Kuuliza si ujinga: Hivi Diwani Athumani kashuka au kapanda?

Sorry kwa uelewa zaidi;
Je Katibu mkuu Ikulu ha deal na PSU ambayo Usalama wamo ndani?
Nafahamu kuna taasisi zipo chini ya Ofisi ya Rais Ikulu, CEOs wao wanareport kwa katibu mkuu Ikulu, mfano TASAF, TAKUKURU nadhani na PSU wenyewe etc......
Katibu Mkuu kiongozi Ikulu ndie Katibu wa Sekretariet ya Usalama wa Taifa
 
Chief Secretary ndo Katibu Mkuu Kiongozi
Ni majina tu katibu mkuu kiongozi nchi kama U.K. anakuwa referred simply as ‘head of civil services’ au ‘cabinet secretary’ kwenye media na bungeni anapotajwa.

Wazungu awatumii ‘chief permanent secretary’ hii na kwa sisi Tanzania labda na waafrika wengine.

Title ya ‘chief of staff’ ina refer to katibu wa Ikulu kwa serikali zao.

Anyway huyo aliyeweka link inayoelezea majukumu ya KMK ameshamaliza utata. KMK ni mkubwa kwa Tanzania, but that is not case sehemu zote duniani.
 
Be serious ndugu!

Yaani awe mkubwa kuliko Mkuu wa watumishi wote serikalini na yeye diwani wa Kata akiwa ni mtumishi wa umma????
Inategemea ofisi ya Ikulu inavyofanya kazi mfano niliokuwa nautumia ni wa uingereza ‘chief of staff’ ni head number 10. Tanzania that is not the case KMK ndio anafanya kazi karibu na raisi pamoja na kuratibu shughuli zake.

kwa nchi kama U.K. ofisi KMK zipo white hall yeye ni kiuongo muhimu wa white hall na number 10.
 
Kwa kuongezea, hata kama tutabadili wakurugenzi wakuu mara hamsini kama hakuna utayari waiasa kuleta mabadiliko ndani ya TISS, basi hata huyu atakwama pia
 
Katibu wa ikulu anakuwaje mkubwa kuliko katibu Mkuu kiongozi? Katibu kiongozi ndio mkuu wa utumishi serikalini na pia ndiye katibu wa baraza la mawaziri.
Muache aendelee kuota...akizinduka atajua maji ni maji, Sio mma
 
Sorry kwa uelewa zaidi;
Je Katibu mkuu Ikulu ha deal na PSU ambayo Usalama wamo ndani?
Nafahamu kuna taasisi zipo chini ya Ofisi ya Rais Ikulu, CEOs wao wanareport kwa katibu mkuu Ikulu, mfano TASAF, TAKUKURU nadhani na PSU wenyewe etc......
Ni kwa Katibu Mkuu Utumishi na Utawala Bora
 
Hii pangua ya watu wa ikulu na usalama wa taifa anaifanya Rais na nani
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 toleo la 2000 inampa Rais wa JMT mamlaka hayo. Further details za vetting and whatsoever zinafanywa na vyombo vilivyo chini yake
 
Haya mambo yapo kimkakati, TISS kuna vitu kaenda kuchota na sasa kaenda ikulu kuviwasilisha na angalia ukaribu wake na Mkurugenzi mpya wa TISS ukoje utakuja kuta bado ana play part yake pale na kupeleka taarifa ikulu kwa ukaribu kabisa
 

Kuna Mnikulu, huyu ni Katibu mkuu wa ikulu au Ndo huyo myeka?
 

Chief of staff kazi yake sio kumshauri Rais mambo ya nchi...
Chief of staff ni mkuu wa watumishi wote wa ikulu, kuratibu safari za Rais, usalama, shughuli zote za ikulu, wageni nk
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…