Kuna muda unatamani kwenda kuroga kwa mganga ili nipate chaneli za pesa

Kuna muda unatamani kwenda kuroga kwa mganga ili nipate chaneli za pesa

Bahati mbaya hela haikai kwenye huruma na upendo, hela hukaa kwenye ukatili unyama na kila aina ya uovu, hela bila ya damu jasho na kila aina ya harassment ni ngumu sana kuipata.
Hili ndo jibu.
Hata ukienda kwa mganga lazima Kuna sharti la kikatili.
Ukienda kwa Masonic the same.
Kwa Mungu the same umlilie haswa kwa ibada na funga .
Hakuna penye hela bila jasho yakhee ..
 
Miye Kwa sasa nabeti japo loss ni kubwa kuliko faida,ila inaniweka mjini,nikipata mkwanja wa umaster kucha nakula,mambo yakiwa tight nabeti,nikipata ya vocha siku inapita,mhindi nikimpiga sana napata Naya kumpa shemeji yenu ahemee


Maisha tight siyo kwako tu,juzi mshahara umetoka,Leo ushaisha,aahaaaaa

Nimeshahemea vitu vya mwezi mzima,na nimeshsanunua vitu vya wanafunzi vya shule Jumatatu ijayoView attachment 2669391
huna mambo mengi mkuu, unajikubali....

hongera kwako
 
Kweli mkuu siwez kwenda kwa mganga ika tu naamini iko siku mambo yatakua poa lakini ndo unabaki kujiuliza mpka lini na hasa ss familia za kimaskini unakuta bado wazazi wanakuangalia ww yaan mtu ndo kwanz una miaka 20-25 halafu wazazi wanakuangalia ww uwasaidie mkuu inaumiza sna apo hujakutana na changamoto za ujana
Nafasi za kazi Oman ujaziona.
Mshahara mkubwa kuliko hata graduate wa Serikali ya bongo Tena mwenye masters
 
Dah ukweli kbsa mkuu.Unakuta bado ujajipata ila una majukumu tayar hapo hata kumiliki demu ni ngumu chamuhimu Mungu atusaidie tupate channel mpya yenye kipato ili tuhudumie familia zetu na ambayo utaitengeneza.
Chanel moja ikigoma unabadili location
 
Fundi bishoo anaenda site kavaa jinsi yake na raba za VANS au converse all star just imagine

Kapiga na cap yake ya new York Yankees NY halafu anabeba tofali[emoji1787][emoji1787]
😁😁Kwaiyo hutaki sisi wazee wa masite tusivae kinyamwezi mkuu
 
Sijajua haswa ni fundi kwa fani gani, lakini kwa vyovyote fundi bila kuongeza thamani unaweza ukabaki kuwa fundi msaidizi wakati wote.
Sote tumepitia kuwa saidia fundi, hio ni kwa sababu huyo fundi nae alikua msaidizi pia ila alijiongeza na kukuza thamani ya ufundi wake na akapata connection kubwa badala ya kufanya kazi mwenyewe akatafuta wasaidizi.

Huko kufanya kazi na fundi ndiko kunakokupa conection, huko kufanya kazi na fundi ndiko kunakupa uzoefu, kunakukutanisha na watu wengi wakiwemo mafundi wengine wenye conection kubwa,

Katika tasnia nzima ya ufundi huwezi kufanya kazi peke yako ni lazima uwe na mjumuiko wa mafundi wengine wengi ili kazi iwe bora, usione shida kufanya kazi za usaidizi kwa sababu ndio mzunguko wa ufundi ilivyo.

Cha kufanya katika kile unachokifanya fanya kama chako, kiongezee thamani, jifunze mbinu mpya za kiufundi.

Nasisitiza kuongeza thamani kwa sababu ukiwa wa thamani hata fundi akikuhitajia kwa kazi yake, kama ulikua wa kumi atakulipa kumi kushuka chini, ila ukiongeza thamani ukawa wa mia basi hata malipo yako yatakuwa ni mia mia hivi.

Ukiisha kupata thamani anza kuweka mikakati ya kuwa na ofisi yako.
Ukiwa na ofisi hali wewe ni fundi utakua unapata kiasi kikubwa sana cha faida .

Ujue kuna watu wana ofisi za kiufundi lakini sio mafundi ila wana mitaji na connection, hao ndio wanaowatuma mafundi na kuwalalia sana, imagine wewe ni fundi, una mtaji una conection! Lazima upige hatua nyingi sana mbele.

La muhimu pia achana kuwa kama mshumaa kubwa angaza wengine hali wewe unateketea , hao ndugu jamaa na marafiki na pengine wazazi wawe sehemi ya mwisho kwenye mapato yako, kipaombele kwenye mapato yako kiwe nikiongeza thamani na kukuza mtaji.
Hapo nmekuelewa mkuu nna miaka 7 kweny ufundi mkuu conection yangu kubwa n kwa mafundi wenzangu sio maboss natfta za mabosi maana mafund wenzangu m nshawapa kiwango bila ya kiasi kadhaa mm sifanyi kazi sasa wao wanataka waendelee kunilipa same money kila mwaka hiko kitu nimekikataa toka mwaka jana novembersasa msoto nnaopitia sio kitoto japokua kuna mda unakata moto
 
Ardhi ndio msingi wa kuwa tajiri kwa mtu masikini ardhi still ni bure Tanzania nenda kakomae nayo
 
Back
Top Bottom