Kuna wanaume wanaishi kwenye ndoa ngumu nyie

Kuna wanaume wanaishi kwenye ndoa ngumu nyie

Mzee alikuwa baharia huyo anazuga na chumvi kumbe anaenda kula mzigo 🤣🤣🤣!!! Kijana unachekelea paja za kuku na kidali mama yako anaenda kuinjoy ndani 😀 wazee mabaharia wanapendwa sana. Sema sahizi hamna matoleo kama yale tumebakia mabaharia wachache sana.
Acha tu kuna siku nimekatiza mahali tunaenda mpirani naona gari hii hapa.
Nikaona hapa mi nazama ndani namkuta.
Dingi vp?
Aah mi nazuga tu hapa,
We umefata nini huku?
Naenda mpirani
Aah mwanangu twende hapo nikurekebishie.
Kanipa mazaga kibao.
Nikamwambia mkeo anakusubiri kule.
Karekebishe.
Hapo najua menu ntaikuta😅😅😅
Naenda jembe langu ila usimwambie umenikuta huku.
Poa.
Miaka ya 80 hapo hamna simu upige.
Ile siri mpk leo sijaisema kwa maza
 
Wanawake wa humu wangekuwa na akili, wisodm kama wewe ingekuwa safi.. kupitia huu uzi taka taka kibao zimeonekana
Unajua nini rafiki, Kila mtu anaruhusiwa kuwa mpumbavu kwa kadri awezavyo, ila mpumbavu huyo anapoamua kueneza upumbavu wake kwenye jamii it is questionable! Kwenye jamii tunategemeana, hivyo mtu mmoja akiamua kutuharibia jamii hapaswi kukaliwa kimya.

Yaani kati ya mafundisho yote ambayo anaweza kuwapa wenzie yeye kaona hilo ndilo linafaa 😅😅😅 kwamba focus yetu wanawake ya kutafuta pesa iwe kwa ajili ya kuwapanda wanaume kichwani? Kwanini isiwe kuchangia kukuza uchumi wa familia na taifa! I'm so done with some people! 🤣
 
Binafsi nawaza haya;
1. Anawafundisha nini wanawake wenzie..! Kwamba ukiwa na hela huagi?
2. Anawafundisha nini watoto wake.?? Kama ana watoto wa kiume, nao wakioa wenye fedha wasiagwe? Au kama ni mtoto wa kike, naye asiwe anaaga kwake kisa ana financial freedom?
3. Mume wa huyu mama, huko kwa washikaji walioiona video hii, anajisikiaje?

USIKUTE, HATA HIZO HELA ZINAZOMFANYA ASIAGE, MUMEWE NDO KAMUWEZESHA.
HUYO HANA mme.....ana Basha anamkanyaga tuu....
 
Sasa hapo huyo ndio kaonekana wa maana wa kuwafundisha wenzie kwenye huo mkutano mpaka mc akampa mic. Yani sijui kasahau au hakumsikiliza raisi samia aliesema yeye pamoja na uraisi wake ila mbele ya mume wake anapiga goti.

Nafikiri kutokana na wanawake wengi kuishi single wakishafanikiwa kifedha sasa wanawadanganya wenzao walio kwenye ndoa ili nao wawaletee kiburi waume zao watimuliwe ili nao wabaki pia single.
Kama hukujua hilo ndivyo akili zao zilivyo.

Wanawake ni wengi ni wanafki sana.
 
Bora huyu haangwi, aisee wanaume wanateseka sana sema tu hawana pa kusemea hasa wale wasio na kipato ndani ya familia - huo unyumba tu unapewa mara moja kwa wiki tena kwa masharti usiweke ufundi.
Usiweke ufundi tena😲😲😲 aisee hatari. Sii mchezo!
 
Mimi najitegemea in fact, lakini hakuna maisha mazuri kama mke na mume kuwa marafiki, mume kumhudumia mke, na mke kumheshimu mume, naenjoy mume wangu akiniwekea vocha nikienda saluni lazima atauliza unataka sh ngapi kama nywele ni elfu 20 na ninajua siku hiyo hana kitu ntamwambia nahitaji 10 ingine nilimuachiaga dada wa saluni chenj yangu, au nyingine ntaongezea utanilipa.

Mwanamke unaesoma hapa elewa hata upate vipi hela please usimnyang'anye mwanaume uanaume wake,(manhood) aidha kwa maneno au matendo yako au kwa kujigamba , maintain his man hood please.

Huyo Mercy Mchechu alieongea hivyo amewapa sababu wanawake wandagaji kumtafuta mumewe.

Tuna maisha ya kawaida lakini mgeni akija kwangu kwa anachokikuta lazima atajifunza kitu, utashangaa sasa limama lizima likija linaniita pembeni eti unanyenyekeaje mwanaume atakuja kukusaliti, wanadam wote wanasaliti, ishi ndoa yako Leo sasa hivi, kwamba ulisalitiwa ilishapita utasalitiwa haijatokea bado, kwa hiyo tunaweza kusema mengi kutaka umaarufu lakini UKWELI upo pale pale, Mwanamke anaeaga ana nafasi kubwa ya kuaminimka kuliko asiyeaga, anayepewa hela kulingana na kipato cha mumewe anapendwa zaidi kuliko asiyepewa.
Aise!!! Wee mwanamke kwa kweli ni great thinker bila ubishi wowote. Kwa mtazamo huo mali zote mume lazima aandike jina lako bila ata kujiuliza mara mbili. Kelsea Aaliyyah Darlin financial services njooni muone mwanamke aliyeolewa akaoleka. Shauri yenu
 
Ni Kweli lakini wanaume nao wamezidi ubinafsi na ujinga. Kila anachokilazimisha Mwanamke kina madhara Kwa Mwanaume awe KIJANA au Mzee. Wabaume hawashtuki tu na kuamua kuunda umoja wao imara na kutengeneza Hata Clubs mbalimbali za michezo na kuinjoi maisha Badala ya ulevi tu na kuibiana wake na kudhalilishana matokeo yake ndo zikivunjika watoto wanaegemea upande Wa mama na mwishowe baba anapoishiwa nguvu anakosa Msaada Mwisho anakufa Kwa msongo Wa Mawazo.

Wanaume wanapaswa kuamka na kuwakataa wanawake magumegume wanaojifanya wanapesa au wasomi Wa digrii au Ajira za Chupi!!
Wee kila jambo lina faida na hasara zake. Sasa hao wanawake waso.i wa digrii na ajira za chupi huoni kuwa ni muhimu kuwepo ili kuwapunguzia stress lecturers? Au mnataka maprof na maboss wasile kwa urefu wa kamba zao?
 
"Tarehe 5 mwezi wa tano tutasafiri kwenda Dar kwaajili ya kikao na Bosi wetu mkuu"
Hii ni
Kuaga?
Kutoa taarifa? Au
Kuomba ruhusa
 
Nimeona video mtandaoni mwanamke mmoja kwenye party ya wanawake wenzake anajigamba kwamba ametoka nyumbani kwake hajaaga ila kampa mumewe taarifa tu kwa vile tu yupo financial stable.

Imagine mke wako anajitapa hivi mtandaoni uko ndani hali ikoje mkeo anatoka kwako bila taarifa how, si anaweza hata kulala nje ya nyumbani bila taarifa kuna ndoa kweli hapo.

Alafu nmemuona brother Maxence Melo anatabasamu kabisa hapo hahahaha dah
 
Back
Top Bottom