Kulikuwa na uhalali gani kwa Chief Mkwawa kutambulika kama 'Shujaa?

Kulikuwa na uhalali gani kwa Chief Mkwawa kutambulika kama 'Shujaa?

Mungu unayemuabudu wewe, na yule aliyeabudiwa na wakoloni hakuwa mungu wa Mkwawa. Ungemuuliza Mkwawa mambo gani mungu wake anayakubali au kuyakataa ungeshangazwa sana na majibu yake.
Kujiua ni uoga wa maisha mkuu na waoga kamwe hawatauona ufalme wa Mungu. Mzalendo hajiua hata siku moja.
 
Shujaa ni mtu yeyote aliyewatetea watu wake walipokabiliwa na adui au janga.
Kwa mantiki hiyo kuna watu wanamuona Kinjekitile ni shujaa wao pia.
Kwani shujaa ni lazima awatete watu wengine? Vp kama akijitetea yeye mwenyewe, hawezi kuitwa shujaa? Samson alipambana na Simba mpaka akafanikiwa kumuua. Je, yeye sio shujaa? Can't he be declared a hero of his own sphere?
 
Mungu unayemuabudu wewe, na yule aliyeabudiwa na wakoloni hakuwa mungu wa Mkwawa. Ungemuuliza Mkwawa mambo gani mungu wake anayakubali au kuyakataa ungeshangazwa sana na majibu yake.
Umejuaje kama hakuwa Mungu wa Mkwawa. Ulimuuliza mkuu? Lini? Wapi? Muda gani? Twenda logically sasa.
 
Kwanza jiulize, why mkwawa alipigana?
Ni pride tu, kuwa yeye hawezi kutawaliwa na wazungu kamwe.
Na ngozi yake kamwe haitokuja guswa na Mzungu.
Ko kiufupi kwa hatua aliyokuwa amefikia ( aliwatandika wajerumani kwenye phase 1) ni shujaa tayari.
Na lengo lake lilitimia, mkwawa hajawahi guswa na wageni akiwa hai.
Mkwawa hakuwahi lipa kodi kwa wakoloni Bali aliitoza misafara ya vibaraka wao.
Mkwawa alijiua akiwa bado kazungukwa na askari wake wawili ( bodyguards) so hakulazimishwa ni option aliyoona inafaa kulinda Heshima yake, na heshima aliipata mpaka Leo hii mimi na wewe tunamjadili, why tusimjadili chief Mangungu
 
Mkwawa alijiua akiwa bado kazungukwa na askari wake wawili ( bodyguards) so hakulazimishwa ni option aliyoona inafaa kulinda Heshima yake, na heshima aliipata mpaka Leo hii mimi na wewe tunamjadili
Kujiua ni heshima mkuu? Vijana wanakata tamaa za maisha na kushindwa kuendelea kupambana nao unashauri wajiue ili walinde heshima zao?...
 
Kujiua kuna mambo mengi mkuu ( ingawa bado suala la Mkwawa kujiua is still debatable, hakuna mwenye uhakika ). Mimi nasoma sana hata habari za Waisrael (sasa Wayahudi ) na wenyewe mara kadhaa viongozi wao walipo elemewa walijiua; iko hivi; KIONGOZI ukitekwa, utateswa hadi useme SIRI yenu, na hilo ndilo ambalo adui hulitafuta, bora ufe na siri yako ili wengine walioachwa wapambane kivyao wakiendelea kuzishikiria codes zenu/zao
Hii pia hufanywa na wale wapiganaji shupavu wa Tamil Tigers akina Syvalassan ambao walikuwa wanatembea na vidonge vya sumu pindi wanapokamatwa hula kidonge ili waepuke kushurutishwa kutoa siri.
 
Habari za wakati huu ndugu zangu wa humu jamiiforums.

Kulikuwa na uhalali gani wa Chief Mkwawa kutambulika kama "shujaa"? Kamwe hakuna askari anayeweza kuitwa shujaa kwa kuogopa adui kisha kujiua mwenyewe.

View attachment 1716322

Mbona Muamar Gadaffi wa Libya na Saddam Hussein wa Iraq hawakujiua kabla ya kukamatwa na wazungu? Mkwawa alikuwa shujaa ama askari muoga?

UOGA SIO SIFA NJEMA YA MWANAUME MPIGANAJI
=====
Uoga ni tabia ambayo hofu nyingi humzuia mtu kupambana na hatari au kukabiliana na adui. Uoga unaonyesha uwezo wa mtu kukosa tabia ya ujasiri wakati wa changamoto. Katika kanuni za kijeshi za nchi nyingi hapa duniani, uoga katika vita ni sawa sawa na uhalifu.

Vitendo vya uoga, kwa muda mrefu tangia vita ya kwanza ya dunia, vimeadhibiwa na sheria za kijeshi, ambazo inafafanua vema makosa yanayohesabika kama uoga, ikiwa pamoja na kumkimbia adui au kujisalimisha kwa adui pasipo kupata amri kutoka kwa wakubwa. Wale ambao walikamatwa walikuwa, mara kwa mara, wakipelekwa mahakamani na adhabu ya vitendo kama hivyo kwa kawaida huwa ni kali sana.

Siku zote ulimwengu umewaheshimu majasiri na kuwalaani waoga. Kuwa jasiri ni muhimu kwa mwanamume kama vile kuwa msafi kwa mwanamke, na muoga kati ya wanaume ana sifa mbaya kama kahaba kati ya wanawake.

Kujiua huitwa ni uoga kwa sababu inahitaji ujasiri wa hali ya juu sana ili uweze kuishi katika dunia iliyojaa kila aina ya changamoto, inahitaji mtu kuwa na mtazamo sahihi juu ya maisha na utulivu mkubwa wa akili. Pamoja na shinikizo na shida zote, vuta nikuvute za maisha ambavyo tunakabiliwa navyo, baadhi ya waoga huamua kuwa na mawazo hasi na kushindwa kupambana tena na badala yake kuchagua kufa.

KWA UFUPI SANA KUHUSU KIFO CHA CHIEF MKWAWA
=====
Kichwa cha mtemi kinasemekana kilikatwa na Wajerumani na kutumwa Berlin kilipohifadhiwa katika makumbusho, awali Berlin na baadaye Bremen. Waingereza waliochukua utawala wa koloni mwaka 1918 baada ya Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia walitaka kuonekana kama mabwana wema.

Mkuu wa serikali ya kikoloni ya Tanganyika alipendekeza kurudisha fuvu kwa sababu Wahehe walishirikiana na Waingereza wakati wa vita. Hivyo kuna kipengele 246 katika mkataba wa Versailles kinachosema: "Katika muda wa miezi 6 baada ya kuthebitishwa kwa mkataba huu. Ujerumani itakabidhi fuvu ya Sultani Mkwawa iliyohamishwa kutoka Afrika ya Mashariki ya Kijerumani na kupelekwa Ujerumani kwa serikali ya Mfalme wa Uingereza.

Wajerumani walikataa habari za fuvu hii na Waingereza waliamua ya kwamba ilishindikana kuikuta. Lakini baada ya vita kuu ya pili ambako Ujerumani penyewe ilivamiwa na wanajeshi wa Uingereza gavana Twining wa Tanganyika alikumbuka habari za fuvu akatembelea Ujerumani na kutazama mafuvu ya makumbusho ya Bremen.

Katika mkusanyiko wa fuvu 2000 zilikuwa 84 zenye namba zilizoonyesha zilitoka kiasili katika Afrika ya Mashariki ya Kijerumani. Hapa alizipanga kufuatana na ukubwa na kutazama zile zilizokuwa na vipimo vya karibu na ndugu za Mkwawa aliowahi kupima kabla ya safari yake. Hapa aliteua fuvu yenye shimo kwa sababu taarifa ya kale ilisema Mkwawa alijiua kwa kujipigia risasi kichwani.

Kulikuwa na uhalali gani kwa askari aliyejiua kutambulika kama "shujaa"?

ANGALIZO: Mimi Infantry Soldier sio askari jeshi wala mtumishi wa ofisi yoyote ya serikali bali ni raia mwema ninayeipenda sana Tanzania. Hili jina nilijpa tu kutokana na changamoto kadhaa nzito nilizowahi kuzipitia katika maisha yangu.

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
alipata matatizo ya akili mwishoni, akawa na paranoia, akahisi mtu yoyote anaweza kumsaliti. uwezo alikua nao mkubwa sana, historia uliyonayo wewe ni ndogo sana, fuatilizia zaidi
 
Habari za wakati huu ndugu zangu wa humu jamiiforums.

Kulikuwa na uhalali gani wa Chief Mkwawa kutambulika kama "shujaa"? Kamwe hakuna askari anayeweza kuitwa shujaa kwa kuogopa adui kisha kujiua mwenyewe.

View attachment 1716322

Mbona Muamar Gadaffi wa Libya na Saddam Hussein wa Iraq hawakujiua kabla ya kukamatwa na wazungu? Mkwawa alikuwa shujaa ama askari muoga?

UOGA SIO SIFA NJEMA YA MWANAUME MPIGANAJI
=====
Uoga ni tabia ambayo hofu nyingi humzuia mtu kupambana na hatari au kukabiliana na adui. Uoga unaonyesha uwezo wa mtu kukosa tabia ya ujasiri wakati wa changamoto. Katika kanuni za kijeshi za nchi nyingi hapa duniani, uoga katika vita ni sawa sawa na uhalifu.

Vitendo vya uoga, kwa muda mrefu tangia vita ya kwanza ya dunia, vimeadhibiwa na sheria za kijeshi, ambazo inafafanua vema makosa yanayohesabika kama uoga, ikiwa pamoja na kumkimbia adui au kujisalimisha kwa adui pasipo kupata amri kutoka kwa wakubwa. Wale ambao walikamatwa walikuwa, mara kwa mara, wakipelekwa mahakamani na adhabu ya vitendo kama hivyo kwa kawaida huwa ni kali sana.

Siku zote ulimwengu umewaheshimu majasiri na kuwalaani waoga. Kuwa jasiri ni muhimu kwa mwanamume kama vile kuwa msafi kwa mwanamke, na muoga kati ya wanaume ana sifa mbaya kama kahaba kati ya wanawake.

Kujiua huitwa ni uoga kwa sababu inahitaji ujasiri wa hali ya juu sana ili uweze kuishi katika dunia iliyojaa kila aina ya changamoto, inahitaji mtu kuwa na mtazamo sahihi juu ya maisha na utulivu mkubwa wa akili. Pamoja na shinikizo na shida zote, vuta nikuvute za maisha ambavyo tunakabiliwa navyo, baadhi ya waoga huamua kuwa na mawazo hasi na kushindwa kupambana tena na badala yake kuchagua kufa.

KWA UFUPI SANA KUHUSU KIFO CHA CHIEF MKWAWA
=====
Kichwa cha mtemi kinasemekana kilikatwa na Wajerumani na kutumwa Berlin kilipohifadhiwa katika makumbusho, awali Berlin na baadaye Bremen. Waingereza waliochukua utawala wa koloni mwaka 1918 baada ya Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia walitaka kuonekana kama mabwana wema.

Mkuu wa serikali ya kikoloni ya Tanganyika alipendekeza kurudisha fuvu kwa sababu Wahehe walishirikiana na Waingereza wakati wa vita. Hivyo kuna kipengele 246 katika mkataba wa Versailles kinachosema: "Katika muda wa miezi 6 baada ya kuthebitishwa kwa mkataba huu. Ujerumani itakabidhi fuvu ya Sultani Mkwawa iliyohamishwa kutoka Afrika ya Mashariki ya Kijerumani na kupelekwa Ujerumani kwa serikali ya Mfalme wa Uingereza.

Wajerumani walikataa habari za fuvu hii na Waingereza waliamua ya kwamba ilishindikana kuikuta. Lakini baada ya vita kuu ya pili ambako Ujerumani penyewe ilivamiwa na wanajeshi wa Uingereza gavana Twining wa Tanganyika alikumbuka habari za fuvu akatembelea Ujerumani na kutazama mafuvu ya makumbusho ya Bremen.

Katika mkusanyiko wa fuvu 2000 zilikuwa 84 zenye namba zilizoonyesha zilitoka kiasili katika Afrika ya Mashariki ya Kijerumani. Hapa alizipanga kufuatana na ukubwa na kutazama zile zilizokuwa na vipimo vya karibu na ndugu za Mkwawa aliowahi kupima kabla ya safari yake. Hapa aliteua fuvu yenye shimo kwa sababu taarifa ya kale ilisema Mkwawa alijiua kwa kujipigia risasi kichwani.

Kulikuwa na uhalali gani kwa askari aliyejiua kutambulika kama "shujaa"?

ANGALIZO: Mimi Infantry Soldier sio askari jeshi wala mtumishi wa ofisi yoyote ya serikali bali ni raia mwema ninayeipenda sana Tanzania. Hili jina nilijpa tu kutokana na changamoto kadhaa nzito nilizowahi kuzipitia katika maisha yangu.

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
mkuu hebu tutolee mfano shujaa kwako ni nani?
 
Maswali yako mepesi sana.
Kwani shujaa ni lazima awatete watu wengine? Vp kama akijitetea yeye mwenyewe, hawezi kuitwa shujaa? Samson alipambana na Simba mpaka akafanikiwa kumuua. Je, yeye sio shujaa? Can't he be declared a hero of his own sphere?
 
Ushujaa wa Mkwawa hatuuangilii kwenye kifo chake angalia alivyowatoa jasho la sehemu za siri alimaarufu kama '' kantyentye ( Lufufu ) wajerumani kwa mfumo ule wa vita ya kuvizia ni dhahili alikua shujaa ila we Infantry Soldier we mjeda bhana
 
Huu ni muktadha tofauti, muktadha wa Vita mkuu.
Ni kawaida kwa warriors na wapambanaji kujiua kwa sababu wanazozijua wao na kwao hii ni heshima kubwa.
Mkuu, hivi unajua ya kuwa maisha pia ni vita na changamoto zake ndio adui yetu?
 
Back
Top Bottom