Kuna siri gani kwenda Pre-Season nje ya nchi kwa timu masikini?

Kuna siri gani kwenda Pre-Season nje ya nchi kwa timu masikini?

Msimu uliuopita Yanga alinangwa hivi hivi kwa kubakia Kigamboni wakati Simba akienda nchi zaidi ya mbili katika pre season lakini mwisho wa siku aliyebakia Kigamboni ndiye aliyebakia hadi fainali mashindano ya CAFCC, bingwa wa NBC premier league, na bingwa wa Azam Federation cup. Endeleeni kujivunia pre season tu
Kwahiyo tuna kubaliana kuwa hamna hela ya kwenda pre season nje ya nchi, na kuhusu muda kuto kutosha ni porojo tu za kuwa pumbaza wana utopolo ?? [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mwisho wa siku wanasajili akina Akpan, sawadogo, okwa, dejan kwa bei ndogo kabisa na kumpa Ahmed Ally awapake mafuta wauzike kwa mashabiki.
Umeanza kuonesha ur true side, kumbe ulikua ni wivu tu,, kunywa maji mengi mkuu maumivu yatapoa tu
 
Kwa hiyo umekaa hapo unahofu Shomari Kapombe anatorosha pembe za ndovu na hayo yote unaamini yanasubiri wakati wa pre-season tu ila msimu mzima timu zinaposafiri ikiwemo Yanga hauna wasiwasi? Wewe hauna wasiwasi, bali una upungufu wa maarifa ukichanganya na wivu.
Hilo jamaa linaonekana hata in real life ni masikini na lina wivu kinoma
 
Kwa hiyo umekaa hapo unahofu Shomari Kapombe anatorosha pembe za ndovu na hayo yote unaamini yanasubiri wakati wa pre-season tu ila msimu mzima timu zinaposafiri ikiwemo Yanga hauna wasiwasi? Wewe hauna wasiwasi, bali una upungufu wa maarifa ukichanganya na wivu.
hili watakujibu wengine. Lakini timu inasafiri kwenda kwenye mechi Malawi kucheza na Big bullets kuna nini cha maana huko Malawi?
 
Sina hakika na mwendelezo wa hili baada ya kipindi Hali hii iliposhamiri kushitukiwa na serikali. Enzi za Abbas Gulamali na Azim Dewji hii Hali ilikuwa juu Sana. Timu iliweza kusafiri na mipira 30 ya mazoezi wakirudi Wanarudi na mipira mipya 30. Mambo yalikuwa mengi kipindi hicho cha Giza Ila sijui kama mpaka Leo bado wanaendelea.
Nikija Kwa hoja ya mleta Uzi kuhusu timu kwenda nje huku ikishindwa kusajili Wachezaji wazuri Kwa hela kubwa, nadhani hili amelijibu mwenyewe. Safari za pre-season zinadhaminiwa na Mtu Kwa malengo na faida yake ya kibiashara. Kwa hiyo anayemlipa Mpiga Ngoma ndiye anayechagua wimbo.
Azim Dewj na Abbas Gulamali walipiga pesa kwa njia mbili kuu, 1 ni hiyo ya mipira 30 na makontena ya TV/Magari ya zawadi za wachezaji 25 tu, 2 ni kwa njia ya betting na kuuza mechi. Hawa friends of Simba/Yanga ni group la kubet na michongo kwa kupitia ama timu au wachezaji wao waliowasajili wao kama wao, (no free lunch)
 
Sina hakika na mwendelezo wa hili baada ya kipindi Hali hii iliposhamiri kushitukiwa na serikali. Enzi za Abbas Gulamali na Azim Dewji hii Hali ilikuwa juu Sana. Timu iliweza kusafiri na mipira 30 ya mazoezi wakirudi Wanarudi na mipira mipya 30. Mambo yalikuwa mengi kipindi hicho cha Giza Ila sijui kama mpaka Leo bado wanaendelea.
Nikija Kwa hoja ya mleta Uzi kuhusu timu kwenda nje huku ikishindwa kusajili Wachezaji wazuri Kwa hela kubwa, nadhani hili amelijibu mwenyewe. Safari za pre-season zinadhaminiwa na Mtu Kwa malengo na faida yake ya kibiashara. Kwa hiyo anayemlipa Mpiga Ngoma ndiye anayechagua wimbo.
Hii ni biashara ya ukoo/familia. Ukifikiria saaaaaana utagundua kuwa sio bure bure bure bure kabisa!!! Kuna tembo wengi sana walipotea kwa njia hii ya ufadhili wa Simba na Yanga, kuna madawa mengi sana yamesafirishwa kwa njiaa hii ya simba na yanga na preseasons.
 
Kwanini ni rahisi mno timu zetu kwenda kuweka kambi nje ya nchi ?
Leo unauliza hili swali, kesho utauliza Mo ameweka 20B kwenye bank gani. Sasa jibu lipo hapo hapo katika maswali yako mawili hayo
 
hili watakujibu wengine. Lakini timu inasafiri kwenda kwenye mechi Malawi kucheza na Big bullets kuna nini cha maana huko Malawi?
Wewe ndiyo umeleta hizo shutuma mbona sasa unarushia wengine mzigo wakujibie?
 
Kwahiyo tuna kubaliana kuwa hamna hela ya kwenda pre season nje ya nchi, na kuhusu muda kuto kutosha ni porojo tu za kuwa pumbaza wana utopolo ?? [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Swala la kusema hakuna ela halina uthibitisho,, Ni swala la maamuzi tu kuamua kwenda wapi kufanyia pre season kulingana na mahitaji ya team ili kujiweka sawa.
 
Serikali chunguza kuna uharifu unatendwa na viongozi wa simba kwenye kichaka cha preseason
Team ya simba haina uchumi wa kuweka timu Turkey kwa week sita
Wanaleta ngada nchini kufanya vijana kuwa mazezeta
 
wivu tu unawasumbua .
Umasikini wenu unaosababisha hadi mshindwe kumlipa Luc Eymael usituletee shida . Endeleeni kula mihogo yenu hapo Avic .Waacheni wenzenu wakale bata wakafurahie Maisha katika nchi za watu

Nyie nendeni kwa wala mihogo wenzenu huko Malawi tuonane ligi ikianza.
Na iwe mwisho kupangiana matumizi ya pesa.
 
Tanzania hakuna timu tajiri, timu nyingi kama sio zote hazina misuli ya fedha za kusajili wachezaji wazuri sana na mabenchi ya ufundi class ya juu. Timu nyingi zinashindwa kuwalipa makocha na wachezaji signing fees zao na mishahara kwa wakati, wachezaji hawana bima na hazina viwanja vyao wenyewe. Kwa ujumla timu zetu zinaendeshwa kwa kubangaiza huku na kule; kwa maneno ya kimpira timu zetu ni feeder clubs kwa timu za kanda nyingine Afrika kutokana na umaskini wao.

Kwanini ni rahisi mno timu zetu kwenda kuweka kambi nje ya nchi lakini ni vigumu kusajili wachezaji wazuri, kulipa mishahara mikubwa ya wachezaji na benchi la ufundi au kujenga uwanja? Majibu ni mengi sana, mojawapo ya majibu hayo ni kwamba kuna uhusiano mkubwa sana kati timu kwenda pre-season za nje ya nchi na sababu za mtu kukubali kuidhamini timu. Sina ushahidi kamili, lakini pre-season hizi za hivi zina uhusiano mkubwa na biashara za magendo (smuggling), madawa ya kulevya au ukwepaji ushuru kwa kutumia jina la timu, wachezaji na benchi la ufundi. Akili ya kawaida tu haiwezi kuamini kwamba timu zetu zina fedha nyingi za kwenda kuweka kambi nje nchi lakini hazina fedha za kusajili wachezaji wazuri wa kuleta mataji.

Jeshi la uhamiaji na wadau wengine hebu tegeni mitego ya kunasa matunda ya pre-season za nje ya nchi kwa timu mbovu kabisa uwanjani na zinazolalamika kuwa hazina pesa za kulipa wachezaji, makocha, kusajili na kujenga viwanja vyao. Mnaweza kugundua chocholo za uovu kwenye hizi safari
Tatizo ni kwamba pesa halitosis kwenye accounts za club. Hakuna ni mtu anatoa. Was wawili wanasema " mlipaji wa mpiga zumari, ndo huchagua nyimbo"
 
Mwaka Jana mlishindwa kwenda pre season kwa sababu pesa yote ilimalizika kwa malipo ya Aziz K, mwaka juzi bando lilikata baada ya kupewa ofa na mwaka huu mmelipa pesa na faini kwa yule kocha aliyewaita wajinga
 
wivu tu unawasumbua .
Umasikini wenu unaosababisha hadi mshindwe kumlipa Luc Eymael usituletee shida . Endeleeni kula mihogo yenu hapo Avic .Waacheni wenzenu wakale bata wakafurahie Maisha katika nchi za watu

Nyie nendeni kwa wala mihogo wenzenu huko Malawi tuonane ligi ikianza.
Na iwe mwisho kupangiana matumizi ya pesa.
Hushangai timu kuongozwa na ukoo mmoja tangu enzi na enzi mababu na mababu mpaka wajukuu, no free lunch bro. 20b ziko kwa nani?
 
wivu tu unawasumbua .
Umasikini wenu unaosababisha hadi mshindwe kumlipa Luc Eymael usituletee shida . Endeleeni kula mihogo yenu hapo Avic .Waacheni wenzenu wakale bata wakafurahie Maisha katika nchi za watu

Nyie nendeni kwa wala mihogo wenzenu huko Malawi tuonane ligi ikianza.
Na iwe mwisho kupangiana matumizi ya pesa.
Daa!!! Azim na Gulamali wakifahamu kuwa mashabiki ni mbumbu, shida Yao ni Yanga ifungwe na Simba au Simba ifungwe na Yanga basi hawana kingine. Walihakikisha kuwa Simba na Yanga zinafingana kwa namna yoyote (kuachiana) ili kupunguza kelele zao.
 
Ngada tu baaaasi!! kuna pre-season gani huko wakati Baleke, Chama, Sakho, na wachezaji wengine hawako Uturuki. Nimemsikia maandazi mmoja anasema Baleke hakwenda Uturuki kwakuwa vibali vyake (passport) vimekwisha< sheeet!! wamegundua lini kuwa vibali vya Baleke vimekwisha? kwani safari ya Uturuki ilikuwa ya ghafla? Chama je?

Iko siri kubwa kwanini watu wanakwenda pre-season maeneo hayo, tena wanatamani kamba ya pre-season iwekwe huko Columbia, Afghanistan, Pakistan au Venezuella.
 
Tanzania hakuna timu tajiri, timu nyingi kama sio zote hazina misuli ya fedha za kusajili wachezaji wazuri sana na mabenchi ya ufundi class ya juu. Timu nyingi zinashindwa kuwalipa makocha na wachezaji signing fees zao na mishahara kwa wakati, wachezaji hawana bima na hazina viwanja vyao wenyewe. Kwa ujumla timu zetu zinaendeshwa kwa kubangaiza huku na kule; kwa maneno ya kimpira timu zetu ni feeder clubs kwa timu za kanda nyingine Afrika kutokana na umaskini wao.

Kwanini ni rahisi mno timu zetu kwenda kuweka kambi nje ya nchi lakini ni vigumu kusajili wachezaji wazuri, kulipa mishahara mikubwa ya wachezaji na benchi la ufundi au kujenga uwanja? Majibu ni mengi sana, mojawapo ya majibu hayo ni kwamba kuna uhusiano mkubwa sana kati timu kwenda pre-season za nje ya nchi na sababu za mtu kukubali kuidhamini timu. Sina ushahidi kamili, lakini pre-season hizi za hivi zina uhusiano mkubwa na biashara za magendo (smuggling), madawa ya kulevya au ukwepaji ushuru kwa kutumia jina la timu, wachezaji na benchi la ufundi. Akili ya kawaida tu haiwezi kuamini kwamba timu zetu zina fedha nyingi za kwenda kuweka kambi nje nchi lakini hazina fedha za kusajili wachezaji wazuri wa kuleta mataji.

Jeshi la uhamiaji na wadau wengine hebu tegeni mitego ya kunasa matunda ya pre-season za nje ya nchi kwa timu mbovu kabisa uwanjani na zinazolalamika kuwa hazina pesa za kulipa wachezaji, makocha, kusajili na kujenga viwanja vyao. Mnaweza kugundua chocholo za uovu kwenye hizi safari.
Sitaki kuamini hizi timu ni maskini.
Kama ni kweli basi ni suala la viongozi wabovu wasio na maono tulionao.
Mfano ukiangalia uhitaji wa kadi za uanachama kwa timu kama Simba ni mkubwa sana.Lakini hakuna kiongozi anayependa timu iwe na wanachama wengi ndio maana kuna ugumu wa kupata kadi na utaratibu haueleweki
 
Back
Top Bottom