DOKEZO Kuweni makini na utapeli nimepigwa milioni na ushee, matapeli wanakuja na njia mpya kila siku

DOKEZO Kuweni makini na utapeli nimepigwa milioni na ushee, matapeli wanakuja na njia mpya kila siku

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Profile ya tapeli mtandaoni inafahamika ukiiona tu mara ya kwanza.

.........Watanzania acheni kuamini watu mitandaoni kirahisi hivyo.
 
k
Pole sana, Mimi kwa falsafa yangu, huwa siamini kama kuna kitu cha bure, au kamserereko!
Nothing goes without a price! Ndio maana huwa saiamini michezo ya kubet!
kubet mbon hamna nothing free mkuu?
 
Mtu yeyote awe ndugu au jamaa au usiyemjua.
Akianza kuongelea pesa zako wewe muweke katika kundi la matapeli.
Wengi wanaotapeliwa kirahisi ni shauli ya tamaa za kupenda mtelemko.
 
kanijia kwa gia ya ku subscribe video za celebrates youtube eti nitalipwa, nikiangalia namba niya kutoka yemen nikasema hili nilitanzania ngoja nilishushue
najua wew ni mtanzania acha utapeli sihitaji offer zako mara lugha ikabadilika kutoka kimalkia hadi kiswahili eti ooo usijali unakaribishwa wakat wowote ukitaka milango ipo wazi
nikajiuliza hivi yeye hiyo pesa haitaki au hana ndugu jamaa na marafiki wa kuwapa huo mchongo mpaka anitafute mim asiyenijua nikasema haibiw mtu pesa haipatikan kirahis hivyo
muhimu nikuwa makini tu na kutopenda vya bure au vinavyopatikana kirahisi
 

Attachments

  • Screenshot_20240405-044637~2.png
    Screenshot_20240405-044637~2.png
    72.5 KB · Views: 9
Kuna njia ya hii ya utapeli ambapo mtu anatengeneza urafiki na wewe kupitia mtandaoni. Kadri siku zinavyoenda mnatengeneza ukaribu na ka imani kanaanza kukuingia kiasi fulani kuwa umepata rafiki mzuri kutoka nchi jirani japokuwa wakati mwingine inaweza kuwa hapa hapa bongo.

Sasa akishaona umemuamini anakwambia fulani nina zawadi kwaajili yako nataka nikutumie, anakuonesha zawadi hizo na mara nyingi zinakuwa ni za gharama kubwa sana. Anakupigia picha akizipaki mpaka siku anazituma na anakupa mawasilianao ya mtu au kampuni inayotakiwa kudeliver mzigo huo.

Mzigo ukifika mtu au kampuni uliyoambiwa itakupatia mzigo huo wanakupigia simu kukujulisha kuwa mzigo umefika, lakini mzigo huwa unakuwa umepelekwa mji tofauti na wewe, na hapo utaambiwa, address ilikosewa au imetokea kutoelewana/sintofamu mzigo umetumwa sehemu nyingine, ili utumiwe mzigo huo unatakiwa kutuma pesa ya usafiri.

Ukiangalia pesa ya usafiri unayotajiwa na thamani ya vitu ulivyotumiwa unaona pesa ya usafiri ni ndogo sana, hivyo huoni hata shida ya kutuma! Ukishatuma tu imekula kwako, kampuni au mtu huyo anakublock inakuwa imetoka hiyo, ushaliwa!

Jambo la kuzingatia ili usije kuingia mkenge, watu hawa huwa hawataki kutumia video call, utabaki kuona profile picture zao na kusikia sauti lakini katu hawakubali kufanya video call ili ujue utambulisho wao.

Watu hawa wamekuwa wakitumia udhaifu wa watu kuwa wapweke kihisia kutapeli watu, sio upande wa mapenzi tu hata urafiki wa kawaida, jinsi wanavyokuchota utaona nimepata rafiki wa kweli kumbe mtu yupo kazini.

Kuweni makini.


Kuibiwa Kozembe sana,
 
Tamaa mbaya sana
Eti urafiki
Kwanza ukiambiwa tu tuma ya kutolea hapo unapotezea kabisa
Na hawataki video call na wewe machale hayakuchezi tu
Hupati pole yangu hapo
 
Kama umetapeliwa Kwa mbinu hiyo, basi wee ni lofa!!!
Na utapigwa tena soon!
 
  • Kicheko
Reactions: len
Mimi akijifanya amekosea sehemu ya kutuma let's say katuna chuga na mimi niko Dar, ninamwambia kuna jamaa yangu anakuja kuvichukua hapo chap.
 
Bado nchi ina watu wajinga sana aisee kama huyu mleta uzi. Kazi ipo.
 
Umetapeliwa kizamani sana, huu wala sio utapeli mpya mjini hapa. Watu kibao wamesha kaangwa
 
  • Thanks
Reactions: len
We MangiTz , alishtukia kuwa huna kitu Mangi Tz na sio kuwa una papara na hela zake ! Alishajua hii njemba apeche alolo ! Akaona atapoteza muda bure !!
 
Haya mambo ya miaka ya 2000 huko mzee.
Wakati huo ndio internet cafe zinaanza. Miaka hiyo email ni Yahoo na Hotmail.
Wazee wa zamani na maafisa wengi wa serikali wamelizwa sana kwa hii mbinu
 
Huu wizi wa 2013 uko ndio umeanza sio Leo waanzilishi wa wizi huu ni Wanageria na watu wa afrika magharibi sema pole umechelewa kujua .

But all in all tu take care wezi uja na mbinu mpya kila Siku!!
Atakua mgeni mjini huyu[emoji81][emoji81] wame jaa uko kwenye email wengine wana jifanya wanajeshi wa Afghanistan wame piga dola hawana pa kuzi peleka wana taka wa invest kupitia wewe .ukiwa ndezi una pigwa
 
Kuna njia ya hii ya utapeli ambapo mtu anatengeneza urafiki na wewe kupitia mtandaoni. Kadri siku zinavyoenda mnatengeneza ukaribu na ka imani kanaanza kukuingia kiasi fulani kuwa umepata rafiki mzuri kutoka nchi jirani japokuwa wakati mwingine inaweza kuwa hapa hapa bongo.

Sasa akishaona umemuamini anakwambia fulani nina zawadi kwaajili yako nataka nikutumie, anakuonesha zawadi hizo na mara nyingi zinakuwa ni za gharama kubwa sana. Anakupigia picha akizipaki mpaka siku anazituma na anakupa mawasilianao ya mtu au kampuni inayotakiwa kudeliver mzigo huo.

Mzigo ukifika mtu au kampuni uliyoambiwa itakupatia mzigo huo wanakupigia simu kukujulisha kuwa mzigo umefika, lakini mzigo huwa unakuwa umepelekwa mji tofauti na wewe, na hapo utaambiwa, address ilikosewa au imetokea kutoelewana/sintofamu mzigo umetumwa sehemu nyingine, ili utumiwe mzigo huo unatakiwa kutuma pesa ya usafiri.

Ukiangalia pesa ya usafiri unayotajiwa na thamani ya vitu ulivyotumiwa unaona pesa ya usafiri ni ndogo sana, hivyo huoni hata shida ya kutuma! Ukishatuma tu imekula kwako, kampuni au mtu huyo anakublock inakuwa imetoka hiyo, ushaliwa!

Jambo la kuzingatia ili usije kuingia mkenge, watu hawa huwa hawataki kutumia video call, utabaki kuona profile picture zao na kusikia sauti lakini katu hawakubali kufanya video call ili ujue utambulisho wao.

Watu hawa wamekuwa wakitumia udhaifu wa watu kuwa wapweke kihisia kutapeli watu, sio upande wa mapenzi tu hata urafiki wa kawaida, jinsi wanavyokuchota utaona nimepata rafiki wa kweli kumbe mtu yupo kazini.

Kuweni makini.

Inatakiwa tufikiri mara mbili mbili hakuna sababu ya kumfanya mtu akupe mamilioni ya pesa kwa nyakati hizi,, anakung'ang'ania utume 200,000/= afu yeye akutumie vitu vya thamani zaidi ya mamilioni hii sio hali ya kawaida ukifikiri vizuri utagundua chenye thamani kinachotakiwa ni 200,000/= na si vinginevyo HAKUNA WAKUKUPA UTAJIRI KIRAHISI HIVO ""TUPUNGUZE MIHEMKO""
 
Back
Top Bottom