Kutoka kwenye Utajiri mpaka kuishi kwenye lindi la umasikini!

Shusha vitu jombaa
 
Wauzaji wa viatu viksli huwa wanawahi Tengeru sokoni 05:00 wanachagua viatu bomba kwa 10k na town wanauza kuanzia 50 hadi 90k
Kweli ata sisi tulikuwa tunawahi ila unakuta raia wameisha jibebea mizigo wanapanda town..

Burudani nyingine kuu kachumbari ya ndizi,viazi na mihogo aisee ilinikuwa inanipa burudani sana
 
Sehemu ya 6

Tulisubiri ishara bila mafanikio ikabidi turudi location yetu tukiwa tumefura hasira ile mbaya. Asubuhi palikucha na Mankah ndo alikuja wa kwanza na kuanza kulalama sana juu ya Warombo kuwa mama huruma na kwamba Adela amesema hatoshiriki na sisi kwenye huo mpango kwa kuwa ameahidiwa kuolewa na Ima pamoja na kujengewa nyumba, hivo tuliambilia hela ya nauli ya kuondokea Mererani. Wote tulitawanyika na kila mtu alishika 50 zake mchongo ulifeli.

Siku ya Jumamosi nikiwa mitaa ya Ngusero napuyanga huku na huko Palangyo alinifata na kuniambia twende Iliboru karibia na shule ya Iliboru ilipo kuna ramani tuliondoka na gari aina ya pegeout504 mpaka Iliboru. Kule tulimkuta Mroso na mimi na Palangyo na Fidee ambaye ndio alikuwa anaendesha hiyo pegeout.

Mchongo tuliusuka vizuri baada ya kupata taarifa kuna Wakenya wamekuja kununua maparachichi Tanzania, na wapo mizani pale back town Ngarenaro.

Tuliondoka na kwenda mpaka mitaa ya kona ya Eso ambapo tulipaki na kwenda kuzengea zengea ili kujua kunaingilika? Na dere naye alienda kuweka full tanka pamoja na mengine kwenye dumu kama dharura. Kweli fuso ile aina ya tandam ilikuwa imeshiba na walikuwa ni Wakenya ambao walikuwa wanasubiri jua lizame waanze safari ya kurudi kwao Kenya kupitia Namanga.

Sisi tuliamua kutangulia na gari ilikuwa ikipepea haswa mpaka tulipofikaOldonyosambu tukapaki pale huku tunachanja gomba na kushtua bangi ili akili zikae sawa tulipoteza kama nusu saa kisha tukaendelea mbele mpaka Longido, pale tulikuta road block tukasimamishwa kwaajili ya ukaguzi kwa kuwa tulikuwa tuna gomba na bangi tukaona tusipotezeane muda tukampooza askari kiasi cha pesa akatabasamu na kututakia kila la kheri.

Tulienda mpaka mbele kuna kamsitu pale tulisimama na kupaki gari barabarani kana kwamba limeharibika tulikaa kama masaa mawili kisha tukaliona gari la wakenya tandam likija lilikuwa kwa juu pale limeandikwa Michelin Naivasha. Gari iliwashwa na kusogezwa katikati ya barabara halafu likazimwa kama limeharibika tena huku tukijaribu kulisukuma.

Dereva alianza kupunguza mwendo mdogo mdogo upande huu mwingine gari za kutoka Namanga zilikuwa zinakuja tukaona hapa ndio penyewe tukalirudisha saiti yetu kuyapisha magari yanayotoka Namanga kwenda Arusha yapite. Palangyo alienda kwa Wakenya yule dereva kuomba msaada yule dereva aligoma ndipo Mroso akaona muda unazidi kupotea akazumguka upande wa abiria siti nyingine hizi akachomoa bunduki ambayo tuliikodi hapo hapo Arusha. Akapiga moja juu na Palangyo naye alichomoa ya kwake kumtisha dereva maana alikuwa ameshaanza kuingiza gia.

Dereva naye wa Pegeout hakuwa mzembe aliirudisha reverse gari mpaka ikaigonga ile tandam kwa mbele kidogo.

Tuliwashusha wote chini na hakukuwa na kupoteza muda kwani tuliwapiga na kuwataka watoe pesa, pesa ilikuwa kwenye mkoba nyuma ya siti maeneo ya cabin. Tuliibeba na kupiga risasi moja juu tena kisha tukatimua vumbi kurudi Longido, kufika Longido tulishika njia moja ya vumbi ya kuelekea Kiserian ili kukwepa polisi ambao wangetufata.

Gari ilikuwa inatembea haswa tulikuja kutoboa Lariboro na kuelekea mpaka Olmotoni kisha kuelekea Mateves ambapo tulipaki mitaa hiyo na kusikilizia kwanza. Tuliamua kutafta nyumba ya kulala wageni maalum kwaajili ya kuhesabu pesa hizo ambazo zilikuwa milioni 27 na chenchi zake. Mgawanyo ulikuwa 6*6*6*9.

Palangyo ndio alikuwa na mchongo hivo alikuwa anakula cha juu zaidi. Hakukuwa na ubishi sana katika mgawanyo kwani mapatano ya mwanzo ni kuwa mwenye ramani ndio mshika hela na ndiyo atagawa kutokana na ugumu wa kazi.

Je nini kitafata usikose kufuatana nami hadi mwisho.
 

Aloooo
 
Ongezea nyingine basi usitiache hivi hivi
 
Dah kama movie vile damn!
 
Sehemu ya 7

Asubuhi na mapema niliondoka na kwenda Ngarenaro nikiwa na mzigo wa milioni 6 hapo kila mtu ashashika njia yake. Pale nilikuwa nina chumba changu mwenyewe kabisa na sikai kule tena kwa Waarusha ila wakiwa na ramani huwa wananiita.

Nikaona hii hela nyingi sana wale jamaa wanaweza nizunguka nikanunua cement na mwiko, ile sakafu nikaivunja kidogo kutengeneza shimo ambako ndio nilipohifadhi hizo hela na kiasi cha matumizi yangu na wadogo zangu nyumbani.

Nikatoka hapo mpaka kwa Muhindi Bensonii kitu cha kwanza kununua ni Ockman zile za kusikilizia muziki ila unaweka cd na head phones. Nikatoka hapo nikaenda kuzengea Kilombero na kuchagua nguo zangu na viatu.

Nikaona niko bomba nikaenda dandia basi la Moshi-Arusha mpaka town Moshi ambapo nilipanda kihaisi cha Rombo.

Nilifika kule nikakuta maisha kidogo madogo wameshazoea na kilugha kama yule mdogo anakielewa vizuri washakuwa wazoefu nilikaa nao kama wiki nzima hapo katikati tulikuwa tukienda mjini nawanunulia nguo na viatu na msosi mzuri, pocket money ilikuwa haikosi. Bibi alianza madodoso sana, umepata kasi wapi hawezi kusema kazi anasema kasi. Mpelekeeni kaka yenu subu hapo akimaanisha supu! Alinichagamkia sana kwa kweli namimi nilipokuwa naondoka sikumwacha kinyonge.

Nilirudi town nikiwa kwenye basi nikawa nasIkia stori za wale wakenya waliovamiwa, kila mtu anasema ya kwake huku watu wengi wakilalamika kukithiri kwa vitendo vya ujambazi mkoani Arusha.

Nilipofika mjini tamaa ikanijia na hamu ya kutaka tena kupiga mshindo mwingine ukanijia hivyo nilimtafuta Palangyo maana alikuwa na ramani sana. Nilimpata huko Sekei anaponda mali tuu yupo na Mroso nami nikaungana kusogeza masaa.

Kesho yake kwa mara ya kwanza niliitwa maeneo ya town katika hotel maarufu ya PM, pale nikamkuta mshua mmoja amekaa pamoja na Mroso na Palangyo wanayajenga nami nikaungana nao kusikilizia kikao kinaendaje.

Kwa muhtasari niliopewa wa kikao ni kuwa kuna gari aina ya VX landcruiser ya msukuma mmoja lazima tupite nayo na tuhakikishe inafika Kisumu Kenya. Na ikifika kuna gari nyingine aina ya nissan patrol inatakiwa kuja Tanzania. Na tukifanikiasha basi kila mtu atalamba milioni 10. Wote kwa pamoja tuliguna ila tukasema ngoja tifikirie na kuagana na huyo mdosi.

Njiani tulishauriana kuwa pesa ni ndogo sana na yeye ndio atapiga mpunga mrefu sana. Palangyo akasema yupo mdosi mwingine maeneo ya Duluti tutamcheki halafu tuangalie yupi ana dau zuri. Palangyo alienda kucheki nae na huyo mdosi alisema kuna ramani nzuri ya hela hapa hapa town, na ramani yenyewe ipo Njiro PPF kule ndio palikuwa pameanza kujengeka sana na washua wengi walikuwa huko. Hivyo kuna hela tulitakiwa kwenda kumwibia muhindi huko Njiro.

Huyo muhindi alikopa hela kwa mdosi kwa riba nafuu, ilipofikaribia wakati wa marejesho muhindi alimtafuta mdosi, mdosi akadai amesafiri hivyo asubiri arudi ndio arejeshe pesa zake. Kumbe mdosi yupo anasuka namna ya kwenda kuzichukua zile hela kwa muhindi na bado abaki anamdai muhindi.

Kwa hiyo mchongo ulikuwa hivyo na tulipewa siku 3 za kwenda kusoma raket na kudekeree maeneo hayo ya ushuani kwa Arusha kabla ya kwenda kupiga tukio la kihistoria.

Palangyo aliuliza mapatano na mgao ila akaambiwa na mdosi huku akicheka kwa dharau umeshaleta hela chalii?

Je? Nini kitaendelea usikose kufuatana nami hadi mwisho.
 
Weka nyingine Poker hatulali hadi kukuche
 
Dah inazidi kunoga
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…