Kutangaza nafasi za ajira kwa watu "Wa ndani ya NSSF" ni Ubaguzi, Rais Samia ingilia kati, unachonganishwa na wananchi!

Kutangaza nafasi za ajira kwa watu "Wa ndani ya NSSF" ni Ubaguzi, Rais Samia ingilia kati, unachonganishwa na wananchi!

Haiingii akilini NSSF wamepata wapi huu ujeuri wa kuamua kuwatenga na kuwabagua watanzania wengine wote ili kuajiri wateule wao tu waliopewa nafasi kinyemela ya mikataba na kwa gia ya "kujitolea". Lazima nyuma yake kuna vigogo vinasukuma hii agenda nyuma ya pazia!

Haishangazi yalishaanza makelele ya baadhi ya vigogo kuishambulia PSRS kwa kutumia kisingizio cha mapungufu yake ili kupenyeza agenda ya taasisi kuajiri wenyewe!

Tayari baadhi ya mawaziri na wabunge walishaanza kuandaa mazingira kwa kutaka waliojitolea kupewa kipaumbele!! Lakini mbaya zaidi si tu hizi taasisi zinaridhika kwa kuajiri zenyewe, lakini zimeenda mbali zaidi na kuamua kuwatenga na kuwabagua watanzania wengine wote kwenye ajira. Tayari walishaweka watu wao bila ushindani na kuwapa mikataba na sasa wanataka kuwathibitisha.

Hii haikubaliki. Ndio maana tunamwomba Rais Samia alikemee hili kwa nguvu zote, vinginevyo Watanzania wataamini kuwa UBAGUZI HUU UNA BARAKA ZA RAIS!

Ninaamini NSSF huenda wanazo nyingi zaidi, na hizi nafasi 392 za mwanzo ni za kupimia kina cha maji tu. Wakifanikiwa hapo huenda hata matangazo ya kazi kwenye tovuti yao wakaacha kuyatoa, wakawa wanatangaziana tu kwenye magroup yao ya Whatsaap. Sehemu ya tangazo lao hilo hapo chini:

INTERNAL VACANCY ANNOUNCEMENT
National Social Security Fund (NSSF) as part of our commitment to encourage growth anddevelopment within the Fund, we are excited to announce 392 internal job opportunities available for all Fund’s employees with specific task contracts. Only candidates who are inspecific task contract term within the Fund should apply.

Naomba watanzania tulipinge jambo hili kwa nguvu zetu zote, vinginevyo hii nchi itakuwa na matabaka ya WATWANA na WATAWALA. Kama huna mtu huko juu hutakuwa na nafasi ya kupenya hata kama uwezo na sifa unazo.

Wakigoma kubadili msimamo niwaombe mawakili kuomba COURT INJUCTION kusimamisha mchakato huu wa ajira za ubaguzi, huku mkifungua kesi mahakamani kuwatetea watanzania walio wengi ambao hawana "Connection" na wanategemea kupata ajira kupitia ushindani wa wazi na wa haki kwa watanzania wote!
Tafadhali mekeni na kwenye mitandao mingine yakijamii ili tukatag watu nakushare mpaka waone aibu hawaaa
 
Serikali ya CCM ni afadhalii ikachezaa na vitu vyote ila sio kufanya mchezo na jobless,,NSSF wanatuletea takataka zao hizo eti ni tangazo la kazi bila hata AIBU,,,,Mkurugenzii wa NSSF atujibu kuwa ni lini walitangaza hizo nafasii za mikataba,,,UPUUZI huu haukubalikii hata kidg tutaukataa kwa nguvuu zotee
Moto utawaka!! Mtu ataridhika akikosa kazi kwenye ushindani wa wazi, siyo kwa kubaguliwa namna hii mchana kweupe!
 
Aliyesababisha haya yote ni mtu mmoja alipewa shirika aendesha akafanya kama vile ni la familia yake.
Alianza kuondoa wote waliotumikia kwa mda mrefu na kuleta wengine wengi zaidi ya 500 ambao alidhani angewamudu kuwa endesha atakavyo kwa mikataba mifupi.
Na hao waliopewa hyo mikataba walipewa kufanya kazi very sensitive.
Wengi wao ndo wameambiwa waombe kazi ili wapate permanent employment.
Huyo nae alikuta tatizo ambalo lilianzia Kwa Dr.Dau Kwa kutumia njia hiyo hiyo kuwabagua wagalatia,na kujaza jamaa wa Imani Kali wakageuza NSSF ni ya kwao
 
Watoe fair competition kwa wote wenye sifa.
Haiwezekani mtumishi ndani ya taasisi ajira yake education level ilikuwa diploma,then aka upgrade na kuwa bachelor holder. Halafu nafasi inapatikana ya mtu mwenye bachelor utegemee achukuliwe wa nje ya taasisi, hiyo never. Na ndio maana Kuna internal recruitment
 
Mtu kajitolea kifanya kazi muda mwingine anapewa hela ya nauli tu leo ajira zimetoka akose dah inaumiza bora wawe kipaumbele nao wasuuzike nafsi. Mtu kajitolea zaidi ya mwaka anasugua tu hajui lininataajiriwa na bado anapiga kazi leo kashaizoea kazi na bahatinimekuja mnataka kuziba rizikinyake.
Sasa kama that is the CASE, kwann wanaojitolea taasisi nyengine wasiruhusiwe kuomba ?? Wakati wote ni wanajitolea??? Yani kwann anayejitolea Halmashauri asiombe?? Wakati zikitoka za Halmashauri huyo wa NSSF Ataomba.
 
Kwa kawaida kwa nafasi zilizo nyingi mchakato wa usaili huwa na hatua mbili: 1. Usaili wa kuandika (written), 2. Usaili wa mahojiano (oral). Kwa sasa kwenye written nafasi moja hugombaniwa na watu wasiopungua 100 (kwa uchache). Kwa hiyo hizo nafasi 392 kwenye hatua ya written inabidi zigombaniwe na watu 39,200. Ina maana huko NSSF kuna watu wa mikataba na wa kujitolea zaidi ya 30,000? Kama sivyo, kwa nini warahisishiwe hivyo wakati kuna malaki ya watanzania wanaotafuta ajira? Kwa nini hawa wapendelewe kwa kuepushwa na ugumu wanaokabiliana nao waombaji wengine kupitia PSRS?

Hata kama huko NSSF wataamua kusiwe na written baliu ni oral tu, hata hivyo kwa sasa nafasi moja kwenye oral huwa inagombaniwa na waombaji wasiopungua 5, ina maana huko NSSF kuna wjitoleaji na watu wa mikataba zadi ya 1,900? Hiyo mikataba ilitangazwa wapi? hizo nafasi za kujitolea zilitangazwa wapi? Hii haikubaliki hata kidogo!! Ninachokiona ni baadhi ya "wateule" kupita bila kupingwa maana hakuna wapinzani!! Hii haikubaliki hata kidogo!!! Kuna mtu asiyejua kuwa kuna malaki ya wasaka ajira mitaani tena wenye sifa stahiki kabisa!!
 
Haiwezekani mtumishi ndani ya taasisi ajira yake education level ilikuwa diploma,then aka upgrade na kuwa bachelor holder. Halafu nafasi inapatikana ya mtu mwenye bachelor utegemee achukuliwe wa nje ya taasisi, hiyo never. Na ndio maana Kuna internal recruitment
Internal recruitment ni kwa wale wenye ajira tayari! Akijiendeleza ndani ya ajira na kupata degree kwa mfano, huyo anafanyiwa re-categorization!! Hakuna internal recruitment kwenye ajira mpya!! Patachimbika hadi mahakama ya rufaa ikibidi!! Wasipotrusikiliza, mchakato wa ajira utasimamishwa kwa COURT INJUCTION!! hadi pale kesi ya msingi ya tuhuma za kutaka kuajiri kwa misingi ya ubaguzi kinyume na katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ibara ya 13(1&4), itakaposikilizwa na kufanyiwa maamuzi.
 
Huyo nae alikuta tatizo ambalo lilianzia Kwa Dr.Dau Kwa kutumia njia hiyo hiyo kuwabagua wagalatia,na kujaza jamaa wa Imani Kali wakageuza NSSF ni ya kwao
Naomba sana huko kwenye udini tusiingie, kutatuondolea mshikamano wetu.!! Hapa wamebaguliwa dini zote walio nje ya NSSF kwa sasa!! Wanataka kuifanya NSSF kama familia fulani ya wateule fulani!!
 
Mtu kajitolea kifanya kazi muda mwingine anapewa hela ya nauli tu leo ajira zimetoka akose dah inaumiza bora wawe kipaumbele nao wasuuzike nafsi. Mtu kajitolea zaidi ya mwaka anasugua tu hajui lininataajiriwa na bado anapiga kazi leo kashaizoea kazi na bahatinimekuja mnataka kuziba rizikinyake.
Hiyo nafasi ya kujitolea iko sawa kwa wote?
Wapi wanaotaka kujitolea na hawapati nafasi hizo.
 
Haiingii akilini NSSF wamepata wapi huu ujeuri wa kuamua kuwatenga na kuwabagua watanzania wengine wote ili kuajiri wateule wao tu waliopewa nafasi kinyemela ya mikataba na kwa gia ya "kujitolea". Lazima nyuma yake kuna vigogo vinasukuma hii agenda nyuma ya pazia!

Haishangazi yalishaanza makelele ya baadhi ya vigogo kuishambulia PSRS kwa kutumia kisingizio cha mapungufu yake ili kupenyeza agenda ya taasisi kuajiri wenyewe!

Tayari baadhi ya mawaziri na wabunge walishaanza kuandaa mazingira kwa kutaka waliojitolea kupewa kipaumbele!! Lakini mbaya zaidi si tu hizi taasisi zinaridhika kwa kuajiri zenyewe, lakini zimeenda mbali zaidi na kuamua kuwatenga na kuwabagua watanzania wengine wote kwenye ajira. Tayari walishaweka watu wao bila ushindani na kuwapa mikataba na sasa wanataka kuwathibitisha.

Hii haikubaliki. Ndio maana tunamwomba Rais Samia alikemee hili kwa nguvu zote, vinginevyo Watanzania wataamini kuwa UBAGUZI HUU UNA BARAKA ZA RAIS!

Ninaamini NSSF huenda wanazo nyingi zaidi, na hizi nafasi 392 za mwanzo ni za kupimia kina cha maji tu. Wakifanikiwa hapo huenda hata matangazo ya kazi kwenye tovuti yao wakaacha kuyatoa, wakawa wanatangaziana tu kwenye magroup yao ya Whatsaap. Sehemu ya tangazo lao hilo hapo chini:

INTERNAL VACANCY ANNOUNCEMENT
National Social Security Fund (NSSF) as part of our commitment to encourage growth anddevelopment within the Fund, we are excited to announce 392 internal job opportunities available for all Fund’s employees with specific task contracts. Only candidates who are inspecific task contract term within the Fund should apply.

Naomba watanzania tulipinge jambo hili kwa nguvu zetu zote, vinginevyo hii nchi itakuwa na matabaka ya WATWANA na WATAWALA. Kama huna mtu huko juu hutakuwa na nafasi ya kupenya hata kama uwezo na sifa unazo.

Wakigoma kubadili msimamo niwaombe mawakili kuomba COURT INJUCTION kusimamisha mchakato huu wa ajira za ubaguzi, huku mkifungua kesi mahakamani kuwatetea watanzania walio wengi ambao hawana "Connection" na wanategemea kupata ajira kupitia ushindani wa wazi na wa haki kwa watanzania wote!
Nenda ukajitolee baada miaka 3....utaajiriwa zikitoka tena
 
Wanachuo wangapi wanataka kujitolea wanakosa kaangalie ule mfuko TAES walivyojaa na nafasi hawapi.

A fair competition kama waliofanya TAA ni nafasi za mda ila tangazo lipo kila mtu aombe .....Wapo watu wamejitolea wanafanya kazi hata majibu ya chuo hajatoka yaani baada ya kumaliza UE ...Niliona watu kibao wakifanya hivyo mwaka wetu tuliomaliza na wamepata kwa connection tena Taasisi za serikali hata field walifanyiw humo.

Usichokijua na wengi hawajui , Taasisi za serikali kama zote zinatoa intership ila inakuwa ni ishu ya internal recruiting ndio maana haiko fair ,leo unaenda kuomba unakuta tangazo kwa HR hakuna nafasi za kujitolea ,ila wengine wanakuja baada yako na wanapiga fresh kisa ndugu au connection.
Uko sahihi sana.
 
Hapa tutaona kama serikali yetu ni sikivu kama ambavyo huwa inadai. Haiwezekani taasisi inayogharimiwa na kodi za watanzania wote, iamue kuwatenga na kuwabagua watanzania walio wengi kwenye ajira!!
Ila hili pendekezo mbona hata bungeni lilitolewa na Spika....mlipiga kelele? Huenda watu ndio wanafanyia kazi ushauri kifupi siki hiz kupata kazi ni kazi. Walianza na vigezo vya kupita JKT...watu wakawa wanapigwa chini...sa hii imeletwa gia mpya! KUJITOLEA. Tutanyoooka tu😅😅😅
 
Ila hili pendekezo mbona hata bungeni lilitolewa na Spika....mlipiga kelele? Huenda watu ndio wanafanyia kazi ushauri kifupi siki hiz kupata kazi ni kazi. Walianza na vigezo vya kupita JKT...watu wakawa wanapigwa chini...sa hii imeletwa gia mpya! KUJITOLEA. Tutanyoooka tu😅😅😅
Tulipiga kelele ndiyo, na sasa wataona kuwa kumbe makelele yetu hayakuwa ya mchezo!! Huyo spika naye ni wa kumhurumia tu!! Yuko pale kutumiwa!!
 
Internal recruitment ni kwa wale wenye ajira tayari! Akijiendeleza ndani ya ajira na kupata degree kwa mfano, huyo anafanyiwa re-categorization!! Hakuna internal recruitment kwenye ajira mpya!! Patachimbika hadi mahakama ya rufaa ikibidi!! Wasipotrusikiliza, mchakato wa ajira utasimamishwa kwa COURT INJUCTION!! hadi pale kesi ya msingi ya tuhuma za kutaka kuajiri kwa misingi ya ubaguzi kinyume na katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ibara ya 13(1&4), itakaposikilizwa na kufanyiwa maamuzi.

Huyo jamaa anadhani wote humu tuna akili kama zake, inawezekana nae anasubiri kula pande huko NSSF kupitia tanngazo lao.
 
Back
Top Bottom