Kupunguza tatizo la ajira serikali iruhusu huduma ya kupokea pesa kupitia PayPal

[emoji1][emoji1]ufipa hawatasema hilo kamwe .. jua kuna mambo ya utakatishaji fedha ndiyo maana kupokea pesa kutoka nje sio rahisi hivyo kama tunavyojipangia sisi
Kulipa nje pesa za kigeni sio utajatishaji ila kupokea pesa za kigeni ndio utakatishaji !!!
very interesting.Nchi yetu Ina mambo mengi na muda Ni mchache.

Vizuizi vya kupokea pesa Ni vingi Hadi vinatisha kwa kisingizio Cha pepo shetani anayeitwa money laundering
 
Ndiyo huwezi jua mtu anapokea zaidi ya dola 60000 kwa dakika kutoka nje ... je haiwezi julikana kama anafadhiliwa na watu toka nje kueneza ugaidi nchini inabidi sheria ziwe makini kuangalia hayo mambo

Ndiyo maana unaona ni ngumu kupokea pesa nyingi kwa mkupuo kutoka nje
 
Cha muhimu Kama mpokeaji anajulikana sio big deal Ni kushughulika na case to case afiatiliwe huyo.lakino isionekane Kama kila mpokeaji pesa wazo la kwanza kuwa Ni money laundering!!!! Viwango vya wenzetu Kenya wanaanza kuangalia mtu Kama anapokea dola laki tano ndio humyaka kutoa maelezo nchi za ulaya na America vivyo hivyo.
Kwetu tu dola elfu kumi.unatakiwa kututolea maelezo .Are we that poor? Kuwa dola elfu kumi Ni utajiri mkubwa wa kuhoji mtu akipata?

Anyway kwa wenzetu nchi zingine kupokea Sheria Wana relax Sana ndio.maana unakuta Wana Hadi banks za Siri za uswisi nk ambako watu huficha pesa .Hii money laundering war Ni ya vinchi vyetu maskini wazungu kutubana kuwa hela zikitoka kwao kuja kwetu zihojiwe na wapewe taarifa.Lakini.za kwetu zikienda kwao.mabenki ya Uswis,Cayman islands na Bahamas kwenye off shore banks huko hawataki tuhoji .

Hi Vita ya money laundering naona nchi zetu ndio.tumevalia njuga kuliko hata walioiamzisha.Upele wa money laundering umemkuta mkunaji
 
Unajua maradha ya kutodhibiti money laundry??
Kama ni kupokea pesa western union au mastercard zaweza kutumika
 
Unajua maradha ya kutodhibiti money laundry??
Kama ni kupokea pesa western union au mastercard zaweza kutumika
Money laundering inatumika tu Kama kisingizio Cha kuzuia nchi.maskini zisitajirike
 
Kwahiyo utatishaji ni dhana fikirika kwako??
Kabisa Ni fikirika ingekuwa halisia ma trillion ya pesa toka Africa zisingejazana mabenki ya uswisi yenye akaunti za Siri ambamo wamiliki Ni hidden
 
Tunajipunja wenyewe.

Kuna kampuni ya nje ilikuja Tanzania, kwenye madini nafikiri, ikaona mishahara ya Watanzania ni midogo sana. Yani kampuni ikaona wawekezaji wake wengine wakijua mishahara ni midogo hivyo, inaweza kuwa scandal ya kimataifa.

Kampuni ikataka kulipa wafanyakazi mishahara mizuri zaidi.

Waziri akaikataza kampuni, akasema mishahara hii ni mikubwa sana kwa Watanzania.

Sasa, serikali yenye mentality hii, inawezekana kabisa inafungia fursa za watu kufanya biashara makusudi.

Kwa kujua kwamba, watu wakijikwamua kiuchumi, kielimu na kisiasa, kuwatawala kwa imla inakuwa ni kazi ngumu sana.
 
Kabisa Ni fikirika ingekuwa halisia ma trillion ya pesa toka Africa zisingejazana mabenki ya uswisi yenye akaunti za Siri ambamo wamiliki Ni hidden
Hidden kwako lakini taarifa zote zipo ila sio kwa ajili yako ndio maana unadhani ni hidden.
Ungelijua madhara ya kushindwa kuthibiti mzunguko wa fedha sidhani kama ungetetea hili suala kwa aina ya hoja ulizoziweka hapa
 
Hidden kwako lakini taarifa zote zipo ila sio kwa ajili yako ndio maana unadhani ni hidden.
Ungelijua madhara ya kushindwa kuthibiti mzunguko wa fedha sidhani kama ungetetea hili suala kwa aina ya hoja ulizoziweka hapa
Tunaongelea mzunguko wa pesa za kigeni kuingia nchini kuwa mkubwa.Hizi zetu za ndani zaweza dhibitiwa au fanyiwa chochote .Hela za nje bado tunazo kidogo udhibiti mkali wa kupindukia wa kuziingiza wa Nini? Pesa za kigeni kuna watu wanafanya mishe mishe zao wanaingiza nchini .Kwa Nini uwawakie wakati huko walikotoka nazo husikii kuwa mtu kakabwa au kaibiwa?
 
Kabisa Ni fikirika ingekuwa halisia ma trillion ya pesa toka Africa zisingejazana mabenki ya uswisi yenye akaunti za Siri ambamo wamiliki Ni hidden
unatumika na mabeberu wewe tutakutafuta tutakupata na tutakushuhulikia wewe na familia yako
 
Sitaki kukulaumu sababu huu ni mjadala huru. Fedha haramu pasi ya kuwa ya ndani au nje inapoingia kwenye mzunguko matokea yake bado ni mabaya sana. Nadhani unakosa elimu ya hili suala embu jipe ufahamu kwa kusoma na kuelewa kabla ya kuleta ubishani usio na tija.
 
Sio kila pesa inayoingia ni haramu, ametoa mfano wa urahisi wa kuuza bidhaa kama vinyago kwenye maduka ya online kama Ebay. Unajua kampuni kama Amazon linachangia kiasi gani kwenye uchumi wa USA?

Kwani nchi ambazo zina huduma ya PayPal zina rate gani ya Ugaidi? Tunashindwa kutumia fursa za technology kwa visingizio duni
 
Money laundering inatumika tu Kama kisongizio Cha kuzuia nchi.maskini zisitajirike
Kungekuwa na Money Laundering akina Chenge wangeficha mabilioni Uswisi na huko Visiwani? Kuna nchi ndio biashara zao hizi.

Nigeria wamerudishiwa mabilioni ya Abacha aliyoyaficha Uswisi baada ya kuyadai kwa muda mrefu.
 
Kwani nchi ambazo zina huduma ya PayPal zina rate gani ya Ugaidi? Tunashindwa kutumia fursa za technology kwa visingizio duni
Uko sahihi tunatumia visingizio duni
 
Usisingizie wazee mkuu.Vijana wengi sana serikalini na kiasi fulani bungeni.

Nikihesabu vijana walio na nafasi ya kutoa maoni yao yakasikilizwa ni wengi.Au una maana gani kusema wazee?
Kigezo Cha kua mbunge c kujua kusoma na kuandika tu, Sasa unatikiria mtu wa namna hiyo anaweza leta mawazo ya kujenga Kama c vituko tu kila siku tunavishuhudia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unajua maradha ya kutodhibiti money laundry??
Kama ni kupokea pesa western union au mastercard zaweza kutumika
wajinga kama nyie vibarua serikalini msiojua kinachoendelea private sekta mnatupotezea muda pumbafu nyie
 
Kama huna ajira nenda ukalime.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unajua maradha ya kutodhibiti money laundry??
Kama ni kupokea pesa western union au mastercard zaweza kutumika
Kwa argument kama hii Raisi Magufuli nakupongeza kwa kutopandisha mishahara na madaraja wafanyakazi wa serikali.Ikiwezekana wapunguze mishahara na madaraja pia

hivi mtu kama huyu ningekuwa Raisi haki ya mungu naapa kukufukuza kazi ningekuwa nimekuhurumia sana hata sijui ningekufanya nini.Angenikoma hadi aliyekufanyia interview na kukuajiri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…