Kuvaa Hijab ni dini au udhaifu wa wanaume?

Kuvaa Hijab ni dini au udhaifu wa wanaume?

Ni dini gani iliyojenga viwanda vya kutengeneza Hijab, kanzu, suti au majuba? Mungu alitosha, anatosha na atatosha hata kesho, mavazi sio dini, hayatengenezwi na dini na wala hayatoki mwa mungu na hutaenda peponi kwa mavazi tu. Tunawaonea wanawake kwanini? Mbona wanaume nao wanatembe vichwa, vifua na mabaya vikiwa wazi? mbona wanawake hawahoji?
Argument yangu mimi iko very simple, sijui hata kwanini umenikandika miswali yote hiyo.

Labda nirudie:
Mwenyezi Mungu ametoa ridhaa ya mwanadamu kuishi kulingana na vile anavyoona inafaa, na pia kuwajibika na madhara au matokeo (consequences) ya machaguo hayo.

Ukiamua kuabudu masanamu, hana shida na wewe, ila uwe tayari kwa consequences za wewe kuchagua kuabudu hayo masanamu. (Angeweza kulizuia hili lisitokee kama angetaka, lakini ameliruhusu litokee kwa sababu anaheshimu UHURU WA MWANADAMU KUJICHAGULIA HATMA YAKE YEYE MWENYEWE)

Hivyo basi, kama wewe KAVULATA unataka kutembea uchi, bila viatu. RUKSA. (Maana huo ndio utaratibu wako)

Wanaotaka kuvaa hijab. RUKSA. (Na wao huo ndio utaratibu wao)

Anayetaka kutembelea mgongo badala ya miguu. RUKSA (Nayeye huo ndio utaratibu wake).

Tatizo ni pale "sisi binadamu" tunapotaka kuanza kuwalazimisha wengine wafuate machaguo yetu.

Mifano:
1. Watu wa Iran wanawalazimisha watu wasiotaka kuvaa hijab, wavae hijab. (TATIZO HILO)
2. Wewe Kavulata unawalazimisha watu wanaoamini kwamba kuvaa hijab ndio utaratibu sahihi, wasiamini hivyo. (TATIZO HILO).
 
According to hadith za kiislam...Umar (Rafiki ake mtume/Swahaba)ndio alitaka wanawake wafunike uso.
Alimfata Muhamad na kumsihi apitishe sheria hii ila muhamad akawa kama haitaki vile.

Umar siku moja akaenda mahali wanakojisaidia wanawake (Enzi hizo hamna vyoo, kulikuwa kuna maeneo tu huko jangwani ya kwenda kujisaidia)
Akapambana mpaka amuone mke wake Mtume akijisaidia...Alipomuona akamuambia "Wewe Aisha nimekujua"

Akaenda kumsimulia hilo tukio Mtume na kumwambia kuwa angejifunika uso, Umar asingemtambua.

Basi Ewala...Mungu fundi, Usiku huo huo Malaika Jibril akashuka na Aya za kuwalazimisha wanawake wafiche sura zao.
Allahu Akbar.
 
Kuvaa hijabu ni amri ya Mwenyezi Mungu kwa wanawake wote wa Kiislamu. Na hii inawasidia wenyewe wasiudhiwe hasa kutokana na maungo yao kuwa ya kuvutia kwa hivyo wakijisitiri hawapati usumbufu.
Haya mavazi ndio hayo hayo aliyoyavaa Mama yake Issa/Yesu (Yaani Mariamu) na ndivyo wanavyo vyaa masista wa katoliki.

QURAN 33: 59
" Ewe Nabii! Waambie wake zako, na binti zako, na wanawake waumini wajiteremshie nguo zao. Hivyo kutafanya watambulikane (kuwa ni wenye kujiheshimu) wasiudhiwe. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu."
Waislamu mnatujulisha alie tunga Hijab ni Umar , Muhammad ka copy kutoka kwake kapachika kwenye Koran, Ilifikia maali mpaka muhammad akasema kama kutakuwa na mtume mwingine baada yake basi angeweza kuwa umar , jamma katunga verse mbali mbali
Umar said: .....both righteous and evil doers enter your wives, so why don't you tell them to observe the hijab? Then the verse of hijab was revealed. ...... Musnad Ahmad 157
 
Kwa sasa Marekani amewekeza nguvu kubwa kwenye kuhamasisha Americanization! Ndani ya hiyo Americanization policy utakutana na kila aina ya ujinga! Ushoga, kuhamasisha civil wars kwenye nchi asizo fungamana nazo, au zile zenye malighafi adimu! Kuhamasisha ugaidi, mmomonyoko wa maadili kupitia mavazi, nk.

Ikumbukwe chokochoko za machafuko kote duniani, chanzo kikuu ni Marekani and Co. Ltd.
kwahiyo yule mtoto aliyevaa hijab vibaya alitumwa na wamarekani, na askari waliomuua nao wametumwa na wamarekani na wanaoandamana pia wanatumwa na marekani. Jamani, marekani kweli wana hila mbalimbali lakini mengine sio ya kwao. kwamfano, watu hapa kama tukiandamana kupinga tozo tutamsingizia nani? hao wanaokapiga hijab wana hoja ya msingi ni kiasi tu cha kuwasikiliza na kutafuta win-win situation. mfano wangeweza kusema wanawake iwe lazima kufunga hijab wakiwa msikitini, kwenye maulid, madrasa na vitu kama hivyo. Lakini sio kumlazimisha avae kab hataka yuko beach, anacheza mpira au rede.
 
Sasa mbona wanaume wanazaliwa na magovi?jee kuyakata ni kumsahihisha Mungu katika uumbaji wake wa mwanaume?
 
kwa hiyo kila ambae hakuvaa hijab ni kahaba?
Swali haliko relevant kabisa !! Ni kwamba hijabu ni kwa kujistiri tu maungo ya mwili mpka kichwa... Sio ambaye havai hijabu ni kahaba ila hakuna kahaba atavaa hijabu akiwa site anatangazwa biashara yake.
 
Kwaiyo mtoa mada hapo ulipo unatembea taking wazi Kwasababu tu mungu hajakuumba na nguo
 
Jamani Dini za watu ziheshimiwe, kama kuna nchi inataka raia Wanawake wavae Hijab muwaache na utamaduni wao na wakiandamana pia muwaache na Serikali yao.

Hii tabia ya Serikali ya Marekani kuingilia Serikali nyingine sio kitu kizuri

Iko hivi, ukisema leo hii pale Iran uanze kuwaacha wanawake wasivae Hijab, hiyo hali ikizoeleka baada ya Miaka kadhaa utashangaa wanawake hao hao wanaanza kuonyesha mikono, pia itakuwa mzozo mtakuja kuwatetea

Hali itaenda miaka mingine kadhaa wataanza kuonyesha Mapaja, mtawatetea na hali itapita,

Wakizoea hapo wataanza kubinjua Matiti yao pia mtawatetea, Baadaye watakuja kuvaa nusu uchi kabisa. Kisha Muje kuwacheka wa IRAN kwamba hawakuwa Seriously.

Hii inanikumbusha, Speech ya Mwalimu Nyerere

Mwalimu Nyerere aliwahi kuhusia na kusema huu Muungano wa Tanganyika na Zanzibar Uheshimiwe.

Tukisema tutengane baadae Tamganyika ikawa kivyake, tutaanza kutengana makabila kwa makabila Wachaga kivyao na nchi yao, wazaramo kivyao. Ndio Mambo yanavyoanzaga hivi.

Chochote kikiruhusiwa awali kwa kuona hijab ni jambo la kupuuzwa kwa wanawake, basi tutegemee baada ya Miaka Mbele Irani itakuja kuwa sehemu mbaya zaidi kwa upande wa Mavazi kwa wanawake.

Haki sawa kwa wanaume na wanawake wakati zinaanza kuja zilikuwa zinaonekana ni kitu cha kawaida sana na kupigiwa chapuo hivihivi

Lakini kwasasa changamoto zishaanza kuonekana na huenda huko miaka ya baadaye hali itakuja kuwa mbaya zaidi.

Nchi ya Iran iachwe na Misimamo yake katika Dini yao wanayoiamini tangu karne na karne, wakiusikiliza ulimwengu itakuja kuwatafuna baadae.

Mtanisamehe kwa uandishi Mbovu.
 
Hivi kati ya wewe "mmatumbi" wa kiparang'anda na huyu dada wa Iran aliyevua Hijab na kuawa ni nani yuko karibu zaidi na nasaba ya Mtume Mohamed? Unaijua dini kuliko hawa wanaoandamana kupinga hijab? jiangalie sana vinginevyo utakuwa msindikizaji wa wengine kwenye safari ya kwenda kwa Mungu.
Pole sana uislamu upo tofauti na iyo dini yako ..Kwenye uislamu hakuna mbora bali yule amchaye mwenyezi mungu wapo watu apa tanzania wana elimu kubwa ya dini kuliko wale waliozaliwa makah au madina..uislamu hauna mmiliki kwenye hii dunia isipokuwa mwenyezi mungu pekee na waislamu wote wanafuata sheria na mafunzo ya mtume muhamad s.a.w .. nije kwenye mada walichofanya askari wa doria apo Iran ni dhambi na siku ya mwisho watawajibika kwa kitendo walichokifanya uislanu una hukumu zake na sheria zake ... mimi ni muislamu lakini walichokifanya wale askari ni kinyume na mafundisho ya Qurani na sunah.
 
Binadamu wote wake kwa waume wanazaliwa wakiwa uchi kabisa, kuvaa nguo ipi na ivaliwe wapi kwa sababu gani ni utashi wa wanajamii wenyewe. Bahati mbaya au nzuri Mwenyezi kuna maeneo na viungo vya mwili ambavyo alishavifunika yeye mwenyewe kwa sababu zake kwa kutumia nywele ndefu na nywele fupi kutokana na umuhimu wake na sababu zake. Mfano, Mungu amekifunika kichwa cha kila mtu kwa nywele ndefu bila kujali jinsia yake, kabila wala dini yake, Mungu akakifunika kinena cha kila mtu aliyebalehe kwa nywele ndefu tunazoziita mav*zi. Hakuishia hapo akakifunika kidevu na kifua cha mwanaume kwa nywele ndefu pia kwa sababu zake mungu mwenyewe. Hakuishia hapo akaifumika ngozi ya mwili ya watu wote kwa nywele fupi tunazoziita malaika kwa sababu zake pia. Hivyo kila nywele ilikuwa na sababu yake na ilitosha kabisa kuifanya kazi iliyokusudiwa.

Ni nani ambae hataki kumuona mwanamke ambae asiyefunika nywele zake? Je, ni mwanamke mwenyewe kwa sababu zipi? Je, ni mwanaume kwa sababu zipi na je, ni Mungu aliyetufanya tuzaliwa uchi lakini akatufunika kwa nywele kwa sababu zipi?

Utafiti wangu kwenye hili ni kwamba, sio Mungu anaetaka wanawake wavae Hijab bali ni wanaume tu kwa sababu ya wivu na kujifanya kuwa wao ni dhaifu kwa kutazama tu nywele, matiti, mapaja na vitovu vya wanawake wakasahau kuwa Mungu angetaka asingeshindwa kuwafanya wanawake wazaliwe wakiwa na hijab tayari. Tuache ujinga wa kuwadhulumu wanawake kwa kujificha kwenye kichaka cha dini. Nini sio Hijab wala nywele za mtu.

Ona haya mauaji na maandamano ya kijinga kabisa, eti msichana hakuvaa hijab.


Kuna watu wana imani za kale zinazopingana na akili, primive mythologies
 
Dini ya Uislaam inataka mwanamke afiche nywele zake hiyo ni Amri na sababu zilizotolewa ni kwamba mwili wa mwanamke ni karubia wote ni Uchi kwamba anatamanisha kwa hiyo anatakiwa auhifadhi.
Huo mwili ni uchi mbele ya nani? Huu ni mfumo dume purely. Tamaa za mwanaume ndiyo zinapelekea mawazo ya kishenzi kama hayo
 
Sio hivyo tu, hata Rais Mwinyi analalamika sana kuhusu wizi na ubadhilifu wa mali ya umma kule Zanzibar, ripoti ya mkaguzi na mdhibiti wa hesabu za serikali, CAG anafichua wizi kila siku. Bila shaka wezi wote hawa wamevaa hijab, baibui, kanzu na balaghashia na wanaswali.
Kuwa muislamu siyo gurantee ya wewe kuwa mwema au muadilifu waislamu ni watu tu kama nyinyi wanafanya dhambi kama nyinyi bali muislamu wa kweli na mcha mungu utamuona ti kwa matendo na maneno yake na kingine cha kuongezea uislamu ni dini iliyokamilika na isiyo na dosari kufanya kwake maasi muislamu akubadilishi mafunzo na taratibu za kiislamu zilizoletwa.
 
Maandamano ya kukataa hijab pia ni Marekani? Uzee zee taaa
Matakwa yameongezeka,Sasa hivi wanataka mabadiliko ya utawala,marekani kalegeza vikwazo ili waandamanaji wawasiliane vizuri...kunaitwa ku-capitalize
 
Huo mwili ni uchi mbele ya nani? Huu ni mfumo dume purely. Tamaa za mwanaume ndiyo zinapelekea mawazo ya kishenzi kama hayo
Tamaa kwa binaadam ni mbaya, yapasa kuzidhibiti,wenye tamaa ya pesa wanaua albino,wanaua ili wapate pesa
 
Hijab ilibuniwa na Umar na Muhammad aka copy kutoka kwake , ilikuwa wake zake muhammad wanavaa ovyo wale gang member wa muhammad wakawa wakiingia wanawatamani , Umar ndio akaja na idea ya Hijab

Umar said:.... , both righteous and evil doers enter your wives, so why don't you tell them to observe the hijab? Then the verse of hijab was revealed. ...... and it was revealed like that. Musnad Ahmad 157
Ningeshangaa kama huu uzi ungekupita na vi adithi vyako uchwara vya kubumba[emoji3][emoji23]
 
Huo mwili ni uchi mbele ya nani? Huu ni mfumo dume purely. Tamaa za mwanaume ndiyo zinapelekea mawazo ya kishenzi kama hayo
Mbele ya wanaume ambao ni halali kukuoa kwahiyo unapo ufunika vizuri unaepusha matamanio kwao hapo ndipo inapelekea Kubakwa au kusumbuliwa
 
Udhaifu tu wa baadhi ya wanaume wa kiislam, hasa wanaojiita masheikh, wengi wazinzi wanaogopana kugongeana mzigo tu, dini hiyo imejengwa kwa hisia za kimwili zaidi kuliko kiroho
Hata zama za Yesu wa wana wa Israel wanawake walikua wanaficha nywele zao sio masheikh ndio walioliasisi jambo hili.
 
Back
Top Bottom