Kwa aina ya mpira anaocheza Kylian Mbappe, atapotea baada ya kufikisha miaka 30

Wanasema mpira wetu kivyetu vyetu

Yani wanataka kujitofautisha na commentators wa huko ulaya kwa kuongeza uswahili

Unaweza kuta mtangazaji anaacha kutangaza kile kinachofanyika uwanjani akajikita kwenye kampeni za CCM
KWA nini uangalie mechi kupita Tbccm kijana hapo unafeli mwenyewe tibiccm wanaubovu wa kudumu
 
Kcha kasema hakuna tatizo na aliongea na Ronaldo kuhusu game plan we unasema tatizo lipo. Yani kati ya mocha wa Ureno na wewe ndugu yangu wa Manzese(no offense) nikusikilize wewe?
Hata ufaransa walikanusha kuhusu benzema lakini ukweli unajulikana kocha aligombana naye. Ureno waliongea vile ili kuleta utulivu kambini.
 
Huo ni ukweli....ukiwa unategemea mbio kwenye mpira lazima utapotea tu umri unapokwenda ....mfano hai ni mimi mwenyewe...kwenye miaka 18-25 nilikuwa na kimbia sana uanjani ,lakini KWA sasa kasi imepungua pakubwa.....sisumbui kama zamani.

Ila Mbape ni mchezaji hatari zaidi KWA sasa Duniani baada ya Messi na R0naldo,bado ana muda mrefu wa kucheza atafqnya makubwa sana kwenye soka.....mimi ni Tim Messi ila Mbape anastahili heshima na yeE kijana ana washa moto.
 
Wewe ni Tuisila Kisinda mkuu?
 
Hata akikaa miaka miwili bila ku train akiingia uwanjani uhakika wa kupewa penati upo

Hapo ndio sehemu pekee naweza kukubaliana na nyinyi

Luca Modric anachukua MVP 2018 WC alikuwa na miaka 17?
 
Kwanza naye alikuwa haoni vizuri kama sisi tu

Nimeshuhudia matukio mawili akiyatafsiri ndivyo sivyo kulingana na low quality ya streaming

Hadi kwenye sub napo alikuwa anachemka anataja watu wasio husika kama ndio wanaofanya mabadiliko
Hivi ni raia Wa TANZANIA yule jamaa,maana lafudhi yake sijaielewa?
 
Chuma ndio kwanza kimepata moto
Ohh ana mbio

Sasa ulidhani mpira unachezwa kwa kutambaa ama kutembea😁

Goooo Mbappe goo🔥🔥🔥🙌
Hii picha ni photoshop, hilo tukio sio halisi kaangalie youtube maana hapo inaonesha mbappe anapiga kwa mguu wa kushoto wakati alipiga mpira kwa mguu wa kulia.
 
🤣🤣🤣
 
Kwa hyo Mbappe ana UEFA cup kweny huo umri mkuu?acha kutupiga kamba bana
 
Na
Kwani Ronaldo hajapotea? Mbona kuanzia nusu fainali ya kombe la dunia hajaonekana?
Na sasa hiv hana hata team...amekuwa mtu wa kujitongozesha kwny club kubwa ili achukuliwe:..yuko desparete sanaa hadi kazinguana na wakala wake
 
Mimi nimeandika uhalisia. Mbappe hana tofauti na Christiano maana asset yake kuu ni mbio. Messi anakupa kila kitu uwanjani.
MISS PENATI hana lolote uwanjani zaidi ya mbeleko tupu.

Ronaldinho ndiye ana uwezo wa kukupatia kila aina ya udambwi dambwi wa soka biriani karne na karne zote atakumbukwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…