Kusema ukweli mtaani hali ni mbaya, cha kushangaza viongozi hawajali kabisa

Kusema ukweli mtaani hali ni mbaya, cha kushangaza viongozi hawajali kabisa

Ulikuwa unaishi kwa hofu kwanini? Kwani ulikuwa unafanya shughuli gani hasa mpaka uwe na hofu na uongozi uliopo?
Kwani watu walio kua wanafungwa kwenye viroba hukuaona, watu walio tekwa na wa siojulikana hukuwasikia, watu waliokua wanaachushwa kazi bila sabb ukuwasikia hayo yote husababisha hofu.
 
Mi nimelia sana usiku nikitaman hata mchoz wangu ugeuke pesa nizikute asubuhi ndo kwanza nimekuta mto umeweka alama.Na shule ndo hizo zinafunguliwa j3😕😤😭
Unalilia kwenda shule au?
 
Hata Mimi mwenye ajira ila Hali mbaya tarehe mbaya hzi tushaliwa hasara hatuna kitu tunatanga tanga kweli hali mbaya na Kama huna hela mjini watakuFir.
 
Ulikuwa unaishi kwa hofu kwanini? Kwani ulikuwa unafanya shughuli gani hasa mpaka uwe na hofu na uongozi uliopo?
Mungumtu ndiye alikuwa anadhibiti akili za watu wote akitaka wafikiri kama alivyokuwa anataka yeye kabla Mungu wa kweli kumpiga stop.
 
Hali ni mbaya hali ni mbaya kupita maelezo, mitaani hali inazidi kuwa tete vitu havishikiki bei nashangaa imekuaje kumekua na mfumuko wa bei za bidhaa wa ghafla namna hii? yani vitu vimepanda bei kwanzia dawa ya mswaki mpaka vifaa vya kielekroniki na vifaa vya ujenzi,

mfumuko wa bei huu unatuathiri sana cha kushangaza viongozi ni kama vile hawajali hii kitu wanaona ni kawaida tu wako bize kutafutana kwaajili ya uchaguzi wa 2025, ajira hakuna, kazi hakuna hela hakuna vitu vinapanda bei hovyohovyo.

nyie viongozi mnajua kua Raia wenu sasa hivi hata chai hawanywi? na mboga tunapika bila mafuta.

inahuzunisha sana asee tunaishi kama digidigi

View attachment 2079053
Wewe cheza na biti kulia Lia hakuta kusaidia,Hali hiyo iko hivyo Duniani kote.

Na unachoita mfumuko wa bei as per govt,ni mfumuko ulio ndani ya target.

Mwisho ukiona mtu anavyosimulia humu mtandaoni unaweza Dhani hakuna maisha kumbe things are running as usual.



Screenshot_20220112-182139.png
 
Mi nimelia sana usiku nikitaman hata mchoz wangu ugeuke pesa nizikute asubuhi ndo kwanza nimekuta mto umeweka alama.Na shule ndo hizo zinafunguliwa j3😕😤😭
Uzikute pesa? Endelea kulia pesa ije, yaani uache kutafuta Kazi uje uanze kulia eti ndio pesa itakuja 😝😝
 
Kusema kweli, hali ni mbaya sana. Vitu vimepanda bei kwa zaidi ya 100%. Kutoka sh.46000 hadi sh.105,000/- hii ni zaidi ya 100%.
 
Nyinyi wakati magu anatunyoosha watumish mlitubeza sana , sasa tunyooke wote.

Tulipofika kuingia barabarani ni lazïma
 
Sera za ujamaa na kujitegemea zimefeli. Serikali inatumia hela kama baharia mlevi wakati kipato chake kinapungua wakati huu wa COVID. Hela inashuka thamani na bei zinafumuka.
 
Back
Top Bottom