Kuna uwezekano Watanzania tuna tatizo la uelewa? Nikimsikiliza Polepole, namuona Mwl. Nyerere. Nyie msiomuelewa Polepole, je Nyerere mngemuelewa?

Enzi zake aliruhusu watu waongee tuanzie hapo
 
Mkuu Paskali, nadhani pia unakumbuka hotuba ya mwalimu kuhusu mala.ya wa kisiasa, Kosa la Polepole kwangu mimi ni hilo. Namuona kama ma.laya wa kisiasa tu, na siwez mfananisha na mwalimu Hata kidogo. Hebu tizama misimamo ya Polepole wakati wa madai ya katiba mpya /bunge la katiba then angalia misimamo yake akiwa msemaji wa chama…u will definitely see two different personalities in one person. Na hili ndilo mwalimu alikemea na kusema ni umalaya wa kisiasa, huna misimamo.
 
Wewe pasikali nyamaza aisee..kiroboto wakati nyumba za ndugu zetu zinabomolewa makusudi kabisa, na za wasukumu zikaamriwa zisiguswe, kitoboto ndo alikuwa injinia wa hayo maamuzi(sera). Maovu ni mengi tumetendewa.. nyamaza mzee, mioyo yetu inavuja damu kwa matendo maovu mengi tuliyotendewa nao. Familia zetu zimeteseka kwa maovu mengi..Tulia au na wewe ulikuwa sehemu ya genge lililotutesa na kutudhalilisha?
Polepole wa nyakati za katiba kurudi chini anaeleweka lakin huyu wa mavieite ya dikteta ni shetani kabisa kama mashetani mengine yote..kiroboto
 
Pascal Mayalla bora umeongea na wewe. Nazani sasa watu wataanza kuelewa vizuri.

Kuna watu wanahisi Polepole anakwamisha mambo..lakini ukweli ndio huo ulioandika.

Safi Sana.
Hakwamishi chochote ila sio busara kuzarau maamuzi ya wengine
Wakati wake ukisema unajikuta jera au tunakuokota
 
Holi ndio jambo la kupima integrity
Mlema alishindwa na Mkapa
Nyerere hakuingilia kuharibu uchaguzi
 
Holi ndio jambo la kupima integrity
Mlema alishindwa na Mkapa
Nyerere hakuingilia kuharibu uchaguzi
Kama kweli alikua mpigania haki angesimama wakati wa dhoruba sio wakati wa hali kama sasa
 
Kitendo cha watu kuchangia katika nyuzi zako kinathibitisha kuwa ni kweli Watanzania wana matatizo ya uelewa.

Kwa upuuzi huu ambao huwa unaandika hukupaswa kupata mchangiaji hata mmoja.Ulipaswa upuuzwe.Watu wanashindwa kukupuuza kwa sababu wana matatizo ya uelewa.
 
Tayari polepole kafananishwa na Nyerere 🤣ila nyie watu nyie!! Mnazidi kumdharaulisha sana Mwalimu. Ni washauri tu tafuteni watu wengine wa kuwafananisha mbona wapo weng sana? Kina Augustine M, na wengine.
 
yani wewe kichwa kimoja unapoanza kuhisi watanzania zaidi ya 40m wana tatizo la uelewa jua kuwa wewe ni tatizo zaidi yao.

nimeishia kwenye heading tu.
 
Yan mtu ambaye juzi tu hapa alikuwa injinia wa biadhara chafu ya kununua vijana wa kitanzania, akitumia kodi zetu tunazozitoa kwa jasho jingi, lengo ili aue demokrasia na uhuru wa nchi hii, leo analilia demekrasia na uhuru!! Huu si ukasuku? Unamlinganisha Mwalimu wa nchi hii na kiroboto?!! Hiv mwalimu angeweza kutumia pesa za walipa kodi kuwanunua wanasiasa?!!!! Wewe pasikali wewe?!!!!
 
umenena vyema sana juu ya huyu mtu
 
Huyu Polepole ambaye leo anaona TCRA inaingilia uhuru wake ndiye huyo huyo Polepole ambaye aliwaambia TCRA wafanye kazi yao kwa anayemsumbua mnyoosha nchi. Ilifikia hatua Polepole aliona ni dhambi kubwa sana kumkosoa Magufuli. Au Paskali umesahau? Huyo Nyerere unayemfananisha naye ni wa mchongo!
 
Wasukuma mmeamu moja, ngoja tuone
 
Pascal Mayalla

Hakuna CCM yoyote wa sasa mwenye kufanana mitizamo ama mawazo na Mwl Nyerere, hakika hakuna...

Huyu Polepole ndani tu ya miaka kama minane au kenda hivi, ameweza kuwa na kama rangi tatu tofauti, mosi rangi ya bunge la katiba; mbili, rangi ya serikali ya JPM; tatu, rangi ya sasa isiyo na jina bado...

Huyu Polepole ndio wa kutuhubiria sasa kwamba watu waachwe waongee kwa kuwa uhuru wa kutoa mawazo kila mwenye mdomo anao!! Huyu si alikuwa ni sehemu ya serikali iliyowaziba midomo wapinzani huyu???
 
Hata yule aliyeongea pale uwanjani siku ya kumbukumbu ya Uhuru mbona Ni nyerere kabisa. Issue siyo unyerere issue ni kuongea kutaka cheo na kutokuwa na msimamo. Nyerere alikuwa na msimamo. Polepole huyu anabadilika badilika kutokana na upepo. Muangalie wakati wa Katiba mpya na Sasa.

Pili polepole kwa kushirikiana na jom wameua watu wengi mpaka wengine walikuwa wanaokotwa kwenye viloba.

Polepole huyuhuyu alikuwa anavizuia na kuvipiga mkwara vyombo vya habari Kama tv au redio kutorusha habari zozote za chadema wakati wa uchaguzi.

Ni polepole huyuhuyu ambaye chadema walikuwa na mkutano pale mlimani city akawapiga mkwara Sana azam tv wasirushe wlakati tayari walikuwa wamejiandaa kwa Hilo halafu yeye Leo ameachwa aongee upumbafu wake. Amshukuru mungu tu tumempata rais wa haki asiyependa torture Kama jpm wa kisukuma na Nina wasiwasi Ni we ni mshamba wa kisukuma.

Siku nyingine ukitaka kuandika use unatumia akiri kidogo siyo kuendeshwa na ushabiki wa siku moja. Msomi anachambua kwa umakini Sana Mana kila neno philosophically lin maana. Jifunze kutoka kwa ask. Bagonza namna ya kupresent issues. Nayo mutama!!!!
 
Nyerere alipinga sana ukigeugeu yeye aliuita UMALAYA, kwaiyo nyerere alikua Malaya wa kisiasa kama polepole? maana Polepole wa tume ya warioba ni tofauti na polepole akiwa katibu mwenezi wa ccm ya mwendazake na huyu polepole wa shule ya uongozi. Yaani hawa Polepole watatu siku wakikutana itakua vita.

Nyerere alikua tayari kuwajibika kwa misimamo, mitazamo na Imani yake,Je polepole ana hizo sifa? zaidi namuona ni mganga njaa, anaangalia upepo ili apate mwendo wa kisiasa kwa maslahi take binafsi na watu wanaomtuma. Polepole hakuwahi kuisemea Katiba mpya wakati akiwa high table labda ni asili ya wanaccm kuwa na unafiki pale wanapokuwa wanafaidika na mfumo.
kiujumla kumfananisha Polepole na Nyerere sio sawa kabisa Polepole hata ndani ya chama ni mtu mdogo sana kufikia kumfananisha na yule mzee labda polepole umfananishe na kina Esta Bulaya au Halima Mdee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…