Kuna ubaya kuuza nyumba ya urithi ili hali marehemu enzi za uhai wake alikataa

Hiyo nyumba msiuze, wosia uheshimike vinginevyo mtauza na hali itazidi kuwa mbaya.

Nna shuhuda zaidi ya tatu za waliokataa mali zao zisiuzwe lakini watoto na wajukuu wakauza, wote hakuna walichofanya cha maana na miji hawana wamebaki kuwa wafanya usafi kwenye maeneo waliyouza.
 
Ushindwe hesabu za kutafuta Mali zako,uweze hesabu ya kuuza jasho la marehemu, sio rahisi kutoboa
Acha ujinga wako, binadamu wanazaliana, kizazi kinapanuka, maisha yanabadilika, hakuna cha milele, Amini kuna wakati hata kaburi lako halitajulikana lipo wapi kwa vitukuu vyako! Life's goes on, soon we shall be forgotten!, hatuko milele!, hata wao hawako milele hata wale hawako milele, mwaka 1500, kulikuwa na watu kama sisi walikuwa na majumba makubwa, Babylon ilikuwa ni sehemu nzuri ajabu sana, ukiiona leo hii utastaajabu sana!
 
Baba ana watoto wa nne, amewaachia nyummba ya urithi watoto wake.
Hawa watoto nao wamekua na wanafamilia zao.
Je, warithi woto wanne wanaweza kurithisha wayoto wao hiyo nyumba moja?
 
I personal practise this exercise and am OK!, ni mwaka wa 20 sasa!,
Warning :-""ASSETS GOES TO ASSET, NEVER TRADE WITH THAT MONEY!, USE PRODUCT OF AN ASSET!.... ""
Mkuu apo ukiangalia mwaka ulio fanya hiyo practice its 20 yrs, dunia ya kipindi kile si sawa na hii ya ushindani wa kuwindana sasahivi tupo katika vita ya uchumi kubwa zaidi.
 
Baba ana watoto wa nne, amewaachia nyummba ya urithi watoto wake.
Hawa watoto nao wamekua na wanafamilia zao.
Je, warithi woto wanne wanaweza kuriyhisha wayoto wao hiyo nyumba moja?
Hapo ndipo panapilazimisha asset ziuzwe.... Unless vurugu, although ktk familia wapo ambao watajaaliwa!
 
Mkuu apo ukiangalia mwaka ulio fanya hiyo practice its 20 yrs, dunia ya kipindi kile si sawa na hii ya ushindani wa kuwindana sasahivi tupo katika vita ya uchumi kubwa zaidi.
Mkuu wakati huu ndiyo wenye advantage zaidi, ila elewa, wakati unaitoa asset, maadui huwa wapo karibu sana na lengo ni UKWISHE, UPOTEE. UTOKE KWENYE RAMANI, UWE ZERO!, WAKUCHEKE, ndiyo mitego hukabili watu wengi, na kwa nguvu kali za giza zinazotupwa endapo haupo makini lazima utapotea!
 
Hata asingesema, kwa kutumia akili tu sio busara kuuza nyumba za urithi.
Ni kutafutiana lawama na maugomvi yasiyoisha.
Pesa usiyoitolea jasho kuitumia hovyo huwa ni rahisi sana, kama wako wengi ndo kabisaa lazima kuna wanaoishi hapo wanategemea wauze wakapange.
Kodi zikiwashinda wataanza kutafuta mchawi nani au nani alipiga pesa ndefu ya mirathi achukiwe na kuzushiwa utapeli.
Kibongobongo wasiuze.
 
Ili hao ndugu waepuke lawama waweke aibu pembeni tu maisha hayahitaji millions of capital ili wafanikiwe as u said apo ukiwa na kitu tu ndo unaongeza maadaui sasa kwa bahati mbaya kitu chenyewe kimepatikana kwa njia ya kuuza mahali za marehemu aisee balaa lake mkuu utatamani marehemu afufuke we ndo ufe.
 
Msingi mkuu upo kwenye, how they program them selves.
 
Kukaa na mali ya urithi mkiwa wengi ndiyo kutafuta ugomvi. Bora muuze kila mtu afe na chake.
 
Kukaa na mali ya urithi mkiwa wengi ndiyo kutafuta ugomvi. Bora muuze kila mtu afe na chake.
Hii kila mtu afe na chake imeangamiza familia nyingi sana, na sio mpango bora, fanyeni kampuni za asset na mali zisizohamishika!, na kila memba kuwa na nyumba bora inakuwa ndiyo msingi mkuu!
 
Unadhani wajukuu zako watakuwa wangapi?
Wataelewana?
Kwa kawaida mali hasa nyumba za urithi ni changamoto sana. huwa zinaleta mpasuko kwa ndg kufikia hadi kuuwana
Ni bora wauze
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…