Kuna muda unaweza kuishiwa pesa hadi ukatamani kumkopa mdada wa kazi

Kuna muda unaweza kuishiwa pesa hadi ukatamani kumkopa mdada wa kazi

mpaka nawaza hivi ni kwa nini naishi!!!
Kwa kweli hapo mtu unatakiwa ujifikirie kama kuna umuhimu wa kuleta viumbe wengine dunia hii.. Lakini kama hali inaruhusu hata wasizidi wawili...ili waweze kusaidiana mbele kwa mbele sio unaleta mmoja halafu ghafla wote mnavuta....sipati picha....

Fikiria maisha magumu unaenda kutoa msongo kwa papuchi ya wife na unamalizia humo
unategemea matokeo yake ni nini..

Tuliwahi kupitia masha magumu sana kifamilia bado wadogo, mpaka nikawa nawaza kwanini baba alituzaa wengi hivi...

Kwa kweli kama sina uwezo sitaleta viumbe vingine kuja kuteseka duniani...
 
Asee sijui kwanini Ila mada zakuishiwa huwa zinanitia moyo kuwa kumbe sipo peke yangu.
Roho ya umasikini inakuandama mkuu. Kwa imani yako ipinge. Maana yake ni kwamba unakuwa na amani sana ukiona wenye shida mpo wengi kuliko mmoja akiondoka kwenye umasikini. Ama badala ya kuongeza bidii unajikuta unarelax kwakuwa mpo masikini wengi.

Nb: Sijaandika kwa ubaya
 
Dah! Mkuu acha tu maisha yasikie tu!

2017 kuna siku niliwahi kuishiwa yaani unajua kuishiwa acheni tu jamani, hasa kwa sisi ambao tunapambana noma sana.

Wazo lilokuja kichwani ni cha kwako ndo kinakusaidia, nikachukua simu yangu nikaitafutia soko kwenye maduka simu kila ninapoingia wananiambia una risit wengine wananipa kiwango ambacho hata shida yangu haiwezi kuisha dah siku hiyo ilikuwa noma sana.

Siku hiyo sikuuza simu asubuhi nikatembea toka Nyamanoro hadi mjini (Mwanza) kazini shida iko pale pale.

Nikawaza nimpige mzinga mama naye maisha kijijini noma nikapiga chini wazo la mama nikakomaa kama siku tatu mpaka nawaza hivi ni kwa nini naishi!!!
Mkuu Nyamanoro mbona karibu tu? Mimi nikiwa nasoma, nilitembea mwaka mzima kwa mguu, nenda rudi kutoka Ilemela (kule wanapopaita kanisani) hadi Lake shule ya msingi. Hiyo ni adhabu nilipewa kwa colabo la mama mzazi na bibi yangu.

Kuna issue nilizingua wakaona kuliko viboko, ninyimwe nauli akili inikae. Nilikuwa natamani hata kuacha shule lakini ndio hivyo nilipambana hadi mwisho.
 
Kufulia hakujawahi muacha mtu salama! Iwe mtu, kampuni au serikali.
Hata serikali pamoja na kwamba inakusanya kila kitu lakini ikiishiwa huwa inawaza kukusanya kodi kwenye barabara na madaraja wakati yamejengwa kwa kodi zao!

Kuna wakati vyuma vinaweza kukaza kila kona hadi ukatamani kumkopa pesa dada wa kazi ilihali hujamlipa mshahara!
Nimekusoma vilivyo mkuu🤣🤣🤣
 
Kuna kipindi nilipanga nyumba yani ukiwa unahela unaona haa hii kodi no ndogo ila ukiwa umefulia unasema,,,daaah hii hela nayotoa nampa mwenye nyumba mbona ni nyingi sana ikiisha pango nitatafuta sehem yenye bei nafuu,,,

cha ajabu ukipat hela yote unasahau unabaki kusema hii nyumba nzuri ndio inafaa kuishi Mimi[emoji1787][emoji1787][emoji1787] umasikini mbaya sana[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Daah nakumbuka msoto niliwahi kupitia kipindi hiko nilivyomaliza form 4, nikakutana na sister yangu mtoto wa mama mkubwa slay queen kipindi hicho ameukwaa u misss Morogoro, maktaba DSM pale navuka zebra yupo kwenye harrier yake mbele na tumeonana kabisa akaangalia pembeni, hapo mfukoni nina 200, nikagonga kioo nimpe hata salamu, akauchuna haangalii kabisa.

Mara taa zikawaka akainua, aisee iliniuma sana ila Mungu alivyo mwema baada ya kuvuka taa tuu hatua mbili tatu nikakutana na mjomba wangu akaniambia twende hivi, tukaishia mgahawa flani nikapata heavy breakfast na laki moja cash, cha ajabu huyu mjomba ni bahili kinoma kwa ndugu zake wengine.

Nilijifunza kuacha kuhukumu kabla hujamjua mtu, mimi na uncle wangu ni du damu kwa muda huu na huyu sister sijawahi kuacha kumsaidia akija na shida zake, na anakuja mara kwa mara, nilisamehe lakini sijawahi kusahau hii scenario... ipo siku nitamkumbusha
 
Ndo maana mnadhulumu wadada wa kazi mwisho wanawapiga viberiti ndani, unamwambia unamtunzia mshahara wake siku akitaka kuondoka kwakuwa kwako vyuma vimekaza unaanza kumpigia hesabu ya vyombo vilivyovunjika ili umtapeli hela yake
 
Kwa kweli hapo mtu unatakiwa ujifikirie kama kuna umuhumi wa kuleta viumbe wengine dunia hii..Lakini kama hali inaruhusu hata wasizidi wawili...ili waweze kusaidiana mbele kwa mbele sio unaleta mmoja halafu ghafla wote mnavuta....sipati picha....
Fikiria maisha magumu unaenda kutoa msongo kwa papuchi ya wife na unamalizia humo
unategemea matokeo yake ni nini..
tuliwahi kupitia masha magumu sana kifamilia bado wadogo, mpaka nikawa nawaza kwanini baba alituzaa wengi hivi...
Kwa kweli kama sina uwezo sitaleta viumbe vingine kuja kuteseka duniani...
Mwenye kuelewa ataelewa
 
Kuna Kaka yangu ambae yeye huwa ndio namtegemea kuwa msaada pindi nikikwama basi naona kipindi Cha Magu mambo yakibana Sana na yeye ananiomba laki mbili sijakah sawa wiki ya pili akaniomba Tena laki na mimi namtumia tu bila kujali mnk najuwa Hana roho ya kunidhulumu ila nilimpa ikaja kufika Kama milion mbili HV na nusu bas nikawa napewa taarifa kuwa jamaa sasa HV Hana hella hata mke wake na alinkopa laki tatu HV.

Baada ya mwezo nae akarudisha ila Broo yeye alikuwa ananikopa kwenda kulewa na asikose hela za gambe mnk anapenda gambe na washkaji zake Broo mwinginee akanijulisha kuwa nisiwe Nampa pesa mnk jamaa anakwenda kuwanunulia watu pombe ila mm sikujali hata Kuna siku kanipigia nikampa laki tano fresh kbsa ikapita muda Sana ananipigia siku moja simu niende kwake akanioneshe kiwanja Changu na hati juu dah nilishkuru Sana.
 
Kuna Siku nilikwama sana, kila nikiwaza sipati jibu, la hela. Nikaona nimwangushie zigo mama watoto, ambae tumeachana miaka minne iliyopita kipindi hicho nina Shida.

Pamoja na kuachana, huwa tunawasiliana mara kwa mara kama wazazi, ingawa tunaishi mikoa tofauti, hivyo baada ya kukosa pesa nikamjaribu, aniazime Tsh 200,000 kama anazo he, akaniambia ndani ya masaa matatu atanitumia, kweli akanitumia yaani nilishukuru sana, alinifanya niendelee kujiamini Siku ile.
Ilikuwaje mkaachana na huyu mama watoto na anakupenda kiasi hiki. Maana mwanamke mpaka akupe hela yake, jua anakupenda.
 
kuna vitu ni muhimu sana.
AKIBA

Kingine jitahidi uwe na vitu vya thamani kama TV,MUSIC SYSTEM, FRIJI, KITANDA, GODORO, N.K niamini hv vitu vinaokoa sana ukifulia maana hata ukiuza ukika sawa vina nunulika
Ukiendekeza kuuza hivyo vitu! Utabaki kununua mabarafu kwa jilani, lazima ujue vibanda umiza, kulala chini kwako liwe jambo la kawaida!
 
Kufulia hakujawahi muacha mtu salama! Iwe mtu, kampuni au Serikali. Hata serikali pamoja na kwamba inakusanya kila kitu lakini ikiishiwa huwa inawaza kukusanya kodi kwenye barabara na madaraja wakati yamejengwa kwa kodi zao!

Kuna wakati vyuma vinaweza kukaza kila kona hadi ukatamani kumkopa pesa dada wa kazi ilihali hujamlipa mshahara.
Kama hujawahi kuishiwa huwezi kuelewa pesa ni nini, hata jero utaiheshimu tu, sitasahau siku nilivoishiwa, ni katoa gari niende kutafuta chochote kwa marafiki, nafika mwenge kwenye mataa gari ikaishiwa mafuta kati kati ya barabara hata shilling mia sina, kwenye simu hata ya kubeep sina wale vijana wa kunisukuma kuniweka pembeni ya barabara kabla trafiki hawajaja wakaniomba elf 5 sina........duh Mungu ndo alioniokoa siku hiyo.
 
Ukiendekeza kuuza hivyo vitu! Utabaki kununua mabarafu kwa jilani, lazima ujue vibanda umiza, kulala chini kwako liwe jambo la kawaida!
Mkuu naongelea ile shida ya mwisho kabisa kiasi umekosa msaada. Yaweza kuwa unaongea kwa kujiami kwakuwa haijawahi kukuta.

Mimi jamaa yangu alipata ishu akawa yuko safi alijaza geto safi. Ila mambo yalikuja kubuma akawa anaomba hadi buku. Alichofanya aliuza tv, friji, kabati akajikita na biashara hadi saizi jamaa ni story nyingine. Na vitu vyake ndo vilimuokoa kuishi
 
Back
Top Bottom