wa SS Otto Günsche alimkuta, alinuka harufu ya sumu kwa Braun akaona damu kweny ekichwa cha Hitler. Jinsi alivyoambiwa kabla ya tendo hili, alipeleka maiti nje akawatupa katika shimo kwenye bustani (kreta kutokana na mlipuko wa bomu iliyowahi kuanguka pale) akaagiza maiti yamwagwe mafuta na kuchomwa. Kundi la watu zaidi ya 8 ambao bado walikuwa wamebaki kwenye handaki walitazama.
Soma yote na historia ya masalia yake (yalikusanywa, kufanyiwa utafiti, kufichwa na jeshi la Kirusi hadi 1970, mwishoni mifupa yalisagwa na kutupwa kwenye mto Biederitz, pale Ujerumani.

Basi jisomee hapa Death of Adolf Hitler lakini usilalamike tena ni mengi. Ni hitimisho fupi, kuna vitabu vingi juu ya swali hilo.
 
Kamwe Shujaa huwa hajiui. Kwangu wala siyo Shujaa, ila nikiambiwa Watu kama akina Tundu Lissu, Mchungaji Msigwa na Freeman Mbowe ni Mashujaa nitakubali na Kuamini upesi mno.
 
Za chini ya kapeti zinadai Mkwawa alidedishwa na Mjerumani kwa kukatwa kichwa, ili kutunza hadhi ndio wakadai kajiua
Kwa hiyo kwa mawazo yako, nani aliyeweka kumbukumbu? Ikiwa ni wajerumani wakachukua uwongo wa waafrika wakautunza?????
 
Alaf unafananishaje mazingira ya kifo cha mkwawa na cha Gaddafi, ikiwa mkwawa alipambana na bunduki kwa mishale kwa asilimia kubwa na tena akipambana na mojawapo ya mataifa makubwa yenye jeshi kubwa na teknojia ya kisasa huku yeye akiwa hata sio taiga bali empire iliyo ndani ya taifa, huku akiwa na teknolojia duni.
Gadaffi pia alikuwa na teknolojia duni mbele ya NATO. Wahehe walikuwa empire ndani ya taifa gani?
 
Unapajua Kalenga na Tosamaganga wajeruman walijipanga zaida ya Mara mbili kuuweza mtiti wa Mkwawa wa leo hata mabomu ya machozi huwezi himili halafu unauliza ushujaa wa Mkwawa
wabishani kama huyu bwana ni wa kupuuza anachobisha kuhusu ushujaa wa mkwawa hata haeleweki sijui alitaka anyongwe kizembe na wajerumani ndio aonekane wa maana?
 
Msiwe mnajiita majina ambayo hamjui maana yake hujui chochote kuhusu kanuni za kivita tena sikutarajia wew kuuliza kitu Kama hichi kujiua n moja ya kanuni za kishujaa ili wanajeshi wako wasione ukiteswa kwa sababu utawavunja moyo
 
Kwa hiyo wale majasusi wanaojiangamiza baada ya kushtukiwa nao siyo mashujaa?

Siyo kweli... nipo tofauti na wewe kwenye hili...
 
Msiwe mnajiita majina ambayo hamjui maana yake hujui chochote kuhusu kanuni za kivita tena sikutarajia wew kuuliza kitu Kama hichi kujiua n moja ya kanuni za kishujaa ili wanajeshi wako wasione ukiteswa kwa sababu utawavunja moyo
Hiyo sababu ni ya uoga na kitoto sana
 
Una maono na hoja nzuri sana ila kwa hili, nikuulize tu inadhani pale kwenye kimfuko kidogo upande wa kushoto wa kombati, ile sumu tunayowekewa pale tuingiapo uwanja wa medani ni ya shoo, au ni ya kujipaka kama urembo na kuingia nayo nyuma ya keyboard za page ya jamii forum kuperuzi, unapozidiwa unalamba sumu unapunguza mengi, kua mateka kusikie tu kwenye muvi za kihindi kijana. Nimesoma tu heading nikaandika aina haja ata ya kusoma main point, askari wote we are born tu die . Mhudumu nigee safari lager kubwa
 
Kujiua kuna mambo mengi mkuu ( ingawa bado suala la Mkwawa kujiua is still debatable, hakuna mwenye uhakika ). Mimi nasoma sana hata habari za Waisrael (sasa Wayahudi ) na wenyewe mara kadhaa viongozi wao walipo elemewa walijiua; iko hivi; KIONGOZI ukitekwa, utateswa hadi useme SIRI yenu, na hilo ndilo ambalo adui hulitafuta, bora ufe na siri yako ili wengine walioachwa wapambane kivyao wakiendelea kuzishikiria codes zenu/zao
Samahani mkuu Siri gani wakati vikosi vyake vilishindwa?
 
Habari za wakati huu ndugu zangu wa humu jamiiforums.

Kulikuwa na uhalali gani wa Chief Mkwawa kutambulika kama "shujaa"? Kamwe hakuna askari anayeweza kuitwa shujaa kwa kuogopa adui kisha kujiua mwenyewe.

View attachment 1716322

Mbona Muamar Gadaffi wa Libya na Saddam Hussein wa Iraq hawakujiua kabla ya kukamatwa na wazungu? Mkwawa alikuwa shujaa ama askari muoga?

UOGA SIO SIFA NJEMA YA MWANAUME MPIGANAJI
=====
Uoga ni tabia ambayo hofu nyingi humzuia mtu kupambana na hatari au kukabiliana na adui. Uoga unaonyesha uwezo wa mtu kukosa tabia ya ujasiri wakati wa changamoto. Katika kanuni za kijeshi za nchi nyingi hapa duniani, uoga katika vita ni sawa sawa na uhalifu.

Vitendo vya uoga, kwa muda mrefu tangia vita ya kwanza ya dunia, vimeadhibiwa na sheria za kijeshi, ambazo inafafanua vema makosa yanayohesabika kama uoga, ikiwa pamoja na kumkimbia adui au kujisalimisha kwa adui pasipo kupata amri kutoka kwa wakubwa. Wale ambao walikamatwa walikuwa, mara kwa mara, wakipelekwa mahakamani na adhabu ya vitendo kama hivyo kwa kawaida huwa ni kali sana.

Siku zote ulimwengu umewaheshimu majasiri na kuwalaani waoga. Kuwa jasiri ni muhimu kwa mwanamume kama vile kuwa msafi kwa mwanamke, na muoga kati ya wanaume ana sifa mbaya kama kahaba kati ya wanawake.

Kujiua huitwa ni uoga kwa sababu inahitaji ujasiri wa hali ya juu sana ili uweze kuishi katika dunia iliyojaa kila aina ya changamoto, inahitaji mtu kuwa na mtazamo sahihi juu ya maisha na utulivu mkubwa wa akili. Pamoja na shinikizo na shida zote, vuta nikuvute za maisha ambavyo tunakabiliwa navyo, baadhi ya waoga huamua kuwa na mawazo hasi na kushindwa kupambana tena na badala yake kuchagua kufa.

KWA UFUPI SANA KUHUSU KIFO CHA CHIEF MKWAWA
=====
Kichwa cha mtemi kinasemekana kilikatwa na Wajerumani na kutumwa Berlin kilipohifadhiwa katika makumbusho, awali Berlin na baadaye Bremen. Waingereza waliochukua utawala wa koloni mwaka 1918 baada ya Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia walitaka kuonekana kama mabwana wema.

Mkuu wa serikali ya kikoloni ya Tanganyika alipendekeza kurudisha fuvu kwa sababu Wahehe walishirikiana na Waingereza wakati wa vita. Hivyo kuna kipengele 246 katika mkataba wa Versailles kinachosema: "Katika muda wa miezi 6 baada ya kuthebitishwa kwa mkataba huu. Ujerumani itakabidhi fuvu ya Sultani Mkwawa iliyohamishwa kutoka Afrika ya Mashariki ya Kijerumani na kupelekwa Ujerumani kwa serikali ya Mfalme wa Uingereza.

Wajerumani walikataa habari za fuvu hii na Waingereza waliamua ya kwamba ilishindikana kuikuta. Lakini baada ya vita kuu ya pili ambako Ujerumani penyewe ilivamiwa na wanajeshi wa Uingereza gavana Twining wa Tanganyika alikumbuka habari za fuvu akatembelea Ujerumani na kutazama mafuvu ya makumbusho ya Bremen.

Katika mkusanyiko wa fuvu 2000 zilikuwa 84 zenye namba zilizoonyesha zilitoka kiasili katika Afrika ya Mashariki ya Kijerumani. Hapa alizipanga kufuatana na ukubwa na kutazama zile zilizokuwa na vipimo vya karibu na ndugu za Mkwawa aliowahi kupima kabla ya safari yake. Hapa aliteua fuvu yenye shimo kwa sababu taarifa ya kale ilisema Mkwawa alijiua kwa kujipigia risasi kichwani.

Kulikuwa na uhalali gani kwa askari aliyejiua kutambulika kama "shujaa"?

ANGALIZO: Mimi Infantry Soldier sio askari jeshi wala mtumishi wa ofisi yoyote ya serikali bali ni raia mwema ninayeipenda sana Tanzania. Hili jina nilijpa tu kutokana na changamoto kadhaa nzito nilizowahi kuzipitia katika maisha yangu.

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Shujaa wa kihehe unamshusha hivyo.
Subiri Wahehe waanze kujinyonga kisa wewe
 
kwanza umeanza kwa kuharibu kudhani israel inaumaalumu wowote ,na sijui imetokeaje kwenye thread za kishujaa,anyway madini hayo yakuletewa,swala la kujiua useme siri nalielewa na mkwawa ni shujaa maana alipambana na wajerumani miaka minne (najua hujui) polini wakiwa wanamzidi technology mbali ,kukamatwa kwake yeye wangekutumia kuwavunja nguvu wahehe ya kimapinduzi maana wangeamua hata kuuburuza mwili wake kila mahali ili kuwakatisha moyo wahehe.
aidha wahehe waliendelea kuwa shida kuwatawala na hata wajerumani kadhaa waliandika kuwa watu wenye kiburi ,wavivu na hasira ,hata mashambani mwao wajerumani waliajiri wakinga na wabena sio wahehe .
Zaid ya kutoa shutuma kuhus Israel but mbona kama umebadiri tu maneno but mantiki nilioisema ni hiyo hiyo na wewe umeirudia? Binafsi naoana mi na wewe tunao mtazamo 1 wa Mkwawa kujiua ( though bado nasisitiza kwamba suala la Mkwawa kujiua is still debatable cause we are not sure ) hi hilo hilo tu
 
Hivi hatuwezi kufungua mashitaka mahakama za kimataifa kuwashitaki hawa wajerumani kwa Uvamizi na mauaji ya watanganyika? Navyojua mimi kosa haliishi kama ni kwa karne 100 utalikuta lipo palepale hata kama muhusika utakufa.

Huu ulikuwa ni uhalifu dhidi ya binadamu - RIP Mkwawa!!
 
Habari za wakati huu ndugu zangu wa humu jamiiforums.

Kulikuwa na uhalali gani wa Chief Mkwawa kutambulika kama "shujaa"? Kamwe hakuna askari anayeweza kuitwa shujaa kwa kuogopa adui kisha kujiua mwenyewe.

View attachment 1716322

Mbona Muamar Gadaffi wa Libya na Saddam Hussein wa Iraq hawakujiua kabla ya kukamatwa na wazungu? Mkwawa alikuwa shujaa ama askari muoga?

UOGA SIO SIFA NJEMA YA MWANAUME MPIGANAJI
=====
Uoga ni tabia ambayo hofu nyingi humzuia mtu kupambana na hatari au kukabiliana na adui. Uoga unaonyesha uwezo wa mtu kukosa tabia ya ujasiri wakati wa changamoto. Katika kanuni za kijeshi za nchi nyingi hapa duniani, uoga katika vita ni sawa sawa na uhalifu.

Vitendo vya uoga, kwa muda mrefu tangia vita ya kwanza ya dunia, vimeadhibiwa na sheria za kijeshi, ambazo inafafanua vema makosa yanayohesabika kama uoga, ikiwa pamoja na kumkimbia adui au kujisalimisha kwa adui pasipo kupata amri kutoka kwa wakubwa. Wale ambao walikamatwa walikuwa, mara kwa mara, wakipelekwa mahakamani na adhabu ya vitendo kama hivyo kwa kawaida huwa ni kali sana.

Siku zote ulimwengu umewaheshimu majasiri na kuwalaani waoga. Kuwa jasiri ni muhimu kwa mwanamume kama vile kuwa msafi kwa mwanamke, na muoga kati ya wanaume ana sifa mbaya kama kahaba kati ya wanawake.

Kujiua huitwa ni uoga kwa sababu inahitaji ujasiri wa hali ya juu sana ili uweze kuishi katika dunia iliyojaa kila aina ya changamoto, inahitaji mtu kuwa na mtazamo sahihi juu ya maisha na utulivu mkubwa wa akili. Pamoja na shinikizo na shida zote, vuta nikuvute za maisha ambavyo tunakabiliwa navyo, baadhi ya waoga huamua kuwa na mawazo hasi na kushindwa kupambana tena na badala yake kuchagua kufa.

KWA UFUPI SANA KUHUSU KIFO CHA CHIEF MKWAWA
=====
Kichwa cha mtemi kinasemekana kilikatwa na Wajerumani na kutumwa Berlin kilipohifadhiwa katika makumbusho, awali Berlin na baadaye Bremen. Waingereza waliochukua utawala wa koloni mwaka 1918 baada ya Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia walitaka kuonekana kama mabwana wema.

Mkuu wa serikali ya kikoloni ya Tanganyika alipendekeza kurudisha fuvu kwa sababu Wahehe walishirikiana na Waingereza wakati wa vita. Hivyo kuna kipengele 246 katika mkataba wa Versailles kinachosema: "Katika muda wa miezi 6 baada ya kuthebitishwa kwa mkataba huu. Ujerumani itakabidhi fuvu ya Sultani Mkwawa iliyohamishwa kutoka Afrika ya Mashariki ya Kijerumani na kupelekwa Ujerumani kwa serikali ya Mfalme wa Uingereza.

Wajerumani walikataa habari za fuvu hii na Waingereza waliamua ya kwamba ilishindikana kuikuta. Lakini baada ya vita kuu ya pili ambako Ujerumani penyewe ilivamiwa na wanajeshi wa Uingereza gavana Twining wa Tanganyika alikumbuka habari za fuvu akatembelea Ujerumani na kutazama mafuvu ya makumbusho ya Bremen.

Katika mkusanyiko wa fuvu 2000 zilikuwa 84 zenye namba zilizoonyesha zilitoka kiasili katika Afrika ya Mashariki ya Kijerumani. Hapa alizipanga kufuatana na ukubwa na kutazama zile zilizokuwa na vipimo vya karibu na ndugu za Mkwawa aliowahi kupima kabla ya safari yake. Hapa aliteua fuvu yenye shimo kwa sababu taarifa ya kale ilisema Mkwawa alijiua kwa kujipigia risasi kichwani.

Kulikuwa na uhalali gani kwa askari aliyejiua kutambulika kama "shujaa"?

ANGALIZO: Mimi Infantry Soldier sio askari jeshi wala mtumishi wa ofisi yoyote ya serikali bali ni raia mwema ninayeipenda sana Tanzania. Hili jina nilijpa tu kutokana na changamoto kadhaa nzito nilizowahi kuzipitia katika maisha yangu.

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
bila shaka ulieandika sio muafrika. au una weza kua sio pan Africanist au unaweza kua puppet wa mbuzi dume
 
bila shaka ulieandika sio muafrika. au una weza kua sio pan Africanist au unaweza kua puppet wa mbuzi dume
Hiyo hekima gani?? Mtu anayeuliza swali (ambalo hupendi) anahitaji ktukanwa ("puppet")???

Sikubaliani na mwanzilishaji wa tredi lakini kama hupo tayari kuheshimu wengine wanaochangia heri uondoke haraka.-
 
Shujaa ni mtu yeyote aliyewatetea watu wake walipokabiliwa na adui au janga.
Kwa mantiki hiyo kuna watu wanamuona Kinjekitile ni shujaa wao pia.
Kwanza kabla ya huu mjadala tupate maana halisi ya neno SHUJAA ili tujue kuwa tunamjadili kwa sifa zipi....??
 
Back
Top Bottom