Kutana na Luludiva; superstar anayeishi nyumba ya tope

Kutana na Luludiva; superstar anayeishi nyumba ya tope

Mimi nina miliki nyumba nzuri zaidi ya tano na mzazi wangu nimemrekebishia nyumba yake hapa Dar anaishi pazuri. Sisi kwetu kabisa ambapo tutazikwa ni Mtwara na huko sijajenga hata banda la bata.

Ina maana siku nikifa nikipelekwa huko ndio kutakuwa kwangu? Najenga nyumba zitakazoniletea faida nikipangisha, siwezi kujenga wakakae mijusi na mapanya. Kule nitaenda kuzikwa tu. Watotocwangu hawawezi kwenda kuishi Masasi huko kusiko na fursa
Zikwa dar sasa usiende mtwara
 
JAMANI MTU KAUGUZA MAMA YAKE MIAKA 9 UGONJWA USIOPONA
UNATEGEMEA ANGEJENGA VIPI?
ACHANE UNAFIKI BWANA
Gari ananunua vipi?
Acha kutetea kwanza unajua kisa cha mama ake kuumwa vile?
 
Tusipende sana kukosoa kila kitu jamani, dada wa watu kapambana mno kumuuguza mama yake tena kwa muda mrefu, na kuuguza kulivyo gharama sasa..
 
Gari ananunua vipi?
Acha kutetea kwanza unajua kisa cha mama ake kuumwa vile?
Wewe kama una bifu binafsi na huyo binti mfuate. Lakini acha kuleta story za kunanga watu tena watoto wa kike waliojitoa kupambana kutafuta maisha kwa njia yoyote. Shida yako ni gari la Luludiva badala ya nyumba? Hayo ni maamuzi yake, wewe kama unaona nyumba ni muhimu kuliko usafiri ni maamuzi yako hatukukosoi.
 
Wengine wamemtete wakisema eti hapa duniani tunapita hakuna haja ya kujenga

Wengine wakasema amjengee nani wakati alikuwa na mama yake tu?

Kwetu tunasema ujenge nyumba ya kulinda makaburi.

Wengine wakamtete eti yeye akifa atazikwa kwa mme wake,je kama hotooelewa? Au akifa kabla ya hiyo ndoa? Ya mungu mengi simsemi vibaya.

Hatumsemi vibaya ila msanii anaeweza vimba mjini na gari kali atawezaje shindwa hata mili 10 tu ajenge nyumba ya kawaida?

Kama angekuwa sisi watu wa kawaida tusokuwa na mishahara sawa hakuna shida.

Wasanii wanamiliki simu za mil 3 anapanga nyumba ya laki 5 kwa mwezi iweje usahau kuna maisha ya baadae?
Mimi uwa mawachekesha watu ofisini.nawambia mimi kama akitokea mzamini akanininulia macho matatu naiuza nanunua sumsung ya laki 4 wanacheka.

Ni kwakuwa sina hela labda ndo maana nina uchungu na hela.

Kwakweli katia aibu. Na mimi nikifa leo mkaenda nizika home mtacheka kidogo sana kuwa nyumba yetu imepitwa na wakati ila sio tope .na pale nyumbani pembeni msingi nilouweka pale mwezi ulotipa sio wa kitoto mtajua ninakoelekea.

Mi siwezi chezea pesa, hata ikitokea fala moja akanihonga hata laki siku zote elfu 50000 lazima niitume nyumbani, cement kwetu ni 26000, nondo 27000 trip ya mawe 70000, mchanga 60000,boma linataka tofali 20000, nataka msauzi bati 70 leo nianze kutumia macho matatu? Ni upuuzi.
Ningekuwa na nafasi ya kama hawa wasanii ningefanya vitu vya maana sana

Wasanii ni watu wa ovyo kabisa.
Una akili Sana Dada mungu akutie wepesi na ufanikishe hitaji lako kwa hii attitude yako tu wewe ni Shujaa, Mimi nna ndugu zangu wengi wanapambana kuboresha na kujenga majumba yao tu, wanasahau kuwa hata wazazi wao wanahitaji maisha mazuri, Nipo napambana kuhakikisha wazazi wangu wanaishi vizuri
 
Kwanza vya nini vyote hivyo si unaona kadanja kaacha kila kitu[emoji848]
Kusema za ukweli lazima mtu uandae pahala pa kuzikwa. Kama hujajenga bora kueleza ndugu na Jamaica kuwa nikifa zikeni kinondoni full stop. Wewe umeenda lakini aibu unaachia walio hai. By the way nyumba yangu ya kwanza nilijenga kijijini. Usisahau kuna kufiwa na huwezi kukataza au ukachagua watu wa kuhani. Aidha ndugu zangu wa TA mbona mnaniangusha pamoja na mashauzi yenu? Nyumba za tope karne hii hapana
 
Pumba tupe ww umejenga kwenu ebu tuachege unafiki na uwongo

Maisha ya leo huwezi jenga kla sehemu unakaa dar ujenge na kijijini nako ujenge

Kwa kipato kipi cha wasanii ad aweze kujenga kijijini na mjini wapo mabilionea , na Viongozi kibao hawajajenga vijijini kwao acha uyo maskini mwenye jina kubwa
 
Una akili Sana Dada mungu akutie wepesi na ufanikishe hitaji lako kwa hii attitude yako tu wewe ni Shujaa, Mimi nna ndugu zangu wengi wanapambana kuboresha na kujenga majumba yao tu, wanasahau kuwa hata wazazi wao wanahitaji maisha mazuri, Nipo napambana kuhakikisha wazazi wangu wanaishi vizuri
Lakini si kutumia k ili uwajengee wazazi
 
Hiyo hela anayo sasa mkuu...uuguze na bado upige plasta ili watu sijui wasikucheke[emoji848]kumbuka yy ndo first n last born hana wa kumsaidia!

Daaah kama mambo yenyewe ndo haya nawashukuru sana kaka zangu kujenga nyumba mpya kijijini kuzaliwa wa mwisho raha asee[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Kwani lazima uzike kwenu? Kinondoni hakupo? Usisahau kinondoni inakuepusha na hizi fedheha
 
Mastaa wetu sijui wanakwama wapi mjini fujo kibao halafu home miyeyusho
Kupitia kanumba
Agnes masogange
Albert mangwea.

Inaonyesha jinsi gani wasanii wetu wanavyotudanga kwenye mitandao ya ukiwakumbusha unaambulia matusi,

Kuna lile uwoya ndo halijielewi kabisa kila siku lipo hotelini.
Mtoe Ngwea na Kanumba hapo
 
Usanii ni GHARAMA sana. Ukiwa msanii kila jicho linakuangalia wewe, wengi wanakuangalia kwa jicho la kukuhukumu na kutafuta kosa na udhaifu wako, ikitokea umekosea kidogo tu, watu wataongea mazito mpaka yasiyokuwepo.

Wasanii wetu wanahisi maisha ya starehe tunayowaona nayo wanayoigiza kwenye runinga ndiyo wanayotakiwa kuishi mitaani, wanaishi maisha ya starehe kulinda hadhi ya umaarufu wao pasipo kukumbuka kujijenga kimaisha. Mwishowe siku zinapita pesa umechezea kwa starehe halafu hujafanya chochote cha maana.


Wasanii mkumbuke kujiimarisha kiuchumi mapema, na kukumbuka kwenu (kujenga nyumba ya kisasa kwenu).
 
Mimi sioni cha ajabu hapo. Lulu Diva ni mpambanaji tu kama walivyo watu wengi nchi hii.

Alianza kuigiza, mambo yakagoma, akawa video vixen na sasa hivi anakomaa na kuimba.

Sasa sioni popote kama kuna sababu ya kushangaa.
Watu wanashadadia tu ili kupata ahueni ya depression zao
 
Back
Top Bottom