Kuna viashiria vikubwa vya uvunjifu wa amani siku zijazo…

Kuna viashiria vikubwa vya uvunjifu wa amani siku zijazo…

Ndugu wajumbe,

Natumia nafasi hii kama raia mtiifu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania kuwaandikieni nyinyi ikiwa ni sehemu ya wajibu wangu wa kiraia na wa kikatiba (1) Mosi kulinda amani ya nchi (2) Pili Kutoa maoni ya kuleta usitawi kwa nchi yangu (3) kutumia haki yangu ya kikatiba kutoa maoni.

Nawaandikieni barua kwa sababu zifuatazo

1. Kuna viashira na kila dalili kuwa wananchi sasa wameanza kuzungumza lugha ambazo miaka michache iliyopita walikuwa wanajicensor wenyewe, au wanazuiana wenyewe kuzitumia wakiwa wanaona kuwa kulinda amani ni jukumu lao kwa mfano

a) Napitia mitandaoni sana, nasoma comment za watu sana, na kusikiliza sauti zao sana. Zimeanza kuwepo dalili watu kuanza kuzungumza zungumza habari za kutamani mapinduzu ya kijeshi nchini. Watu hawa wanatoa sababu eti, mifumo ya kawaida ya kuendesha nchi imefeli kwenye Checks and balances, wanasema Mahakama, Bunge na serikali vimefunga ndoa haramu na hivyo ni kupoteza muda kutegemea mahakama kusimamia haki pindi kunapokuwepo mgogoro baina ya wananchi na serikali yao au hata bunge lao. Na wanasema kuwa Bunge haliwezi kuizuia serikali kufanya udhalimu dhidi ya wananchi, wanatolea mifano vitendo vya kutisha vya uonevu wa raia dhidi ya wananchi katika hifadhi kama huko Umasaini Ngorongoro, utwaaji wa ardhi Mbarali, Operesheni za kuharibu mali za raia kwa jina la kupanga miji vizuri ( operesheni dhidi ya wamachinga) n.k

2. Wananchi wameanza kuonyesha Dalili za kuona Bunge, Mahakama na serikali si vyombo vyao tena bali ni vya kikundi cha watu wachache wenye masilahi yao.
Wananchi mitandaoni wanasema wazi kuwa Namna Serikali ilivyolithibiti bunge, mfano mzuri kitendo cha Spika wa bunge kuondolewa kwa sababu ya kutoa maoni yake, Na namna Spika wa sasa anavyoliendesha bunge utadhani ni idara tiifu ya mhimili wa Executive( serikali), kwamba yuko tayari kufanya lolote serikali isiwajibishwe bungeni na kwamba amejigeuza kuwa mwanasheria mkuu wa serikali bungeni badala ya kufanya kazi za uspika. Kunawafanya wananchi wengi niliofuatilia michango yao waone kuwa bunge hili si lao bali ni bunge la serikali hususan chama cha Mapinduzi.

Kwa upande wa mahakama, wananchi wanasema, Kitendo cha kuwepo kwa Jaji Mkuu kinyume cha katiba, Na kauli ya Jaji huyo kutamka kuwa "Mahakama ikifanya hukumu iangalie na mihimili mingine inataka nini", badala ya kwamba mahakama iangalie sheria za nchi zinataka nini, nayo pia imepelekea wananchi wengi ninaowasoma kukosa imani kwa mhimili wa mahakama.
Lakini pia ukizingatia na aina ya mashauri na namna mashauri hayo yalivyoendeshwa mahakamani ikiwemo Kesi ya Ugaidi ya Mbowe, Jinsi majaji walivyokuwa wakibadilishwa bila sababu za kuonyesha mashiko za ubadilishwaji mbele ya raia na Jaji mwingine kupandishwa cheo wakati shauri likiendelea. Kimsingi mambo haya yanaondoa imani katika mfumo wa serikali na mahakama.
Lakini pia ongezeko la Mahakama kukwepa wajibu wake wa kutoa haki nchini kwa kutumia mtindo wa "Kutupa kesi za msingi na za haki muhimu za wananchi kirahisirahisi tu based on technicalities". Haya mambo yamepelekea imani ya wananchi kupungua sana kwa mifumo ya kawaida ya kuongoza nchi.

3. Uchaguzi wa mwaka 2019 na 2020 umeacha donda kwa wananchi.

Watu mitandaoni na mitaani hawana imani kuwa wanaweza kuweka serikali waitakayo madarakani kwa Sanduku la kura. Tena hili ni jambo la muhimu sana la kuzingatia. Wananchi wanasema kwamba, kwa mujibu wa katiba hii ya sasa jinsi ilivyo na tume hii jinsi ilivyo, Ni rahisi kuwa abused na wenye madaraka kuminya haki za uchaguzi wa wananchi, wanasema tume inayoteuliwa na mshindani wa wengine katika uchaguzi itakataje mkono ulioipa ulaji?, Sheria zinazokataa matokeo ya urais kupingwa mahakamani, wakitangaza mshindi ambaye si halali then kura zina thamani gani?, Kwamba Ukivuruga uchaguzi halafu una kinga ya kisheria ya kutoshitakiwa kwa hayo unayoyafanya, sasa Uchaguzi una faida gani. Watu wanatoa maoni hayo

4. Wananchi wanalalamikia mnyororo wa kulindana na kutoa nafasi ya watu kuabuse mamlaka.

Ndugu, Wajumbe kwa kadri nilivyofuatilia comments za watu mitandaoni, na katika mazungumzo ya wananchi katika vijiwe vya kahawa. Wananchi wanahoji hii kinga ya Kutoshitakiwa mahakamani ya Jaji Mkuu, Spika, Naibu Spika, Waziri Mkuu na Makamu wa Rais ya nini?, na Ililenga nini?- Kwa upande wa rais angalau pamoja na kwamba na yenyewe ina shida kwa baadhi ya makosa ikiwemo kwa mfano haki za binadamu za wananchi lakini angalau kwa yale makosa aliyoyatenda huku akitimiza wajibu wake anavumilika kutokana na uzito wa ofisi yake kama mkuu wa nchi. Je hawa wengine nao Kinga ya kutoshitakiwa ya nini?.
Ndugu Wajumbe jambo hili nalo wananchi wanasema ni miongoni mwa mambo yanayopelekeana kulindana kwa mifumo na hivyo kuondoa uwezekano wa wananchi kuheshimiwa na mfumo, ndiyo maana baadhi yao wanazungumzazungumza habari za kuondoa mfumo kwa kutumia nguvu.

5. Imeanza kuwepo minong'ono ya malipizi ya visasi.

Katika pitia yangu mitandaoni, ile ya maandishi na Sauti. Nimeanza kusikia habari za watu kushauriana na kukubaliana kuanza kutumia njia za malipizi ya visasi kwa matendo yanayofanywa na jeshi la polisi.
Watu sasa wameanza kuzungumza habari za "Polisi mnajua wanapokaa mnashindwaje kudeal nao mmojammoja" , "Mnashindwaje magari ya wabunge na mawaziri kuyatia moto", "Tit-for-tat is a fair game". Hizi kauli zimeanza kuwa ni hoja za kushauriana namna ya kudeal na hicho ambacho wanasema ni kudeal na injustice.

6. Kibaya zaidi watu sasa wameanza kuzungumza kuhusu kudeal na viongozi na familia zao.

Ndugu wajumbe wa Baraza la Usalama, hii nukta ninayoizungumza hapa ni muhimu mkaizingatia sana kwa sababu athari zake ni kubwa mno. Katika kusikiliza na kusoma mitandaoni, Watu wameanza kuzungumza na kushauriana kuwa. Maadamu Bunge halipo nao, Maadamu Mahakama haipo nao, Maadamu serikali haiwasikilizi basi njia ya kudeal na watu wenye maamuzi ni kuwapelekea maumivu ili ama wastuke, au wajute au ama watende haki wanayoitaka. Miaka iliyopita, suggestions za hivi zilikuwa zinakataliwa mara moja na wachangiaji wa mada wao wenyewe kwa wenyewe, lakini sasa inaonyesha kuwa thinking ya hivyo imeanza kupenya katika kukubaliana baina ya watu wafanyao mijadala hiyo. Hii ni hatari kubwa sana, Ipo haja ya kulifanyia kazi.

7. Wananchi wameanza kuzungumza kwa sauti za kuukataa muungano, na kudai serikall ya Tanganyika.

Watu kuitaka serikali ya Tanganyika siyo tatizo, lakini Sauti hizi zimeanza kuwa nyingi sana. Na hili limeanza kutokea baada ya watu kuanza kufunguka macho zaidi juu ya muundo wa muungano ambao umekaa kiuzungumkutiuzungumkuti. Watu wanazungumzia muundo wa muungano ambao Katiba za Zanzibar na ya Muungano zinapingans waziwazi kstika issues kadha wa kadha lakini watu wamefukia vichwa vyao udongoni kama mbuni. Watu wanazungumzia kuwa inakuwaje Wazanzibar wawe na Sauti ya kimaamuzi kwenye mambo ya Tanganyika yasiyo ya muungano, wakati Hakuna Mtanganyika anayeweza kuwa na Sauti kwenye mambo ya Zanzibar yasiyo ya muungano. Na pia watu kutoka Zanzibar wanalalamika juu ya Tanfanyika kuvaa koti la muungano.

Ushauri wangu kwa Baraza la Usalama

1. Likae chini lijadili kwa kina na lichukue hatua za kudeal na manung'uniko ya wananchi namna nchi yao inavyoongozwa. Mifumo ya Serikali , Bunge na Mahakama viache "Ushosti". Kila kimoja kifanye kazi kwa uhuru na kwa haki na si kulindana kisiasa

2. Zinahitajika reforms nchini za kuongeza nguvu zaidi kwa wananchi, haki zaidi kwa wananchi,kuweka accountability kwa viongozi na kuondoa impunity ambayo baadhi ya sheria zimewapa watu.

3. Chaguzi ni jambo Sacred katika nchi, Ukiiba kura, au kuchezea chaguzi unazalisha bunge lisilojiamini, unazalisha executive dmbayo haisikilizi raia maana siyo walioiweka madarakani, na hapa lazima migongano mbeleni itokee

4. Baraza lisidharau "Lone actors". Pengine inaweza kudhania kuwa ni rahisi kuthibiti vikundi vyenye kubeba silaha vya watu wengiwengi kwa kutumia taarifa za Intelijensia iliyojisimika ktk society yetu. Lakini Baraza lijue kuwa ni vigumu kudeal na mtu mmojammoja mwenye dhamira yake, aliyeamua kuifanyia mazoezi yeye mwenyewe ili aitekeleze yeye mwenyewe bila kuhusisha "wengi".
Na njia mojawapo ni kuondoa hizi dissatisfactions nyingi miongoni mwa raia.

5. Baraza liishauri serikali iache kamatakamata hizi zisizo na tija, iache hizi bambikizia kesi zisizo na tija. Hivi vitu vinachochea hasira, na vinasaidia kuwafanya watu waamini kuwa njia pekee ya kudeal na watu wa mifumo ni violence ya tit-for-tat

Kwa mapenzi mema ya Taifa langu, na kwa kutimiza wajibu wangu nawasilisha.

Mwenye masikio na asikie!
1. Mbona umekwepa kuwataja TISS kupewa kinga zaidi dhidi ya vitendo vya jinai wanavyotenda wakiwa kazini..kinga za namna hii hazina afya kabisa kwa jamii inayotaka kustaarabika..
2. Umekwepa pia tatizo la UDINI lipo wazi kwa sasa, watu wanatetea MABAYA vile tu yamefanywa na mtu wa IMANI yao..unafiki wa aina hii una madhara mabaya tena ya haraka!
3. Sijajua kama hilo baraza la usalama huwa linasubiri kuamshwa pale mambo yanapoashiria mwelekeo wa hali ya hatari..inawezekana baraza nalo lina upande, kwa watawala au kwa wananchi.
4. Maelezo yako ni kama uko kati pamoja na kueleza viashiria vya hatari inayokuja kwa taifa..ni vyema hata hivyo kuwaeleza watawala kuwa WAACHE hayo wanayofanya katiba iko wazi kwenye ibara ya 8 MAMLAKA YOYOTE ILIYOPO INATOKANA NA WANANCHI..wao ndiyo mamlaka ya kuamua hatma yao wenyewe, kama jambo wamelikataa unashupaza shingo kwa nini? Waache na si kuwaambia wafanyie kazi!
 
1. Mbona umekwepa kuwataja TISS kupewa kinga zaidi dhidi ya vitendo vya jinai wanavyotenda wakiwa kazini..kinga za namna hii hazina afya kabisa kwa jamii inayotaka kustaarabika..
2. Umekwepa pia tatizo la UDINI lipo wazi kwa sasa, watu wanatetea MABAYA vile tu yamefanywa na mtu wa IMANI yao..unafiki wa aina hii una madhara mabaya tena ya haraka!
3. Sijajua kama hilo baraza la usalama huwa linasubiri kuamshwa pale mambo yanapoashiria mwelekeo wa hali ya hatari..inawezekana baraza nalo lina upande, kwa watawala au kwa wananchi.
4. Maelezo yako ni kama uko kati pamoja na kueleza viashiria vya hatari inayokuja kwa taifa..ni vyema hata hivyo kuwaeleza watawala kuwa WAACHE hayo wanayofanya katiba iko wazi kwenye ibara ya 8 MAMLAKA YOYOTE ILIYOPO INATOKANA NA WANANCHI..wao ndiyo mamlaka ya kuamua hatma yao wenyewe, kama jambo wamelikataa unashupaza shingo kwa nini? Waache na si kuwaambia wafanyie kazi!
Umeongezea nukta muhimu sana. Haya mambo pia yafaa kuzingatiwa.
 
Ningekuwa moderator ningeku BAN life kabisa hapa JF. Watu ka ninyi sijui kwa nini mlizaliwa. Muacheni Mama afanye kazi kwa ajili ya maendeleo ya watanzania. Bila CCM hakuna amani, ndiyo maana tunaendelea kushinda chaguzi zote.
Exactly
 
Wananchi wapo busy na shughuli za maendeleo hako kakikundi kanakopinga maamuzi ya serikali ni wana chadema wanafuta mileage ya kisiasa. Baraza la usalama la Taifa siyo chombo kidogo kudil na vitu vya kipuuzi hivi.
 
Huu ndiop ukweli, na ndio maneno yanayozungumzwa waziwazi hadi vijijini!
Na tatizo kubwa ni rushwa, ufisadi na wizi unaofanywa na watawala!
Inafikirisha: matumizi makubwa ya kuendesha SERIKALI yangu mimi na wewe, ... YETU ... sisi WATANGANYIKA!
ANASA inakua kipaumbele na mbadala wa KUFANYIA kazi viapo vile na kujikita kwenye ANASA hadi ubongo unanenepeana. Haijalishi SISI tunaendelea kuzidiwa na UFUKARA ule ule ... kule ulikotokea wewe KIONGOZI mwizi, FISADI mla rushwa wewe! Leohii baada ya kujaaliwa madaraka unaona saizi yako ni ANASA. Amin nasema, LAANA inakuhusu wewe na vizazi. Karma is a bad assed bitch!
 
Mimi siyo Mkatoliki, lakini naona dhahiri kabisa kwamba kumekuwa na mvutano mkubwa ambapo wasomi wengi wa kiislamu wanafurahia hicho kinachofanyika kwasababu wanadhani wanawakomoa Wakatoliki. Imefikia hadi wengine kusema mbona wakatoliki wanapiga kelele kuhusu mkataba wa DP-WORLD ilhali wao wamesaini Memoranda of Understanding (MoU) na serikali kwenye masuala ya elimu na afya.

Kihistoria, Tanzania ni nchi inayoongozwa kwa kupitia muafaka (Compromise) baina hizi dini kubwa mbili hapa nchini. Ili mambo yaende vizuri nchini ni lazima mzani ukae sawa (The Scale has to balance/Balance of Power). Upande mmoja wa mzani ukionesha unataka kuzidi mwingine tunaishia kupata matatizo makubwa. Changamoto ya hatari zaidi ni kwamba Tanzania ina uzoefu wa kupambana na ukabila, ila siyo udini katika kiwango kikubwa hivi.

Wafuasi wa dini hizi kubwa mbili (Waislamu + Wakristo) hapa nchini wako kwenye kada zote nyeti ndani ya hili taifa na wote wameshatoa hadi maraisi zaidi ya mara moja. Ikionesha kwamba upande mmoja unamwaga ugali mwingine utamwaga mboga. Kiuhalisia tulipofika sidhani kama nchi itakuja kurudi kuwa na ule umoja na kuvumiliana kama zamani (National Cohesion & Tolerance). Hili linaloendelea hapa nchini lilitokea nchini Singapore na linawagharimu hadi leo:

Singapore kuna jamii aina tatu zenye dini zao. Wachina ambao ni wengi ni Buddhists, Wahindi wanaofuatia ni Hindus, na Wamalay ambao ni wachache zaidi ni Muslims. Hizi jamii zilishindwa kuvumiliana kabisa utawala wa Lee Kuan Yew unapoanza, hasahasa Muslims waliwahi kusababisha maandamano makubwa nchini hadi kupelekea nchi kutaka kuanguka. Alikuwa akiingia kiongozi wa Kihindi basi Wachina na Wamalay wanaanza kulalamika na kuleta taharuki za dini na kikabila kwamba wanaonewa.

Mwishowe kabisa Lee-Kuan-Yew kuokoa nchi akaamua kwenda kutafuta watu wa vyombo vya usalama kama polisi kutoka nchi nyingine. Mpaka leo hii nayozungumza Singapore inatumia polisi kutoka nchi ya Nepal waitwao The Ghurkas Regiment. Wangetumia polisi wa nchini kwao na ikatokea polisi wa kichina kamuua muhindi basi matatizo yataanza upya. Leo hii nchini Singapore ukifanya kosa huwezi kuachwa wala kusamehewa. Baada ya huu mkakati kuna watu walijaribu na walikiona cha mtema kuni.

Ukiangalia nje, unaweza kusema Singapore ina maendeleo makubwa kiuchumi, lakini ule upendo wa mtu wa jamii moja au dini nyingine kucheka na mwingine haupo kabisa. Wananchi wameungana kwasababu ya maslahi ya pamoja kiuchumi, ila siyo upendo wa kitaifa. Leo hii Singapore ikifilisika au kukosa uchumi ambao unawaunganisha hawa watu, ni lazima kuchafuke.

Mwalimu Nyerere aliwahi kulizungumzia hili la Singapore miaka ya 90's mwanzoni akihojiwa na vyombo vya habari vya Marekani. Akasema mbali na umasikini wetu ila sisi watanzania tunapendana sana na tunaelewana. Ila leo hii tumeruhusu Bandari imetuvuruga kiasi ambacho tumeyaamsha mambo ambayo yalikuwa yamelala kwa muda mrefu. Hivi kweli uwekezaji wa Bandari ni muhimu kuliko amani ya nchi, ??? Kuna wale ambao wanasema NDIYO...

NB 1: Ila tatizo kubwa zaidi ni vyombo vya dola kuamini kwamba tatizo lolote likitokea nchini basi litaishia humu-humu ndani ya mipaka na watalimaliza. Hili tatizo la bandari halijaanzia Tanzania na kuna wasiwasi wa wahusika wengine kutoka nje ya Tanzania kuhusika na huu mgogoro kwa namna moja ya nyingine. Mambo ni mabaya sana....

 
Acha upuuzi wewe,nyie wachochezi ndio mnatakiwa kushughulikiwa.

Hiyo lugha Huwa unasikia wewe tuu? Mbona Mimi sijawahi sikia wakiongea?

Serikali msiwakalie kimya watu dizaini ya huyu mtoa mada.

Pengine “umeziba masikio”.

Au unasikia tu kile unachopenda sikia.
 
Ndugu wajumbe,

Natumia nafasi hii kama raia mtiifu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania kuwaandikieni nyinyi ikiwa ni sehemu ya wajibu wangu wa kiraia na wa kikatiba (1) Mosi kulinda amani ya nchi (2) Pili Kutoa maoni ya kuleta usitawi kwa nchi yangu (3) kutumia haki yangu ya kikatiba kutoa maoni.

Nawaandikieni barua kwa sababu zifuatazo

1. Kuna viashira na kila dalili kuwa wananchi sasa wameanza kuzungumza lugha ambazo miaka michache iliyopita walikuwa wanajicensor wenyewe, au wanazuiana wenyewe kuzitumia wakiwa wanaona kuwa kulinda amani ni jukumu lao kwa mfano

a) Napitia mitandaoni sana, nasoma comment za watu sana, na kusikiliza sauti zao sana. Zimeanza kuwepo dalili watu kuanza kuzungumza zungumza habari za kutamani mapinduzu ya kijeshi nchini. Watu hawa wanatoa sababu eti, mifumo ya kawaida ya kuendesha nchi imefeli kwenye Checks and balances, wanasema Mahakama, Bunge na serikali vimefunga ndoa haramu na hivyo ni kupoteza muda kutegemea mahakama kusimamia haki pindi kunapokuwepo mgogoro baina ya wananchi na serikali yao au hata bunge lao. Na wanasema kuwa Bunge haliwezi kuizuia serikali kufanya udhalimu dhidi ya wananchi, wanatolea mifano vitendo vya kutisha vya uonevu wa raia dhidi ya wananchi katika hifadhi kama huko Umasaini Ngorongoro, utwaaji wa ardhi Mbarali, Operesheni za kuharibu mali za raia kwa jina la kupanga miji vizuri ( operesheni dhidi ya wamachinga) n.k

2. Wananchi wameanza kuonyesha Dalili za kuona Bunge, Mahakama na serikali si vyombo vyao tena bali ni vya kikundi cha watu wachache wenye masilahi yao.
Wananchi mitandaoni wanasema wazi kuwa Namna Serikali ilivyolithibiti bunge, mfano mzuri kitendo cha Spika wa bunge kuondolewa kwa sababu ya kutoa maoni yake, Na namna Spika wa sasa anavyoliendesha bunge utadhani ni idara tiifu ya mhimili wa Executive( serikali), kwamba yuko tayari kufanya lolote serikali isiwajibishwe bungeni na kwamba amejigeuza kuwa mwanasheria mkuu wa serikali bungeni badala ya kufanya kazi za uspika. Kunawafanya wananchi wengi niliofuatilia michango yao waone kuwa bunge hili si lao bali ni bunge la serikali hususan chama cha Mapinduzi.

Kwa upande wa mahakama, wananchi wanasema, Kitendo cha kuwepo kwa Jaji Mkuu kinyume cha katiba, Na kauli ya Jaji huyo kutamka kuwa "Mahakama ikifanya hukumu iangalie na mihimili mingine inataka nini", badala ya kwamba mahakama iangalie sheria za nchi zinataka nini, nayo pia imepelekea wananchi wengi ninaowasoma kukosa imani kwa mhimili wa mahakama.
Lakini pia ukizingatia na aina ya mashauri na namna mashauri hayo yalivyoendeshwa mahakamani ikiwemo Kesi ya Ugaidi ya Mbowe, Jinsi majaji walivyokuwa wakibadilishwa bila sababu za kuonyesha mashiko za na Jaji mwingine kupandishwa cheo wakati shauri likiendelea ambayo iliyafsirika ni rushwa ya serikali kwa majaji ili wasitende haki. Kimsingi mambo haya yanaondoa imani ya wananchi katika mfumo wa serikali na mahakama.
Lakini pia ongezeko la Mahakama kukwepa wajibu wake wa kutoa haki nchini kwa kutumia mtindo wa "Kutupa kesi za msingi na za haki muhimu za wananchi kirahisirahisi tu based on technicalities". Haya mambo yamepelekea imani ya wananchi kupungua sana kwa mifumo ya kawaida ya kuongoza nchi.

3. Uchaguzi wa mwaka 2019 na 2020 umeacha donda kwa wananchi.

Watu mitandaoni na mitaani hawana imani kuwa wanaweza kuweka serikali waitakayo madarakani kwa Sanduku la kura. Tena hili ni jambo la muhimu sana la kuzingatia. Wananchi wanasema kwamba, kwa mujibu wa katiba hii ya sasa jinsi ilivyo na tume hii jinsi ilivyo, Ni rahisi kuwa abused na wenye madaraka kuminya haki za uchaguzi wa wananchi, wanasema tume inayoteuliwa na mshindani wa wengine katika uchaguzi itakataje mkono ulioipa ulaji?, Sheria zinazokataa matokeo ya urais kupingwa mahakamani, wakitangaza mshindi ambaye si halali then kura zina thamani gani?, Kwamba Ukivuruga uchaguzi halafu una kinga ya kisheria ya kutoshitakiwa kwa hayo unayoyafanya, sasa Uchaguzi una faida gani. Watu wanatoa maoni hayo

4. Wananchi wanalalamikia mnyororo wa kulindana na kutoa nafasi ya watu kuabuse mamlaka.

Ndugu, Wajumbe kwa kadri nilivyofuatilia comments za watu mitandaoni, na katika mazungumzo ya wananchi katika vijiwe vya kahawa. Wananchi wanahoji hii kinga ya Kutoshitakiwa mahakamani ya Jaji Mkuu, Spika, Naibu Spika, Waziri Mkuu na Makamu wa Rais ya nini?, na Ililenga nini?- Kwa upande wa rais angalau pamoja na kwamba na yenyewe ina shida kwa baadhi ya makosa ikiwemo kwa mfano haki za binadamu za wananchi lakini angalau kwa yale makosa aliyoyatenda huku akitimiza wajibu wake anavumilika kutokana na uzito wa ofisi yake kama mkuu wa nchi. Je hawa wengine nao Kinga ya kutoshitakiwa ya nini?.
Ndugu Wajumbe jambo hili nalo wananchi wanasema ni miongoni mwa mambo yanayopelekeana kulindana kwa mifumo na hivyo kuondoa uwezekano wa wananchi kuheshimiwa na mfumo, ndiyo maana baadhi yao wanazungumzazungumza habari za kuondoa mfumo kwa kutumia nguvu.

5. Imeanza kuwepo minong'ono ya malipizi ya visasi.

Katika pitia yangu mitandaoni, ile ya maandishi na Sauti. Nimeanza kusikia habari za watu kushauriana na kukubaliana kuanza kutumia njia za malipizi ya visasi kwa matendo yanayofanywa na jeshi la polisi.
Watu sasa wameanza kuzungumza habari za "Polisi mnajua wanapokaa mnashindwaje kudeal nao mmojammoja" , "Mnashindwaje magari ya wabunge na mawaziri kuyatia moto", "Tit-for-tat is a fair game". Hizi kauli zimeanza kuwa ni hoja za kushauriana namna ya kudeal na hicho ambacho wanasema ni kudeal na injustice.

6. Kibaya zaidi watu sasa wameanza kuzungumza kuhusu kudeal na viongozi na familia zao.

Ndugu wajumbe wa Baraza la Usalama, hii nukta ninayoizungumza hapa ni muhimu mkaizingatia sana kwa sababu athari zake ni kubwa mno. Katika kusikiliza na kusoma mitandaoni, Watu wameanza kuzungumza na kushauriana kuwa. Maadamu Bunge halipo nao, Maadamu Mahakama haipo nao, Maadamu serikali haiwasikilizi basi njia ya kudeal na watu wenye maamuzi ni kuwapelekea maumivu ili ama wastuke, au wajute au ama watende haki wanayoitaka. Miaka iliyopita, suggestions za hivi zilikuwa zinakataliwa mara moja na wachangiaji wa mada wao wenyewe kwa wenyewe, lakini sasa inaonyesha kuwa thinking ya hivyo imeanza kupenya katika kukubaliana baina ya watu wafanyao mijadala hiyo. Hii ni hatari kubwa sana, Ipo haja ya kulifanyia kazi.

7. Wananchi wameanza kuzungumza kwa sauti za kuukataa muungano, na kudai serikall ya Tanganyika.

Watu kuitaka serikali ya Tanganyika siyo tatizo, lakini Sauti hizi zimeanza kuwa nyingi sana. Na hili limeanza kutokea baada ya watu kuanza kufunguka macho zaidi juu ya muundo wa muungano ambao umekaa kiuzungumkutiuzungumkuti. Watu wanazungumzia muundo wa muungano ambao Katiba za Zanzibar na ya Muungano zinapingans waziwazi kstika issues kadha wa kadha lakini watu wamefukia vichwa vyao udongoni kama mbuni. Watu wanazungumzia kuwa inakuwaje Wazanzibar wawe na Sauti ya kimaamuzi kwenye mambo ya Tanganyika yasiyo ya muungano, wakati Hakuna Mtanganyika anayeweza kuwa na Sauti kwenye mambo ya Zanzibar yasiyo ya muungano. Na pia watu kutoka Zanzibar wanalalamika juu ya Tanfanyika kuvaa koti la muungano.

Ushauri wangu kwa Baraza la Usalama

1. Likae chini lijadili kwa kina na lichukue hatua za kudeal na manung'uniko ya wananchi namna nchi yao inavyoongozwa. Mifumo ya Serikali , Bunge na Mahakama viache "Ushosti". Kila kimoja kifanye kazi kwa uhuru na kwa haki na si kulindana kisiasa

2. Zinahitajika reforms nchini za kuongeza nguvu zaidi kwa wananchi, haki zaidi kwa wananchi,kuweka accountability kwa viongozi na kuondoa impunity ambayo baadhi ya sheria zimewapa watu.

3. Chaguzi ni jambo Sacred katika nchi, Ukiiba kura, au kuchezea chaguzi unazalisha bunge lisilojiamini, unazalisha executive dmbayo haisikilizi raia maana siyo walioiweka madarakani, na hapa lazima migongano mbeleni itokee

4. Baraza lisidharau "Lone actors". Pengine inaweza kudhania kuwa ni rahisi kuthibiti vikundi vyenye kubeba silaha vya watu wengiwengi kwa kutumia taarifa za Intelijensia iliyojisimika ktk society yetu. Lakini Baraza lijue kuwa ni vigumu kudeal na mtu mmojammoja mwenye dhamira yake, aliyeamua kuifanyia mazoezi yeye mwenyewe ili aitekeleze yeye mwenyewe bila kuhusisha "wengi".
Na njia mojawapo ni kuondoa hizi dissatisfactions nyingi miongoni mwa raia.

5. Baraza liishauri serikali iache kamatakamata hizi zisizo na tija, iache hizi bambikizia kesi zisizo na tija. Hivi vitu vinachochea hasira, na vinasaidia kuwafanya watu waamini kuwa njia pekee ya kudeal na watu wa mifumo ni violence ya tit-for-tat

Kwa mapenzi mema ya Taifa langu, na kwa kutimiza wajibu wangu nawasilisha.

Mwenye masikio na asikie!
tumia muda wako kufanya mambo ya maana siyo kuja kuandika huu upupu usio na kichwa wala miguu. Hao wanacnhi unakuwaga nao pengine usingizini siyo hawa tunaoishi nao. Inakuwaje mtu na akili zako unakaa unatunga stori za kipuuzi km hizi, nani anakulipa kwa muda ulioupoteza kuandika mambo ya kipuuzi namna hii?
 
upendo wa mtu wa jamii moja au dini nyingine kucheka na mwingine haupo kabisa. Wananchi wameungana kwasababu ya maslahi ya pamoja kiuchumi, ila siyo upendo wa kitaifa.
Siku hizi vijana wa Tanzania wanasema pesa ndio kila kitu.
 
Ukisoma maneno ya mitandao vinywele vinaweza sisimka ukashindwa kutoka hata nje ilihali life linasonga kama kawa na watu wanakula bata.
we unazingatia maupuzi ya kwenye mitandao, yale yaache kule kule, wananchi wetu wengi kwanza hawana muda wa kufuatilia hayo maupuuzi wako kwenye site zao za uzalishaji. Hao ni wale wavivu wachache wanaofikiri kuna serikali itawapelekea mkate nyumbani
 
Back
Top Bottom