Kuna wanaume wanaishi kwenye ndoa ngumu nyie

Kuna wanaume wanaishi kwenye ndoa ngumu nyie

Shemela Evelyn Salt, Bantu Lady, Mideko, lovely love, Kapeace, binti kiziwi, Dejane, Kalpana, Lanlady, Lovelovie, Numbisa, Mamndenyi etc embu elezeni kama huyu mama yupo sawa au la..!!
This is inappropriate! Kama mtu kwake kunafukuta hahitaji kuhamasisha na kwa wenzio kuungue!

Young girls hawatakiwi kuambiwa haya, wanatakiwa wafundishwe kuwa na uhuru wa kipato, na pia wajifunze kuwa wake wema kwa waume zao, is that too much to ask?

Lazima tuelewe kuwa kwa kufuata utamaduni ambao si wakwetu, tunajikomoa wenyewe, tunakomoa our own future!

Binafsi nawaza sana, yawezekana kabisa wazazi waliolea watoto wao vyema wanapata shida sana kuwaoza watoto wao kwa vijana ambao hawajui upbringing yao, imagine uoe binti wa huyo mama ambaye kwa bahati ambaya asiwe an independent thinker!
 
This is very crazy. Kama moto upo sijajua mishkaki itakua mingapi. Hili si jambo la kuongea proudly kwenye hadhara. What is the young generation learning🤔. Nakuhurumia mwanangu, unaenda kuoa watoto wa huyu mama..kiruuu😓😓
Ni ajabu yakuwa tumefikiri kitu kinachofanana, nimecomment kama hivi pia, nasoma comments now nakutana na comment yao. I guess hii ni worry ya wazazi wengi kwa sasa.
 
Huyu dada Mercy Luhanga. Mke wa Nehemia Mchechu. Ngonja nikamnyakie Mchechu nimpe heshima zote na mapenzi kama yote. Hahahhaha.Mbona Mercy atatia akili.Jamani ninatania tu,nimeokoka siwezi iba mme wa mtu.
😅😅😅😅😅 hahaha aisee!
 
Huyu kama anaweza kumdharau mume wake wazi wazi hivi, atatutreaty vipi akina sisi? Charity begins at home! Ukishindwa kuyajenga nyumbani kwako huku mitaani hata ukijifanya mkarimu na mpole kiasi gani tunajua tu unatuigizia. Kuwa na pesa haikupi tiketi ya kumdharau na kumpanda kichwani mtu yeyote sembuse Mume?

Sisi wenyewe we are not perfect, ila hatujafikia level ya kuhamasisha jamii upumbavu. Huyo mwanamama aambiwe ukweli kuwa ametoa boko!
 
Nimeona video mtandaoni mwanamke mmoja kwenye party ya wanawake wenzake anajigamba kwamba ametoka nyumbani kwake hajaaga ila kampa mumewe taarifa tu kwa vile tu yupo financial stable.

Imagine mke wako anajitapa hivi mtandaoni uko ndani hali ikoje mkeo anatoka kwako bila taarifa how, si anaweza hata kulala nje ya nyumbani bila taarifa kuna ndoa kweli hapo.

Financial independence ni muhimu sana kwa mwanamke kwa kuwa pia inapunguza domestic violence. Kwa sisi tuliopitia ukatili tunaona ni namna gani ni muhimu kumuwezesha mtoto wa kike kielimu na kiuchumi ili aweze kusimama hasa pale atakapopitia changamoto za unyanyasaji.
Tukirudi kwenye swala la kuaga: Kama mwanaume utasimama kama mume kqa nyanja zote na sio kukoroma tu bila kusimamia majukum yako kweli utaombwa ruhusa kwa heshima kabisaaa. Ila mwanaume ukipwaya kwenye nafasi yako jua tu utapewa taarifa
 
Hii ni madhara ya kuishi katika egalitarian marriage.Wote mnakuwa vichwa vya familia mwanaume na mwanamke wote wanakuwa huru kufanya chochote.Ni Mbaya Sana hakuna sehemu ambayo Haina uongozi katika ulimwengu huu.

Pale unapoingia tu katika ndoa Inatakiwa mwanaume amwage sera zake zote anazotaka Kwa mwanamke akae akijua kabisa anatakiwa kufanya mapenzi ya mume wake na kutii.

Hawa Hawa wanawake wanataka wanaume watakaowaongoza lakini hawapo tayari kuongozwa.Nguvu ikiwemo kipigo lazima itumike Kwa wanawake wa aina hii la sivyo hatakuja kamwe kukusikiliza.
 
Itabidi muanze kuzoea tuu, wengine tulishazoea, sina shida kama anasema anaenda wapi kwa shughuli gani, kama huwezi sema umeshindwa bila ugomvi utoke ukatafute yule wa kukuomba ruhusa, enzi za kumkataza mwanamke asiende kwenye shughuli zake kwa sababu umeamua tuu ni kujitafutia pressure tuu na ugomvi wa bure, mimi kufua nguo zangu, kusafisha nyumba au kupika hainisumbui nafanya mwenyewe mpaka mke wangu anakasirika sometimes, tatizo ukinidanganya au usiponiaga unaenda wapi utajuta
 
Binafsi nawaza haya;
1. Anawafundisha nini wanawake wenzie..! Kwamba ukiwa na hela huagi?
2. Anawafundisha nini watoto wake.?? Kama ana watoto wa kiume, nao wakioa wenye fedha wasiagwe? Au kama ni mtoto wa kike, naye asiwe anaaga kwake kisa ana financial freedom?
3. Mume wa huyu mama, huko kwa washikaji walioiona video hii, anajisikiaje?

USIKUTE, HATA HIZO HELA ZINAZOMFANYA ASIAGE, MUMEWE NDO KAMUWEZESHA.
Hawezi kuwa na mume huyo, ukiniambia ana kisharobaro anakifuga nitakuelewa ila sio mume. Mwanamke mwenye mume hawezi fungua mdomo akaongea kauli kama hiyo.
 
Nimeona video mtandaoni mwanamke mmoja kwenye party ya wanawake wenzake anajigamba kwamba ametoka nyumbani kwake hajaaga ila kampa mumewe taarifa tu kwa vile tu yupo financial stable.

Imagine mke wako anajitapa hivi mtandaoni uko ndani hali ikoje mkeo anatoka kwako bila taarifa how, si anaweza hata kulala nje ya nyumbani bila taarifa kuna ndoa kweli hapo.

Mamaee
 
Nimeona video mtandaoni mwanamke mmoja kwenye party ya wanawake wenzake anajigamba kwamba ametoka nyumbani kwake hajaaga ila kampa mumewe taarifa tu kwa vile tu yupo financial stable.

Imagine mke wako anajitapa hivi mtandaoni uko ndani hali ikoje mkeo anatoka kwako bila taarifa how, si anaweza hata kulala nje ya nyumbani bila taarifa kuna ndoa kweli hapo.

Halafu hili lishangazi linaonekana lina kiburi sana na lijeuri kwa mume wake ,wenye ndoa wanapitia mazito
 
Back
Top Bottom