Kutangaza nafasi za ajira kwa watu "Wa ndani ya NSSF" ni Ubaguzi, Rais Samia ingilia kati, unachonganishwa na wananchi!

Ndugu zangu habari ya saa hizi,

Kuna kazi zimetangazwa na NSSF, sasa wamesema kabisa wanaopaswa ku'apply ni wale walio kwenye kazi za mkataba NSSF.

Sasa sisi ambao hatupo kwa nini wanatubagua? Maana hata hao waliopo kwenye kazi za Mkataba wameunganishiwa na ma'godifaza yao.

Watoto wa wakulima hatupaswi kufanya kazi NSSF?

Nimeumia sanaa
 
Tangazo la kazi NSSF limetoka na limetaka wa'apply walio kwenye kazi za mkataba. Sisi tulio nje ambao hatumjui hata muhudumu kutupa kazi za mkataba sio watanzania?

Kwa nini mnatubagua sisi tusio kuwa na mtetezi? Nimekukumbuka Magufuli mtetezi wa wanyonge, ungekuwepo yasingetokea haya kweliView attachment TANGAZO LA KAZI NSSF-3.pdf
 
Kweli kabisa!!
 
CHADEMA hivi wanafanya kazi gani? Hizi si ndio ajenda za kutetea wananchi wa hali ya chini? Ndio maana CCM itazidi kutawala kwa miaka mingi sana sababu ya wapinzani uchwara.
Mimi Binafsi nimepata ajira shilika moja la serikali bila connection yeyote, bila PSRS ingekuwa ndoto isiyowezekana
 
Nafasi za ajira lazima ziwe wazi kwa watanzania wote weye sifa!! Siyo kinyongo bali ni kupigania haki!! Hao waliopewa hiyo mikataba kwanza haikuwa kwenye ushindani wa wazi!! Watu wamepachika ndugu zao hapo, hii haikubaliki!!
Mkuu ni kwamba unakataa format ya Internal Vacant?
hii inafanyika Dunia nzima
 
Jamani hii issue mimi nimeisoma sana yoote na kuielewa mbona wamesema wazi tu kuwa ni wale ambao wanamkataba maalum tu ndio wanaomba kwa maneno mengine ni kazi za ndani sasa hapa kuna ambacho hatuelewi?
 
Jamani hii issue mimi nimeisoma sana yoote na kuielewa mbona wamesema wazi tu kuwa ni wale ambao wanamkataba maalum tu ndio wanaomba kwa maneno mengine ni kazi za ndani sasa hapa kuna ambacho hatuelewi?
Maana yake si walikuwepo na taasisi inawatambua vizuri na taarifa zao zipo, Kwa Nini waombe kama wanatuma Maombi upya wakati ulitakiwa kufanyika mchakato wa ndani tu?

Kama ni kwa watu wa ndani pekee lakini taarifa zimetoka nje ,maana yake Kuna uwezekano taarifa tena za siri kusambaa bila utaratibu?

Anatafutwa nani kutoka nje ikiwa taasisi zina mfumo wa mawasiliano ya kitaasisi, Kwa Nini usingetumika mfumo huo?

Ni kweli kujitolea kunahitaji kufanyiwa hisani kwenye ajira ikiwa kujitolea ni mapenzi ya mtu na hakuna uhusiano wa moja kwa Moja kati ajira na kujitolea?

Kilichofanywa na NSSF kikija kufanywa kwingine na taasisi nyingine, utaendelea kuona ni sawa ?

Nijibu hayo tafadhali
 
Hapo MaHR wanatafuta mkona mrefu....
Maana wameona kwa mama(rais) sasa hivi kila mtu anakula urefu wa kamba yake....
wanataka kutumia ipasavyo ili akija mwingine akibana atakuwa kafaidi haitaleta madhara kwake
 
Jamani hii issue mimi nimeisoma sana yoote na kuielewa mbona wamesema wazi tu kuwa ni wale ambao wanamkataba maalum tu ndio wanaomba kwa maneno mengine ni kazi za ndani sasa hapa kuna ambacho hatuelewi?
Mkuu Kuna rafu nyingi sana hapo nssf, mtiti unaanzia kwanza namna hao watu walivyopatikana anzia volunteer na hao intern bila connection unatoka Kapa, wamefanikiwa Kwa ilo Sasa wameamua wawapitishe directly.
 
Hizo taasisi 28 za kiserikali zilizopatiwa mamlaka 100% kwenye uendeshaji na kujisimamia ,je NSSF haipo?
 
Mambo yote hayo na figisu zote juu ya PSRS wote uo ni uoga pamoja na kwamba PSRS wanamapungufu uzuri ni kwamba yanarekebishika vizuri tu. ni namna tu yakupitisha mamluki wao sababu wanaujua hawamudu mikando ya PSRS, mara kumi elfu waachiwe tu PSRS waendeshe hii michakato ya ajira
 
Mkuu Kuna rafu nyingi sana hapo nssf, mtiti unaanzia kwanza namna hao watu walivyopatikana anzia volunteer na hao intern bila connection unatoka Kapa, wamefanikiwa Kwa ilo Sasa wameamua wawapitishe directly.
Tena jamani inaonekana huyu aliyeleta hapa alikuwa na muhemko tu, shida ya kutoelewa taarifa tuu, hii kitu imejieleza watanzania wenzangu tuwe tunasoma hivi vitu
 
Nimeona hii kitu mdau pamoja na kuweka vifungu vyako vya Sheria hapa

Nafasi za ajira lazima ziwe wazi kwa watanzania wote weye sifa!! Siyo kinyongo bali ni kupigania haki!! Hao waliopewa hiyo mikataba kwanza haikuwa kwenye ushindani wa wazi!! Watu wamepachika ndugu zao hapo, hii haikubaliki!!
Samahani kidogo, wajumbe kuna kitu kinanitatiza hapa kidogo, inamaana hii taarifa sote tunaandika sana hapa hivi hatuoni kilicho andikwa , tuwe tunasoma vizuri kabisa ili tusipotoshe umma
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…