Steven Joel Ntamusano
JF-Expert Member
- Jun 17, 2023
- 5,203
- 3,913
Kabla ya kupigiwa kura kuna michakato mingi, elewa maana pana ya sentensi yangu achana na hizo issue za Mwamposya.Mungu hachagui mtu kuongoza nchi Steve, kumbuka hapa ni JamiiForums na sio Kanisani kwa Mwamposa, acha tantalila!
Rais wa nchi anachaguliwa kwa kura na wananchi, na mtu kuonesha nia ya kutaka kuwaongoza wengine sio dhambi wala kosa kisheria. Dunia ya sasa lazima uoneshe nia thabiti ya kutaka kitu ndio upate, haya mambo ya sijui mtu kutumia nguvu nyingi kuutaka urais atakuwa na shida fulani ni imani za kipumbavu na kilofa tu.
Kabla ya kupigiwa kura kuna michakato mingi, elewa maana pana ya sentensi yangu achana na hizo issue za Mwamposya.
Hongera Mkuu unachambua kwa hoja nina imani Bams atakuelewa tuSasa kama kashfa haikuwa ya Lowassa, ilikuwa ya serikali nzima, Lowassa kutaka kujiuzulu yeye ni kimbelembele.
Na mtu kimbelembele anaweza kuleta matatizo katika uongozi.
Ni hivi, ingekuwa Kikwete kamtuma Lowassa ajiuzulu, kamwambia "Edward, haya maji ni marefu, inabidi tumtoe mtu hapa ili kuinusuru serikali, tena mtu mzito, nakuomba kama rafiki yangu ujiuzulu ili kuinusuru serikali, halafu hapo baadaye mambo yakipoa, tutakurudisha ugombee urais nikimaliza mimi".
Halafu Lowassa akasema "Kweli? Serikali inaweza kuanguka? Na mimi kujiuzulu kwangu ndiko kutainusuru? Mnanitaka nijiuzulu halafu nitakuwa rais baada yako? Hapo hakuna shida, najiuzulu"
Halafu Lowassa akajiuzulu.
Halafu baadaye, alipotaka kuwa rais, Kikwete akamruka. Akamkata.
Hapo sawa, ungeweza kusema Kikwete mtu jahili na laghai, kamuhadaa mwenzake ajiuzulu, kwa ahadi kuwa atamfanya awe rais, mwenzake akajiuzulu, na urais akamkata.
Lakini mambo hayakuwa hivyo. Kwa maelezo yako, Kikwete hakutaka Lowassa ajiuzulu. Hata Lowassa alivyotaka kujiuzulu, Kikwete alikataa, Lowassa akalazimisha kujiuzulu.
Sasa hapo mpango wa Kikwete wa Lowassa kuendelea kuwa Waziri Mkuu umekataliwa na Lowassa.
Aliyemsaliti mwenzake kati ya Kikwete na Lowassa ni nani hapo?
Na kama Lowassa alikataa mpango wa Kikwete kuendelea kuwa Waziri Mkuu, kwa nini unafikiri ni sawa Kikwete kukubali mpango wa Lowassa kuja kuwa rais?
Huoni sababu ya kamanda aliyekimbia uwanja wa vita si kamanda anayefaa kuongoza majeshi kuwa ni sababu tosha?Sijui sababu zilizopelekea JK kutoingiza jina la Lowassa katika mojawapo ya majina ya kupelekwa kwa wajumbe kupigiwa kura ila kama ni hiyo sababu ya kujiuzulu kinyume na ushauri wake basi itakuwa sababu dhaifu sana na gubu la aina yake.
100%Kila neno lako uliloandika, nimesema Amen!
Mungu atatenda sawia, kila mja atalipwa sawasawa na matendo yake.
Nasikia hakufanya kwa Lowassa tu...bali kwa wengeni wengiMadaraka makubwa, usipokuwa na hekima, hasa hekima ya Mungu, yanalevya. Na ukikosa hekima unaweza kudhania kuwa wewe ni kila kitu, kwa sababu hakuna wa kukuhoji wala kukuadhibu.
Mathalani madaraka ya Rais wa Tanzania, anaweza kuyatumia vyovyote apendavyo, hata kuua, akitaka, na asihojiwe wala kushtakiwa mahali popote Duniani.
Lakini hawa watawala, kwa kukosa hekima huwa wanaamini kuwa hawawezi kuhojiwa Duniani, ahera wala hata na nafsi zao.
Marehemu Lowasa, aliuishi uaminifu kwa urafiki wake na Kikwete, lakini Kikwete alimsaliti na kumdhulumu rafiki yake.
Lowasa alijitoa kwa nguvu na moyo wake wote katika kuhakikisha Kikwete anakuwa Rais. Hata ndege iliyompeleka Kikwete Dodoma wakati anautafuta Urais, naambiwa iligharamiwa na Lowasa.
Serikali ya Kikwete ipopata msukosuko kutokana na kashfa ya Richmond, huku Msabaha akitamka wazi kuwa zigo la Richmond halikuwa lake kama waziri, kwa sababu wakati wote aliwasiliana na Serikali kupitia Waziri Mkuu, na hivyo kama kuna makosa, basi ni makosa ya Serikali nzima, Lowasa alimwendea Kikwete kumweleza kuwa yeye ameamua kujiuzulu ili kuilinda Serikali. Kikwete alikataa ombi la Lowasa kujiuzulu, lakini marehemu alishikilia msimamo wake, akiamini ndiyo njia ya kuiokoa Serikali ya Kikwete isidondoke, na pengine ipate imani ya aina fulani toka kwaWabunge.
Katikati ya safari yao, tofauti na makubaliano yao ya awali kuwa yeye marehemu amsaidie Kikwete kuwa Rais 2005, halafu Kikwete amsaidie marehemu kuutafuta Urais mwaka 2015, Kikwete alimtosa rafiki yake na kutaka Urais uende kwa mdogo wake.
Kikwete akifahamu wazi kuwa hakukuwa na mgombea yeyote ndani ya CCM na hata nje, wa kumzidi marehemu, akatumia madaraka yake, kuliondoa jina la Lowasa, lisipelekwe kwenye mkutano mkuu wa CCM.
Huku zaidi ya wajumbe 2,000 wa mkutano mkuu wa CCM wakiwa wamejiandaa kumpigia kura Lowasa RIP, kwa mshangao mkubwa wakaambiwa jina la Lowasa halipo.
Wajumbe wa mkutano mkuu, baada ya kuujua ukweli namna Kikwete alivyodhulumu haki ya rafiki yake wa awali ili Urais uende kwa mdogo wake, wakaitana nje, wakaambizana kuwa wale wote waliokuwa wamejiandaa kumchagua Lowasa, kura zao wampe mgombea aliyeonekana dhaifu kuliko wote, na ambaye amewekwa na Kikwete kama chambo. Ndipo ushindi ulipomwangukia Magufuli RIP.
Lowasa hakukata tamaa, aliamua kugombea nafasi ile ile kupitia CHADEMA. Sote tunayakumbuka mafuriko ya Lowasa. Lakini Kikwete akiwa amefunga mkataba wa kudumu wa kumdhulumu marehemu, huku majumuisho ya kura kutoka vituoni yakionesha wazi kuwa Lowasa alikuwa anaongoza kwa kura nyingi, aliwatuma Polisi kwenda kuvamia kituo cha ujumlishaji kura za Lowasa, wakapora computers zote, na kuwaweka mahabusu wajumlishaji wa kura.
Watanzania, nyakati hizi, tunaombeleza msiba wa Edward Lowasa, ambaye kiuhalisia ndiye aliyechaguliwa na wananchi kuwa Rais wa JMT mwaka 2015.
Lakini ni Kikwete pia, ndiye aliyemdhulumu ushindi wa Urais wa Zanzibar, Maalim Seif RIP.
Dhuluma ya Kikwete kwa marehemu hawa, itaitafuna nafsi yake mpaka siku yake ya mwisho. Madaraka yalimlevya, akaisahau haki. Akasahau kuwa madaraka ni kitu cha kuja na kupita, lakini haki huamua maisha yako ya leo na ya umilele.
Nina hakika, hata wakati huu wamsiba, watu watamtazama Kikwete kwa kujiuliza maswali mengi sana. Je, anaupenda sana na kuisikitikia mwili wa marehemu kuliko nafsi ya marehemu ilipokuwa hai?
Ndugu zangu, tutendeni haki ili tuwe na amani hadi siku za uzee wetu.
Kwa heri Lowasa, mtu uliyependwa na Watanzania walio wengi, ukadhulumiwa na wachache.
Mungu wa rehema, tunakuomba umtuze mja wako kwa raha ya milele kwani aliyathamini uhai wa wengine kuliko madaraka yake binafsi.
Kama hoja ni Lowassa kukatwa kwa sababu ya kashfa ya Rushwa na angekuwa mzigo mzito kwa chama chake kumuuza kwa wapiga kura hapo nitaelewa hata kama sijui alihusika kiasi gani na kashfa yenyewe, japo pia maswali yanabaki hasa ikijulikana mgombea yeyote ambaye angepitishwa na CCM angeshinda tu kwa namna yoyote ile na hiyo hudhihirika kwa hadhi wanayopewa wagombea wa chama hicho na dola pale wanapoteuliwa hata kabla ya kushika dola yenyewe.Huoni sababu ya kamanda aliyekimbia uwanja wa vita si kamanda anayefaa kuongiza majeshi kuwa ni sababu tosha?
Huoni sababu ya huyu ana wingu la kashfa ya ufisadi mpaka kajiuzulu, na tukimteua awe ngombea wetu, kabla ya kuanza kutangaza ajenda yetu katika kampeni, tutakuwa na mzigo wa ziada wa kumsafisha mgombea wetu kutoka kwenye wingu hili la kashfa ya rushwa, na kwa nini tujipe kazi hiyo ya ziada, ikiwa kuna wengine wengi ambao hawana hilo wingu la kashfa na tunaweza kuanza nao kampeni bila mzigo wa kuwasafisha, huoni hoja hii inatosha kumuondoa Lowassa?
Kikwete ndiye aliyekata jina la Lowassa nisiende kupigiwa kura ya kuwa mgombea urais kupitia ccm!!JK inawezekana ana matatizo yake, mengi tu.
Lakini, kwenye hili la Lowassa.
Mimi sielewi kwa nini JK analaumiwa kwenye hili.
Mpaka sasa JK ana 74 hao Marehemu waliotangulia hata 72 hawakufikisha sasa hapo nani amepelekwa haraka?Laana ya Lowassa na JPM Kwa JK itampeleka Kwa haraka sana.
Kwanini alikata jina la Lowassa kwenda kupigiwa kura ya kuwa mgombea wa urais kupitia ccm?Alipewa nafasi ya uwaziri mkuu amelipwa chake JK hana baya
Hakuna contradiction mkuu.Hapa hakuna logical non sequitur wala nini,
Kwa sababu umejenga hoja kwamba maamuzi aliyofanya Lowassa huenda yalionyesha ni kiongozi mwenye papara hadi ukatolea na mfano wa Sokoine wa farasi, sasa mimi natumia hoja yako hiyo hiyo uliyoijenga na kukuuliza kwamba ina maana gani sasa kama aliyepitishwa na baadaye akashinda kisha lawama zikawa nyingi kuliko kwake kwamba ana maamuzi ya papara pia.
Mimi kwangu hii ni hoja yenye contradiction.
Akikatwa kama wengine.Kwanini alikata jina la Lowassa kwenda kupigiwa kura ya kuwa mgombea wa urais kupitia ccm?
Huoni sababu ya kamanda aliyekimbia uwanja wa vita si kamanda anayefaa kuongiza majeshi kuwa ni sababu tosha?
Huoni sababu ya huyu ana wingu la kashfa ya ufisadi mpaka kajiuzulu, na tukimteua awe ngombea wetu, kabla ya kuanza kutangaza ajenda yetu katika kampeni, tutakuwa na mzigo wa ziada wa kumsafisha mgombea wetu kutoka kwenye wingu hili la kashfa ya rushwa, na kwa nini tujipe kazi hiyo ya ziada, ikiwa kuna wengine wengi ambao hawana hilo wingu la kashfa na tunaweza kuanza nao kampeni bila mzigo wa kuwasafisha, huoni hoja hii inatosha kumuondoa Lowassa?
Anaongelewa Lowassa kwasabu yeye Katika wote alikuwa na potential ya kushinda!Wewe mpuuzi waliotangaza nia walikuwa 38 na majina yalihitajika matano. Kwanini unamuongelea mtu mmoja tu?
JK ana bullet proof ya kisaikolojia kwenye hivi vimaneno maneno vya mtaani.Imani ya Lowassa kwa rafiki yake ndio iliyomponza.
Baada ya yote kutokea, sasa ndio narudi kule juu kwa mleta mada aliposema; "JK ataumaliza uzee wake bila amani", kwa sababu ya usaliti aliomfanyia Lowassa.
Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Naunga mkono hojaMadaraka makubwa, usipokuwa na hekima, hasa hekima ya Mungu, yanalevya. Na ukikosa hekima unaweza kudhania kuwa wewe ni kila kitu, kwa sababu hakuna wa kukuhoji wala kukuadhibu.
Mathalani madaraka ya Rais wa Tanzania, anaweza kuyatumia vyovyote apendavyo, hata kuua, akitaka, na asihojiwe wala kushtakiwa mahali popote Duniani.
Lakini hawa watawala, kwa kukosa hekima huwa wanaamini kuwa hawawezi kuhojiwa Duniani, ahera wala hata na nafsi zao.
Marehemu Lowasa, aliuishi uaminifu kwa urafiki wake na Kikwete, lakini Kikwete alimsaliti na kumdhulumu rafiki yake.
Lowasa alijitoa kwa nguvu na moyo wake wote katika kuhakikisha Kikwete anakuwa Rais. Hata ndege iliyompeleka Kikwete Dodoma wakati anautafuta Urais, naambiwa iligharamiwa na Lowasa.
Serikali ya Kikwete ipopata msukosuko kutokana na kashfa ya Richmond, huku Msabaha akitamka wazi kuwa zigo la Richmond halikuwa lake kama waziri, kwa sababu wakati wote aliwasiliana na Serikali kupitia Waziri Mkuu, na hivyo kama kuna makosa, basi ni makosa ya Serikali nzima, Lowasa alimwendea Kikwete kumweleza kuwa yeye ameamua kujiuzulu ili kuilinda Serikali. Kikwete alikataa ombi la Lowasa kujiuzulu, lakini marehemu alishikilia msimamo wake, akiamini ndiyo njia ya kuiokoa Serikali ya Kikwete isidondoke, na pengine ipate imani ya aina fulani toka kwaWabunge.
Katikati ya safari yao, tofauti na makubaliano yao ya awali kuwa yeye marehemu amsaidie Kikwete kuwa Rais 2005, halafu Kikwete amsaidie marehemu kuutafuta Urais mwaka 2015, Kikwete alimtosa rafiki yake na kutaka Urais uende kwa mdogo wake.
Kikwete akifahamu wazi kuwa hakukuwa na mgombea yeyote ndani ya CCM na hata nje, wa kumzidi marehemu, akatumia madaraka yake, kuliondoa jina la Lowasa, lisipelekwe kwenye mkutano mkuu wa CCM.
Huku zaidi ya wajumbe 2,000 wa mkutano mkuu wa CCM wakiwa wamejiandaa kumpigia kura Lowasa RIP, kwa mshangao mkubwa wakaambiwa jina la Lowasa halipo.
Wajumbe wa mkutano mkuu, baada ya kuujua ukweli namna Kikwete alivyodhulumu haki ya rafiki yake wa awali ili Urais uende kwa mdogo wake, wakaitana nje, wakaambizana kuwa wale wote waliokuwa wamejiandaa kumchagua Lowasa, kura zao wampe mgombea aliyeonekana dhaifu kuliko wote, na ambaye amewekwa na Kikwete kama chambo. Ndipo ushindi ulipomwangukia Magufuli RIP.
Lowasa hakukata tamaa, aliamua kugombea nafasi ile ile kupitia CHADEMA. Sote tunayakumbuka mafuriko ya Lowasa. Lakini Kikwete akiwa amefunga mkataba wa kudumu wa kumdhulumu marehemu, huku majumuisho ya kura kutoka vituoni yakionesha wazi kuwa Lowasa alikuwa anaongoza kwa kura nyingi, aliwatuma Polisi kwenda kuvamia kituo cha ujumlishaji kura za Lowasa, wakapora computers zote, na kuwaweka mahabusu wajumlishaji wa kura.
Watanzania, nyakati hizi, tunaombeleza msiba wa Edward Lowasa, ambaye kiuhalisia ndiye aliyechaguliwa na wananchi kuwa Rais wa JMT mwaka 2015.
Lakini ni Kikwete pia, ndiye aliyemdhulumu ushindi wa Urais wa Zanzibar, Maalim Seif RIP.
Dhuluma ya Kikwete kwa marehemu hawa, itaitafuna nafsi yake mpaka siku yake ya mwisho. Madaraka yalimlevya, akaisahau haki. Akasahau kuwa madaraka ni kitu cha kuja na kupita, lakini haki huamua maisha yako ya leo na ya umilele.
Nina hakika, hata wakati huu wamsiba, watu watamtazama Kikwete kwa kujiuliza maswali mengi sana. Je, anaupenda sana na kuisikitikia mwili wa marehemu kuliko nafsi ya marehemu ilipokuwa hai?
Ndugu zangu, tutendeni haki ili tuwe na amani hadi siku za uzee wetu.
Kwa heri Lowasa, mtu uliyependwa na Watanzania walio wengi, ukadhulumiwa na wachache.
Mungu wa rehema, tunakuomba umtuze mja wako kwa raha ya milele kwani aliyathamini uhai wa wengine kuliko madaraka yake binafsi.
Mkuu,Kama hoja ni Lowassa kukatwa kwa sababu ya kashfa ya Rushwa na angekuwa mzigo mzito kwa chama chake kumuuza kwa wapiga kura hapo nitaelewa hata kama sijui alihusika kiasi gani na kashfa yenyewe, japo pia maswali yanabaki hasa ikijulikana mgombea yeyote ambaye angepitishwa na CCM angeshinda tu kwa namna yoyote ile na hiyo hudhihirika kwa hadhi wanayopewa wagombea wa chama hicho na dola pale wanapoteuliwa hata kabla ya kushika dola yenyewe.