Kumbe Tanzania ilikopa fedha World Bank kuendeleza bandari, DP World anakuja kutumia fedha hizo kufanya kazi ambayo Tanzania imeikopea fedha WB-SOMA

Kumbe Tanzania ilikopa fedha World Bank kuendeleza bandari, DP World anakuja kutumia fedha hizo kufanya kazi ambayo Tanzania imeikopea fedha WB-SOMA

Kwa hiyo kwenye haya, huyu muwekezaji atacontribute kitu gani?

Anaenda kuboresha sehemu inayotumiwa na abiria na sehemu ya majahazi.

Atawekeza kwenye crane za kisasa kuanzia berth 1 to 7 kila berth.

Anaenda kuboresha miundombinu ya njia za kuingia bandarini kuongeza inflow and outflow of shipments za port. Na Dry port za kurasini na kwala.

Ana kwenda kugharamia uamishaji wa Ro-Ro yard ilipo sasa na kuipeleka sehemu nyingine ambapo atajenga multi storey car park ya kuhifadhia magari. Na hiyo sehemu iliyokuwa RoRo yard ya sasa ataigeuza kuwa container port itakayoweza weka container nyingi zaidi.

Anakwenda kuwekeza kwenye ICT system ambayo wahusika wote wa bandari watakuwa na access nayo kupata information za mizigo yao, wateja, clearing agencies na serikali.

Anakwenda ku introduce mifumo ya kuendesha bandari ambayo inamfanya mteja mfalme kama ilivyo duniani kwengine.

In return atapewa maeneo aya-manage na ayaendeshe mwenyewe kurudisha hela. Na maeneo mengine kusaidiana na TPA ku-manage wakati operation zitafanywa na TPA wenyewe watakavyokubaliana.

Akimaliza kuimarisha hapo yupo tayari kwa kuongozwa na TPA kufanya phase 2 kuimarisha lake ports ili mizigo ya nchi jirani iende upande wa pili kwa ufanisi zaidi logistically from Dar port.

Huo uwekezaji ni game changer
 
Kwanini bandari wakati mengi yapo tofauti mangapi yameshindikana halafu kimya. Tatizo hata hao walio beba zamana wanakwenda na yakwao na wala siyo ya wananchi, bado taabu ipo palegale.
 
Volume isipoongezeka? Tumkamate nani?
Kama wana akili timamu kutakuwa na kipengele cha kupimana na kutokumuongezea muda akishindwa.

Hila kwenye nchi ambayo meli zina subiri kutia nanga majini kwa siku kadhaa kisa uwezo mdogo wa kushusha mizigo; sioni ufanisi ukiongezeka na mizigo isiongezeke jumlisha na nchi zinazotumia hiyo bandari na zenyewe zinakuwa kiuchumi.

Dar port ni cash cow which hasn’t been utilised efficiently it’s time ya kuita watu wenye uzoefu wa kimataifa tena kwenye busiest ports duniani kama Rotterdam, Antwerp, Sharjah na Southampton; DP world wapo kote huko.
 
Kwahiyo tukusikilize Wewe tuachane na waziri wa fedha na hizo taasisi?
Wizara ya fedha waliwaita credit agency kuja kuwafanyia tathmini ya kukopa wamepata B1+ hizo sifa wanazopewa ni sawa na kutoka F10% na baada ya tathmini ukapewa F20% bado sana kufikia ata pass mark ya chini C40%.

Ndio wanachojisifia wana F ya afadhali ila ni junk credit, nenda kwenye website zao wanaelezea what each credit rating means from AAA to the bottom. B rating ni junk .
 
View attachment 2676204

Kwa kuanzia tu bandarini kuna multi storage car park?

Kingine wanampago wa kuamisha Ro-Ro kutoka hapo ilipo.

Wana mpango wa kuboresha terminal ya abiria na majahazi.

Wana mpango wa kuongeza uwekezaji kurasini kuweka kupokea mizigo mingi inayokwenda nje ya nchi.

Wana mpango wa kuweka ICT system inayoweza track mzigo unapoingia melini kokote duniani mpaka unatoka ata wewe mteja unaweza jua mzigo wako ulipo.

Mambo yote yameelezwa hapo phase 1 wao watafanya nini.
Maria anasema haya yote yanafanywa na mkopo wa World Bank
 
duniani Rotterdam, Antwerp, Sharjah na Southampton ni amongst the busiest ports duniani na DP world wapo kote huko.
Huko Antwerp, Southampton, na Rotterdam , wazungu walioingia mkataba na waarabu kwa mkataba sawa sawa na kama huu tunaohimiza urekebishwe?
 
Sijui kwa nini watu hawaoni umhimu na ufanis wa DPW na hawasemi tatizo ni nini wako too general.
Lakini mkuu,kila mwenye kupinga mkataba huo kaweka na vipengele anavyovipinga,wanasema uwekezaji hata wa hao dp si tatizo,tatizo wameliona kwenye huo mkataba mnaouita makubaliano,na wameviainisha kabisa,sasa nyie mnaoutetea mungefanya kama walivyofanya hao wanaoupinga mungetupq imani kubwa kwa mradi huo,ila hamjafanya chochote ktuaminisha sisi wananchi ubora wa uwekezaji huo ni upi,ona, kila siku wenzenu wanakuja na hoja mpya zenye references,nyie mnaishia kuwapinga wanaopinga badala ya kutuambia ubora wa mkataba huo kwa ushahidi kama wanavyofanya wenzenu,hadi hapa sisi wananchi common tunalazmika kuwaamini hawa wenye kupinga kwa ushahidi,wanasema mmelipwa kuutetea,na tunalazimika kuamini hivyo.
 
Huko Antwerp, Southampton, na Rotterdam , wazungu walioingia mkataba na waarabu kwa mkataba sawa sawa na kama huu tunaohimiza urekebishwe?
Sharjah ni kama nyumbani kwao ipo UAE

Huko Antwerp, Rotterdam na Southampton kila sehemu watakuwa na mikataba tofauti.

Mfano Southampton wana operation contract ya container terminal, wameingia mkataba tena na operator mwingine humo humo ndani ya kuwafanyia services machines zao, bado wana contract ya security ya port nzima.

Sio mambo ya kukariri kila nchi watakuwa na mikataba yao, maswali mengine kuyajibu yanataka research ya kutosha wana mikataba gani kila sehemu.

Tanzania watakuwa na mkataba wa development sehemu zilizotajwa tu kwenye appendix 1 (na term zenyewe bado awajakubaliana na TPA) si ajabu wakashindwana huko mbele kufikia muafaka.

Kwa hivyo kusema watakuwa na mkataba kama wetu wakati aupo bado ni upotoshaji.

Kilichopo kwa sasa ni framework ya kuingia mkataba lakini hakuna mkataba wowote wa utekelezaji ambao wameshakubaliana mpaka sasa katika maeneo ya ushirikiano yaliyo orodheshwa.
 
Kwani mkataba wa Dp world na Tpa tayari? Mbona mnaendekeza Cheap Politics hivi?

Dp world vifaa vyao sio vya kitoto eti waje watumie Existing infrastructure, Hizo Crane na miundombinu mingine capability yake wanayo wao tu ama ni kampuni chache zenye uwezo huo.

Kusema kwamba Dp world wanatutegemea sisi eti mkopo wetu wa World Bank uwawezeshe wao ni chai ya mchana.
Nonsense. Hata huelewi kilichoandikwa unaumia roho tu kwa hisia za wakwetu.
 
Huo ndo ukweli na tatizo ni lipi waseme bayana siyo kuwa too general na kupotosha umma. Kama mtu hana capacity ya kuchambua hili bora kukaa kimya.
Tulishashindwa miaka kibao mpaka KAGAME alitucheka tukamjibu kwa kuwatimua Raia wa nchi yake.
Ulishindwa wewe?au serikali hii hii? Serikali iliyoshindwa kufanya,iliyoshindwa kupanga,na ikashindwa kuamua leo tuisifie kwa kufanya maamuzi yenye kutia shaka? Eti kwa sababu inafanya kitu lichoshindwa kukifanya vyema?tunaaminje kuwa this time wanafanya kwa ufanisi? Tena huko nyuma serikali ili "die trying" this time ni kama ime give up,think big
 
Timeframe ya mktaba
Hiyo itatokana na kukaa chini kupigiana hesabu how much it will cost to invest in those areas.

Kufanya estimation on volumes za mizigo itayoongezeka, estimate ya mapato na kuamua jinsi ya kumrudishia hela yake.

Wanaweza sema achukue mapato yote kila mwaka arudishe hela yake haraka wachukue Port based on anticipated future income, wanaweza sema achukue kiasi kadhaa iwe ni finance cost kwenye mkataba, halafu faida wagawane 50-50 mpaka hela yake itakapo rudi na kwa utaratibu huo watalipa corporate tax.

Kwa kifupi mimi na wewe atujui what consideration watakazokubaliana huko; ila kama wana akili timamu watu kama kina Kakoko wanatakiwa kuwa kwenye team ya majadiliano. Wakimuweka yule mkurugenzi wa TPA tuandike maumivu pale hamna kitu kuna brazaman.

Ni hivi development zinazo kusudiwa kwa ujumala wake both phase 1 and 2 strategically zina tija sana kwa taifa. Sasa tena terms watakazoenda ingia TPA huko mbeleni sote atujui na busara kila mtu ashike rozali yake au tasbir na kuomba mungu wasiingie makubaliano ya ovyo huko mbele kwenye ‘project agreements’.
 
Back
Top Bottom