Kuna gari ukiendesha unaonekana 'muhuni', inasikitisha sana

Wabongo ndivyo walivyo. Hata kwenye huu uzi 99.9% hawana hata Pikipiki[emoji1787][emoji1787]
Mkuu hili taifa lina shida ya unafiki na majungu ni mengi mno kuliko uhalisia wa mambo
Please watafutaji msiwasikilize hao wajinga wajinga tafuteni pesa nunua kitu chochote ambacho binafsi kinakupa furaha

Haiwezekani nadrive then nikufuatishe wewe na mwendo wako kila mtu na maisha yake na ratiba yake sasa nikikupita haijalishi gari gani usiseme kwamba ni kijana au mhuni bali ni kila mtu aishi maisha yake

Hii tabia sio kwa gari ndogo tu hata hizi range, Toyota vx na zingine eti akikupita unaanza kubana au kusema jamaa wanaringa sana kumbe mtu ana ratiba yake na size ya gari yake inamruhusu kufanya hivyo sasa shida ipo wapi
 
Nyingi sio namba D. Zipo za namba A lkn bado zipo vizuri. Uimara wa gari ni matunzo.
Sawa basi mengi ni namba za zamani sababu kipindi hicho ushuru wake ulikua unalipika..sasa hivi ni adimu hizo sababu ushuru wake umesimamia ukucha..ingawa ni magari mazuri...
 
Nadhani hauna unachokijua..kwa kifupi hizo gari zilizotajwa hapo juu hakuna mpya nyingi ni usajili wa zamani sio kwamba watu hawaoni au hawapendi magari aliyoyataja hizo GC8, N12 au WRX...nakuongezea na hii SG9 usajili ni wazamani sababu ushuru wake haushikiki sasa sijui mambo ya engine gear box yanatoka wapi hayo...😂😂😂😂 au na wewe ni shahidi wa hisia...😂😂😂😂
 
Wewe nawe mbona unakuwa kichwa maji.

Mm naongelea tabia za watanzania kupenda namba bila kujali ubora. Nimereply kwenye ujumbe wako sababu na wewe umeongelea namba.

Hayo mambo ya GC8 sijui subaru wrx ni yenu vijana wa mbio na maperfomance.
 
Matoleo mapya ya VW polo SA walichukua polisi kwa hiyo wote wanaonekana wahuni? Golf 7 mpaka 10 ndio watata bara barani kwa mbio VW polo wanatumia maofisa wengi na pisi ni gari zisizo na makeke na watumiaji wake sio kama wa GTI 8 yenye exhaust za makelele...wenyewe wanaita kujamba na Benz sports zipo za makelele pia hata BMW pia wanatengeneza magari kutokana na soko linataka nini...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…