Kwa Askofu Kakobe - Baada ya kufunga ndoa, maharusi wapanda daladala na pikipiki kwenda makwao

Haha mkuu
Miaka 16 iliyopita nilifanya harusi na ilikuwa by far more cheaper than this , sikosoi bali nashangaa hiyo staging , haileti maana.

Uwe na asubuhi njema
Barikiwa sana, uwe na amani na mafanikio kwa kila ufanyalo kikubwa tu liwe la halali
 
ndoa shirikisha ndugu , marafiki na majirani ili hata siku mmojawapo wa wanandia akifa isiwe taabu ushirikisha ndugu , marafiki na majirani

Hapo hao wanandoa wa Kakobe wanewabania ndugu , majirani na marafiki wanajifanya ndoa inawahusu wenyewe wawili tu !!! Akifa mmojawapo hapo wanaanza kusumbua mitangazo kila kona ohhh ndugu,jirani na marafiki nasikitika kutangaza kifo cha mwenza wangu karibuni tushirikiane maombolezo na mazishi .Msiba ni watu na watu ndio nyie ndugu zangu , majirani na marafiki.Unafiki mtupu

Ndoa ni kitu cha community hiyo staili selfish ya hao wanandoa wa Kakobe haiko sahihi
 
Masihi mwenyewe alikuwepo kwenye harusi moja huko kana, divai ikaisha akafanya mambo yake watu wakaendelea kunywa kwa furaha.
 
... poverty ni kitu kibaya sana! Wala kuwa maskini sio utakatifu au kinyume chake. Utakatifu ni kulishika na kuliishi neno la Mungu regardless ya kipato chako.

Je majizo na lulu ni maskini.. mbona nao hawajafanya sherehe
 
Kwa hakika kuna funzo hapo kwa vijana wengine.

Mambo ya vikao vya harusi kwa miezi minne kutafuta michango kwa nguvu, kutumbua mamilioni lukuki kwa siku moja tu, na kisha kuanza maisha kukiwa na madeni ni shida.

Hongera Askofu Kakobe!
Hili swala la michango ya harusi na gharama zake kama wanajamii hebu tulitazamie upya especially nyakati hizi za ugumu wa maisha......
 
Kwahio hao ni wanaume kwa wanaume au ni malaika?? Acha upotoshaji
Amesemea kuhusu kupata mwanamke ambae atakuwa tayari kufanya ndoa ya gharama nafuu ni nadra. Hajasema kuwa hakuna mwanamke wa kufanya nae ndoa nafuu.
 
Unaweza kuta ndugu zao hawasali kanisa hilo, au walikuwapo ila hawajapiga picha tu.
 
Nadhani walikuwa wanapiga picha tu kuonyesha kuwa ndoa yao haikuwa na mambo mengi kama misafara na kadhalika. Ila ndugu wanakosekanaje katika tukio kama hilo.
 
Vikao miezi 4, michango niyakuifukuzia, bajeti haiwiani na pesa mliyo ikusanya mnaingia madeni, kisa sherehe kubwaaa kama ya fulani mburaaaa, nikufunga ndoa halafu fyuuu jumbani kula kilichopo kesho yake kibaruani, wamependeza na kufanya lililojema.
Tatizo tunaishi jamii ya watu wanafiki sana. Wanaojifanya hawaoni kinachoendelea kwasababu ya unafiki tu. Gharama za ndoa ni unnecessary kwa maisha ya kijana wa sasa. Na hii ndio inafanya vijana kujizungusha zungusha inapokuja swala la ndoa wanakosa maamuzi ya wakati.

Ndio maana wale wanaoamua kufunga ndoa za fasta huwa hawapotezi muda....
 
Je majizo na lulu ni maskini.. mbona nao hawajafanya sherehe
... walipiga picha wakiwa wamepanda daladala na kuzirusha kwenye mitandao? Tunazungumzia ujumbe uliotumwa kwa jamii; hoja sio kufanya au kutofanya sherehe.
 
Hivi kwa nn wale mabibi harusi wengine uvaa mashera yale meupe tena yanameremeta kweli kwli lakini hawa maharusi wa kakobe mbona wamevaa magauni kama wanaenda kwenye send-off au kitchen part ila ongera zao
 
ISSUE HAPA NI KUTAKA KUUFANYA UMASIKINI FASHION ZA KUJISIFIA/KUJIVUNIA. HICHO NDICHO NINACHOKIKATAA! SEMA SINA PESA NAPANDA DALADALA! NITAKUSIFU
Hapana mkuu ishu hapa ni kuonyesha tofauti ya ndoa na harusi na pia kuonyesha sio kila ndoa ifuatiwe na harusi, pia haiitaji uwe na pesa ndio ufunge ndoa
 
Maisha tunatofautiana...kila MTU afanye kwa uwezo wake...masuala yakufanya harusi babkubwa huku maisha yako una unga unga ili kisa tu nawe uonekane ni ujinga.
 
Hahahahahah daaah Safi Sana very simple hakuna mbwembwe Wala majotroo[emoji1]
 
Kuna wadada mjini watasugua sana benchi na watarundikana makanisani wapate waume kumbe sometimes vitu huwa simple......kuna mdada alimpa MTU condition eti anataka Pete ya Tanzanite plus harusi yake ifunike ya wenzie...saiv yule mwanamke anazidi kufubaa tu mwaka wa tano yuko sokoni wateja hamna
 

Mkuu unajaribu kupotosha uma!,hii inaitwa kubariki ndoa na wala sio ndio,hii ni kwa wale wanaoishi uchumba sugu na wanapika na kupakua,utakuwa hauelewi vizuri ndoa ni nini na kubariki ndoa ni nini !
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…