Jamani hali ni mbaya sana, watu wanajua kuhesabu lakini kusoma na kuandika ni utapia kichwa, utapia ujinga unaangamiza taifa nyakati za sasa katika uga wa mawasiliano kwa njia ya maandishi, sms, chats etc.
Mungu aingilie kati hili anguko, naogopa sana tuko tuendako.
Ni hayo tu.
Wadiz
Mimi mwenyewe naona limekuwa tatizo kubwa sana..
Ntaanza kukurekebisha wewe kwanza
Utapia ujinga -Ninaamini kabisa lengo lako lilikuwa kuandika watu waliozidi ujinga yaani utapia akili..
utapia maana yake ni ukosefu wa ubora wa kitu kwa mfano utapia mlo ni ukosefu wa mlo bora ..
Hivyo basi ukisema
utapia ujinga maana yake ni ukosefu wa ujinga maana mtu huyo atakuwa na akili sana
Nyakati za sasa tumia tu neno wakati wa sasa nyakati huweza kumaanisha miaka mingi sana kama generation au enzi kwa english tungesema (era) na kwa maelezo yako umesema shida imeanza siku za hivi karibuni kwa hiyo neno zuri ni wakati wa sasa
Naogopa sana tuko-Nina
hakika ulitaka kusema huko...
Hoja yako!
Swala la kwanza
hoja yako ina mashiko na Pana sana ila ilipaswa kuangalia Swala moja kubwa ambalo ni swala la lahaja..
Tanganyika na nchi ya East Africa (Kipindi cha ukoloni) kwa pamoja ilipata azimio na Kwa pamoja Walikubaliana kutumia Lahaja ya Kiunguja kama lahaja ya kiswahili Sanifu...
Lakini hii haikuwa kifo cha lahaja zingine kama kihadimu(Kimakunduchi) , kimrina (Inayopatikana pangani), kimgao,kipate ,kingozi kibajuni,kipemba,kivumba (Tanga) ,kimtangang'ata (Tanga) ,Kingazija na etc..
Ambazo nazo kwa ongezeko la watu hao zinakua kwa kasi hivyo kudhibiti matumizi ya lahaja zingine inabidi liwekwe azimio jingine la chaguzi ya lahaja kimaandishi na kimisemo...
Swala la pili
kiufupi ni kwamba kipofu hawezi kumuongoza kipofu mwenzake na wote wakawa sawa ni Vyema aongozwe na wale Wanaoweza kuona...
Miongoni mwa lahja mbovu kimaumbo na kimatamshi zinatoka Tanzania Bara..
Huku lahaja bora zikitoka pwani na Visiwani kwa mujibu huo ni wazi sasa Sifa mojawapo ya walimu kufundisha kiswahili isiwe ufaulu wa kukariri ila iwe ni Mmoja atokaye katika moja ya lahaja bora ikiwemo Kiunguja na kimakunduchi ili kuokoa taifa hili...
Maana yake Wale wote wenye lahaja hizi wahimizwe kufundisha kiswahili kuliko Kumkuta mwalimu wa kiswahili ni Msukuma au Mkurwa lazma kiswahili cha wanafunzi kiharibike ...
Asanteni