Kuna baadhi ya Vijana wa Chuo ni wajinga sana

Kuna baadhi ya Vijana wa Chuo ni wajinga sana

Ukiwa msomi hutakiwi kuogopa kusikiliza watu popote. Msomi unatakiwa usikilize halafu ndio utumie usomi wako kujuwa upungufu wa ulicho ambiwa. Pia unatumia usomi kukubaliana au kukataa baada ya kusikiliza. Sasa wewe unataka wasomi wasikilize tu watu wanao fanana na mwalimu wao?
Upo sawa mkuu. Kutapeliwa it has nothing to do with intellect mindset Ni akili binafsi isiyofunzwa darasani , inatokana tu na uzoefu wa matukio ya nyuma.

Ndiyo maana katika mazingira ya chuo huwezi kwenda Kwa mwanafunzi moja Kwa moja that's why kuna uongozi.

Ili kuonesha kwamba wewe Ni mtu halali na unachokigawa Hakina madhara Hasi Kwa mpokeaji.

Unanisimamisha na PC zako, najuaje kama haunibebeshi mabomu nikajitoe muhanga? What if upo kwenye mission ya kuua watu?

Ndomaana hizo checks lazima zifanyike na uongozi then mtoa mada angepewa mtu akaambatana naye ambaye Ni rahisi wanafunzi kumfahamu.

Chuo sio Bar nahisi mtoa mada alihisi anatembezea nguo za mitumba Bar watu wapo wanapata mvinyo.
 
Kuhusu vijana wa chuo upo sahihi Wao huwaza haya mambo

@ simba
@ Yanga
@ Ngono

Ila kuhusu PC ..... Na dharau I'm not sure
 
Hongera na pole kwa changamoto ila ungeanzia ofisi ya dean kule wangekupa majina ya wanaofaa kunufaika na huo msaada
 
Soma wewe hata ukiwa mkulima Tanzania wakulima wakubwa wa estates mashamba makubwa sana wamesoma na ulaya na marekani ndio usiseme.Kuna maprofessor wakulima wako vizuri kichwani

Kuwa mkulima sio excuse ya kutosoma sana au kuwa na digrii kibao za kilimo au ufugaji
Mkuu mimi kadigrii haka nilikonako kananitosha,hivi sasa natafuta pesa zije zinisaidie uzeeni!
 
Niajiri mie niwe nasimamaia hayo mashamba, yako Ruvuma wilaya ipi? Songea? Mbinga? Tunduru? Namtumbo au Nyasa?
Mkuu wewe niwa mjini,hiyo kazi inatuhusu sisi watoto wa mbwa tusiochagua kazi!
 
Sawa Endelea kuwa chawa wa Msweden.

Pia Boston Ni state ya Bonyokwa au?

Umesahau kutuambia alikulipa Nini kumfanyia hiyo Kazi ya kusimamisha watu ovyo kama kichaa?


Tafuta Kazi ya kudumu, uchawa sio Dili
Uchawa unalipa mkuu,huoni chawa mwijaku anakuzidi kila kitu!

Ambacho napenda kukushauri ni ufanye urudi huko mkoani kwenu ukapambane vinginevyo hapa mjini Dar es salaam utaishia kutangatanga kama mwehu!
 
Hivi ni kweli Kuna hela zinagawiwa kwa watu burebure kama maelezo yako mleta mada?

Us dollar 1= Tshs 2500/=
Dollar 500 × 2500 = 1,250,000/= Kuna mtu anagawa hela hivo na laptop Bure kweli?

Kama ndivyo basi na mimi nahitaji😀
 
Hata kama unataka kusaidia kitu kwa nia njema,ungetafuta approach nzuri sio ya kugawa PC na pesa kama PiPi.kwanza kugawa fedha bure bure ni kosa kisheria.
Siku ingine anzisha hata ka program fulani ili tu ubaini wenye uhitaji
 
Hata kama unataka kusaidia kitu kwa nia njema,ungetafuta approach nzuri sio ya kugawa PC na pesa kama PiPi.kwanza kugawa fedha bure bure ni kosa kisheria.
Siku ingine anzisha hata ka program fulani ili tu ubaini wenye uhitaji
Sheria namba ngapi na ya mwaka gani mkuu inakataza kugawa pesa bure kwa ajili ya kusaidia wanafunzi?

Hebu let kifungu mtaalamu wa sheria ili na mimi ambaye sijui sheria uenda nikabadilika!
 
Hivi ni kweli Kuna hela zinagawiwa kwa watu burebure kama maelezo yako mleta mada?

Us dollar 1= Tshs 2500/=
Dollar 500 × 2500 = 1,250,000/= Kuna mtu anagawa hela hivo na laptop Bure kweli?

Kama ndivyo basi na mimi nahitaji😀
Hakika watawala wamewafanya watanzania muone umasikini ni kitu cha kujivunia!,Aisee

Hivi $ 500 ni kiasi cha pesa ambacho kinakushangaza?,Au unadhani wewe kuziona nyingi na wengine pia wanaziona nyingi?
 
Hakika watawala wamewafanya watanzania muone umasikini ni kitu cha kujivunia!,Aisee

Hivi $ 500 ni kiasi cha pesa ambacho kinakushangaza?,Au unadhani wewe kuziona nyingi na wengine pia wanaziona nyingi?
Usiongee sana ndugu, nimekuomba na Mimi hizo $ 500 na hiyo laptop Bure, maneno yasiwe mengi
 
Back
Top Bottom