Kumbe Tanzania ilikopa fedha World Bank kuendeleza bandari, DP World anakuja kutumia fedha hizo kufanya kazi ambayo Tanzania imeikopea fedha WB-SOMA

Kumbe Tanzania ilikopa fedha World Bank kuendeleza bandari, DP World anakuja kutumia fedha hizo kufanya kazi ambayo Tanzania imeikopea fedha WB-SOMA

Badala ya kutafuta makala ya bandari ya Dar na kumsikiliza mkurugenzi wa port.

Yote hayo keshayaongelea issue ni cranes za kisasa ambazo hazitoshi.

Pili wawekezaji wameelezea wanachoenda kuongezea wao hapo bandarini.

Wewe unatoka kwenda kumsikiliza kichaa mmoja Twitter ndio source yako; badala ya kuwasikiliza wahusika tena video wameonyesha ya kilichofanyika bandarini.
Huyo mkurugenzi wa bandari kaongea maneno na fikra zake tu, lakini mengi aliyoongea hayako popote kwenye mkataba, hivyo muwekezaji hafungwi popote kuyatekeleza.

Jiulize haya yote aliyosema mkurugenzi wa bandari.
Je, yanahitaji kwa lazima muwekeza binafsi ili kuyatekeleza?
Je, serikali haiwezi kuyatekeleza?
Je, yanahitaji mkataba wa milele kutekelezwa?
Je, yanahitaji muwekezaji kupewa bandari zingine zote ili yatekelezwe?
 
Nimekwambia uelewa wako umekomea hapo... sasa DP world anakuja kuwekeza nini? Unajua maana ya kuwekeza?
Kwa hiyo ni wewe tu hapa Tanzania ndo unaejua physical meaning ya kuwekeza? mfano sema specific kwenye huo mkataba tatizo ni nini? na je kwenye mataifa yote DPW walikowekeza nao hawajui maana ya uwekezaji?
 
Umeambiwa report za World Bank na CAG. Tulipewa fedha $21M kwaajili ya mifumo na DP World ndio wametajwa watekelezaji! Jamani hapa hatufanyi siasa! This is very serious National matters. Binafsi sijasoma hizo report lakini kwa credibility ya Maria hawezi kusema jambo linalogusa taasisi nyeti bila ushahidi.

Inaogopesha sana!
Mkuu Ina maana $21 Million ndio mtaji wa kuendesha bandari ya Dar es salaam?

Then alichopost Maria ni consultancy services za DP world kuandaa mfumo na sio kuendesha bandari. Ni mambo mawili tofauti kabisa
 
Hayo yote ya nini jambo muhimu ni ufanisi ili serikali iongeze mapato kupitia bandari........na hilo Dp world ndo imekuja kutekeleza basi, hata kama mkataba ni wa miaka 100 as long serikali ina pata faida na inahudumia wananchi wake vizuri na kufanya maendelo hamna shida tuache fitina za kijinga.
Wewe ni uchafu. Yaani wewe ni takataka
 
Hii ni kutoka report ya Worl Bank .................................BY MARIA SARUNGI

Muhimu kuhusu DPW na mradi wa Benki ya Dunia

Pesa za mkopo wa @WorldBankAfrica zimetumika (na kukamilika)
👉🏽 kupanua na kuimarisha Gati 1-7 na kujenga gati mpya Gerezani
👉🏽kupanua mlango wa bandari hadi Gati 11
👉🏽kuboresha na kuunganisha na reli
👉🏽 Kupanua na kuimarisha Gati 8-11
👉🏽Kuna RORO terminal ilijengwa na kukamilishwa

Sasa tuangalie wanachodai DP World kufanya kwa mujibu wa IGA
Cha kwanza kikubwa eti kujenga, kuendesha na kusimamia RoRo terminal na Gati 1-4 na gati 5-7
🙄
Yaani pesa zote zimewekezwa za walipa kodi kupitia mradi wa sasa wa WB alafu wao wanakuja kuendesha na kusimamia? Wanawekeza nini??

Ndiyo maana mkataba haujawekwa thamani ya uwekezaji wao 😄 kumbe wanadandia mradi unaoelekea kukamilika waje wajisifu!

YAANI KIUFUPI WANAKUJA KUTEKELEZA MRADI WA PESA ZA MKOPO WA WORLD BANK

Nyieeeeeeeeee!
Mnaotetea mkataba huu mnajua kuwa mnatumika kutetea ulaji wa genge ndogo!?
Ila #TutaelewanaTu
Source vipi ?
 
Kwa hiyo ni wewe tu hapa Tanzania ndo unaejua physical meaning ya kuwekeza? mfano sema specific kwenye huo mkataba tatizo ni nini? na je kwenye mataifa yote DPW walikowekeza nao hawajui maana ya uwekezaji?
Yaani mpaka leo hujui kwenye mkataba kuna tatizo gani!!? Wewe ulitakiwa uwe milembe
 
Hayo yote ya nini jambo muhimu ni ufanisi ili serikali iongeze mapato kupitia bandari........na hilo Dp world ndo imekuja kutekeleza basi, hata kama mkataba ni wa miaka 100 as long serikali ina pata faida na inahudumia wananchi wake vizuri na kufanya maendelo hamna shida tuache fitina za kijinga.
Basi serikali iseme inakodi kampuni ya kusimamia uendeshaji wa bandari kama vile Mkapa alivyowaleta Net group Solution waendeshe TANESCO na isiseme inaleta wawekezaji. Maana hakuna wanachokuja kuwekeza
 
Wewe ni uchafu. Yaani wewe ni takataka
Leta hoja leta ujinga bandari imeka miaka mingapi hatuna faida nao wakati serikali inahitaji pesa kununua dawa, na kutoa huduma kwa wana nchi
 
..badala ya kununua ma-V8 serikali ikajenge hiyo multi storage car park.

..tukiwaruhusu Dp wajenge hiki au kile iko siku watakuja kutuliza.
Serikali kulipa madeni yake shida, kutoa huduma shida za jamii inajikwamua. Ikawekeze tena bandarini wakati kuna mtu yupo tayari. Ambae kwanza anaweka hela yake, analipia kodi ya eneo bandari, anagawana mapato yake na TPA, na anaongeza volumes za mizigo TRA ipate kodi zaidi kwenye forodha.

Na akisharudisha hela yake na kutupa uzoefu maeneo yenyewe aliyopewa anawarudishia TPA; unataka nini tena kama ndio serikali.

Issue hapo ni kuingia mikataba mizuri ya utekelezaji; lakini IGA aina shida yoyote.
 
Basi serikali iseme inakodi kampuni ya kusimamia uendeshaji wa bandari kama vile Mkapa alivyowaleta Net group Solution waendeshe TANESCO na isiseme inaleta wawekezaji. Maana hakuna wanachokuja kuwekeza
Hapana hao DP world wana kuja na mitambo yao pamoja na technology yao wana fanya oparation mantainance and investment manaake wata panua bandari iwe kubwa zaidi
 
Let us agree to disagree, usinilazimishe niamini unacho amini, hoja yangu ni kwa DP world itaongeza ufanisi na mapato serikalini yataongezeka.......sisi wabongo tumeshindwa kuendesha bandari kwa mda mrefu
Hivi hao wanaoendesha bandari wanapatikana kwa utaratibu gani?!

Sikubaliani na wewe kuwa Watanzania tumeshindwa kuendesha bandari. Labda ujisemee wewe mwenyewe lakini si ku- generalize.
 
Huyo mkurugenzi wa bandari kaongea maneno na fikra zake tu, lakini mengi aliyoongea hayako popote kwenye mkataba, hivyo muwekezaji hafungwi popote kuyatekeleza.

Jiulize haya yote aliyosema mkurugenzi wa bandari.
Je, yanahitaji kwa lazima muwekeza binafsi ili kuyatekeleza?
Je, serikali haiwezi kuyatekeleza?
Je, yanahitaji mkataba wa milele kutekelezwa?
Je, yanahitaji muwekezaji kupewa bandari zingine zote ili yatekelezwe?
Mtu ambae kazi yake ni kusimamia uendeshwaji wa bandari ya Dar na amekuonyesha kilichofanyika.

Mtu ambae atakuwa kwenye team ya concession agreement itakayoamua muda wa mikataba na share of revenue ya sehemu watakazowapa DPW.

Wewe unajua kushinda huyo mtu kisa Maria Sarungi amekwambia; wow just amazing.
 
Hayo yote ya nini jambo muhimu ni ufanisi ili serikali iongeze mapato kupitia bandari........na hilo Dp world ndo imekuja kutekeleza basi, hata kama mkataba ni wa miaka 100 as long serikali ina pata faida na inahudumia wananchi wake vizuri na kufanya maendelo hamna shida tuache fitina za kijinga.
Fikra ndogo sana!!

Kama ndiyo hivyo, basi tuwaulize Waingereza na Wajerumani kama wanaweza kurudi na kutufanya koloni lao, halafu wakatupatia maendeleo. Kama wakisema wanaweza, basi tubakie koloni lao milele. Tuingie nao mkataba usio na mwisho, maana tunachotaka ni wananchi wetu tu wapate huduma bora. Unalipnaje hilo bwana Covax?
 
Serikali kulipa madeni yake shida, kutoa huduma shida za jamii inajikwamua. Ikawekeze tena bandarini wakati kuna mtu yupo tayari. Ambae kwanza anaweka hela yake, analipia kodi ya eneo bandari, anagawana mapato yake na TPA, na anaongeza volumes za mizigo TRA ipate kodi zaidi kwenye forodha.

Na akisharudisha hela yake na kutupa uzoefu maeneo yenyewe aliyopewa anawarudishia TPA; unataka nini tena kama ndio serikali.

Issue hapo ni kuingia mikataba mizuri ya utekelezaji; lakini IGA aina shida yoyote.

..una mawazo mazuri sana.

..sasa labda ungetupa na mifano ya nchi ambazo Dp imefanya hayo uliyoeleza.

..ni nchi gani Dp waliwekeza, wakaendesha bandari, halafu wakarudisha thamani ya uwekezaji wao, na mwisho wakakabidhi bandari kwa nchi husika?

..Na sio lazima iwe Dp. Unaweza kutupa mfano wa nchi nyingine yoyote ambako hayo mema unayodai tutatafanyiwa na Dp yamefanyika?

..Kama suala la kuongeza UFANISI wa bandari yetu ushauri mzuri ni Dp kuwa management company na sio wamiliki na wajenzi wa miundombinu hapo bandarini.
 
Hayo yote ya nini jambo muhimu ni ufanisi ili serikali iongeze mapato kupitia bandari........na hilo Dp world ndo imekuja kutekeleza basi, hata kama mkataba ni wa miaka 100 as long serikali ina pata faida na inahudumia wananchi wake vizuri na kufanya maendelo hamna shida tuache fitina za kijinga.

kama ni ufanisi basi hata serikali yenyewe ibinafsishwe maana imeshindwa kuuleta huo ufanisi na yenyewe pia sio fanisi.
 
Hii ni kutoka report ya Worl Bank .................................BY MARIA SARUNGI

Muhimu kuhusu DPW na mradi wa Benki ya Dunia

Pesa za mkopo wa @WorldBankAfrica zimetumika (na kukamilika)
👉🏽 kupanua na kuimarisha Gati 1-7 na kujenga gati mpya Gerezani
👉🏽kupanua mlango wa bandari hadi Gati 11
👉🏽kuboresha na kuunganisha na reli
👉🏽 Kupanua na kuimarisha Gati 8-11
👉🏽Kuna RORO terminal ilijengwa na kukamilishwa

Sasa tuangalie wanachodai DP World kufanya kwa mujibu wa IGA
Cha kwanza kikubwa eti kujenga, kuendesha na kusimamia RoRo terminal na Gati 1-4 na gati 5-7
🙄
Yaani pesa zote zimewekezwa za walipa kodi kupitia mradi wa sasa wa WB alafu wao wanakuja kuendesha na kusimamia? Wanawekeza nini??

Ndiyo maana mkataba haujawekwa thamani ya uwekezaji wao 😄 kumbe wanadandia mradi unaoelekea kukamilika waje wajisifu!

YAANI KIUFUPI WANAKUJA KUTEKELEZA MRADI WA PESA ZA MKOPO WA WORLD BANK

Nyieeeeeeeeee!
Mnaotetea mkataba huu mnajua kuwa mnatumika kutetea ulaji wa genge ndogo!?
Ila #TutaelewanaTu


Kwani kitu mbaya hapo ni nini hao jamaa wa DP world wakipewa kuwekeza au kuisimamia Bandari yetu kwa mujibu wa Sheria?
Mbaya iko upande gani nami nipate kuelewa
 
Back
Top Bottom