Kutoka 21:10 huu ni uzinzi au ndoa ya mke zaidi ya moja ilikuwa halali?

Kutoka 21:10 huu ni uzinzi au ndoa ya mke zaidi ya moja ilikuwa halali?

R-K-O

JF-Expert Member
Joined
Jun 27, 2023
Posts
482
Reaction score
2,178
Kutoka 21:10

Kama huyo bwana akioa mke mwingine, lazima aendelee kumtosheleza mkewe wa kwanza kwa chakula, mavazi na haki zake za ndoa.

Hata mitume na manabii wapo waliooa wake wengi, je walikuwa wanazini?

Kinachofatwa ni maandiko au tamaduni za Ulaya ambazo ilibidi makanisa yalioanzishwa Ulaya yafate?
 
Kutoka 21:10

Kama huyo bwana akioa mke mwingine, lazima aendelee kumtosheleza mke we wa kwanza kwa chakula, mavazi na haki zake za ndoa.

Hata mitume na manabii wapo waliooa wake wengi, je walikuwa wanazini?

Kinachofatwa ni maandiko au tamaduni za ulaya ambazo ilibidi makanisa yalioanzishwa ulaya yafate?
Wewe soma Mkwawa alikuwa na wake wangapi? Mirambo wake wangapi? Bwana Heri wake wangapi? Mangi Meli,Mangi sina kinjikitile Ngwale utafaidika zaidi kumbuka ndoa zao hazijawahi vunjika na zilikuwa na ubora wa viwango vya juu.

Amka toka huko usingizini na kufikiri kitabu cha kurejea ni hicho tu . Laibon Laizer kufunga ndoa na wake wanne utajiri wa kutosha watoto wengi tena nidhamu ya juu kabisa unahangaika na mambo ya kufikirika mpaka wanaanza kusema mpandane sijui subiria mwezi shenzi kabisa.

Tokea mpaka kuzaliwa mpaka kufa Afrika imejitosheleza katika Imani na ndiyo maana walivyoleta Imani Shaka Zulu wakamwambia tenda abudu Mungu nje ya hapo utachomwa moto Shaka Zulu akamueleza Afrika tunakula moto na bado haujatuchoma Tokeni hapa.
Karibu Afrika
 
Tena wanaume wakiuona watasema kumbe ni ruhusa kuwa na wanawake wawili😅
haya makanisa huwa yanakwepa kujikanyaga hii mistari ni mwiko kuhubiri, wanajua hatari ya wafu wengi kuanza kuhoji
 
Na wanawake saba watamshika mume mmoja, nakusema tule kwa chakula chetu ila tuitwe kwa jina lako .
Ndiyo shida ya kusoma Biblia kama gazeti. Biblia imeandikwa kimafumbo inabidi utulize akili ili upate maana kamili. Tafuta nyoka au nge umkanyage kwasababu umepewa mamlaka

Luka 10:19​

" Nimewapa mamlaka ya kukanyaga nyoka na nge na kushinda nguvu zote za yule adui; wala hakuna kitu cho chote kitakachoweza kuwadhuru".​

 
Ndiyo shida ya kusoma Biblia kama gazeti. Biblia imeandikwa kimafumbo inabidi utulize akili ili upate maana kamili. Tafuta nyoka au nge umkanyage kwasababu umepewa mamlaka

Luka 10:19​

" Nimewapa mamlaka ya kukanyaga nyoka na nge na kushinda nguvu zote za yule adui; wala hakuna kitu cho chote kitakachoweza kuwadhuru".​

Mbona tunawakanyaga sana tu mpaka wanakufa
 
Inakupasa uanze kusoma kuanzia mstari wa kwanza ndo utaelewa vizuri hicho kifungu vizuri na utapata kuelewa ni sheria gani ilikuwa inawekwa hapa na Musa..zingatia hiyo mikolezo..
 
noma sana
Isaya 4: 1
"Na siku hiyo wanawake saba watamshika mtu mume mmoja wakisema, Tutakula chakula chetu, na kuvaa nguo zetu wenyewe, lakini tuitwe tu kwa jina lako; utuondolee aibu yetu"
Ukisoma Biblia kama gazeti huwezi kupata maana kamili na utaishia kupata maana isiyo sahihi
Soma vizuri huo mstari mwisho unasema utoondelee aibu yetu? kwanini wanasema utoondelee aibu yetu?
Mungu hajaruhusu ndoa ya wake wengi, ameruhusu ndoa ya mke mmoja na mme mmoja tu. Amri kuu ya ndoa ilianza kwa Adamu na Eva kwenye bustani ya Edeni.
Mwanzo 2:22-25
"na ule ubavu alioutwaa katika Adamu BWANA Mungu akaufanya mwanamke, akamleta kwa Adamu. Adamu akasema, Sasa huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu, basi ataitwa mwanamke, kwa maana ametwaliwa katika mwanamume. Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja. Nao walikuwa uchi wote wawili, Adamu na mkewe, wala hawakuona haya"

Turudi kwenye mstari wako.
Huu mstari ni kama ilitabiriwa itakuwa hivyo ila haijaruhusiwa kuwa na mwanamke zaidi ya mmoja.
Baada ya binadamu kuingia kwenye dhambi, akamuasi Mungu na kufuata matendo yao. Tamaa zikawa miongoni mwao ndiyo tunaona haki sawa kwa wanawake na mwanaume, wanawake wanataka mtu mwenye mali, hela, anajua kuoga, wanadanga, wanavaa nguo nusu uchi, wanaanza mapenzi wakiwa kwenye umri mdogo n.k
"Utakuta mwanamke anasema mimi naingiza milion 20 kwa mwezi na mwanaume anaingiza laki 5 kwa mwezi, unataka nikufulie nguo? Haiwezekani." Mwanamke kama huyu unaweza kumuoa? huwezi hata kumtuma akuletee maji ya kunywa. Ndiyo hao baadae watajikusanya wakitaka waolewe lakini watajihudumia wenyewe
Wanawake wanamali lakini matendo yao maovu na wamekosa watu wa kuwaoa kwasababu hawana sifa ndiyo unapata mstari utuondolee aibu yetu" Utakuta mwanamke anasema, nipe mimba nilee ili mradi tu awe na mtoto.
Jitahidini kusoma Biblia vizuri na haisomwi kama gazeti
 
Kutoka 21:10

Kama huyo bwana akioa mke mwingine, lazima aendelee kumtosheleza mke we wa kwanza kwa chakula, mavazi na haki zake za ndoa.

Hata mitume na manabii wapo waliooa wake wengi, je walikuwa wanazini?

Kinachofatwa ni maandiko au tamaduni za Ulaya ambazo ilibidi makanisa yalioanzishwa Ulaya yafate?
Mathayo 19:1-11
1 Ikawa Yesu alipomaliza maneno hayo, akatoka Galilaya akafika mipaka ya Uyahudi, ng'ambo ya Yordani.
2 Makutano mengi wakamfuata, akawaponya huko.
3 Basi Mafarisayo wakamwendea, wakamjaribu, wakimwambia, Je! Ni halali mtu kumwacha mkewe kwa kila sababu?
4 Akajibu, akawaambia, Hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba mtu mume na mtu mke,
5 akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja?
6 Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe.
7 Wakamwambia, Jinsi gani basi Musa aliamuru kumpa hati ya talaka, na kumwacha?
8 Akawaambia, Musa, kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu, aliwapa ruhusa kuwaacha wake zenu; lakini tangu mwanzo haikuwa hivi.
9 Nami nawaambia ninyi, Kila mtu atakayemwacha mkewe, isipokuwa ni kwa sababu ya uasherati, akaoa mwingine, azini; naye amwoaye yule aliyeachwa azini.
10 Wanafunzi wake wakamwambia, Mambo ya mtu na mkewe yakiwa hivyo, haifai kuoa.
11 Lakini yeye akawaambia, Si wote wawezao kulipokea neno hili, ila wale waliojaliwa.
MAANA YAKE
Hutakiwi umuache mkewe isipokuwa kwa uasherati tu. Kama umemfuma kwa uasherati na ukavunja ndoa basi unatakiwa hudumie famili yako mtoto/watoto ukipendezwa na mkeo ila si kuingiliana kimwili. Kwasababu tayari umemuacha, hapo utakuwa umeoa mke mwingine ila kama umemsamehe hautakiwi kuoa mwanamke mwingine kwasababu unafanya uasherati (wazini).
Turudi kwenye mstari wako, hapa umeoa na ndoa yako haijavunjika na una mke mwingine. Ndoa inayotambulika ni ya yule ya mke wa kwanza tu (elewa). Ya mke wa pili utakuwa unafanya usherati kwahiyo unatakiwa uendelee kumhudumia mke wako wa kwanza kwa kila kitu na umtosheleze kwa mahitaji yake kwasababu ndiyo Mungu anayoitambua. Ila mke wa pili haitambuliwi na unafanya uasherati. Ukiamwacha ukahamia kwa mke wa pili bado unaendeleza ushaerati (wazini). Unatakiwa umhudumie mkeo wa kwanza kwa kila kitu.
Ndoa ya mke wa pili haijaruhusiwa ndiyo maana Mungu anatambua ndoa ya mke mmoja na mume mmoja ile ya kwanza na hutakiwi umuache. Mhudumie
Someni Biblia vizuri. Biblia haisomwi kama gazeti.
 
Thubutu! .
Someni Biblia vizuri, Biblia haisomwi kama gazeti. Ndiyo maana mnapata maana tofauti
Usifanye maisha kuwa magumu, sio kila mstari lazima uwe na maana zaidi ya moja. Hao nge na nyoka huku kiumeni tunawakanyaga ile mbaya na hawatoboi
 
Thubutu! .
Someni Biblia vizuri, Biblia haisomwi kama gazeti. Ndiyo maana mnapata maana tofauti
Usifanye maisha kuwa magumu, sio kila mstari lazima uwe na maana zaidi ya moja. Hao nge na nyoka huku kiumeni tunawakanyaga ile mbaya na hawatoboi
 
Mathayo 19:1-11
1 Ikawa Yesu alipomaliza maneno hayo, akatoka Galilaya akafika mipaka ya Uyahudi, ng'ambo ya Yordani.
2 Makutano mengi wakamfuata, akawaponya huko.
3 Basi Mafarisayo wakamwendea, wakamjaribu, wakimwambia, Je! Ni halali mtu kumwacha mkewe kwa kila sababu?
4 Akajibu, akawaambia, Hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba mtu mume na mtu mke,
5 akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja?
6 Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe.
7 Wakamwambia, Jinsi gani basi Musa aliamuru kumpa hati ya talaka, na kumwacha?
8 Akawaambia, Musa, kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu, aliwapa ruhusa kuwaacha wake zenu; lakini tangu mwanzo haikuwa hivi.
9 Nami nawaambia ninyi, Kila mtu atakayemwacha mkewe, isipokuwa ni kwa sababu ya uasherati, akaoa mwingine, azini; naye amwoaye yule aliyeachwa azini.
10 Wanafunzi wake wakamwambia, Mambo ya mtu na mkewe yakiwa hivyo, haifai kuoa.
11 Lakini yeye akawaambia, Si wote wawezao kulipokea neno hili, ila wale waliojaliwa.
MAANA YAKE
Hutakiwi umuache mkewe isipokuwa kwa uasherati tu. Kama umemfuma kwa uasherati na ukavunja ndoa basi unatakiwa hudumie famili yako mtoto/watoto ukipendezwa na mkeo ila si kuingiliana kimwili. Kwasababu tayari umemuacha, hapo utakuwa umeoa mke mwingine ila kama umemsamehe hautakiwi kuoa mwanamke mwingine kwasababu unafanya uasherati (wazini).
Turudi kwenye mstari wako, hapa umeoa na ndoa yako haijavunjika na una mke mwingine. Ndoa inayotambulika ni ya yule ya mke wa kwanza tu (elewa). Ya mke wa pili utakuwa unafanya usherati kwahiyo unatakiwa uendelee kumhudumia mke wako wa kwanza kwa kila kitu na umtosheleze kwa mahitaji yake kwasababu ndiyo Mungu anayoitambua. Ila mke wa pili haitambuliwi na unafanya uasherati. Ukiamwacha ukahamia kwa mke wa pili bado unaendeleza ushaerati (wazini). Unatakiwa umhudumie mkeo wa kwanza kwa kila kitu.
Ndoa ya mke wa pili haijaruhusiwa ndiyo maana Mungu anatambua ndoa ya mke mmoja na mume mmoja ile ya kwanza na hutakiwi umuache. Mhudumie
Someni Biblia vizuri. Biblia haisomwi kama gazeti.
Ugumu wa mioyo kwani ulishaisha?
 
Ndiyo shida ya kusoma Biblia kama gazeti. Biblia imeandikwa kimafumbo inabidi utulize akili ili upate maana kamili. Tafuta nyoka au nge umkanyage kwasababu umepewa mamlaka

Luka 10:19​

" Nimewapa mamlaka ya kukanyaga nyoka na nge na kushinda nguvu zote za yule adui; wala hakuna kitu cho chote kitakachoweza kuwadhuru".​

Hakuna mafumbo bana vitu viko wazi,mkipewa msitari unaenda kinyume na Imani yenu mnaanza habari za roho mtakatifu,mafumbo
 
Hakuna mafumbo bana vitu viko wazi,mkipewa msitari unaenda kinyume na Imani yenu mnaanza habari za roho mtakatifu,mafumbo
Ndiyo maana mnakuja na maana tofauti. Biblia inatakiwa isomwe na watu wenye utulivu wa akili kwasababu ukisoma nje ya hapo utakuja na maana ambayo watu watabaki wanakushangaa.
Ngoja nikurudishe shule kidogo.
Shuleni tulikuwa tunaulizwa kilo moja ya manyoa na kilo moja ya mawe ipi ni nzito? Gari ilipata ajali mpakani mwa Kenya na Tanzania majeruhi watazikwa wapi?
Unaposema Biblia unatakiwa uwe na utulivu wa nafsi.
Isaya 4: 1
"Na siku hiyo wanawake saba watamshika mtu mume mmoja wakisema, Tutakula chakula chetu, na kuvaa nguo zetu wenyewe, lakini tuitwe tu kwa jina lako; utuondolee aibu yetu"
Hapa ukisoma juu juu lazima uchangayikiwe lazima ujiulize tuondolee aibu yetu, aibu gani?. Huu mstari unahusu nini, ulianzia wapi? kwanini wanawake 7 wamekusanyika waende kwa mwanaume mmoja? sababu ni ipi wanawake wamekuwa wengi au? Hayo majibu yote yapo kwenye Biblia.
 
Back
Top Bottom