Kuna muda unaweza kuishiwa pesa hadi ukatamani kumkopa mdada wa kazi

Kuna muda unaweza kuishiwa pesa hadi ukatamani kumkopa mdada wa kazi

Kufulia hakujawahi muacha mtu salama! Iwe mtu, kampuni au Serikali. Hata serikali pamoja na kwamba inakusanya kila kitu lakini ikiishiwa huwa inawaza kukusanya kodi kwenye barabara na madaraja wakati yamejengwa kwa kodi zao!

Kuna wakati vyuma vinaweza kukaza kila kona hadi ukatamani kumkopa pesa dada wa kazi ilihali hujamlipa mshahara.
Ulichosema ni kweli, sikia jambo lingine lakini sio kuchacha, hata bendi ya Wanamsondo waliwahi kuimba. "Maradhi yote ugua lakini kuchacha usiombee"
 
Daah nakumbuka msoto niliwahi kupitia kipindi hiko nilivyomaliza form 4, nikakutana na sister yangu mtoto wa mama mkubwa slay queen kipindi hicho ameukwaa u misss Morogoro, maktaba DSM pale navuka zebra yupo kwenye harrier yake mbele na tumeonana kabisa akaangalia pembeni, hapo mfukoni nina 200, nikagonga kioo nimpe hata salamu, akauchuna haangalii kabisa, mara taa zikawaka akainua, aisee iliniuma sana ila Mungu alivyo mwema baada ya kuvuka taa tuu hatua mbili tatu nikakutana na mjomba wangu akaniambia twende hivi, tukaishia mgahawa flani nikapata heavy breakfast na laki moja cash, cha ajabu huyu mjomba ni bahili kinoma kwa ndugu zake wengine.

Nilijifunza kuacha kuhukumu kabla hujamjua mtu, mimi na uncle wangu ni du damu kwa muda huu na huyu sister sijawahi kuacha kumsaidia akija na shida zake, na anakuja mara kwa mara, nilisamehe lakini sijawahi kusahau hii scenario... ipo siku nitamkumbusha
Mkuu ndugu wakikwambia ndugu yao bahili usiamini. Yani ukianza wasaidia ndugu mara nyingi ndo wanajiachia na ukiacha wanaanza kukusema na kukushushia lawama.
Huenda aliwasaidia sana mpaka akachoka
 
Kufulia hakujawahi muacha mtu salama! Iwe mtu, kampuni au Serikali. Hata serikali pamoja na kwamba inakusanya kila kitu lakini ikiishiwa huwa inawaza kukusanya kodi kwenye barabara na madaraja wakati yamejengwa kwa kodi zao!

Kuna wakati vyuma vinaweza kukaza kila kona hadi ukatamani kumkopa pesa dada wa kazi ilihali hujamlipa mshahara.
Kopa tu kwa dada, hiyo ndio ile mikopo serikali inaita ya masharti nafuu...
 
Ilikuwaje mkaachana na huyu mama watoto na anakupenda kiasi hiki
Maana mwanamke mpaka akupe hela yake, jua anakupenda
Ni hadithi ndefu, kwakweli, Nadhani kulikuwa na mtu, anamsukuma kufikia uamuzi huo, bila kujali kuwa tuna watoto na tayari tulikuwa na miaka 13 ya ndoa.

Ila sasa hivi, anajutia uamuzi wake, ila hana namna, maana wanaume wameshamzalisha tayari. Mimi niko vile vile na watoto wangu.
 
Ndugu yangu hamna namna inaweza kufanya mkarudiana aisee?

Please nakuomba toka ndani ya moyo wangu kama hakuna kizuizi cha moja kwa moja mrudiane.
Ni mwaka wa sita sasa tangu tuachane, ingawa sijaoa tena, ila yeye amezalishwa na mwanamme mwingine, kitu ambacho kwangu ni kichefuchefu, yaani hata nikiongea nae kwa Simu nikisikia sauti ya yule mtoto, moyo inaingia ganzi.
Hata hivyo akiwa na shida namsaidia.
 
Kwa kweli kufulia kubaya sana. Nilifulia kipindi fulani, nikaenda zangu benki nilikuwa na 20k ya mwisho dadeq. Nikaichukua nikajisemea sasa nakuwa Eliya wa baiboni aisee, sijui unga robo na mafuta kidogo...daah...

Nimekaa siku mbili nikamcheki mwamba wangu yupo Norway kipindi hicho, sijui nilikumbuka vipi lakini yule mwamba kuna siku alikuja tz akatumia pesa zote, akanitafuta nimpe 500k, nilimpa bila hata kuambiana atanilipa vipi...nilivyomcheki tu akaniambia nimpe account namba na swift yake..kesho yake nakutana na msg ya 2.5m, nilihisi dunia yote yangu maniner!!
 
Dah wakuu! Hii situation ya kuishiwa ni mbaya sana na ndo ninayoipitia sasa. Yaani hapa ninavyoandika hii comment mfukoni nimebaki na buku 3 tu! Then ndani stock ya chakula imekata, umeme imebaki unit 1.63 halafu sijala chochote toka asbh na harakati zangu zimeyumba kwa kipindi hiki sio mchezo, mbaya zaidi wife kuanzia kesho siku yoyote anarudi home maana alienda kwao kusalimia mara moja.

Yaani hapa nilipo nimechill gheto nawaza vitu vingi hadi kichwa kinauma. Nilichoamua hapa nimeenda kuchukua unga nusu nitoe kitu badae mishale ya jioni then unga utakaobaki wa kesho, nitachukua na fungu la dagaa, najua kwenye buku 3 itabaki kama 1300 hv hii nitaamka nayo kesho na akili mpya.

Ila ndugu zangu kuishiwa kubaya sana, hapa nimezima kila kitu kinachotumia umeme ili tu usije kukata maana muda wote naichungulia hiyo unit ili inifikishe kesho nijue nafanyaje kusurvive na siku mpya.

NB: Najua hii changamoto ninayopitia mimi kuna mtu pia mahali anaipitia at the same time, hivyo cha muhimu ni kujua na kuamini kila jambo linatokea kwa kusudi maalumu na litakwisha tu.
 
Dah wakuu! Hii situation ya kuishiwa ni mbaya sana na ndo ninayoipitia sasa. Yaani hapa ninavyoandika hii comment mfukoni nimebaki na buku 3 tu! Then ndani stock ya chakula imekata, umeme imebaki unit 1.63 alafu sijala chochote toka asbh na harakati zangu zimeyumba kwa kipindi hiki sio mchezo, mbaya zaidi wife kuanzia kesho siku yoyote anarudi home maana alienda kwao kusalimia mara moja.

Yaani hapa nilipo nimechill gheto nawaza vitu vingi hadi kichwa kinauma. Nilichoamua hapa nimeenda kuchukua unga nusu nitoe kitu badae mishale ya jioni then unga utakaobaki wa kesho, nitachukua na fungu la dagaa, najua kwenye buku 3 itabaki kama 1300 hv hii nitaamka nayo kesho na akili mpya.

Ila ndugu zangu kuishiwa kubaya sana, hapa nimezima kila kitu kinachotumia umeme ili tu usije kukata maana muda wote naichungulia hiyo unit ili inifikishe kesho nijue nafanyaje kusurvive na siku mpya.

NB: Najua hii changamoto ninayopitia mm kuna mtu pia mahali anaipitia at the same time, hivyo cha muhimu ni kujua na kuamini kila jambo linatokea kwa kusudi maalumu na litakwisha tu.
Nitumie namba yako ya mita nikubusti kidogo
 
Back
Top Bottom