Kutana na Luludiva; superstar anayeishi nyumba ya tope

Kutana na Luludiva; superstar anayeishi nyumba ya tope

Sio kweli ,wachaga nyumbani kwao migombani kuna MANSIONS ambazo wanazitumia wakati wa Xmas wakiwa mapumzikoni lakini muda mwingine wote zinakuwa nyumba za panya!!!
The problem mnachanganya kati ya Wachaga na Wachaga Wenye Uwezo kiasi kwamba mnataka kuaminisha watu Wachaga wengi wana mansions wakati uhalisia ni Wachaga wachache mno wenye hizo unazoita mansions na majority wana nyumba za kawaida tu, na wengine hata hizo za kawaida, hawana!! Kikubwa ninachokiona na kunifurahisha kwa Wachaga ni kile ambacho siku hizi kinaanza kuenea kwenye vijiji vingine. Uchagani, tangu zamani hizo, walikuwa wanajitahidi sana kujenga nyumba za bati hata kama ni ndogo wakati vijiji vya maeneo mingine zikijaa nyumba za tope na majani.
 
Hiyo hela anayo sasa mkuu...uuguze na bado upige plasta ili watu sijui wasikucheke[emoji848]kumbuka yy ndo first bn last born hana wa kumsaidia!

Daaah kama mambo yenyewe ndo haya nawashukuru sana kaka zangu kujenga nyumba mpya kijijini kuzaliwa wa mwisho raha asee[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Best nikuambie kitu ukiamua hushindwi,ila tunajifunza kupitia matatizo yetu
 
Hiyo hela anayo sasa mkuu...uuguze na bado upige plasta ili watu sijui wasikucheke[emoji848]kumbuka yy ndo first n last born hana wa kumsaidia!

Daaah kama mambo yenyewe ndo haya nawashukuru sana kaka zangu kujenga nyumba mpya kijijini kuzaliwa wa mwisho raha asee[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Kwa sie tuliotoka kuuguza juzi juzi tu huku tukiwa hatuna kampani, tutakuelewa sana!! Watu ambao katu sitajaribu kuwa-judge ni mtu anayeuguza au mwenye watoto na/au tegemezi wanaosoma private schools!
 
Mimi nina Anko wangu mmoja alikuwa na cheo kikubwa tu cha polisi, ingawa ni kweli alikuwa ni mpenda bata lakini yeye alizaliwa Dar na mpaka amekuwa na kuwa mkubwa akijua kwao ni Dar na ndiko baba yake alijenga.

Alivyoingia kazini akaandika kwao ni Dar.

Sasa baba yake alifariki kwanza, ikabidi asafirishwe kwenda Musoma ( huko baba yake alikuwa na eneo kubwa tu ila ni kama alikuwa kawaachia ndugu zake tu ).

Baada ya msiba kuisha sasa ndio ikabidi jamaa aanze route za kwenda Musoma mara kwa mara na kutafuta njia ya kujenga hata kijumba.

Mara ghafla, mwaka juzi amedandia Noah akapata ajali wakafa watatu na yeye akiwemo.

Polisi wakaangalia documents zake, kaandika kwao ni Dar. Na huku Dar baba na mama hawapo, walishatangulia. Huku wamebaki wadogo zake ambao nao ni wahuni tu na kibaya zaidi vyumba vyite wamepangisha maana yake hata ysehemu ya kufikia wageni hakuna.

Kilichofuata polisi wakasema ukoo uamue, msiba upelekwe wapi kama ni Dar au Musoma. Ikabidi iwe Musoma.

Basi akapelekwa Musoma, lakini hakukuwa na nyumba ya maana. Nyumba iliyokiwepo ilikuwa ya mama mdodo na yeye anakomaa tu kibishi kujenga akiuza mahindi.

Hivyo ikabidi msiba ufukie humo.

Askari wenzake na ndugu baada ya musiba wakawa wanacheka na kupiga majungu balaa kwamba jamaa hata kujenga home ameshindwa.

Unaweza kuona mtu hajajenga home kumbe hujui yaliyoko nyuma ya pazia.

unavoeleza inaonyesha kisaikolojia haupo sawa !.kuna kitu kina kusumbua kwenye hili swala kuhusu kwenu na angalau hata katofali kwenu
 
Hayo ni makaburi ya ukoo na hiyo ni nyumba ya ukoo wala sio kwake Luludiva.

Huyo dada ni mpambanaji na ametokea familia ya chini sana na ananyanyuka na amefikia hatua kubwa tu mpk ya kumiliki magari na kupanga nyumba nzuri. Na kwa sasa anajenga nyumba nzuri tu Ila bado haijaisha.

Ni wangapi humu wenye elimu mara 5 ya Lulu Diva na wanakwea daladala na hawajui lini watamiliki hata bodaboda? Ni wangapi humu wanashindwa hata kulipa kodi ya chumba kimoja? Ni wangapi humu hawana hata kiwanja a hili mbali msingi wa nyumba?

Tusimhukumu kwa kuangalia nyumba ya kwenye eneo la ukoo.
 
Mimi nina miliki nyumba nzuri zaidi ya tano na mzazi wangu nimemrekebishia nyumba yake hapa Dar anaishi pazuri. Sisi kwetu kabisa ambapo tutazikwa ni Mtwara na huko sijajenga hata banda la bata.

Ina maana siku nikifa nikipelekwa huko ndio kutakuwa kwangu? Najenga nyumba zitakazoniletea faida nikipangisha, siwezi kujenga wakakae mijusi na mapanya. Kule nitaenda kuzikwa tu. Watotocwangu hawawezi kwenda kuishi Masasi huko kusiko na fursa
 
Kila kitu kinaenda kwa mipango...Sasa ulitaka ajenge hapo halafu akae Nani??

Pia kuna vijiji ukijenga nyumba nzuri wanakijiji wanakuonea wivu kinachofata ni kurogwa
Usharogwa mara ngapi?
Unaushirikina sana weye unaonekana
 
Back
Top Bottom