Kwa dhuluma ambayo Jakaya Kikwete alimfanyia Mzee Lowassa, ataumaliza uzee wake bila amani

Kwa dhuluma ambayo Jakaya Kikwete alimfanyia Mzee Lowassa, ataumaliza uzee wake bila amani

Madaraka makubwa, usipokuwa na hekima, hasa hekima ya Mungu, yanalevya. Na ukikosa hekima unaweza kudhania kuwa wewe ni kila kitu, kwa sababu hakuna wa kukuhoji wala kukuadhibu.

Mathalani madaraka ya Rais wa Tanzania, anaweza kuyatumia vyovyote apendavyo, hata kuua, akitaka, na asihojiwe wala kushtakiwa mahali popote Duniani.

Lakini hawa watawala, kwa kukosa hekima huwa wanaamini kuwa hawawezi kuhojiwa Duniani, ahera wala hata na nafsi zao.

Marehemu Lowasa, aliuishi uaminifu kwa urafiki wake na Kikwete, lakini Kikwete alimsaliti na kumdhulumu rafiki yake.

Lowasa alijitoa kwa nguvu na moyo wake wote katika kuhakikisha Kikwete anakuwa Rais. Hata ndege iliyompeleka Kikwete Dodoma wakati anautafuta Urais, naambiwa iligharamiwa na Lowasa.

Serikali ya Kikwete ipopata msukosuko kutokana na kashfa ya Richmond, huku Msabaha akitamka wazi kuwa zigo la Richmond halikuwa lake kama waziri, kwa sababu wakati wote aliwasiliana na Serikali kupitia Waziri Mkuu, na hivyo kama kuna makosa, basi ni makosa ya Serikali nzima, Lowasa alimwendea Kikwete kumweleza kuwa yeye ameamua kujiuzulu ili kuilinda Serikali. Kikwete alikataa ombi la Lowasa kujiuzulu, lakini marehemu alishikilia msimamo wake, akiamini ndiyo njia ya kuiokoa Serikali ya Kikwete isidondoke, na pengine ipate imani ya aina fulani toka kwaWabunge.

Katikati ya safari yao, tofauti na makubaliano yao ya awali kuwa yeye marehemu amsaidie Kikwete kuwa Rais 2005, halafu Kikwete amsaidie marehemu kuutafuta Urais mwaka 2015, Kikwete alimtosa rafiki yake na kutaka Urais uende kwa mdogo wake.

Kikwete akifahamu wazi kuwa hakukuwa na mgombea yeyote ndani ya CCM na hata nje, wa kumzidi marehemu, akatumia madaraka yake, kuliondoa jina la Lowasa, lisipelekwe kwenye mkutano mkuu wa CCM.

Huku zaidi ya wajumbe 2,000 wa mkutano mkuu wa CCM wakiwa wamejiandaa kumpigia kura Lowasa RIP, kwa mshangao mkubwa wakaambiwa jina la Lowasa halipo.

Wajumbe wa mkutano mkuu, baada ya kuujua ukweli namna Kikwete alivyodhulumu haki ya rafiki yake wa awali ili Urais uende kwa mdogo wake, wakaitana nje, wakaambizana kuwa wale wote waliokuwa wamejiandaa kumchagua Lowasa, kura zao wampe mgombea aliyeonekana dhaifu kuliko wote, na ambaye amewekwa na Kikwete kama chambo. Ndipo ushindi ulipomwangukia Magufuli RIP.

Lowasa hakukata tamaa, aliamua kugombea nafasi ile ile kupitia CHADEMA. Sote tunayakumbuka mafuriko ya Lowasa. Lakini Kikwete akiwa amefunga mkataba wa kudumu wa kumdhulumu marehemu, huku majumuisho ya kura kutoka vituoni yakionesha wazi kuwa Lowasa alikuwa anaongoza kwa kura nyingi, aliwatuma Polisi kwenda kuvamia kituo cha ujumlishaji kura za Lowasa, wakapora computers zote, na kuwaweka mahabusu wajumlishaji wa kura.

Watanzania, nyakati hizi, tunaombeleza msiba wa Edward Lowasa, ambaye kiuhalisia ndiye aliyechaguliwa na wananchi kuwa Rais wa JMT mwaka 2015.

Lakini ni Kikwete pia, ndiye aliyemdhulumu ushindi wa Urais wa Zanzibar, Maalim Seif RIP.

Dhuluma ya Kikwete kwa marehemu hawa, itaitafuna nafsi yake mpaka siku yake ya mwisho. Madaraka yalimlevya, akaisahau haki. Akasahau kuwa madaraka ni kitu cha kuja na kupita, lakini haki huamua maisha yako ya leo na ya umilele.

Nina hakika, hata wakati huu wamsiba, watu watamtazama Kikwete kwa kujiuliza maswali mengi sana. Je, anaupenda sana na kuisikitikia mwili wa marehemu kuliko nafsi ya marehemu ilipokuwa hai?

Ndugu zangu, tutendeni haki ili tuwe na amani hadi siku za uzee wetu.

Kwa heri Lowasa, mtu uliyependwa na Watanzania walio wengi, ukadhulumiwa na wachache.

Mungu wa rehema, tunakuomba umtuze mja wako kwa raha ya milele kwani aliyathamini uhai wa wengine kuliko madaraka yake binafsi.
Mnarumu.
 
mkuu unamwonea imani Lowasa vp ufisadi wake alioufanya kutajirisha familia yake...hutuonei huruma sisi watanzania!!!
au na wewe family member
Kaka, mafisadi ni wengi mnoo ndani ya CCM, wengi mnooo. Ila ilibidi EL achafuliwe kwa makusudi ili mambo 'yao' yaende. TIS ni ufisadi, madini kuna ufisadi, madawa, MSD, kuna ufisadi, Sukari ufisadi, Mafuta ya kula na ya mitambo ufisadi, ufisadi umeota mizizi ndani ya CCM, ila EL amefanywa alama ya taifa ya ufisadi! TANAPA na TANESCO kuna ufisadi wa kuda mtu
 
Mkuu farsasi anavumilia kuliko punda???? [emoji1787] [emoji1787] [emoji1787]
Mkuu sijamlinganisha Farasi na Punda, japo hawatofautiani sana katika kuvumilia ila nilikuwa nakataa hiyo kauli ya huyo balozi kwamba farasi walikuwa wanahitajia maandalizi ya kipekee sana kubeba Wakuu wa Wilaya vijijini ili wasife.

Ninachofahamu farasi wametumika kwa maelfu ya miaka kubeba binadamu na mizigo na hata kutumika katika kupigana vita tena katika mazingira mengine magumu zaidi kuliko hata ya Tanzania.
 
Madaraka makubwa, usipokuwa na hekima, hasa hekima ya Mungu, yanalevya. Na ukikosa hekima unaweza kudhania kuwa wewe ni kila kitu, kwa sababu hakuna wa kukuhoji wala kukuadhibu.

Mathalani madaraka ya Rais wa Tanzania, anaweza kuyatumia vyovyote apendavyo, hata kuua, akitaka, na asihojiwe wala kushtakiwa mahali popote Duniani.

Lakini hawa watawala, kwa kukosa hekima huwa wanaamini kuwa hawawezi kuhojiwa Duniani, ahera wala hata na nafsi zao.

Marehemu Lowasa, aliuishi uaminifu kwa urafiki wake na Kikwete, lakini Kikwete alimsaliti na kumdhulumu rafiki yake.

Lowasa alijitoa kwa nguvu na moyo wake wote katika kuhakikisha Kikwete anakuwa Rais. Hata ndege iliyompeleka Kikwete Dodoma wakati anautafuta Urais, naambiwa iligharamiwa na Lowasa.

Serikali ya Kikwete ipopata msukosuko kutokana na kashfa ya Richmond, huku Msabaha akitamka wazi kuwa zigo la Richmond halikuwa lake kama waziri, kwa sababu wakati wote aliwasiliana na Serikali kupitia Waziri Mkuu, na hivyo kama kuna makosa, basi ni makosa ya Serikali nzima, Lowasa alimwendea Kikwete kumweleza kuwa yeye ameamua kujiuzulu ili kuilinda Serikali. Kikwete alikataa ombi la Lowasa kujiuzulu, lakini marehemu alishikilia msimamo wake, akiamini ndiyo njia ya kuiokoa Serikali ya Kikwete isidondoke, na pengine ipate imani ya aina fulani toka kwaWabunge.

Katikati ya safari yao, tofauti na makubaliano yao ya awali kuwa yeye marehemu amsaidie Kikwete kuwa Rais 2005, halafu Kikwete amsaidie marehemu kuutafuta Urais mwaka 2015, Kikwete alimtosa rafiki yake na kutaka Urais uende kwa mdogo wake.

Kikwete akifahamu wazi kuwa hakukuwa na mgombea yeyote ndani ya CCM na hata nje, wa kumzidi marehemu, akatumia madaraka yake, kuliondoa jina la Lowasa, lisipelekwe kwenye mkutano mkuu wa CCM.

Huku zaidi ya wajumbe 2,000 wa mkutano mkuu wa CCM wakiwa wamejiandaa kumpigia kura Lowasa RIP, kwa mshangao mkubwa wakaambiwa jina la Lowasa halipo.

Wajumbe wa mkutano mkuu, baada ya kuujua ukweli namna Kikwete alivyodhulumu haki ya rafiki yake wa awali ili Urais uende kwa mdogo wake, wakaitana nje, wakaambizana kuwa wale wote waliokuwa wamejiandaa kumchagua Lowasa, kura zao wampe mgombea aliyeonekana dhaifu kuliko wote, na ambaye amewekwa na Kikwete kama chambo. Ndipo ushindi ulipomwangukia Magufuli RIP.

Lowasa hakukata tamaa, aliamua kugombea nafasi ile ile kupitia CHADEMA. Sote tunayakumbuka mafuriko ya Lowasa. Lakini Kikwete akiwa amefunga mkataba wa kudumu wa kumdhulumu marehemu, huku majumuisho ya kura kutoka vituoni yakionesha wazi kuwa Lowasa alikuwa anaongoza kwa kura nyingi, aliwatuma Polisi kwenda kuvamia kituo cha ujumlishaji kura za Lowasa, wakapora computers zote, na kuwaweka mahabusu wajumlishaji wa kura.

Watanzania, nyakati hizi, tunaombeleza msiba wa Edward Lowasa, ambaye kiuhalisia ndiye aliyechaguliwa na wananchi kuwa Rais wa JMT mwaka 2015.

Lakini ni Kikwete pia, ndiye aliyemdhulumu ushindi wa Urais wa Zanzibar, Maalim Seif RIP.

Dhuluma ya Kikwete kwa marehemu hawa, itaitafuna nafsi yake mpaka siku yake ya mwisho. Madaraka yalimlevya, akaisahau haki. Akasahau kuwa madaraka ni kitu cha kuja na kupita, lakini haki huamua maisha yako ya leo na ya umilele.J

Nina hakika, hata wakati huu wamsiba, watu watamtazama Kikwete kwa kujiuliza maswali mengi sana. Je, anaupenda sana na kuisikitikia mwili wa marehemu kuliko nafsi ya marehemu ilipokuwa hai?

Ndugu zangu, tutendeni haki ili tuwe na amani hadi siku za uzee wetu.

Kwa heri Lowasa, mtu uliyependwa na Watanzania walio wengi, ukadhulumiwa na wachache.

Mungu wa rehema, tunakuomba umtuze mja wako kwa raha ya milele kwani aliyathamini uhai wa wengine kuliko madaraka yake binafsi.
Hakuna mnafiki aliyejaa ghiliba kama Jakaya! amemuambukiza na mchepuko wake saa100!
Kikwete alifanya maasi mengi sana kimya kimya huku akitoa meno nje kama anatabasamu la mbwa aliyeona mfupa!
Jakaya alijipendekeza akaanzisha mchakato wa katiba mpya baadaye akaja akaufuta. Huyu ndiye majinuni mkubwa kwenye taifa hili.
Jakata alishiriki wizi wote mkubwa kuanzia richmond (ambayo alimsukumia EL akafa nayo.
Escrow: Magunia ya Noti yalipelekwa ikulu kwa maelekezo ya Jakaya. Huyu ni wa kukamata kabla hajatutoka! kupoteza ushahidi!!!
Uchunguzi huru ukifanyika utawakamata Jakaya na saa100 kwa mauti ya Magu! trust me>
Kurogana vile vile vilikuwa wazi mno!
 
Na pia kuna kujiuzulu ili kumnusuru Bosi na maswahiba!

Rais H.A. Mwinyi wa Zanzibar ameeleza, alimwandikia Rais Kikwete barua ya kujiuzulu uwaziri wa Ulinzi kutokana na milipuko ya Mabomu, na ilitokea mara mbili. Rais Kikwete alimkatalia kujiuzulu.

Kuhusu ENLowassa
Rais Kikwete alikuwa na uwezo wa kuita 'caucus' ya Chama chake kulijadili suala
Kikwete alikuwa na option ya kutishia kulivunja au kulivunja Bunge kama litamwandama Waziri mkuu wake
Rais Kikwete akiwa sehemu ya Bunge angeomba kwenda kulihutubia Bunge kwa kadhia hiyo.

Rais Kikwete hakufanya jitihada zozote na kumwacha ENL akikaangwa na Bunge.

Hapa simaanishi kwamba kulikuwa na makosa kumkaanga, la hasha lakini ni ukweli kwamba 'rafiki yake ' hakumsaidia. Pengine Kikwete alijua huo ndio utakuwa mwisho wa ushawishi wa ENL katika siasa za Tanzania

Lowassa alibaki na machaguo mawili, kwanza, akomae kutojiuzulu, Bunge limpigie kura ya kutokuwa na imani.
Kuondolewa kwa 'vote of no confidence' kungehitimisha ndoto na safari yake kisiasa once and for all

Pili, ajiuzulu kama sehemu ya kuwajibika na kuinusuru serikali ili apate nafasi mbele ya safari.
Hii ilikuwa '' viable option'' na tumeona ilimsaidia kurudia katika ulingo kwa mara nyingine akiwa na nguvu kubwa.

Kwanini Kikwete analaumiwa? Si kwasababu hakumpa mshirika wake Urais.

JK analaumiwa kwa mambo mawili, kwanza kumtosha ENL wakati alijua mafisadi walivyosaidia mtandao uliomweka madarakani. Kama Rais wa nchi , JK alijua mauza uza ya Richmond na walioko nyuma yake! alijua!

Pili, ENL alijijenga tena baada ya anguko la Uwaziri mkuu. Utaratibu wa chama ni majina kupitiwa na lenye kura nyingi linasonga mbele kwa mchujo zaidi. JK alijua ushawishi wa Lowassa.

Kwa kujua Lowassa hana Kikwakzo na ameshinda kwa uhalali na kwa kujua mbinu za kumzuia kwa kumuanguasha u-P,M zimeshindwa, JK akakata jina la Lowassa si kwa kushindwa bali kwa hiyana tena kinyuma na taratibu za upatikanaji wa mgombea.


Kikwete hakumdhulum Urais , alimdhulumu Lowassa kwa kuvunja taratibu zilizokuwa zinapeleka jina na Lowassa mbele. Alikata jina, Lowassa hakushindwa! hiyo ni dhuluma inayoongelewa
Madini mazito sana haya[emoji109]
 
It's not necessarily lazima ni JK!, sometimes wahafidhina wana nguvu kuliko rais!, ila mkubwa ni jalala!.

Ni kweli kwasababu by that JK alikuwa bado ni mjamaa, na EL alikuwa tayari ni bepari!, sasa wote ni mabepari!.

Sina uhakaki kama makubaliano haya yalikuwepo!, ila kunafanyika vitu vingi ambavyo sio, mfano kutoa fomu moja, kugombea kwa msesereko, kupokezana Mkristo na Muislam.

Sii kweli, jina la Lowassa lilichinjiwa baharini hata kwenye CC halikujadiliwa, ila akina sisi tuliisha muandaa kisaikolojia Elections 2015 - Licha ya kukubalika, Jina la Lowassa halitafika hata CC!

Sii kweli, jina la EL halikutoka hata CC, hivyo halikuingia hata NEC, ule wimbo wa "Tunaimani..." ni uliimbwa NEC! Elections 2015 - Edward Lowassa sio lazima yeye tu ndiye awe Rais wetu 2015, Rais wetu wa 2015 ni...

Sii kweli!, wanaoamua nani awe ngombea wa CCM, sio wana CCM, ni kitu kinachoitwa "the inner circle" angalia tarehe ya bandiko hili Elections 2015 - Mgombea wa Urais Kwa tiketi ya CCM, 2015 "Could Be" John Pombe Magufuli

Sii kweli!, kura zote mpaka za urais zimehesabiwa vituoni na kila msimamizi alipewa copy ya matokeo!, TV Program Alert: Msidanywe na Wanasiasa Kuhusu Uchaguzi Mkuu: Ulikuwa Huru na wa Haki!. Shuhudia! ila kwa upande wa Zanzibar, kule ndio kweli EL alimbwaga JPM Elections 2015 - Imethibitishwa pasi na shaka kuwa ni kweli kabisa, Zanzibar, Maalim Seif na CUF ndio walioshinda

Hii sii kweli, Elections 2015 - Kama Hii ni Kweli, Then, Serikali Yetu ni Serikali Dhalimu?, Haramu?. Hukumu ya Karma ii Juu Yake! makarateka yalifanywa uchaguzi wa 2020!.

Sii kweli, ni wahafidhina!, kwa siasa za Zanzibar, ni lazima CCM ishinde for the sake of Muungano!, ukisikia Muungano tutaulinda kwa gharama yoyote, ushindi wa lazima wa CCM Zanzibar ni moja ya gharama hizo. Iwapo CCM itashindwa Zanzibar, Nini Majaaliwa ya Muungano?

ukitenda wema mwingi kuliko ubaya karma inarekebisha "The Power of 'Karma'- Ndio Hukumu Pekee ya Haki Kamili Hapa Duniani!, Unahukumiwa kwa Matendo Yako!

Baada ya ushauri huu, Ushauri wa bure kwa Rais Kikwete, muombe msamaha Lowassa kabla ya October 25!

Amen
mmh nawe daah
 
CCM walikuwa wanalinda brand ...It was a technical trick..
CCM gani wewe unayoizungumzia? Hiyo ambayo wajumbe wengi wakiwemo kina Nchimbi, Sophia Simba, Kimbisa, Bashe, Musukuma n.k walifura hadi kuanza kuimba wana imani na Lowassa baada ya kutoliona jina lake??
 
Lowasa alikuwa mgonjwa kila mtu alikuwa anajua

Kwani wewe hakuna wakati ulipowahi kuugua? Wewe ni mzima kwa 100% perfection? Kikwete hakuwa mgonjwa? Magufuli hakuwa mgonjwa?

Binadamu karibia wote tuwagonjwa. Tunatofautiana kwa kiwango tu. Hapo ulipo kuna vitu katika mwili wako vina-depreciate bila ya wewe kujua.

Tunachoangalia ni je, huyo anayetajwa kuwa yu mgonjwa ni mgonjwa wa kushindwa kutimiza majukumu yake?
 
Barua ya kujiuzulu kumnusuru bosi na maswahiba utaiandikaje?

Hata ukisema "mimi sina makosa, ila najiuzulu kwa kuinusuru serikali kutoka kwenye matatizo yanayohusiana na mimi kuwapo serikalini" tayari unanuka, tayari umejiweka katika matatizo ya kukufanya uwe untenable. Kuna calculations fulani umekosea hapo.

Bismarck said Politics is tge art of the possible.

Caesar's wife must be above suspicion.

Kuhusu Kikwete.

Kwanza kabisa mna uhakika gani Kikwete alikata jina la Lowassa? Kwa uamuzi wake tu. Hizi habari zina uhakiki gani? Was Kijwete realky that powerful?

Pili,

Chama kinapeleka vipi mbele jina la mtu aliyejiuzulu kwa kashfa kubwa ya rushwa na kutoa angalau optics kwamba ama ameshiriki moja kwa moja katika hiyo rushwa, ama ameshindea kusimamaia wizara rushwa hiyo isitokee?

Yani chama badala ya kujikita kwenye ilani na kampeni, kianze kumsafisha mgombea na ku explain kwa nini mgombea alijiuzulu, huku wapinzani wakimpiga mawe kwamba huyu ni mla rushwa aliwahi mpaka kujiuzulu kwa rushwa?

Kwa nini chama kichague mgombea huyo wakati kina wagombea wengine ambao hawana wingu hilo la kashfa ya rushwa na wanaweza kuanza kampeni moja kwa moja bila kuhitaji kusafishwa?
Mbona ANC ilimchagua Jacob Zuma kuwa mgombea wake akiwa ananuka rushwa na ufisadi mtupu? Kwenye de facto monoparty kama hii yetu chama kinaweza kumpa mtu yeyote nafasi yoyote wanayotaka
 
Inaonekana mfumo mzima wa kuteua mgombea CCM una usiri na matatizo mengi.

Ndiyo maana kuna habari hata Kikwete alikuwa victim wa mifumo hii 1995.

Mfumo ni opaque kiasi kwamba ni vigumu kumlaumu Kikwete beyond reasonable doubt, hapa tunapata maneno mengi ya hearsay na innuendo.
Ni siri iliyo wazi kwamba mfumo huo mzima unafuata maelekezo, muongozo na matamanio ya mwenyekiti
 
Hii ni danganya toto ya wanasiasa, uongozi unatoka kwa wanadamu kwa kura halali, za wizi, mapinduzi au kurithi.
Mazuzu huwa yanadanganywa sana mkuu, eti uongozi unatoka kwa mungu, kama mungu ndio anatuletea mijitu inaiba rasilimali za taifa bila huruma basi huyo mungu inabidi ajitafakari sana. Hiyo mijizi isingekuwa hata na haja ya kupiga kampeni wala kuiba kura ingesubiri mungu awateue
 
Wanachadema wanasahau kuwa ni wao walioandika List of shame mwaka 2007 na kuisoma pale mwembe Yanga huku Marehemu akiwa ndani ya kikosi cha kwanza
Slaa anasema aliiandika hiyo list of shame mwenyewe, huenda aliwaangiza wenzake mkenge ukizingatia baadaye alirejea CCM.
 
Madaraka makubwa, usipokuwa na hekima, hasa hekima ya Mungu, yanalevya. Na ukikosa hekima unaweza kudhania kuwa wewe ni kila kitu, kwa sababu hakuna wa kukuhoji wala kukuadhibu.

Mathalani madaraka ya Rais wa Tanzania, anaweza kuyatumia vyovyote apendavyo, hata kuua, akitaka, na asihojiwe wala kushtakiwa mahali popote Duniani.

Lakini hawa watawala, kwa kukosa hekima huwa wanaamini kuwa hawawezi kuhojiwa Duniani, ahera wala hata na nafsi zao.

Marehemu Lowasa, aliuishi uaminifu kwa urafiki wake na Kikwete, lakini Kikwete alimsaliti na kumdhulumu rafiki yake.

Lowasa alijitoa kwa nguvu na moyo wake wote katika kuhakikisha Kikwete anakuwa Rais. Hata ndege iliyompeleka Kikwete Dodoma wakati anautafuta Urais, naambiwa iligharamiwa na Lowasa.

Serikali ya Kikwete ipopata msukosuko kutokana na kashfa ya Richmond, huku Msabaha akitamka wazi kuwa zigo la Richmond halikuwa lake kama waziri, kwa sababu wakati wote aliwasiliana na Serikali kupitia Waziri Mkuu, na hivyo kama kuna makosa, basi ni makosa ya Serikali nzima, Lowasa alimwendea Kikwete kumweleza kuwa yeye ameamua kujiuzulu ili kuilinda Serikali. Kikwete alikataa ombi la Lowasa kujiuzulu, lakini marehemu alishikilia msimamo wake, akiamini ndiyo njia ya kuiokoa Serikali ya Kikwete isidondoke, na pengine ipate imani ya aina fulani toka kwaWabunge.

Katikati ya safari yao, tofauti na makubaliano yao ya awali kuwa yeye marehemu amsaidie Kikwete kuwa Rais 2005, halafu Kikwete amsaidie marehemu kuutafuta Urais mwaka 2015, Kikwete alimtosa rafiki yake na kutaka Urais uende kwa mdogo wake.

Kikwete akifahamu wazi kuwa hakukuwa na mgombea yeyote ndani ya CCM na hata nje, wa kumzidi marehemu, akatumia madaraka yake, kuliondoa jina la Lowasa, lisipelekwe kwenye mkutano mkuu wa CCM.

Huku zaidi ya wajumbe 2,000 wa mkutano mkuu wa CCM wakiwa wamejiandaa kumpigia kura Lowasa RIP, kwa mshangao mkubwa wakaambiwa jina la Lowasa halipo.

Wajumbe wa mkutano mkuu, baada ya kuujua ukweli namna Kikwete alivyodhulumu haki ya rafiki yake wa awali ili Urais uende kwa mdogo wake, wakaitana nje, wakaambizana kuwa wale wote waliokuwa wamejiandaa kumchagua Lowasa, kura zao wampe mgombea aliyeonekana dhaifu kuliko wote, na ambaye amewekwa na Kikwete kama chambo. Ndipo ushindi ulipomwangukia Magufuli RIP.

Lowasa hakukata tamaa, aliamua kugombea nafasi ile ile kupitia CHADEMA. Sote tunayakumbuka mafuriko ya Lowasa. Lakini Kikwete akiwa amefunga mkataba wa kudumu wa kumdhulumu marehemu, huku majumuisho ya kura kutoka vituoni yakionesha wazi kuwa Lowasa alikuwa anaongoza kwa kura nyingi, aliwatuma Polisi kwenda kuvamia kituo cha ujumlishaji kura za Lowasa, wakapora computers zote, na kuwaweka mahabusu wajumlishaji wa kura.

Watanzania, nyakati hizi, tunaombeleza msiba wa Edward Lowasa, ambaye kiuhalisia ndiye aliyechaguliwa na wananchi kuwa Rais wa JMT mwaka 2015.

Lakini ni Kikwete pia, ndiye aliyemdhulumu ushindi wa Urais wa Zanzibar, Maalim Seif RIP.

Dhuluma ya Kikwete kwa marehemu hawa, itaitafuna nafsi yake mpaka siku yake ya mwisho. Madaraka yalimlevya, akaisahau haki. Akasahau kuwa madaraka ni kitu cha kuja na kupita, lakini haki huamua maisha yako ya leo na ya umilele.

Nina hakika, hata wakati huu wamsiba, watu watamtazama Kikwete kwa kujiuliza maswali mengi sana. Je, anaupenda sana na kuisikitikia mwili wa marehemu kuliko nafsi ya marehemu ilipokuwa hai?

Ndugu zangu, tutendeni haki ili tuwe na amani hadi siku za uzee wetu.

Kwa heri Lowasa, mtu uliyependwa na Watanzania walio wengi, ukadhulumiwa na wachache.

Mungu wa rehema, tunakuomba umtuze mja wako kwa raha ya milele kwani aliyathamini uhai wa wengine kuliko madaraka yake binafsi.
Lowasa alimwendea Kikwete kumweleza kuwa yeye ameamua kujiuzulu ili kuilinda Serikali. Kikwete alikataa ombi la Lowasa kujiuzulu, lakini marehemu alishikilia msimamo wake, akiamini ndiyo njia ya kuiokoa Serikali ya Kikwete isidondoke, na pengine ipate imani ya aina fulani toka kwaWabunge. Nilivyosoma tu hii sehemu niliangalia ID, hivi we lini utakuja kuwa na akili? We ni bure kabisa, umeshajichanganya mwenyewe na kuanza uzushi km ulivyo siku zote. Kweli mwongo n i mwongo tu na tabia haina dawa. Acha uzushi na uwongo havina posho
 
Sasa, kama Lowassa alimwambia Kikwete anataka kujiuzulu, Kikwete akakataa, lakini Lowassa akalazimisha kujiuzulu, huoni Lowassa kajitakia mwenyewe kupigwa chini kwa kulazimisha kujiuzulu?

Ulitegemea vipi Kikwete aendelee ku support mbio za Urais za Lowassa baada ya Lowassa mwenyewe kulazimisha kujiuzulu kutokana na kashfa ya Richmond?

Yani ulitaka Kikwete ampigie kampeni ya urais Lowassa aliyeshindwa Uwaziri Mkuu kwa kashfa?

Huoni kwamba Lowassa ndiye aliyemsaliti Kikwete hapo kwa kulazimisha kujiuzulu na kumuachia manyanga Kikwete, wakati labda alihitajika kupambana akiwa upande wa serikali?

Mtu aliyejiuzulu Uwaziri Mkuu kutokana na msukosuko wa kashfa, unajuaje akipata urais na kupata msukosuko wa kashfa hatajiuzulu tena?

Lowassa alipewa mtihani wa uongozi, akashindwa. Kikwete akaona huyu kashindwa, twende na wengine.

Hata mimi ningemshangaa sana Kikwete kama angempigia kampeni Lowassa kwa sababu ni rafiki yake tu.
Hilo bwege we hujalizoea? Amejiconfuse mwenyewe. Eti CHADEMA ndiyo inamtegemea km mshauri wao?
 
Back
Top Bottom