Kuoga na mume au mke wako...

Kuoga na mume au mke wako...

Sasa Shishi mimi huyu basi tena amenichuna vya kutosha naachana nae kabisa. Amenitumia sms oooh dear naomba ijumaa unisaidie laki moja kuna nguo nimeona Mr.Price,nimemjibu nimefulia.

mhh ya kweli haya!inaonekana wewe mtoaji kwelikweli,kutakuwa na maendeleo hapokweli?au kila week saloon!but kama zipo toa..
 
ni jambo zuri lakini madhala yake ni makubwa, maana hii inapelekea pindi mkeo akisafiri tu tayari anapiga hodi nyumba ndogo ili aoge nayo, la sivyo atamvaa house girl aoge naye, wanawake mpoooooo...............

Endekeza kuoga na mmeo, ukisafiri............???!!!!!
 
Yeah lazima nikupe kupaumbele kuna watu wananyemelea nafasi yako mama.

........... Ndo nawaona ila mh unahonga dau kubwa sana bana... unakumbuka ule wimbo
.... aisee mume wangu mie, anatoa pesa nyingi x 2
kuliko ile mahari aliyotoaaaa.........
 
........... Ndo nawaona ila mh unahonga dau kubwa sana bana... unakumbuka ule wimbo
.... aisee mume wangu mie, anatoa pesa nyingi x 2
kuliko ile mahari aliyotoaaaa.........

Hehehe sasa mtu kalia khali yanini mkono uwe mfupi mama namsaidia kumbe yeye ananichuna.
 
Jamani tusiuane humu ndani,suala la usafi linategemea mambo mengi yakiwepo mazingira,utamaduni,kipato,malezi,imani,utashi wa mtu binafsi,hulka na mengine kama hayo. Ku generalize kwamba 'wanawake ni wachafu' au 'wanaume ni wachafu' tunakuwa hatutendeani haki.Wadau si mnajua kwa makabila mengine kujipaka udongo ndio usafi au kujipaka mafuta ya ng'ombe mazito yale ndo usafi.Linaloweza kuonekana kwako ni uchafu si ajabu kwa mwenzio ndo manjonjo. Tustahimiliane wadau!
teh teh teh Kwani Uchafu ni nini?
 
Wenye mwelekeo kama Maane utawajua tu tangia uchumba.Ukiona mwanaume hana interest kujua unaji maintain vipi hata kama hakuwezeshi kifedha, ujue huyo ni bomu.Ukiona mwanaume kila mara anashangaa inakuwa vipi kila mara unataka kwenda salon au kwa beautician wako hata kama hatoi pesa mfukoni mwake..ujue mbele ya safari kuna shida.Ogopa mwanaume anayekushangaa kwanini unatumia pesa kwa ajili ya usafi wako binafsi, wake na familia - ati haoni kwanini ununue sabuni na shower gels, shampoo, bathroom cleaning agents etc akidai ati nunua Ommo au mbuni ni multi purpose utajuuuuuta kuolewa nae baadae!
You single ladies out there, msiseme hamkuambiwa!

WOS,

Kwa uzoefu wangu...hakuna mwanaume anayependa mwanamke mchafu....tuliowengi tuna penda wanawake wanaopendeza na kuvutia....na nijuavyo mimi kila mwanamke akipewa mahitaji stahili yake ataoendeza na kuvutia tu!

Tatizo nilionalo mimi ni kuwa kuna baadhi ya wanaume japo wanapenda vilivyo nona kulisha inakuwa vigumu sana either kutokana na uchumi au ubahiri au kutoelewa kuwa urembo hugharimiwa sana.....hivyo waume hao huishia kupata one off satisfaction kutoka kwa vimada nje vilivyo pendezeshwa na wengine at considerable cost....nako wakizidiwa huingia mitini.....hawawezi kumaintain for long time!

Pia kuna waume wengine wenye uwezo tu mzuri kwa maisha ya kibongo wangependa wake zao wapendeze na kuvutia....tatizo wake hao hawajitambui wao ni kina nani, hawajui kuwatumia vizuri waume zao ili kuimarisha ndoa zao....waswahili walisema ...kwenye miti mingi hakuna wajenzi....yaani wao bora wameshavishwa pete au kuwekwa ndani basi mchezo umeisha.....hawako creative katika kuiweka miili yao katika hali ya kuwavutia waume zao ambao uwezo wakufanya hivyo upo! Hawatoi budget za kujimaintain wao kwa waume zao, hata kama mme akimpa pesa anaishia kufanya saving kwa ajili ya matumizi mengine anayoyajua yeye etc!

Binafsi my wife is not much demanding as I expected though sio mchafu....lakini I guess angeweza kutumia rasirimali tulizonazo vizuri zaidi....!ofcourse she is concerned may be akiangalia other responsibilities I have.....but still she could have been more proactive and ensuring that a big position of money is spent to maintain her body because we are capable of!

So haya mambo ya wanandoa really yanategemeana na vitu vingi sana.....huwezi ukaa umlaumu mwanamke kwamba ni mchafu wakati huwezeshwi....kama anawezeshwa una haki yakumshikia bango kwa kweli! Vinginevyo kaa kimya tu!
 
Wewe binafsi unaonaje? Fuata moyo wako wala usijali wengine wanafanya nini.
Nimejaribu kuufuata moyo wangu lakini inaonekana namkwaza mwenzangu.Mazingira niliyokulia bwana kuingia pamoja bafuni na mke wangu inaniwia ugumu kweli..najitahidi kujifunza kukubali kama nilivyoweza kujifunza calculas na algebra na chemia na kila kitu.
 
mmm Maane mbona watutia wivu we nawe...hivi mdogo wako yupo???? ahahahhaha. but am very impressed kwa kweli ni wachache watafanya hayo yote.. kazi kukwambia tangu tuoanane u no longer have a waist line duhhh mijiume mingine bwana!!! ukisema wataka cleanser waambiwa ya pesa nyingi halafu akitoka nje wanatawatamani wale wenye nyuso kama za watoto...hapo patawezekana kweli???


Oh Sishi. Wadogo zangu wapo wawili tu, mmoja ni mwanaume ana mji wake tayari and is committed family man! mwingiine ni dada ameolewa. Wote wana umri mkubwa tu na sidhnani kama angeweza kukuoa, pengine wewe ni mdogo mno kwake.

Pengine kijana wangu ila tatizo ni kuwa sitapenda kumchagulia mke maana mama yao ni chaguo langu na si la wazazi. Tuombe Mungu huenda mkakutana na mwishowe tukaja kufahamiana kumbe wewe ni Shishi wa JF.

Kama familia ina uwezo isione gharama kuhudumia mke na watoto wa kike. Vinginevyo hasa kwa mabinti zetu kama hutafanya hivyo atataka naye apendeze at the expense of nothing else but her body. Take it from me. Hata mabinti wakifikia 12 years anza kumhimiza mama yao wawe wanampa bajeti ya mahitaji yao. It is extremely important, na utamfanya asiwe na tamaa. Of course, hapa ni lazima uwe makini kukaa naye kupitia hiyo list kuona kweli it is ok. From the beginning unamfundisha ku-list yale mahitaji muhimu na awe mwaminifu na iwe mazoea. Kama mzazi utatumika pia kumlea binti kuwa mke mwaminifu si kama yule wa rafiki yangu Fidel80 sijui kimada au girlfriend anataka 70,000 za hair retouch. Nimechoka mbavu. Kama ni kwa ajili ya body cleaning saloon hiyo ni nyingi na unaweza kufanya pedicure, manicure, massage, facial, na mambo kibao wanamama wanafahamu watatutajia.
 
Pengine kijana wangu ila tatizo ni kuwa sitapenda kumchagulia mke maana mama yao ni chaguo langu na si la wazazi. Tuombe Mungu huenda mkakutana na mwishowe tukaja kufahamiana kumbe wewe ni Shishi wa JF.


Hapa poa we tulia tu tutaletana nyumbani lol.



Kama familia ina uwezo isione gharama kuhudumia mke na watoto wa kike. Vinginevyo hasa kwa mabinti zetu kama hutafanya hivyo atataka naye apendeze at the expense of nothing else but her body. Take it from me. Hata mabinti wakifikia 12 years anza kumhimiza mama yao wawe wanampa bajeti ya mahitaji yao. It is extremely important, na utamfanya asiwe na tamaa. Of course, hapa ni lazima uwe makini kukaa naye kupitia hiyo list kuona kweli it is ok. From the beginning unamfundisha ku-list yale mahitaji muhimu na awe mwaminifu na iwe mazoea. Kama mzazi utatumika pia kumlea binti kuwa mke mwaminifu si kama yule wa rafiki yangu Fidel80 sijui kimada au girlfriend anataka 70,000 za hair retouch. Nimechoka mbavu. Kama ni kwa ajili ya body cleaning saloon hiyo ni nyingi na unaweza kufanya pedicure, manicure, massage, facial, na mambo kibao wanamama wanafahamu watatutajia.

kwa kweli hiki ni kitu cha muhimu, usipomtimizia bintiyo haya mahitaji ndio anakwenda chuoni kukutana na kina Fidel na YoYo.....mfano tu jamani msiniue mwenzenu! kumbe malezi pia muhimu sana!! ahsante sana kwa hiyo shule hapo!
 
mke mwaminifu si kama yule wa rafiki yangu Fidel80 sijui kimada au girlfriend anataka 70,000 za hair retouch. Nimechoka mbavu.

Nina home work kubwa sana kupata mke/mchumba mwaminifu yaani ni kazi kweli kweli Bro. huyu ananikamua sana tena hiyo sabini nayo toa bado analalamika akitoka saloon nakuta uso na nywele za kawaida tu sijui ni usafi au nini sielewi ananidanga tu anatumia vipodozi vya Japan ni ghali sana kuliko vya US au South Africa.
 
kwa kweli hiki ni kitu cha muhimu, usipomtimizia bintiyo haya mahitaji ndio anakwenda chuoni kukutana na kina Fidel na YoYo.....mfano tu jamani msiniue mwenzenu! kumbe malezi pia muhimu sana!! ahsante sana kwa hiyo shule hapo!

Hehehehe akija chuoni akikuatana na sie si tunasaidiana kulea kwani kuna tatizo? Si kama huyo naye mpa 70,000/= kwa wiki kwa kutengeneza nywele tu.
 
Hehehehe akija chuoni akikuatana na sie si tunasaidiana kulea kwani kuna tatizo? Si kama huyo naye mpa 70,000/= kwa wiki kwa kutengeneza nywele tu.

teh teh teeeh sana mkuu, wazazi wanapunguziwa majukumu hapo!.
 
Ni ubwege tu, ukiona hivyo ujue hamna plan ya maana ya kufanya au hamko bussy

...kabisaa, mimi hutumia 'privacy' na burudani ya maji ya mvua/shower kutafakari haya na yale, nikipanga na kupangua. Asikwambie mtu bana, raha ya kukoga ukoge peke yako,...

mambo ya kusuguana mgongo yalibakia huko huko enzi za uchumba,...siku hizi matumizi ya shower-brush na madodoki kwa wingi!

876210516390P.JPG

Nina home work kubwa sana kupata mke/mchumba mwaminifu yaani ni kazi kweli kweli Bro. huyu ananikamua sana tena hiyo sabini nayo toa bado analalamika akitoka saloon nakuta uso na nywele za kawaida tu sijui ni usafi au nini sielewi ananidanga tu anatumia vipodozi vya Japan ni ghali sana kuliko vya US au South Africa.

...Fidel, nakuhakikishia 95% hiyo 'posho' anamhonga dogo dogo wake, mamsapu anavyokulalamikia wewe hazimtoshi, naye analalamikiwa hivyo hivyo na Serengeti boy wake... ongeza dau mkuu!
 
akidai ati nunua Ommo au mbuni ni multi purpose utajuuuuuta kuolewa nae baadae!
You single ladies out there, msiseme hamkuambiwa!
hahahahhahahaha WoS umenimaliza kabisaaaaa Mungu wangu kweliii mbona ni mbuni multipurpose hahahhahaha, mnaogea hiyohiyo , mnafulia hiyohiyo ,mnaoshea vyombo hiyohiyo, mhhhhh kuoshea mabafu na magari je? nilisahau kumbe omo . tena anaweza kukuincourage akawa anakusifia kila siku unakuwa soft ukiogea omo....... weeee tena unabaki "MWE"😕!!!
 
Mkuu mosquito nimekupata yaani leo nimefunguka macho anataka anikamue eti kaona nguo hapo Mr.Price nimpe Ijumaa laki 1 aende akabebe nguo hiyo hapo hapo anasisitiza eti ooh dear jmosi nataka nikasuke za kimasai Msasani nikamwambia mbona Ilala pale wanasuka ooh wale wachafu duh sh.ngapi ooh dear nipe kama themanini itatosha.
Nimemjibu mama nimefulia.
 
Chaku
inategemea na miundo mbinu ya nyumba yako, kama nyumba yako ina bafu la nafasi, lakini kama haina bafu la nafasi basi shughuli ipo
wazee wengi wanarudi nyumbani kwa nyakati tofauti wengine wanabipitia kwenye dili wengine baa...
 
hahahahhahahaha WoS umenimaliza kabisaaaaa Mungu wangu kweliii mbona ni mbuni multipurpose hahahhahaha, mnaogea hiyohiyo , mnafulia hiyohiyo ,mnaoshea vyombo hiyohiyo, mhhhhh kuoshea mabafu na magari je? nilisahau kumbe omo . tena anaweza kukuincourage akawa anakusifia kila siku unakuwa soft ukiogea omo....... weeee tena unabaki "MWE"😕!!!

Yaani!
Hii topic inachekesha sana lakini ina mafundisho mengi ndani yake kwa wote wanawake, wanaume, wenye wenza na wasiokuwa nao.
Wenye kuendekeza ushauri kama huo....ati omo ni multi purpose!
Halafu utakapoanza kukakamaa ngozi..akikugusa akisikia ngozi ngumu kama kenge..anajimuvuzisha taratiibu nyumba ndogo,,,, huko anakutana na baby soft skin! Utashangaa matokeo ya multi purpose.


Mwaya jitunze jipendezeshe kwa manufaa yako mwenyewe.
 
Back
Top Bottom