Pre GE2025 Kutofautiana kauli na mtizamo wa Katibu Mkuu na Mwenezi CCM kunaashiria nini kuelekea Uchaguzi?

Pre GE2025 Kutofautiana kauli na mtizamo wa Katibu Mkuu na Mwenezi CCM kunaashiria nini kuelekea Uchaguzi?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Salaam, Shalom!!

Katibu MKUU wa CCM ameanza ziara yake kivyake na anasema yake, wakati huo huo Mwenezi naye ameendelea na uelekeo wake.

KM anasema, viongozi wa CCM wasiwakaripie hadharani watendaji wa Serikali, wakati huo huo Mwenezi Yeye ameendelea kupiga simu akiwahoji na Kutoa maelekezo.

Swali ni je; upi uelekeo wa chama kuelekea uchaguzi?

Wanajenga taswira Gani Kwa wanachama na wananchi?

Karibuni [emoji120]
Yaache yaparurane

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nchimbi yeye anapenda sana mambo ya sirini ili na yeye apewe hongo na watendaji wazembe serekalini, we need a transparent government ! Makonda yuko sahihi!!
Ndo tunataka uelekeo na muono wa pamoja.

Wakae na kuelewana.
 
Umenisoma vizuri? Mkuu rudia tena. Nimesema kuwa kwenye nchi ya ma-nyumbu, usanii wa Bashite hupendwa zaidi kuliko wachapakazi wa kweli. Huu ni ukweli mchungu. Nikuulize: Huko Bashite anakopita kila siku tena na msafara wa kitajiri akijifanya kutatua matatizo, kwa nini anapata wasikilizaji wengi kabisa na wengine wanafikia hatua ya kumlilia shida zao? Jibu ni kwamba wananchi hawana upeo wa kuona kuwa hata huyo Bashite na msafara wake, na ufanyajikazi wake ndiye anasababisha matatizo wanayotaka yatatuliwe. Kwa kifupi ni kwamba wananchi wanaliangukia na kulisihi tatizo kubwa liwatatulie matatizo yao madogo madogo.
Watanzania wengi sana bado hawajaelewa kuwa Makonda anafanya mazingaombwe tu.
 
Watanzania wengi sana bado hawajaelewa kuwa Makonda anafanya mazingaombwe tu.
Ikiwa Mwenezi anaigiza,

Nani Hasa anatetea maslah ya Wananchi ndani ya chama bila kuigiza?
 
Chama chenyewe ni Chama Cha Maigizo.
Ikiwa chama Cha KIJANI ni Cha maigizo,

Basi Mwenezi ni Actor mzuri!!

Na ikiwa ndivyo ilivyo, basi wakae chini na kutengeza script ya pamoja.
 
Ikiwa chama Cha KIJANI ni Cha maigizo,

Basi Mwenezi ni Actor mzuri!!

Na ikiwa ndivyo ilivyo, basi wakae chini na kutengeza script ya pamoja.
Huyu Mwenezi alikuwa bench, wakamuita, huku wakimjua. Wamepanga yote haya.
 
Huyu Mwenezi alikuwa bench, wakamuita, huku wakimjua. Wamepanga yote haya.
Najiuliza huo mpango, unamnufaisha au kumuharibia mkt Kwa kiwango Gani?

Umeme, sukari nk nk Bado kizumgumkuti pamoja na maigizo yote!!
 
KM anasema, viongozi wa CCM wasiwakaripie hadharani watendaji wa Serikali, wakati huo huo Mwenezi Yeye ameendelea kupiga simu akiwahoji na Kutoa maelekezo.

Nini maana ya kukaripia?
 
Najiuliza huo mpango, unamnufaisha au kumuharibia mkt Kwa kiwango Gani?

Umeme, sukari nk nk Bado kizumgumkuti pamoja na maigizo yote!!
Sasa maigizo si ndiyo yawawaondoa watu katika reli?

Mshairi mahiri wa enzi za Warumi aliyeitwa Juvenal, katika kitabu chake cha "Kejeli Namba 10" (Satires X), aliandika kwamba, ili kuwatawala watu simple, wape vitu viwili. Mkate (chakula cha chini kabisa kwa Warumi, kama Ugali kwetu) na michezo ya sarakasi (circuses).

Maana yake watakula kuondoa njaa, wakishiba watatazama sarakasi. Hakuna atakayetaka mabadiliko ya uongozi wala uchumi.

Sasa sisi naona tunapata sarakasi tupubila hata chakula.
 
Katibu Mwenezi wa chama tawala amemuagiza waziri wa Tamisemi kumsimamisha KAZI mkurugenzi wa Pangani haraka.

Cc: Lucas mwashambwa
Mheshimiwa Makonda ni mtetezi wa wanyonge.ni sauti ya wanyonge.ni Kiongozi anayezungumza yake yaliyo katika vifua na mioyo ya watanzania.ndio maana unaona namna watu wanavyofurika na kumiminika katika mikutano yake ili kupeleka kero zao .
 
Elewa jambo ccm hata watofautiane vip linapokuja swala la uchaguzi niwamoja so achana nao
Siwezi kuwaacha, nawasaidia wananchi kujua mbivu na mbichi.

Chama kimoja njia na uelekeo unaokinzana!!
 
Makonda mmoja ni sawa na mkusanyiko wa kamati kuu nzima ya CHADEMA na bado wataburuzwa tu. Kwa sasa nchi nzima imetega masikio na kuelekeza macho yake katika ziara za Mheshimiwa Makonda kufuatilia kinachojili huko.
 
Mheshimiwa Makonda ni mtetezi wa wanyonge.ni sauti ya wanyonge.ni Kiongozi anayezungumza yake yaliyo katika vifua na mioyo ya watanzania.ndio maana unaona namna watu wanavyofurika na kumiminika katika mikutano yake ili kupeleka kero zao .
Mamlaka ya kuagiza waziri wa Tamisemi kumfuata KAZI mkurugenzi wa Pangani yameainishwa kifungu kipi katika KATIBA ya chama Cha MAPINDUZI CCM?
 
Makonda mmoja ni sawa na mkusanyiko wa kamati kuu nzima ya CHADEMA na bado wataburuzwa tu. Kwa sasa nchi nzima imetega masikio na kuelekeza macho yake katika ziara za Mheshimiwa Makonda kufuatilia kinachojili huko.
CHADEMA haiongelewi hapa🙏
 
Back
Top Bottom