Kwa bajeti ya 10M - 12M naweza kupata gari gani used kutoka Japan?

Kwa bajeti ya 10M - 12M naweza kupata gari gani used kutoka Japan?

Kwa gari ya familia kubwa kwa brand ya Toyota, zitakazokufaa ni Wish, Spacio, Sienta, na Raum. Ila bajeti yako ipo chini. Ungeongeza angalau ifike 14mil utapata kwa kuagiza. Miaka 5 iliyopita kwa bajeti hiyo ungeweza kupata Raum nzuri tu. Ila kwa sasa angalau uwe na 14mil kwenda juu. Corona ilileta mabadiliko. Freight charges zimepanda kutoka $800 hadi $1800.

BTW, nimeangalia Beforward asubuhi hii, Sienta ya 2004 (7 seater) ni $2994 (7mil) na ushuru wake ni 5.2mil. Hapo bado charges za bandari, clearance, na service ya kuanzia.
Nashukuru kwa ushauri mkuu. Ngoja na mimi nitaingia huko Beforward nikaangalie bei zake. Huo ushuru wa 5.2 mil umepataje? Na hizo gharama zingine kama charges za bandari, clearance na service ya kuanzia, naweza kuzipata wapi ili nijipange nikienda niwe najua naenda kulipia tsh ngapi?
 
Probox nitapata kwa tsh ngapi mkuu?
Iangalie hii succeed ambayo ni sawa tu na probox, ipo leo be foward ila watu wanaitolea macho sana
Milioni 6.5 kununua na kuagiza , ushuru na port charges wharfage na clearance fees haziwezi zidi 6 mil
 

Attachments

  • Screenshot_20230409_140250_Chrome.jpg
    Screenshot_20230409_140250_Chrome.jpg
    133.1 KB · Views: 54
Chukua chuma hiki,kitakufaa kabisa kwa bajeti yako

TRA Used Motor Vehicle Valuation Details
Reference Number:22233056322
Make:MAZDA
Model:DEMIO - DE3/DE5
Body Type:HATCHBACK
Year of Manufacture:2008
Country:JAPAN
Fuel Type:PETROL
Engine Capacity:1001 - 1500 CC
Customs Value CIF (USD):1,779.97
Import Duty (USD):444.99
Excise Duty (USD):111.25
Excise Duty due to Age (USD):667.49
VAT (USD):582.30
Custom Processing Fee (USD):10.68
Railway Dev Levy (USD):26.70
Total Import Taxes (USD):1,843.41
Total Import Taxes (TSHS):4,278,308.42
Vehicle Registration Fee (TSHS):450,000.00
TOTAL TAXES (TSHS):4,728,308.42

View attachment 2582001
Mhh, mkuu haka sijakapenda aisee.
 
Imekaa kiume how ist ingekua gari mbovu isingekua inanunuliwa kwa wingi kuliko hizo spacio
Umeambiwa anatembea roughroad km 70 unamwambia achukue babywalker. Mkuu wewe magari huyajui huwezifananisha spacio na ist hata siku moja.

Ist kwanza ni 7 seater hata ukisanya njian unapata hela za kutosha. Pia ni gari kubwa acha ist kamebanana ndani, kwenye rough road ina stability na ni nzito kidogo kuliko ist na imekaa kiume zaidi kuliko ist
 
Nashukuru kwa ushauri mkuu. Ngoja na mimi nitaingia huko Beforward nikaangalie bei zake. Huo ushuru wa 5.2 mil umepataje? Na hizo gharama zingine kama charges za bandari, clearance na service ya kuanzia, naweza kuzipata wapi ili nijipange nikienda niwe najua naenda kulipia tsh ngapi?
Ushuru unapata kupitia TRA unaweza kuingia mtandaoni search TRA used motorvehicle evaluation utajaza details za gari ambayo unahitaji kuimport kama mwaka, CC, mafuta inayotumia na details nyingine itacalculate na kukuletea ushuru.

Kuhusu charges za bandari zinatozwa kulingana na CBM juzi nimetoa Nissan note CBM 11 gharama yake ilikuwa 226,000Tsh.

Clearing and Forwading Agent gharama yake ni 250,000Tshs mpaka usajiri.

Kama ukiagiza nipe kazi BabaMorgan meli inashusha leo kesho nakupa ndinga yako.
 
Si uchukue Rav4 old model mkononi hapa hapa bongo mkuu ukitulia ukajipa muda utapata usiweke vipengele vingi sna unapotaka nunua gari wakati hela ni ya manati[emoji16][emoji16][emoji16][emoji23]
Wakati huo huo gari iwe offroader, ile mafuta 10-15 km/l, ibebe watu 6 na bei iwe nafuu..

Jamaa atulize kichwa anunue noah mkononi kwa 12M atapa nzuri tu!!
 
Mkuu nununua tu carina haswa ukipata S.I Utakuja kunishukuru baadae ukiagiza inaweza zidi kidogo lakini haitoenda mbali na budget yako. Nilinunuaga kwa mhindi 2014 nikaifanyia Tax miaka 5 baadae nikauuza Milioni 5 mwaka 2020 kwa mwenyeji wa Tunduma mpaka leo inapiga kazi na ipo. So kwa mazingira uliyokuwepo nunua tu Carina itakusave kwa nyakati zote.
 
Nashukuru kwa ushauri mkuu. Ngoja na mimi nitaingia huko Beforward nikaangalie bei zake. Huo ushuru wa 5.2 mil umepataje? Na hizo gharama zingine kama charges za bandari, clearance na service ya kuanzia, naweza kuzipata wapi ili nijipange nikienda niwe najua naenda kulipia tsh ngapi?
Ingia kwenye website ya TRA, tafuta calculator ya magari yaliyotumika. Ukiingiza taarifa za gari, mwisho uta click 'calculate'. Zipo nyuzi kadhaa humu ambazo tushaelekeza jinsi ya kuingiza hizo details za gari.
 
Nimetembelea Beforward na BTI Japan nimeona magari mengi yaliyopendekezwa na wadau yana angukia kwenye tsh 14mil hadi 16mil. Gari nyingi za 12mil zinasoma km 120,000 na kuendelea. Mimi napendelea gari isiyozidi 100Km kushuka chini. Nikiwa na 15mil naweza kupata Spacio, Succeed au Raum. Haya ndiyo nimeridhika nayo
 
Ingia kwenye website ya TRA, tafuta calculator ya magari yaliyotumika. Ukiingiza taarifa za gari, mwisho uta click 'calculate'. Zipo nyuzi kadhaa humu ambazo tushaelekeza jinsi ya kuingiza hizo details za gari.
Shukran mkuu! Baada ya kutoka kanisani nimetumia muda mwingi kwenye internet kufanya ka utaafiti kidogo. Nimeingia kwenye website ya TRA na nimefanya calculation ya baadhi ya magari.

Nimegundua kwa bajeti ya 12mil nikiongezea kidogo nitapata gari yenye ubora mzuri. Spacio, Succeed na Raum naweza kupata. Zipo zingine pia kama Karina TI, Premio, Cami, Wish, n.k naweza kupata pia ila ngoja niendelee na utafiti wa hizo 3 za mwanzo kwanza.
 
Back
Top Bottom