Kutangaza nafasi za ajira kwa watu "Wa ndani ya NSSF" ni Ubaguzi, Rais Samia ingilia kati, unachonganishwa na wananchi!

Kutangaza nafasi za ajira kwa watu "Wa ndani ya NSSF" ni Ubaguzi, Rais Samia ingilia kati, unachonganishwa na wananchi!

Tatizo la watanzania ni kama mandondocha.
Hili jambo lilitarajiwa baada ya tume ya ajira kupokwa mamlàka ya kuajiri na taasisi kutaka zianze kuajiri direct.
Hapa ndipo mlitakiwa kupiga kelele!
Kwasasa ni kelele za chuma tu
Lazima watanzania kwa umoja wetu tukatae huu ubaguzi!! Haiwezekani kodi tulipe wote lakini kundi moja dogo lijifanye kana kwamba NSSF ni yao binafsi!! Wakiachwa wakafanikiwa katika ubaguzi huu Tanzania itakuwa ya mabaka!! Na taasisi zingine zitaiga huu ubaguzi wa NSSF, kijana akimaliza chuo tu anapewa kujitolea mahali au anapewa mkataba halafu baadaye anatangaziwa nafasi za ajira kwa "walioko ndani". Wengine wakimaliza chuo wanabanana mitaani wakati wenzao wameingizwa ndani!!
 
Lazima watanzania kwa umoja wetu tukatae huu ubaguzi!! Haiwezekani kodi tulipe wote lakini kundi moja dogo lijifanye kana kwamba NSSF ni yao binafsi!! Wakiachwa wakafanikiwa katika ubaguzi huu Tanzania itakuwa ya mabaka!! Na taasisi zingine zitaiga huu ubaguzi wa NSSF, kijana akimaliza chuo tu anapewa kujitolea mahali au anapewa mkataba halafu baadaye anatangaziwa nafasi za ajira kwa "walioko ndani". Wengine wakimaliza chuo wanabanana mitaani wakati wenzao wameingizwa ndani!!
Ajira kupitia tume ya ajira ilipunguza sana urasimu pamoja na kuwa hakuna kitu kinakuwa sahihi asilimia mia.
Ni ngumu sana kwa taasisi kuajiri zenyewe direct kukakosekana undugunisation.
Ajira lazima zitaañzia kwa walioajiriwa kwanza.
Mfumo huu wa ajira ndio wakupigia kelele si vinginevyo, tena mapema kabla haujazoeleka.
Hata wakiwaita wote kwenye usaili bado watakaopata ajira ni walengwa tu.
 
Yaan hi ndo hasara yakuamka usingizin ukafungu Jf huku unawashawasha macho.. hapo ndo umeongea nn

Mbona wanaopeleka maombi wanapewa na ndiyo hao waliojitolea kwa muda zaidi ya mwaka sasa ulitaka upewe wewe roho mbaya tu na ulivyo kilaza wewe mtu wa kulialia utawezaje kuwa mtendaji bora, haya ni mashirika yanaendeshwa kwa taratibu hakuna mwenye mamlaka ya kuendesha shirika anavyotaka sio mali ya mtu wala sio ya baba yako ni mali ya umma,
 
Bado naamini PSRS ni sehemu salama zaidi kwenye ajira, PSRS ifanyiwe maboresho makubwa kama kuajiri watumishi wengi wa kuwezesha michakato ya ajira kwa haraka na wepesi lakini hili la Taasisi kuajiri wenyewe malalamiko ni mengi sana na CCM ikifanya mzaha itachochea Chuki na hasira kwa vijana na inaweza kupelekea maamuzi ya hasira 2025.

Kilichofanywa na NSSF kitafanywa kwingine kama kisipodhibitiwa.

1. Mchakato wa ajira uwe wazi na huru kwenye taasisi za serikali hata kama taasisi zinaajiri zenyewe basi pasioneshe namna ya upendeleo wowote.

2. Kujitolea ni sawa lakini kisiwe kigezo Cha ajira maana huko mbeleni tutashuhudia makubwa kwenye kujitolea. Kama kitatumika kama kigezo, nafasi za kujitolea zitaadimika na kufanya zitolewe Kwa upendeleo.

3. Mpaka mtu kaamua kujitolea yanakuwa ni mapaenzi binafsi ya mtu hivyo isitumike kama njia ya kumuajiri moja kwa moja kama kumlipa hisani au fadhila anayefanya hivyo.

Tafadhali Rais Samia tazama hili suala kwa jicho la tatu, rejesha michakato ya ajira UTUMISHI
Umeongea pointi tupu
 
Haiingii akilini NSSF wamepata wapi huu ujeuri wa kuamua kuwatenga na kuwabagua watanzania wengine wote ili kuajiri wateule wao tu waliopewa nafasi kinyemela ya mikataba na kwa gia ya "kujitolea". Lazima nyuma yake kuna vigogo vinasukuma hii agenda nyuma ya pazia!

Haishangazi yalishaanza makelele ya baadhi ya vigogo kuishambulia PSRS kwa kutumia kisingizio cha mapungufu yake ili kupenyeza agenda ya taasisi kuajiri wenyewe!

Tayari baadhi ya mawaziri na wabunge walishaanza kuandaa mazingira kwa kutaka waliojitolea kupewa kipaumbele!! Lakini mbaya zaidi si tu hizi taasisi zinaridhika kwa kuajiri zenyewe, lakini zimeenda mbali zaidi na kuamua kuwatenga na kuwabagua watanzania wengine wote kwenye ajira. Tayari walishaweka watu wao bila ushindani na kuwapa mikataba na sasa wanataka kuwathibitisha.

Hii haikubaliki. Ndio maana tunamwomba Rais Samia alikemee hili kwa nguvu zote, vinginevyo Watanzania wataamini kuwa UBAGUZI HUU UNA BARAKA ZA RAIS!

Ninaamini NSSF huenda wanazo nyingi zaidi, na hizi nafasi 392 za mwanzo ni za kupimia kina cha maji tu. Wakifanikiwa hapo huenda hata matangazo ya kazi kwenye tovuti yao wakaacha kuyatoa, wakawa wanatangaziana tu kwenye magroup yao ya Whatsaap. Sehemu ya tangazo lao hilo hapo chini:

INTERNAL VACANCY ANNOUNCEMENT
National Social Security Fund (NSSF) as part of our commitment to encourage growth anddevelopment within the Fund, we are excited to announce 392 internal job opportunities available for all Fund’s employees with specific task contracts. Only candidates who are inspecific task contract term within the Fund should apply.

Naomba watanzania tulipinge jambo hili kwa nguvu zetu zote, vinginevyo hii nchi itakuwa na matabaka ya WATWANA na WATAWALA. Kama huna mtu huko juu hutakuwa na nafasi ya kupenya hata kama uwezo na sifa unazo.

Wakigoma kubadili msimamo niwaombe mawakili kuomba COURT INJUCTION kusimamisha mchakato huu wa ajira za ubaguzi, huku mkifungua kesi mahakamani kuwatetea watanzania walio wengi ambao hawana "Connection" na wanategemea kupata ajira kupitia ushindani wa wazi na wa haki kwa watanzania wote!
1.samia ni dhaifu hawezi fanya chochote.

2.Ukizingatia pale wamejaa kobazi"Dauism".

3.Hakuna hatua yoyote itakayochukuliwa.

Mungu tumekukosea nini mpaka tunapewa rais dhaifu asiyejali raia wake?
 
Inaumiza sana, inauma sana Iv Sheria ni nini? Democracy ni nini? Tunu za taifa ni nini, kwanini haya mambo wanayapuuza Ivi, dharau za wazi wazi, watu wanalifanya taifa kama familia Yao! Lolote watakalo wanalifanya na hii iwekwe wazi ni dharau kwa Rais wetu, yote haya wanataka kumchafua Tu sio kwa huu uzembe wa NSSF.
 
Tuambie kidogo hiyo manual ya NSSF inasemaje kwenye kuajiri bila kushindanisha watu?

Bila kushindanisha watu?
Nop! Wanashindanishwa watu wa ndani kwanza.
Akikosekana mwenye sifa anatufutwa mtu wa nje.
That is how many employers retain and promote best employees.
Is this new to you?
Gosh!
 
unavyojua ww ubaguzi mpk wa rangi et....
Ila tabaka mwenye nacho na asikuwa nacho hamlioni et....
Hii nchi aliyesema mbinguni ni station ya vituko hajakosea....
Kwa hiyo Samia tunambagua kwa sababu ya tabaka. Samia ni tabaka gani, masikini ?

Mnashindwa kutueleza. Samia tunambagua kwa kipi, Samia ni albino ??????
 
Mtendaji mkuu wa NSSF amevunja katiba ya nchi ibara ya 13, inayokataza ubaguzi wa aina yoyote. Kutangaza ajira kwa kuwabagua baadhi ya waombaji watanzania wenye sifa, huko ni kukiuka katiba ya nchi, AWAJIBIKE AU AWAJIBISHWE!!

Katiba nya Jamhuri ya muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, ibara ya:
13(4). Ni marufuku kwa mtu yeyote kubaguliwa na mtu au na mamlaka yoyote inayotekeleza madaraka yake chini ya sheria yoyote au katika utekelezaji wa kazi au shughuli yoyote ya mamlaka ya nchi.

NSSF imekiuka klifungu hiki cha katiba ya nchi yetu kwa kuwabagua watanzania wengine wote wenye sifa za kuomba ajira zilizotangazwa pale NSSF, na kuwapendelea watanzania waliomo ndani ya NSSF aidha kwa kujitolea au kwa mikataba mifupi (ambao bila shaka waliingia humo kwa kupendelewa pia-uchunguzi inabidi ufanyike) ili wao pekee ndio waziombe nafasi hizo za ajira!

Inabidi Mtendaji mkuu wa NSSF ajiuzulu kwa kuvunja katiba ya nchi yetu! Hili jambo siyo dogo, na wakilipuuzia tutaenda mahakamani!! Maana haki, wajibu na maslahi ya kila mtu hulindwa na mahakama kwa mujibu wa ibara ya 13(3) ya katiba ya nchi nyetu inayosema: Haki za raia, wajibu na maslahi ya kila mtu na jumuiya ya watu yatalindwa na kuamuliwa na mahakama na vyombo vinginevyo vya mamlaka ya nchi vilivyowekwa na sheria au kwa mujibu wa sheria.



NSSF - government private ATM (?)

Mahakama - government (conveniently) toothless dog (?)




Tuendelee ‘kumuomba’ Rais Samia.
 
sana kwa taasisi kuajiri zenyewe direct kukakosekana undugunisation.
Ajira lazima zitaañzia kwa walioajiriwa kwanza.
Mfumo huu wa ajira ndio wakupigia kelele
Eti leo ndio tumeamka.

Siku ile Rais alipotangaza mashirika yaajiri yenyewe hakuna aliyehoji.

Maamuzi makubwa makubwa ya kitaifa anaachiwa yule Mama. Watu Milioni 60 tunaweka rehani maisha yetu kwenye kichwa cha mtu mmoja.

Dhana na zama za "Zidumu Fikra za Mwenyekiti wa Chama" bado tunazo.
 
JENGA nchi inayotawaliwa na mifumo, na taasisi, na taratibu za kitawala na kisheria.

Kwa nini unarukia kwa Samia akuhurumie ??? What if she doesn't give a fvck ??? Samia kasema juzi Mtwara hana muda wa vidukuduku vyenu, mambo ni mengi na Tanzania ni kubwa! Matatizo yako na mapambano yako na hali yako peleka kwa Mbunge! Ndio mentality ya Rais!

Una hakika gani kama Samia hana mentality hizi hizi za wakubwa wa NSSF ???

Samia ndio alisema hadharani mashirika yaajiri yenyewe, hata hajui na hajali kwa nini ajira zilirudishwa UTUMISHI. Kama alivyosema Dr. Nshala, Rais hajui Uchifu ulifutwa lini na kwa nini, yeye kaurudisha tu Uchifu ghafla bila maelezo, hajui historia ya nchi, haelewi, hajali!

Rais hakueleza serikali yake ita mitigate vipi athari za mashirika kuajiri yenyewe, she don't give a rats ass!!! Get a clue! Nenda mahakamani!

Us common wananchi still believe in huruma ya Rais.

Bado tunaogopa hata Mahakama tukidhani ni nyumba ya wahalifu na majambazi tu.


Elimu ya kujitambua na kutambua haki na wajibu ilifutwa ama haikuwahi kuwepo?

Kila mtu analia hakuna aliye tayari kutuonyesha kwa vitendo haswa.
 
Mtu kajitolea kifanya kazi muda mwingine anapewa hela ya nauli tu leo ajira zimetoka akose dah inaumiza bora wawe kipaumbele nao wasuuzike nafsi. Mtu kajitolea zaidi ya mwaka anasugua tu hajui lininataajiriwa na bado anapiga kazi leo kashaizoea kazi na bahatinimekuja mnataka kuziba rizikinyake.
Shida hakuna namna nzuri ya kupata hizo ajira za kujitolea
Watu wanatumia gap hilo kuingiza ndugu zao
 
Eti leo ndio tumeamka.

Siku ile Rais alipotangaza mashirika yaajiri yenyewe hakuna aliyehoji.

Maamuzi makubwa makubwa ya kitaifa anaachiwa yule Mama. Watu Milioni 60 tunaweka rehani maisha yetu kwenye kichwa cha mtu mmoja.

Dhana na zama za "Zidumu Fikra za Mwenyekiti wa Chama" bado tunazo.
Hizo ni dharau sasa.
Hayo maamuzi ulitaka uachiwe wewe
Kumbe ni mjinga sana wewe
 
Back
Top Bottom