Habari wana Jf ,kwa mara ya kwanza nimejikuta nasikitishwa sana na umasikini na Ugumu wa maisha unaoendelea kuongezeka huku kukiwa hakuna suluhisho la kueleweka Kutoka CCM .
Nimewaza sana na kujikuta naona ni Bora Tundu lissu ambae anaonekana ndiye mtu pekee kwa sasa mwenye ushawishi na uwezo wa kuongoza Nchi hasa kuiondoa CCM madarakani kupitia Chama chochote hata kipya aandaliwe na kuweza kuja kuiondoa hii CCM.
CCM imeongoza Nchi kwa zaidi ya miaka 40 lakini imeshindwa hata kuwatua kinamama ndoa za Maji mijini kote na imeshindwa kwa kiwango kikubwa katika kupiga vita Ufisadi , kuendeleza na kujenga viwanda ,kuondoa shida ya ajira ,kuboresha huduma za Afya na nk .
2025 CCM inaweza Ondoka aandaliwe vizuri tu .