Kusema ukweli, wakoloni Tanzania yetu hawakuiibia kitu!

Kusema ukweli, wakoloni Tanzania yetu hawakuiibia kitu!

Kwani sasa hivi tunatawaliwa kwa ridhaa yetu?? Je Elimu yetu haina matabaka?? Je udini haupo??? Je kwenye utawala tulionao ukabila haupo??

Mwisho ni je CCM na mkoloni nani mnyonyaji zaidi??

Sent using Jamii Forums mobile app

Ccm anafaidisha makada wachache mkoloni alifaidisha wote,soma kuhusu colonial economics vs after independent economy
 
Ukoloni ni mbaya ila kosa kubwa lililofanywa na Baba wa Taifa baada ya Tanganyika kupata uhuru ni kufukuza na kutaifisha mali za wawekezaji wa kizungu, naamini hata huko aliko hili kosa analijutia kwa kudhani watanganyika tungeweza viendeleza hivyo vyanzo vya uchumi.

Sent using Jamii Forums mobile app

True angewapa haki ya ulowezi yeye abakie kwenye siasa wao waachie mambo ya uchumi,tungekuwa mbali sana
 
Kama wakoloni walikuwa wabaya na awajafanya kuti hawa wakoloni weusi si wangefanya zaidi ya wakoloni tumeona hata robo awajayafikia
 
Nyerere aliiharibu hii nchi kwa kutudanganya kuhusu wakoloni na ukoloni. Kiuhalisia wale jamaa wangeachwa hapa wangefanya makubwa kuliko haya ya leo. Dar, Tabora, tanga walizipanga vizuri sisi tumepangua vizuri

Sent using Jamii Forums mobile app
 
RWEGOSHORA FROLIAN,

Kumwambia mtu (Engineer) MPUMBAVU KWENYE HADHARA NI UKOLONI GANI?

Kama hajatimiza wajibu wake, fuata taratibu (kanui) KISHA MFUKUZE KAZI
 
Barbarosa,
Watu kutawaliwa tu ni kuibiwa dignity yao.

Tanzania hatukupata kuwekewa settlers sana kwa sababu wakati Mjerumani kajiweka sawa, alipigwa kwenye vita, na Muingereza alivyokuja kaja kwa mpango wa "protectorate" kwa hivyo alijua hatakaa sana. Hakuwa na mipango ya muda mrefu.

Kwa Congo na Kenya, nitataja vitabu vya kusoma tu mwenye kutaka avitafute.

Congo. Kasome "King Leopold's Ghost: A Story of Greed, Terror, and Heroism in Colonial Africa" cha Adam Hochschild.

Kwa Kenya soma "Imperial Reckoning: The Untold Story of Britain's Gulag in Kenya" cha Caroline Elkins.
 
Nachotaka kusema, hakuna binadamu mkamilifu, na ukitaka kulinganisha utawala wa kikoloni na utawala wa sasa wote wanamapungufu yao, lakini nakataa kama utawala wa sasa ni katili sana kuliko wa kikoloni. Kwa serikali iliyochaguliwa na wananchi wenywe huwezi kulinganisha na serikali ya mkoloni iliyojipa madaraka bila ridhaa ya mtu yoyote na inachukiwa maamizi nje ya nchi na kufaidisha watu wao wa nje.
*Nukuu*
Nachotaka kusema, hakuna binadamu mkamilifu.

[emoji115] Nadhani unapaswa kukomea hapo tu.
hisani ya mkoloni kwa watanganyika ilikuwa ni kubwa zaid kuliko ya serikali zote zilizopita.

Mabaya mengi tunayosimuliwa dhidi ya mkoloni na kusoma kwenye vitabu ni tungo tupu..

kuna mambo ambayo Mtanganyika wa utawala wa mkoloni aliyapata lakini leo hayapatikani nchini mwetu.

Nyerere alikuwa akiwa pinga wakoloni kwa kupitia mikutano, mahakama na maandamano, lakini leo hakuna anae thubutu kuyafanya hayo chini mkoloni mpya mwenye rangi ya ngozi kama letu.


waliotunga hayo matango mwitu walikuwa wana tafuta sympathy ya watanganyika, wakakoleza uongo mwingi sana na kwa hilo walifanikiwa.
lakini itoshe kwa kusema mkoloni alikuwa Bora zaid kuliko mkoloni ngozi nyeusi.





Sent using Jamii Forums mobile app
 
Chochote walichokifanya wakoloni, walifanya kwa manufaa yao mapana.

Hata sasa bado sie ndio soko la bidhaa zao, chanzo cha mali ghafi za viwanda vyao n.k.

Tukiwa na dunia yenye amani na utulivu, watauza wapi silaha zao ikiwa wao ndio wazalishaji wa silaha?

Walijenga reli na barabara wakati uke zirahisishe usafirishaji wa bidhaa ziende kwao, hapo bidhaa inajumuisha watumwa, mafini, mazao n.k.

Tafiti walizofanya kuhusu maeneo yenye madini na miundo mbinu nayo ilikua kwa kusudi lilelile, kuwanufaisha wao.

Kusingekua ni kwa ajili ya maslahi yao kwanini waligombania maeneo ya Afika hadi kufikia kufanya mkutano wa kugawana bara letu?

Maovu na uzembe wa viongozi wetu baada ya uhuru umekithiri kiasi cha kufanya tuwakumbuke wakoloni, lakini haiondoi ukweli kwamba mkoloni hakufanya chochote kisicho na faida kwake.

Barbarosa pole sana, mbaya zaidi umesahau kusema kuna jamaa sasa hivi ametuletea lugha ya kuwaita wazungu mabeberu huku akiendelea kuwaomba watusaidie na kuwasifia kila wanapofanya hivyo.

Wakoloni hawa kama kweli wana kusudi na nia njema, UN wapo kuhakikisha dunia inakua salama na hatuna migogoro kati ya nchi na nchi huku haki za binadam zikipewa kipaumbele, lakini hilo halijawahi kufikiwa.

Mashirika yake ya maendeleo yamekuwepo zaidi ya miaka 70 wakijinasib kusaidia nchi kupambana na umaskini, kuimarisha utawala bora, kueneza demokrasia n.k lakini hakuna nchi hata moja wanaweza kuitolea mfano kwamba waliikuta na hali mbaya, wameisaidia na sasa imefikia pazuri wanaweza kuiacha ikajiendesha yenyewe, haipo.

Nabaki na msimamo wangu kwamba mkoloni alifanya yote kwa maslahi yake binafsi.
 
Wewe ungekuwa mtumwa,ungefurahi kuwa kwenye hiyo hali,cwatoto wako, mke wako, kulatiwa kutumiwa na so called Boss anavyopenda, hata kwa matumizi binafsi.

Mamilioni waliuwawa, mamilioni wakapelekwa utumwani.

Hujui historia yako.
hayo ya kulawitiwa nazo ni moja ya tungo tu zilizotungwa na akina nyerere, Abdul sky's etc ili kupta sympathy ya watanganyika ili wapewe nchi.

alafu ni bora ufanyiwe hivyo vitendo na mtu baki na sio mtu wa nyumbani mwako..

Hayo unayoyataja hapa ni simulizi tu na hakuna uhalisia wowote.

Lakini mambo yenye taswila hiyo ya natokea nchini mwetu na kiongozi wa hayo anajulikana lakini nani wa kumfungia paka kengere?.

wapo wanao filwa kwa tenki na watekaji.

miili ya watu kwenye Vitoba ufukweni.

na mengineyo mengi tu.. mkoloni mweusi ndo kinara wa hizo mambo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwani wakati wa mkoloni kulikuwa na huo uchaguzi? Mchaguwane ili mpange njama ya kuwadhuru wakoloni. Jaribuni hata mjifunze mawili matatu nini kilitokewa wakati wa mkoloni. Mkoloni alikuwa anateua watu anaojua hawezi kumletea shida (ma DC an RC). Nchi ilikuwa inaongozwa na Gavana Mzungu aliteuliwa na watawala wake wa Ulaya.
Leo hii ma DC na RC unawapigia kura?

Halafu ninyi wa digrii 4 majanga kweli kweli.
We unajua ni utaratibu upi ulitumika ili Nyerere waziri mkuu?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukoloni ni mbaya ila kosa kubwa lililofanywa na Baba wa Taifa baada ya Tanganyika kupata uhuru ni kufukuza na kutaifisha mali za wawekezaji wa kizungu, naamini hata huko aliko hili kosa analijutia kwa kudhani watanganyika tungeweza viendeleza hivyo vyanzo vya uchumi.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kama ni makosa ya Mwl.Nyerere kwanini hatuyarekebishi katika awamu zote zilizofuata?Tatizo letu ni kuogopa kuchukua hatua ya kujipanga upya kama Taifa,Watawala wakihofia kisasi cha watakaofuata na hatujathubutu kujenga mifumo imara ya kujitawala wenyewe kifikra,kiuchumi au kijamii kwa manufaa ya wote.Ubinafsi na ubaguzi ndiyo kansa yetu.

Watanzania tujipange upya kwa kutafuta maridhiano na kutengeneza Katiba ya Wananchi ili tupate maendeleo ya kweli.Nchi hii ni yetu sote na hakuna MTU/watu wenye haki kuliko mwingine/wengine.

Tunajenga nyumba moja Tanzania kwa ajili na manufaa ya Watanzania.Hatuhitaji approval ya yeyote namna tunavyotaka nchi yetu iwe na vipaumbele vyetu,tujitambue.
 
Wamejenga MUHIMBILI.
Waasisi wa tanu na ccm ni watu wa mwambao ambao wengi walipokea dini ya mwarabu hawa ndiyo waliochangia kujaza propaganda kuwa wazungu wa ile dini ya magharibi kuwa ni wabaya sana. watu hawa wa mwambao wameshiriki sana katika kuandika vitabu vya kufundishia shule zetu, vitabu vyenye kujaa historia ya upotoshaji.

Jiulize jambo moja: ni wapi waarabu walijenga japo mita moja ya reli? ukinitajia nidai buku.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watanzania hivi sasa yuko pande mbili kati ya wanaoshabikia ujenzi wa miundombinu kuwa ni maendeleo na wasioshabikia hilo.

Mimi niwahoji wanaoshabikia, Muingereza alijenga meli Ziwa Tanganyika (Mjerumani) na Ziwa Victoria (Muingereza) na bado zipo zinafanyakazi mpaka leo.

Pia viwanja vya ndege kila mkoa, reli ya kati, hospitali kila mkoa, shule na chuo cha DIT (hivi sasa), bandari Tanga, Dar na Mtwara, mabarabara yaliyounganisha mikoa yote na kupitika muda wote nchini ya vikosi vya PWD.

Elimu ya kiwango cha kimataifa toka Cambridge na mitihani ilitoka huko lakini bado tukasema Muingereza ondoka imetosha.

Kwanini hatukumuacha?
 
Historia haiwezi kuwa objective kwakua wazungu wanaiandika kwa kuji-favour wao na waafrika vile vile tunaji-favour.
Ukweli ni kuwa mabaya na mema yote yalitendeka so tusilaumu au kusifia tu ukoloni Tanganyika
 
Back
Top Bottom