Tetesi: Kuna tetesi kwamba Marekani inapanga kutangaza vikwazo kwa Serikali ya Tanzania

Tetesi: Kuna tetesi kwamba Marekani inapanga kutangaza vikwazo kwa Serikali ya Tanzania

na underson ndambo.

Taifa la Marekani linatarajia kushusha rungu la aina yake kwa serikali ya Tanzania kufuatia hali ya sintofahamu inayoendelea nchini kutokana na sakata la uchaguzi mkuu wa Zanzibar.
Habari zinadokeza kuwa taifa hilo kubwa duniani litaweka vikwazo vya kiuchumi kwa Tanzania hali itakayopelekea Tanzania kuandika historia nyingine mbaya mbele ya uso wa dunia.

Serikali ya Marekani tayari imezuia misaada mbalimbali kwa Tanzania na pia ndiyo iliyoshinikiza Tanzania kunyimwa fedha za MCC, pamoja na kuzishawishi nchi zengine. Serikali ya Tanzania ipo hatarini kukumbwa na janga la njaa, ikiendelea kupuuza juhudi za kimataifa kuitaka kuumaliza kwa haraka mgogoro wa Zanzibar unaofukuta kwa kuacha haki itendeke kabla ya Febr 2017.

Habari zinadokeza kuwa balozi wa Marekani nchini atatoa msimamo unaoelezwa kuwa 'mkali' ili kuishinikiza serikali ya Tanzania kuheshimu maamuzi ya wananchi kwenye uchaguz mkuu wa Zanzibar uliofanyika 25th Oct 2015.
huu ni uchochezi sasa!! UTASKIA MUDA SI MREFU BALOZI KARUDISHWA KAO
 
Umafia wa CCM ndio utaliangamiza taifa sio CUF na CHADEMA, na hakuna anaefurahia nchi kuwkewa vikwazo bali ni CCM wenyewe ndio wanafurahia.
Lazima tujifunze kuwa huru, tujifunze kujitegemea. Hatuwezi kuburuzwa kwa silaha ya vikwazo vyao. US wenyewe mfumo wao umelalamikiwa, si wa kidemokrasia, watoe kwanza miboriti yao ndo waje kuviona vibanzi vyetu.

Si jambo la kushadadia hata kidogo, si kwakuwa tunanyimwa misaada, bali kwakuwa tunaoneshwa jinsi gani sisi bado si taifa. Ni kama ka State kao tu, watu labda hawazijui hizi njia.
Nijaribu kuwapa mwanga kidogo, ktk katiba kuu la UN kuhusu Human Rights, Decralation ya 48,haki ya mtu kusoma, kula, kuishi, kupata huduma nzuri za kijamii, si za msingi zaidi (a mere second generation of Human Rights) zidi ya haki ya kupiga kura, kuandamana, kuunda vyama vya siasa nk (first generation of Human Rights).
Hapa kwa mwenye kufikiri sana ataona uwalakini. Tz tunahitaji ustawi wa jamii na kamwe si demokrasia.
 
Tutaishi km korea kaskazini tena itatusaidia kukuza taaluma zetu wenyewe tuta komaa wenyewe kwenda mbele hadi kiieleweke na ndege tulizo agiza kwao tutasitisha
 
Hivi vikiwekwa vikwazo vya kiuchumi wanaoumia ni viongozi ama wananchi wa kawaida.
Kiuhalisia nchi yoyote ni ya wananchi lakini ujinga (upu.mba.vu na ulofa) ukitamalaki inageuka ya watawala.
Na watawala wengi ni waoga sana ndio maana wanatumia sana majeshi kujihakikishia uwepo wao lakini wanajua nguvu ya umma ni kubwa kuliko majeshi na umma husika sababu ya ujinga wao hauelewi na kuliamini hilo. Siku umma ukielevuka ndio mambo kama ya ndugu yako Yahya Jameh yanaanza.
Sasa basi Wamarekani wanafanya hivi wakijua wananchi wataumia huku wakiamini hayo 'maumivu' yatawaoungezea uelewa (na hasira) utakao pelekea kuwaadabisha watawala. Pia wanajua principle kubwa kabisa ya mabadiliko na maendeleo ni SACRIFICE, hivyo wanajua hii inamfanya mwananchi wa kawaida kupima maumivu anayoyapata kutokana na mienendo ya watawala against maumivu atakayoyapata kutokana na kudai haki yake! Umeelewa?
 
Umeandika kinazi...utakuwa ni CUF au CHADEMA...unafurahia Tanzania kuwekewa vikwazo...dah...Watanzania wengine bwana kazi ipo...haya endeleeni kuandika hivyo...tutaona mwisho wake utakuwaje...Lakini lililo wazi ni kuwa Maalim Seif hawezi kuwa Rais wa Zanzibar na haitatokea kuwa hivyo...

Mbona baba j anafurahia watz kuwa maskini na anaapa kabisa lazima aendelee kubana pesa ili tuishi kama mashetani , humshangai?
Nasisi tunasema bora hao wahisani watunyime misaada kama kufa tufe tu ili nchi iwashinde kuongoza watz wafunguke akili
 
Hivi jamani kila uongozi ni kweli unawekwa na mungu. Huu wa Tanzania nina mashaka sana
Hivi jamani kila uongozi ni kweli unawekwa na mungu. Huu wa Tanzania nina mashaka sana
Mkuu nani alikuambia kila utawala huwekwa na Mungu?
Hebu jiulize hapa chini.
1.Idd Amin aliwekwa na Mungu?
2.Bokassa(Central Africa) aliwekwa na Mungu?
3.Adolf Hitler aliwekwa na Mungu?
4.Mussolin (Italy) aliwekwa na Mungu?
5.Habre (Chad) aliwekwa na Mungu?
6.Sani Abacha (Nigeria) aliwekwa na Mungu?
7.Saddam Hussein aliwekwa na Mungu?
8.Mobutu Seseko aliwekwa na Mungu?
9.Charles Taylor (Liberia)aliwekwa na Mungu?
10.Ferdinand Marcos (Philippines) aliwekwa na Mungu?

Kuna tawala zinatoka Kwa Lucifa moja Kwa moja, maana hata Lucifa hujiita mungu.
 
Umeandika kinazi...utakuwa ni CUF au CHADEMA...unafurahia Tanzania kuwekewa vikwazo...dah...Watanzania wengine bwana kazi ipo...haya endeleeni kuandika hivyo...tutaona mwisho wake utakuwaje...Lakini lililo wazi ni kuwa Maalim Seif hawezi kuwa Rais wa Zanzibar na haitatokea kuwa hivyo...


Umeandika kinazi...utakuwa ni CCM au CUF Lipumba...unafurahia uporaji wa ushindi wa CUF Zanziabar walioufanya CCM? Wacha vikwazo viwekwe ..dah...Watanzania wengine bwana kazi ipo...haya endeleeni kuandika hivyo...tutaona mwisho wake utakuwaje...Lakini lililo wazi ni kuwa CCM haiwezi kutawala milele...
 
Umeandika kinazi...utakuwa ni CUF au CHADEMA...unafurahia Tanzania kuwekewa vikwazo...dah...Watanzania wengine bwana kazi ipo...haya endeleeni kuandika hivyo...tutaona mwisho wake utakuwaje...Lakini lililo wazi ni kuwa Maalim Seif hawezi kuwa Rais wa Zanzibar na haitatokea kuwa hivyo...
Bora waweke vikwazo labda tutakua na ya njaa chakula lakini tukawa na shibe ya demokrasia na kuepusha michafuko inayoweza kutokea kwa makijani kukutaa uamuzi kura kutumia majeshi kunyang'anya haki wa watanzania
 
Kumbe hamwajui wamarekani nyie.

As long as maslahi yao yanalindwa hapa Tz, hakuna kitu kama hicho.
 
Umeandika kinazi...utakuwa ni CUF au CHADEMA...unafurahia Tanzania kuwekewa vikwazo...dah...Watanzania wengine bwana kazi ipo...haya endeleeni kuandika hivyo...tutaona mwisho wake utakuwaje...Lakini lililo wazi ni kuwa Maalim Seif hawezi kuwa Rais wa Zanzibar na haitatokea kuwa hivyo...
kwa jinsi ulivyohitimisha andiko lako hata wewe umeandika kinazi.
 
Shein naona anahemea juujuu muda huu
 
Hata TETESI huwa zina source!! Haya mtandika viroba mchana tupe source za hizo tetesi zako koko.
 
na underson ndambo.

Taifa la Marekani linatarajia kushusha rungu la aina yake kwa serikali ya Tanzania kufuatia hali ya sintofahamu inayoendelea nchini kutokana na sakata la uchaguzi mkuu wa Zanzibar.
Habari zinadokeza kuwa taifa hilo kubwa duniani litaweka vikwazo vya kiuchumi kwa Tanzania hali itakayopelekea Tanzania kuandika historia nyingine mbaya mbele ya uso wa dunia.

Serikali ya Marekani tayari imezuia misaada mbalimbali kwa Tanzania na pia ndiyo iliyoshinikiza Tanzania kunyimwa fedha za MCC, pamoja na kuzishawishi nchi zengine. Serikali ya Tanzania ipo hatarini kukumbwa na janga la njaa, ikiendelea kupuuza juhudi za kimataifa kuitaka kuumaliza kwa haraka mgogoro wa Zanzibar unaofukuta kwa kuacha haki itendeke kabla ya Febr 2017.

Habari zinadokeza kuwa balozi wa Marekani nchini atatoa msimamo unaoelezwa kuwa 'mkali' ili kuishinikiza serikali ya Tanzania kuheshimu maamuzi ya wananchi kwenye uchaguz mkuu wa Zanzibar uliofanyika 25th Oct 2015.


Hata kama ni kweli, USA mpya inazaliwa Januari 20. D.Trump hataki huo ujinga!
 
Back
Top Bottom