Kuna ulazima hayo mashindano ya Quran yafanyike Mkapa Stadium? Siku ya mchezo Simba vs Orlando!?

Kuna ulazima hayo mashindano ya Quran yafanyike Mkapa Stadium? Siku ya mchezo Simba vs Orlando!?

11 April 2022

CAF, TFF, SIMBA, ALHIKIMA WOTE WAKUBALIANA MASHINDANO YA QURAN NA MPIRA VITAFANYIKA SIKU MOJA TAREHE 17 APRIL 2022




MECHI ya kwanza ya Robo Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika baina ya wenyeji, Simba SC na Orlando Pirates ya Afrika Kusini itafanyika sambamba na mashindano ya Quran Jumapili ijayo.

Hayo yamesemwa na Meneja Habari na Mawasiliano wa klabu ya Simba, Ahmed Ally katika mkutano wake na Waandishi wa Habari jana Jijini Dar es Salaam.

“Maswali yamekuwa mengi kuhusu Uwanja wa Mkapa sababu siku ya mchezo dhidi ya Orlando Pirates kutakuwa na mashindano makubwa ya Quran, na inafahamika kwamba uwanja unatakiwa kuwa wazi kwa masaa 72 kabla ya mchezo,”.


“Baada ya mazungumzo baina ya Simba, CAF, TFF na waandaaji wa mashindano ya Quran tumekubaliana matukio yote yatafanyika ndani ya siku hiyo moja na CAF wamebariki hilo,” amesema Ahmed Ally.

Mechi hiyo inatarajiwa kuanza Saa 1:00 usiku.


Safi sana,,,nawasubiri wagalatia ambao hawakupenda iwe hivyo
 
Msemaji wa Simba aliulizwa Kama ikitokea mtu akigoma kotoka ili aangalie mpira mtafanyaje? Hakuwa na jibu la moja kwa moja akasema wanaweza wakafanya namna ili aangalie mpira tu bure

Sasa wanangu wa dar Kama wameskia yale mahojiano hapo wanaingia asbh hii kwenye mashindano ya quiran hlf hawatoki
 
Msemaji wa Simba aliulizwa Kama ikitokea mtu akigoma kotoka ili aangalie mpira mtafanyaje? Hakuwa na jibu la moja kwa moja akasema wanaweza wakafanya namna ili aangalie mpira tu bure

Sasa wanangu wa dar Kama wameskia yale mahojiano hapo wanaingia asbh hii kwenye mashindano ya quiran hlf hawatoki
Watatoka tu usijali
 
Tunajua sote jinsi mchezo huu ulivyo muhimu kwa Simba na Taifa kwa ujumla, ndio wa kwanza katika historia ya Nchi yetu kutumia teknolojia ya usaidizi wa Video kwa Mwamuzi (VAR).

Zaidi ya hayo Sheria za CAF zinataka uwanja kuwa wazi angalau saa 72 kabla ya mchezo.

Pamoja na kwamba Wanasema saa 7 kamili hao washindani wa Quran watatolewa kwa usaidizi wa Polisi...

Lakini naona kabisa hapa kuna lawama zinaenda kutengenezwa sisi Waswahili tunajijua katika kutunza muda.

Lakini vipi kama mtu akaingia then akagoma kutoka ili aangalie mechi?

Lakini vipi kama hayo mashindano yakachelewa kwisha baada ya saa 7?

Ndio maana nauliza kuna ulazima haya mashindano kufanyika Lupaso?

N.B
Sina nia ya kukashifu Dini ya mtu.

Zaidi soma hapa..

Sheikh umeona waislam walivyoujaza uwanja?
 
Msemaji wa Simba aliulizwa Kama ikitokea mtu akigoma kotoka ili aangalie mpira mtafanyaje? Hakuwa na jibu la moja kwa moja akasema wanaweza wakafanya namna ili aangalie mpira tu bure

Sasa wanangu wa dar Kama wameskia yale mahojiano hapo wanaingia asbh hii kwenye mashindano ya quiran hlf hawatoki
Hio ni siasa, atapigwa mtu mpka achakae
 
Udini utakuua

Wewe na wenzio ndio wadini,,,,tokea ramadhani ianze ni mwendo wa kutushambulia

وَلَنْ تَرْضَىٰ عَنْكَ الْيَهُودُ وَلَا النَّصَارَىٰ حَتَّىٰ تَتَّبِعَ مِلَّتَهُمْ ۗ قُلْ إِنَّ هُدَى اللَّهِ هُوَ الْهُدَىٰ ۗ وَلَئِنِ اتَّبَعْتَ أَهْوَاءَهُمْ بَعْدَ الَّذِي جَاءَكَ مِنَ الْعِلْمِ ۙ مَا لَكَ مِنَ اللَّهِ مِنْ وَلِيٍّ وَلَا نَصِيرٍ
Mayahudi hawawi radhi nawe, wala Wakristo, mpaka ufuate mila yao. Sema: Hakika uwongofu wa Mwenyezi Mungu ndio uwongofu. Na kama ukifuata matamanio yao baada ya ujuzi ulio kwisha kujia, hutapata mlinzi wala msaidizi kwa Mwenyezi Mungu.
 
Nadhani mashindano yameisha salama na Waislamu wamekuwa wastarabu Kabisa kutoka..
Inshallah hakuna usumbufu utatokea
 
Back
Top Bottom