Kwa dhuluma ambayo Jakaya Kikwete alimfanyia Mzee Lowassa, ataumaliza uzee wake bila amani

Kwa dhuluma ambayo Jakaya Kikwete alimfanyia Mzee Lowassa, ataumaliza uzee wake bila amani

Mungu hachagui mtu kuongoza nchi Steve, kumbuka hapa ni JamiiForums na sio Kanisani kwa Mwamposa, acha tantalila!

Rais wa nchi anachaguliwa kwa kura na wananchi, na mtu kuonesha nia ya kutaka kuwaongoza wengine sio dhambi wala kosa kisheria. Dunia ya sasa lazima uoneshe nia thabiti ya kutaka kitu ndio upate, haya mambo ya sijui mtu kutumia nguvu nyingi kuutaka urais atakuwa na shida fulani ni imani za kipumbavu na kilofa tu.
Kabla ya kupigiwa kura kuna michakato mingi, elewa maana pana ya sentensi yangu achana na hizo issue za Mwamposya.
 
""KINACHONIUMIZA BINAFSI NI UTU WA LOWASSA, ALIKUBALI KUBEBA FURUSHI LA LAWAMA ALIMRADI AMUOKOE RAFIKI YAKE""
Walutheri wangekuwa na sera za utakatifu basi Lowassa alistahili.
 
Kabla ya kupigiwa kura kuna michakato mingi, elewa maana pana ya sentensi yangu achana na hizo issue za Mwamposya.
Hakuna maana pana hapo mkuu, mchakato wote unahusisha watu na watu ndio wanapitisha watu wachaguliwe kuwa marais. Rais Kikwete inaaminika alienda Dodoma na majina yake matano ya mfukoni, labda kama unataka kusema Mzee Kikwete ni Mungu.

Mungu amekupa Pumzi uyatafute maarifa, Mungu hajawahi kumfanyia mtu chaguo hapa duniani.
 
Sasa kama kashfa haikuwa ya Lowassa, ilikuwa ya serikali nzima, Lowassa kutaka kujiuzulu yeye ni kimbelembele.

Na mtu kimbelembele anaweza kuleta matatizo katika uongozi.

Ni hivi, ingekuwa Kikwete kamtuma Lowassa ajiuzulu, kamwambia "Edward, haya maji ni marefu, inabidi tumtoe mtu hapa ili kuinusuru serikali, tena mtu mzito, nakuomba kama rafiki yangu ujiuzulu ili kuinusuru serikali, halafu hapo baadaye mambo yakipoa, tutakurudisha ugombee urais nikimaliza mimi".

Halafu Lowassa akasema "Kweli? Serikali inaweza kuanguka? Na mimi kujiuzulu kwangu ndiko kutainusuru? Mnanitaka nijiuzulu halafu nitakuwa rais baada yako? Hapo hakuna shida, najiuzulu"

Halafu Lowassa akajiuzulu.

Halafu baadaye, alipotaka kuwa rais, Kikwete akamruka. Akamkata.

Hapo sawa, ungeweza kusema Kikwete mtu jahili na laghai, kamuhadaa mwenzake ajiuzulu, kwa ahadi kuwa atamfanya awe rais, mwenzake akajiuzulu, na urais akamkata.

Lakini mambo hayakuwa hivyo. Kwa maelezo yako, Kikwete hakutaka Lowassa ajiuzulu. Hata Lowassa alivyotaka kujiuzulu, Kikwete alikataa, Lowassa akalazimisha kujiuzulu.

Sasa hapo mpango wa Kikwete wa Lowassa kuendelea kuwa Waziri Mkuu umekataliwa na Lowassa.

Aliyemsaliti mwenzake kati ya Kikwete na Lowassa ni nani hapo?

Na kama Lowassa alikataa mpango wa Kikwete kuendelea kuwa Waziri Mkuu, kwa nini unafikiri ni sawa Kikwete kukubali mpango wa Lowassa kuja kuwa rais?
Hongera Mkuu unachambua kwa hoja nina imani Bams atakuelewa tu
 
Sijui sababu zilizopelekea JK kutoingiza jina la Lowassa katika mojawapo ya majina ya kupelekwa kwa wajumbe kupigiwa kura ila kama ni hiyo sababu ya kujiuzulu kinyume na ushauri wake basi itakuwa sababu dhaifu sana na gubu la aina yake.
Huoni sababu ya kamanda aliyekimbia uwanja wa vita si kamanda anayefaa kuongoza majeshi kuwa ni sababu tosha?

Huoni sababu ya huyu ana wingu la kashfa ya ufisadi mpaka kajiuzulu, na tukimteua awe ngombea wetu, kabla ya kuanza kutangaza ajenda yetu katika kampeni, tutakuwa na mzigo wa ziada wa kumsafisha mgombea wetu kutoka kwenye wingu hili la kashfa ya rushwa, na kwa nini tujipe kazi hiyo ya ziada, ikiwa kuna wengine wengi ambao hawana hilo wingu la kashfa na tunaweza kuanza nao kampeni bila mzigo wa kuwasafisha, huoni hoja hii inatosha kumuondoa Lowassa?
 
Madaraka makubwa, usipokuwa na hekima, hasa hekima ya Mungu, yanalevya. Na ukikosa hekima unaweza kudhania kuwa wewe ni kila kitu, kwa sababu hakuna wa kukuhoji wala kukuadhibu.

Mathalani madaraka ya Rais wa Tanzania, anaweza kuyatumia vyovyote apendavyo, hata kuua, akitaka, na asihojiwe wala kushtakiwa mahali popote Duniani.

Lakini hawa watawala, kwa kukosa hekima huwa wanaamini kuwa hawawezi kuhojiwa Duniani, ahera wala hata na nafsi zao.

Marehemu Lowasa, aliuishi uaminifu kwa urafiki wake na Kikwete, lakini Kikwete alimsaliti na kumdhulumu rafiki yake.

Lowasa alijitoa kwa nguvu na moyo wake wote katika kuhakikisha Kikwete anakuwa Rais. Hata ndege iliyompeleka Kikwete Dodoma wakati anautafuta Urais, naambiwa iligharamiwa na Lowasa.

Serikali ya Kikwete ipopata msukosuko kutokana na kashfa ya Richmond, huku Msabaha akitamka wazi kuwa zigo la Richmond halikuwa lake kama waziri, kwa sababu wakati wote aliwasiliana na Serikali kupitia Waziri Mkuu, na hivyo kama kuna makosa, basi ni makosa ya Serikali nzima, Lowasa alimwendea Kikwete kumweleza kuwa yeye ameamua kujiuzulu ili kuilinda Serikali. Kikwete alikataa ombi la Lowasa kujiuzulu, lakini marehemu alishikilia msimamo wake, akiamini ndiyo njia ya kuiokoa Serikali ya Kikwete isidondoke, na pengine ipate imani ya aina fulani toka kwaWabunge.

Katikati ya safari yao, tofauti na makubaliano yao ya awali kuwa yeye marehemu amsaidie Kikwete kuwa Rais 2005, halafu Kikwete amsaidie marehemu kuutafuta Urais mwaka 2015, Kikwete alimtosa rafiki yake na kutaka Urais uende kwa mdogo wake.

Kikwete akifahamu wazi kuwa hakukuwa na mgombea yeyote ndani ya CCM na hata nje, wa kumzidi marehemu, akatumia madaraka yake, kuliondoa jina la Lowasa, lisipelekwe kwenye mkutano mkuu wa CCM.

Huku zaidi ya wajumbe 2,000 wa mkutano mkuu wa CCM wakiwa wamejiandaa kumpigia kura Lowasa RIP, kwa mshangao mkubwa wakaambiwa jina la Lowasa halipo.

Wajumbe wa mkutano mkuu, baada ya kuujua ukweli namna Kikwete alivyodhulumu haki ya rafiki yake wa awali ili Urais uende kwa mdogo wake, wakaitana nje, wakaambizana kuwa wale wote waliokuwa wamejiandaa kumchagua Lowasa, kura zao wampe mgombea aliyeonekana dhaifu kuliko wote, na ambaye amewekwa na Kikwete kama chambo. Ndipo ushindi ulipomwangukia Magufuli RIP.

Lowasa hakukata tamaa, aliamua kugombea nafasi ile ile kupitia CHADEMA. Sote tunayakumbuka mafuriko ya Lowasa. Lakini Kikwete akiwa amefunga mkataba wa kudumu wa kumdhulumu marehemu, huku majumuisho ya kura kutoka vituoni yakionesha wazi kuwa Lowasa alikuwa anaongoza kwa kura nyingi, aliwatuma Polisi kwenda kuvamia kituo cha ujumlishaji kura za Lowasa, wakapora computers zote, na kuwaweka mahabusu wajumlishaji wa kura.

Watanzania, nyakati hizi, tunaombeleza msiba wa Edward Lowasa, ambaye kiuhalisia ndiye aliyechaguliwa na wananchi kuwa Rais wa JMT mwaka 2015.

Lakini ni Kikwete pia, ndiye aliyemdhulumu ushindi wa Urais wa Zanzibar, Maalim Seif RIP.

Dhuluma ya Kikwete kwa marehemu hawa, itaitafuna nafsi yake mpaka siku yake ya mwisho. Madaraka yalimlevya, akaisahau haki. Akasahau kuwa madaraka ni kitu cha kuja na kupita, lakini haki huamua maisha yako ya leo na ya umilele.

Nina hakika, hata wakati huu wamsiba, watu watamtazama Kikwete kwa kujiuliza maswali mengi sana. Je, anaupenda sana na kuisikitikia mwili wa marehemu kuliko nafsi ya marehemu ilipokuwa hai?

Ndugu zangu, tutendeni haki ili tuwe na amani hadi siku za uzee wetu.

Kwa heri Lowasa, mtu uliyependwa na Watanzania walio wengi, ukadhulumiwa na wachache.

Mungu wa rehema, tunakuomba umtuze mja wako kwa raha ya milele kwani aliyathamini uhai wa wengine kuliko madaraka yake binafsi.
Nasikia hakufanya kwa Lowassa tu...bali kwa wengeni wengi

Kama yote yasemwayo ni kweli basi kwa hakika Kikwete hatakuwa na amani
 
Japo nilikua bado mdogo kipindi hicho lakini mambo hayakua marahisi kama ulivyo andika. Right kama mzee kikwete angefanikiwa kuwaweka hao wawili ulio wazungumzia sidhani kama CCM ingepona. Kuhusu kwamba Lowassa alimshinda kura JPM sio kweli. Kilichokua kinaenda kuiua CCM kama Lowassa angegombea kupitia CCM ni zile kashfa. CCM ingekufa palihitajika mtu aliyekua msafi ili CCM ipate kushinda lasivyo CCM ingekufa. Hongera Lowassa, Kikwete na JPM kwa kuiokoa CCM. Na ukumbuke agenda zote za CHADEMA za mambo ya ufisadi zilikua zinamhusu Lowassa na CCM. Mimi kwa mtazamo wangu nawapongeza wote Lowassa, JPM na Kikwete kwa kuendelea kuiwezesha CCM kusurvive.
 
Huoni sababu ya kamanda aliyekimbia uwanja wa vita si kamanda anayefaa kuongiza majeshi kuwa ni sababu tosha?

Huoni sababu ya huyu ana wingu la kashfa ya ufisadi mpaka kajiuzulu, na tukimteua awe ngombea wetu, kabla ya kuanza kutangaza ajenda yetu katika kampeni, tutakuwa na mzigo wa ziada wa kumsafisha mgombea wetu kutoka kwenye wingu hili la kashfa ya rushwa, na kwa nini tujipe kazi hiyo ya ziada, ikiwa kuna wengine wengi ambao hawana hilo wingu la kashfa na tunaweza kuanza nao kampeni bila mzigo wa kuwasafisha, huoni hoja hii inatosha kumuondoa Lowassa?
Kama hoja ni Lowassa kukatwa kwa sababu ya kashfa ya Rushwa na angekuwa mzigo mzito kwa chama chake kumuuza kwa wapiga kura hapo nitaelewa hata kama sijui alihusika kiasi gani na kashfa yenyewe, japo pia maswali yanabaki hasa ikijulikana mgombea yeyote ambaye angepitishwa na CCM angeshinda tu kwa namna yoyote ile na hiyo hudhihirika kwa hadhi wanayopewa wagombea wa chama hicho na dola pale wanapoteuliwa hata kabla ya kushika dola yenyewe.
 
JK inawezekana ana matatizo yake, mengi tu.

Lakini, kwenye hili la Lowassa.

Mimi sielewi kwa nini JK analaumiwa kwenye hili.
Kikwete ndiye aliyekata jina la Lowassa nisiende kupigiwa kura ya kuwa mgombea urais kupitia ccm!!
 
Hapa hakuna logical non sequitur wala nini,
Kwa sababu umejenga hoja kwamba maamuzi aliyofanya Lowassa huenda yalionyesha ni kiongozi mwenye papara hadi ukatolea na mfano wa Sokoine wa farasi, sasa mimi natumia hoja yako hiyo hiyo uliyoijenga na kukuuliza kwamba ina maana gani sasa kama aliyepitishwa na baadaye akashinda kisha lawama zikawa nyingi kuliko kwake kwamba ana maamuzi ya papara pia.
Mimi kwangu hii ni hoja yenye contradiction.
Hakuna contradiction mkuu.

Mimi nakataa papara popote.

Kwa Nyerere, kwa Sokoine, kwa Lowassa, kwa Magufuli. Kwa Makonda.

Kwa aliyepita, kwa akiyekatwa. Kwa aliyekufa, kwa anayeishi.

Nikikataa papara kwa aliyekatwa, halafu wewe ukanipa mfano wa aliyepita kwamba mbona huyu naye ana papara, nitakwambia hata huyo naye papara yake niliikataa.

Ushindi wa mtu katika uchaguzi hauoneshi kwamba yuko sawa. Hata Hitler alishinda uchaguzi. Kwa ulaghai.

Inawezekana Watanzania hawajafikia kiwango cha kuielewa na kukataa papara popote wanapoiona, wakaona papara ya Magufuli au ya Makonda ndiyo uongozi wanaouhitaji.

Mimi nasimama palepale kupinga uongozi wa papara, bila kujali huyu kiongozi anapendwa vipi, kachaguliwa kama Magufuki au kakatwa kama Lowassa.

Ameshafariki au anaishi kama Makonda.

Papara ni papara tu.

Sasa wewe ukija na objection yako "mbona Magufuli kachaguliwa wakati alikuwa ana papara" hilo ni kosa la Watanzania waliomchagua, si langu.

Mimi sijawahi kumpigia kura Magufuli, na nimekuwa nikimsema sana utawala wake wote na mpaka kesho namsema kwa papara.

Sasa, hilo swali lako halifai kunitupia mimi, mimi sijamchagua Magufuli. Mimi nimepiga kura uchaguzi wa 1995 tu, baada ya hapo nimekipa kitu viwanja vikubwa, nimepiga kura kwa miguu yangu kuondoka Tanzania.

Kawatupie swali hilo waliomchagua Magufuli.
 
Huoni sababu ya kamanda aliyekimbia uwanja wa vita si kamanda anayefaa kuongiza majeshi kuwa ni sababu tosha?

Huoni sababu ya huyu ana wingu la kashfa ya ufisadi mpaka kajiuzulu, na tukimteua awe ngombea wetu, kabla ya kuanza kutangaza ajenda yetu katika kampeni, tutakuwa na mzigo wa ziada wa kumsafisha mgombea wetu kutoka kwenye wingu hili la kashfa ya rushwa, na kwa nini tujipe kazi hiyo ya ziada, ikiwa kuna wengine wengi ambao hawana hilo wingu la kashfa na tunaweza kuanza nao kampeni bila mzigo wa kuwasafisha, huoni hoja hii inatosha kumuondoa Lowassa?

Kwenye kashfa ya Richmond, Lowasa hakutuhumiwa kwa rushwa. Tuhuma za uzembe zilielekezwa wizara ya madini na nishati, kwa nini waipe tenda kubwa ya kuzalisha umeme kampuni isiyo na uwezo. Katika kujitetea, waziri wa madini na nishati akasema kuwa asilaumiwe yeye pekee kwa sababu maamuzi yalifanywa na Serikali nzima.

Lowasa alijiuzulu kutokana na nafasi yake kama kiongozi mkuu wa Serikali bungeni.
 
Imani ya Lowassa kwa rafiki yake ndio iliyomponza.

Baada ya yote kutokea, sasa ndio narudi kule juu kwa mleta mada aliposema; "JK ataumaliza uzee wake bila amani", kwa sababu ya usaliti aliomfanyia Lowassa.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
JK ana bullet proof ya kisaikolojia kwenye hivi vimaneno maneno vya mtaani.

Mtoto wa Saigon yule kazoea matani ya wazee wa Kiswahili yale ya kujambishana kwenye vikao vya kahawa chungu nyeusi na kashata.

Vikao vile kama huna kifua cha kuhimili maneno huviwezi, na JK ndiyo vikao vyake.

Sasa Mswahili kama yule unafikiri unaweza kumtisha kwa maneno tu?

Kashasema "Huo ni upepo tu, utapita" wakati yupo katikati ya heavy scandal.

Unafikiri ataogopa maneno ya waombolezaji msibani?

Mtu kashajipitia life expectancy ya wabongo, kashakula mazuri ya nchi yote, kashaandaa vizazi na vizazi kukaa vizuri hata akifa kesho, anahudumiwa na taifa mpaka kufa, anataka amani gani zaidi ya hiyo?
 
Madaraka makubwa, usipokuwa na hekima, hasa hekima ya Mungu, yanalevya. Na ukikosa hekima unaweza kudhania kuwa wewe ni kila kitu, kwa sababu hakuna wa kukuhoji wala kukuadhibu.

Mathalani madaraka ya Rais wa Tanzania, anaweza kuyatumia vyovyote apendavyo, hata kuua, akitaka, na asihojiwe wala kushtakiwa mahali popote Duniani.

Lakini hawa watawala, kwa kukosa hekima huwa wanaamini kuwa hawawezi kuhojiwa Duniani, ahera wala hata na nafsi zao.

Marehemu Lowasa, aliuishi uaminifu kwa urafiki wake na Kikwete, lakini Kikwete alimsaliti na kumdhulumu rafiki yake.

Lowasa alijitoa kwa nguvu na moyo wake wote katika kuhakikisha Kikwete anakuwa Rais. Hata ndege iliyompeleka Kikwete Dodoma wakati anautafuta Urais, naambiwa iligharamiwa na Lowasa.

Serikali ya Kikwete ipopata msukosuko kutokana na kashfa ya Richmond, huku Msabaha akitamka wazi kuwa zigo la Richmond halikuwa lake kama waziri, kwa sababu wakati wote aliwasiliana na Serikali kupitia Waziri Mkuu, na hivyo kama kuna makosa, basi ni makosa ya Serikali nzima, Lowasa alimwendea Kikwete kumweleza kuwa yeye ameamua kujiuzulu ili kuilinda Serikali. Kikwete alikataa ombi la Lowasa kujiuzulu, lakini marehemu alishikilia msimamo wake, akiamini ndiyo njia ya kuiokoa Serikali ya Kikwete isidondoke, na pengine ipate imani ya aina fulani toka kwaWabunge.

Katikati ya safari yao, tofauti na makubaliano yao ya awali kuwa yeye marehemu amsaidie Kikwete kuwa Rais 2005, halafu Kikwete amsaidie marehemu kuutafuta Urais mwaka 2015, Kikwete alimtosa rafiki yake na kutaka Urais uende kwa mdogo wake.

Kikwete akifahamu wazi kuwa hakukuwa na mgombea yeyote ndani ya CCM na hata nje, wa kumzidi marehemu, akatumia madaraka yake, kuliondoa jina la Lowasa, lisipelekwe kwenye mkutano mkuu wa CCM.

Huku zaidi ya wajumbe 2,000 wa mkutano mkuu wa CCM wakiwa wamejiandaa kumpigia kura Lowasa RIP, kwa mshangao mkubwa wakaambiwa jina la Lowasa halipo.

Wajumbe wa mkutano mkuu, baada ya kuujua ukweli namna Kikwete alivyodhulumu haki ya rafiki yake wa awali ili Urais uende kwa mdogo wake, wakaitana nje, wakaambizana kuwa wale wote waliokuwa wamejiandaa kumchagua Lowasa, kura zao wampe mgombea aliyeonekana dhaifu kuliko wote, na ambaye amewekwa na Kikwete kama chambo. Ndipo ushindi ulipomwangukia Magufuli RIP.

Lowasa hakukata tamaa, aliamua kugombea nafasi ile ile kupitia CHADEMA. Sote tunayakumbuka mafuriko ya Lowasa. Lakini Kikwete akiwa amefunga mkataba wa kudumu wa kumdhulumu marehemu, huku majumuisho ya kura kutoka vituoni yakionesha wazi kuwa Lowasa alikuwa anaongoza kwa kura nyingi, aliwatuma Polisi kwenda kuvamia kituo cha ujumlishaji kura za Lowasa, wakapora computers zote, na kuwaweka mahabusu wajumlishaji wa kura.

Watanzania, nyakati hizi, tunaombeleza msiba wa Edward Lowasa, ambaye kiuhalisia ndiye aliyechaguliwa na wananchi kuwa Rais wa JMT mwaka 2015.

Lakini ni Kikwete pia, ndiye aliyemdhulumu ushindi wa Urais wa Zanzibar, Maalim Seif RIP.

Dhuluma ya Kikwete kwa marehemu hawa, itaitafuna nafsi yake mpaka siku yake ya mwisho. Madaraka yalimlevya, akaisahau haki. Akasahau kuwa madaraka ni kitu cha kuja na kupita, lakini haki huamua maisha yako ya leo na ya umilele.

Nina hakika, hata wakati huu wamsiba, watu watamtazama Kikwete kwa kujiuliza maswali mengi sana. Je, anaupenda sana na kuisikitikia mwili wa marehemu kuliko nafsi ya marehemu ilipokuwa hai?

Ndugu zangu, tutendeni haki ili tuwe na amani hadi siku za uzee wetu.

Kwa heri Lowasa, mtu uliyependwa na Watanzania walio wengi, ukadhulumiwa na wachache.

Mungu wa rehema, tunakuomba umtuze mja wako kwa raha ya milele kwani aliyathamini uhai wa wengine kuliko madaraka yake binafsi.
Naunga mkono hoja
 
Kama hoja ni Lowassa kukatwa kwa sababu ya kashfa ya Rushwa na angekuwa mzigo mzito kwa chama chake kumuuza kwa wapiga kura hapo nitaelewa hata kama sijui alihusika kiasi gani na kashfa yenyewe, japo pia maswali yanabaki hasa ikijulikana mgombea yeyote ambaye angepitishwa na CCM angeshinda tu kwa namna yoyote ile na hiyo hudhihirika kwa hadhi wanayopewa wagombea wa chama hicho na dola pale wanapoteuliwa hata kabla ya kushika dola yenyewe.
Mkuu,

Hata kama CCM inajua mgombea yeyote atakayeteuliwa na CCM atashinda, bado wana CCM, hususan viongozi, wana haki ya kusema hawataki mgombea atakayewapa mzigo mkubwa kumnadi kwenye kampeni.

That is perfectly reasonable.
 
Back
Top Bottom