Kwa dhuluma ambayo Jakaya Kikwete alimfanyia Mzee Lowassa, ataumaliza uzee wake bila amani

Kwa dhuluma ambayo Jakaya Kikwete alimfanyia Mzee Lowassa, ataumaliza uzee wake bila amani

Madaraka makubwa, usipokuwa na hekima, hasa hekima ya Mungu, yanalevya. Na ukikosa hekima unaweza kudhania kuwa wewe ni kila kitu, kwa sababu hakuna wa kukuhoji wala kukuadhibu.

Mathalani madaraka ya Rais wa Tanzania, anaweza kuyatumia vyovyote apendavyo, hata kuua, akitaka, na asihojiwe wala kushtakiwa mahali popote Duniani.

Lakini hawa watawala, kwa kukosa hekima huwa wanaamini kuwa hawawezi kuhojiwa Duniani, ahera wala hata na nafsi zao.

Marehemu Lowasa, aliuishi uaminifu kwa urafiki wake na Kikwete, lakini Kikwete alimsaliti na kumdhulumu rafiki yake.

Lowasa alijitoa kwa nguvu na moyo wake wote katika kuhakikisha Kikwete anakuwa Rais. Hata ndege iliyompeleka Kikwete Dodoma wakati anautafuta Urais, naambiwa iligharamiwa na Lowasa.

Serikali ya Kikwete ipopata msukosuko kutokana na kashfa ya Richmond, huku Msabaha akitamka wazi kuwa zigo la Richmond halikuwa lake kama waziri, kwa sababu wakati wote aliwasiliana na Serikali kupitia Waziri Mkuu, na hivyo kama kuna makosa, basi ni makosa ya Serikali nzima, Lowasa alimwendea Kikwete kumweleza kuwa yeye ameamua kujiuzulu ili kuilinda Serikali. Kikwete alikataa ombi la Lowasa kujiuzulu, lakini marehemu alishikilia msimamo wake, akiamini ndiyo njia ya kuiokoa Serikali ya Kikwete isidondoke, na pengine ipate imani ya aina fulani toka kwaWabunge.

Katikati ya safari yao, tofauti na makubaliano yao ya awali kuwa yeye marehemu amsaidie Kikwete kuwa Rais 2005, halafu Kikwete amsaidie marehemu kuutafuta Urais mwaka 2015, Kikwete alimtosa rafiki yake na kutaka Urais uende kwa mdogo wake.

Kikwete akifahamu wazi kuwa hakukuwa na mgombea yeyote ndani ya CCM na hata nje, wa kumzidi marehemu, akatumia madaraka yake, kuliondoa jina la Lowasa, lisipelekwe kwenye mkutano mkuu wa CCM.

Huku zaidi ya wajumbe 2,000 wa mkutano mkuu wa CCM wakiwa wamejiandaa kumpigia kura Lowasa RIP, kwa mshangao mkubwa wakaambiwa jina la Lowasa halipo.

Wajumbe wa mkutano mkuu, baada ya kuujua ukweli namna Kikwete alivyodhulumu haki ya rafiki yake wa awali ili Urais uende kwa mdogo wake, wakaitana nje, wakaambizana kuwa wale wote waliokuwa wamejiandaa kumchagua Lowasa, kura zao wampe mgombea aliyeonekana dhaifu kuliko wote, na ambaye amewekwa na Kikwete kama chambo. Ndipo ushindi ulipomwangukia Magufuli RIP.

Lowasa hakukata tamaa, aliamua kugombea nafasi ile ile kupitia CHADEMA. Sote tunayakumbuka mafuriko ya Lowasa. Lakini Kikwete akiwa amefunga mkataba wa kudumu wa kumdhulumu marehemu, huku majumuisho ya kura kutoka vituoni yakionesha wazi kuwa Lowasa alikuwa anaongoza kwa kura nyingi, aliwatuma Polisi kwenda kuvamia kituo cha ujumlishaji kura za Lowasa, wakapora computers zote, na kuwaweka mahabusu wajumlishaji wa kura.

Watanzania, nyakati hizi, tunaombeleza msiba wa Edward Lowasa, ambaye kiuhalisia ndiye aliyechaguliwa na wananchi kuwa Rais wa JMT mwaka 2015.

Lakini ni Kikwete pia, ndiye aliyemdhulumu ushindi wa Urais wa Zanzibar, Maalim Seif RIP.

Dhuluma ya Kikwete kwa marehemu hawa, itaitafuna nafsi yake mpaka siku yake ya mwisho. Madaraka yalimlevya, akaisahau haki. Akasahau kuwa madaraka ni kitu cha kuja na kupita, lakini haki huamua maisha yako ya leo na ya umilele.

Nina hakika, hata wakati huu wamsiba, watu watamtazama Kikwete kwa kujiuliza maswali mengi sana. Je, anaupenda sana na kuisikitikia mwili wa marehemu kuliko nafsi ya marehemu ilipokuwa hai?

Ndugu zangu, tutendeni haki ili tuwe na amani hadi siku za uzee wetu.

Kwa heri Lowasa, mtu uliyependwa na Watanzania walio wengi, ukadhulumiwa na wachache.

Mungu wa rehema, tunakuomba umtuze mja wako kwa raha ya milele kwani aliyathamini uhai wa wengine kuliko madaraka yake binafsi.
Siasa za Tz ni mchezo mchafu
 
Kwamba Lowassa 'Urais ulikuwa ni Haki yake kutoka Kwa Mungu' kwahiyo kadhulumiwa?

Cha ajabu wanaolia Lia na hili ni Chadema...kama Lowassa aliona Ccm wamemdhulumu why alirudi CCM?
Kama alisamehe why Chadema inawauma sana?
Lowassa hii Haki ya kuwa Rais ilitoka wapi?si na Kambona nae watoto wake watadai Nyerere alimdhulumu Urais?watoto wa Sokoine je waseme Baba Yao aliuwawa ili asiwe Rais?

Mijitu mizima inalialia na consipiracy theory za kitoto kabisa
Wazee wa matukio hao tushawajua, kwahiyo hawatuumizi kichwa
 
Mkuu,

Hata kama CCM inajua mgombea yeyote atakayeteuliwa na CCM atashinda, bado wana CCM, hususan viongozi, wana haki ya kusema hawataki mgombea atakayewapa mzigo mkubwa kumnadi kwenye kampeni.

That is perfectly reasonable.
Hiyo ya 2015 labda ilikuwa CCM tofauti kabisa na ile ya 2020, ngoja tuone ya 2025 itakavyokuwa.
 
Kikwete ndiye aliyekata jina la Lowassa nisiende kupigiwa kura ya kuwa mgombea urais kupitia ccm!!
Hata hili nalo bado linahitaji uhakiki.

Kwa sababu michakato yetu haina uwazi.

Lakini, hata kama ikiwa kweli, Lowassa mwenyewe alijijengea mazingira ya kukatwa kwa kujiuzulu (against Kikwetes advice per Bams).

Sasa, ikiwa Kikwete alikuwa na choice, CCM iende na mgombea ambaye hana wingu la kashfa za ufisadi, ambaye itaweza kuanza naye kampeni moja kwa moja bila kumsafisha, au iende na mgombea mwenye wingu la kashfa za ufisadi, mpaka akajiuzulu, kiasi kwamba huyu mwenye kashfa, chama kabla ya kuanza kampeni, kitahitaji kutumia nishati na muda wa ziada kumsafisha kwanza, kabla ya kuongelea ajenda za chama kwenye kampeni.

Hapo kweli mnaona Kikwete alipaswa kukubali mgombea mwenye wingu la ufisadi aende ku distract message ya ajenda za CCM na kuwabebesha mzigo wana CCM kumsafisha kwanza kabla ya yote?

Kikwete aliona twende na mtu asiye na mzigo wa ziada wa kashfa. Tujikite kwenye kuelezea ilani ya chama zaidi kuliko kumsafisha mtu.
 
Japo nilikua bado mdogo kipindi hicho lakini mambo hayakua marahisi kama ulivyo andika. Right kama mzee kikwete angefanikiwa kuwaweka hao wawili ulio wazungumzia sidhani kama CCM ingepona. Kuhusu kwamba Lowassa alimshinda kura JPM sio kweli. Kilichokua kinaenda kuiua CCM kama Lowassa angegombea kupitia CCM ni zile kashfa. CCM ingekufa palihitajika mtu aliyekua msafi ili CCM ipate kushinda lasivyo CCM ingekufa. Hongera Lowassa, Kikwete na JPM kwa kuiokoa CCM. Na ukumbuke agenda zote za CHADEMA za mambo ya ufisadi zilikua zinamhusu Lowassa na CCM. Mimi kwa mtazamo wangu nawapongeza wote Lowassa, JPM na Kikwete kwa kuendelea kuiwezesha CCM kusurvive.
Ili ccm kiendelee kutesa watu kama sahivi
 
Ypu do not get my point.

Hapa tunaongelea dhuluma, siyo kumsaidia.

Kikwete alimdhulumu Lowasa haki ya kupigiwa kura na wajumbe, tena wengi waliokuwa wakimtaka awe mgombea kupitia CCM.

Lowasa akaondoka CCM, akagombea kupitia CHADEMA, akashinda katika kupata uwingi wa kura, Kikwete tena akamdhulumu kwa kutumia madaraka yake.

CCM Wana taratibu zao na yeye ndio alikuwa mwenyekiti wa hicho kikao, kilichomkataa EL ni taratibu za CCM wenyewe ndani ya vikao vyao sio JK.

toka 1995 ninasikia upinzani umeshinda na umeibiwa kura, Watanzania wengi bado ni wajinga ndio maana CCM inashinda maana wengi wanaamini katika CCM. 2015 binafsi nikipiga kura Kwa mara ya kwanza na kura yangu ilienda kwa JPM maana niliamini kwa JPM na ilivyokuwa kwa Watanzania wengi 2015 madai yako EL alishinda na kuconclude alidhulumiwa hayana mashiko zaidi ya "hearsay" maana hakuna chombo huru kilichothibisha hili.
 
Kwenye kashfa ya Richmond, Lowasa hakutuhumiwa kwa rushwa. Tuhuma za uzembe zilielekezwa wizara ya madini na nishati, kwa nini waipe tenda kubwa ya kuzalisha umeme kampuni isiyo na uwezo. Katika kujitetea, waziri wa madini na nishati akasema kuwa asilaumiwe yeye pekee kwa sababu maamuzi yalifanywa na Serikali nzima.

Lowasa alijiuzulu kutokana na nafasi yake kama kiongozi mkuu wa Serikali bungeni.
Hizo ni minutiae za nuance ambayo big picture optics haijali.

Kwa nini Lowassa alikubali kujiuzulu? Kwa nini alishindwa kusimamia Wizara ya Madini kama PM?

Wananchi wachache sana wanaweza kuchambua mambo hivyo.

Lowassa alivyojiuzulu, Rais George Bush aliipongeza serikali ya Tanzania kwa kuliondoa jizi hilo Lowassa. Alisema kitu kuipongeza Tanzania "for getting rid of that crook".

Ndivyo ilivyoeleweka hata kimataifa huko. Ndivyo wananchi wengi walivyoelewa, Lowassa fisadi kajiuzulu.

Sasa Tanzania ingeonekana vipi ikiwa "that crook" anarudi kuwa rais na Kikwete anampigia kampeni?

Ingeonekana kumbe haya yote maigizo ya Pwagu na Pwaguzi, hawa wote majambazi tu yanatuchezea akili.

Ndicho Kikwete alichokataa hicho.

Kwenye siasa, hata kama umejiuzulu kwa sababu wewe kiongozi tu, hukushiriki moja kwa moja, optics, imagery matters.
 
JK ana bullet proof ya kisaikolojia kwenye hivi vimaneno maneno vya mtaani.

Mtoto wa Saigon yule kazoea matani ya wazee wa Kiswahili yale ya kujambishana kwenye vikao vya kahawa chungu nyeusi na kashata.

Vikao vile kama huna kifua cha kuhimili maneno huviwezi, na JK ndiyo vikao vyake.

Sasa Mswahili kama yule unafikiri unaweza kumtisha kwa maneno tu?

Kashasema "Huo ni upepo tu, utapita" wakati yupo katikati ya heavy scandal.

Unafikiri ataogopa maneno ya waombolezaji msibani?

Mtu kashajipitia life expectancy ya wabongo, kashakula mazuri ya nchi yote, kashaandaa vizazi na vizazi kukaa vizuri hata akifa kesho, anahudumiwa na taifa mpaka kufa, anataka amani gani zaidi ya hiyo?
Unanishangaza unavyoamini kupitiliza maneno ya JK, mpaka unajigeuza kabisa kuwa kama msemaji wake!.

Angekuwa haogopi maneno yule;

- Asingehangaika kumtuma Makonda akampige ngumi Mzee Warioba wakati wa utawala wake.

- Asingehangaika kuyavuruga maandamano ya Chadema kule Arusha, kwa kutumia polisi na kuwaumiza waandamanaji.

- Wala asingehangaika kumteka Dr. Ulimboka, aliyekuwa akipigania haki za madaktari, akaokotwa ameumizwa kwenye msitu wa Mabwepande, wakati ule wa utawala wake.

Hapo hakuna cha Saigon wala upepo.... tafakari. Anawadanganya na wenzio kwa maneno matupu, mnadanganyika, huku chini chini anachukua hatua kwa vitendo, ndicho alichomfanya Lowassa.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Hiyo ya 2015 labda ilikuwa CCM tofauti kabisa na ile ya 2020, ngoja tuone ya 2025 itakavyokuwa.
Tutaona.

2025 si "Mama" anamalizia, au kuna nani mwingine tena?

Mkuu,

Kabla ya uchaguzi wa 2005 mimi nilikuwa nakaa na January katika "smart set" yetu na kina Rev. Kishoka, tunazungumza kampeni. Tukawa tunajadili nani anafaa kuwa rais.

January akaomba udhuru asichangie mada hiyo kwa sababu yeye ana mgombea wake wa karibu sana in real life, atakuwa biased, next thing I know, January karudi Bongo namuona anazunguka na Kikwete nchi nzima kumuombea kura, kujibu hoja, kupanga mikakati. Watu wanazunguka nchi nzima.

Hawa watu wanaozunguka nchi nzima ni lazima wawe strategic katika kumchagua mgombea wao, wakiwa na option ya mtu mwenye urahisi kumnadi, of course watachagua hiyo.
 
 
Madaraka makubwa, usipokuwa na hekima, hasa hekima ya Mungu, yanalevya. Na ukikosa hekima unaweza kudhania kuwa wewe ni kila kitu, kwa sababu hakuna wa kukuhoji wala kukuadhibu.

Mathalani madaraka ya Rais wa Tanzania, anaweza kuyatumia vyovyote apendavyo, hata kuua, akitaka, na asihojiwe wala kushtakiwa mahali popote Duniani.

Lakini hawa watawala, kwa kukosa hekima huwa wanaamini kuwa hawawezi kuhojiwa Duniani, ahera wala hata na nafsi zao.

Marehemu Lowasa, aliuishi uaminifu kwa urafiki wake na Kikwete, lakini Kikwete alimsaliti na kumdhulumu rafiki yake.

Lowasa alijitoa kwa nguvu na moyo wake wote katika kuhakikisha Kikwete anakuwa Rais. Hata ndege iliyompeleka Kikwete Dodoma wakati anautafuta Urais, naambiwa iligharamiwa na Lowasa.

Serikali ya Kikwete ipopata msukosuko kutokana na kashfa ya Richmond, huku Msabaha akitamka wazi kuwa zigo la Richmond halikuwa lake kama waziri, kwa sababu wakati wote aliwasiliana na Serikali kupitia Waziri Mkuu, na hivyo kama kuna makosa, basi ni makosa ya Serikali nzima, Lowasa alimwendea Kikwete kumweleza kuwa yeye ameamua kujiuzulu ili kuilinda Serikali. Kikwete alikataa ombi la Lowasa kujiuzulu, lakini marehemu alishikilia msimamo wake, akiamini ndiyo njia ya kuiokoa Serikali ya Kikwete isidondoke, na pengine ipate imani ya aina fulani toka kwaWabunge.

Katikati ya safari yao, tofauti na makubaliano yao ya awali kuwa yeye marehemu amsaidie Kikwete kuwa Rais 2005, halafu Kikwete amsaidie marehemu kuutafuta Urais mwaka 2015, Kikwete alimtosa rafiki yake na kutaka Urais uende kwa mdogo wake.

Kikwete akifahamu wazi kuwa hakukuwa na mgombea yeyote ndani ya CCM na hata nje, wa kumzidi marehemu, akatumia madaraka yake, kuliondoa jina la Lowasa, lisipelekwe kwenye mkutano mkuu wa CCM.

Huku zaidi ya wajumbe 2,000 wa mkutano mkuu wa CCM wakiwa wamejiandaa kumpigia kura Lowasa RIP, kwa mshangao mkubwa wakaambiwa jina la Lowasa halipo.

Wajumbe wa mkutano mkuu, baada ya kuujua ukweli namna Kikwete alivyodhulumu haki ya rafiki yake wa awali ili Urais uende kwa mdogo wake, wakaitana nje, wakaambizana kuwa wale wote waliokuwa wamejiandaa kumchagua Lowasa, kura zao wampe mgombea aliyeonekana dhaifu kuliko wote, na ambaye amewekwa na Kikwete kama chambo. Ndipo ushindi ulipomwangukia Magufuli RIP.

Lowasa hakukata tamaa, aliamua kugombea nafasi ile ile kupitia CHADEMA. Sote tunayakumbuka mafuriko ya Lowasa. Lakini Kikwete akiwa amefunga mkataba wa kudumu wa kumdhulumu marehemu, huku majumuisho ya kura kutoka vituoni yakionesha wazi kuwa Lowasa alikuwa anaongoza kwa kura nyingi, aliwatuma Polisi kwenda kuvamia kituo cha ujumlishaji kura za Lowasa, wakapora computers zote, na kuwaweka mahabusu wajumlishaji wa kura.

Watanzania, nyakati hizi, tunaombeleza msiba wa Edward Lowasa, ambaye kiuhalisia ndiye aliyechaguliwa na wananchi kuwa Rais wa JMT mwaka 2015.

Lakini ni Kikwete pia, ndiye aliyemdhulumu ushindi wa Urais wa Zanzibar, Maalim Seif RIP.

Dhuluma ya Kikwete kwa marehemu hawa, itaitafuna nafsi yake mpaka siku yake ya mwisho. Madaraka yalimlevya, akaisahau haki. Akasahau kuwa madaraka ni kitu cha kuja na kupita, lakini haki huamua maisha yako ya leo na ya umilele.

Nina hakika, hata wakati huu wamsiba, watu watamtazama Kikwete kwa kujiuliza maswali mengi sana. Je, anaupenda sana na kuisikitikia mwili wa marehemu kuliko nafsi ya marehemu ilipokuwa hai?

Ndugu zangu, tutendeni haki ili tuwe na amani hadi siku za uzee wetu.

Kwa heri Lowasa, mtu uliyependwa na Watanzania walio wengi, ukadhulumiwa na wachache.

Mungu wa rehema, tunakuomba umtuze mja wako kwa raha ya milele kwani aliyathamini uhai wa wengine kuliko madaraka yake binafsi.

Kwanini wafanye biashara kwenye mali ambayo sio ya kwao? Tanzania si mali binafsi ya mtu yoyote. Ni ya watanzania.

Wote walifanya makosa kama kweli walikubaliana hivyo. Na lazima itakuwa shubiri sababu ilikuwa biashara ya upatu
 
Sasa kama kashfa haikuwa ya Lowassa, ilikuwa ya serikali nzima, Lowassa kutaka kujiuzulu yeye ni kimbelembele.

Na mtu kimbelembele anaweza kuleta matatizo katika uongozi.

Ni hivi, ingekuwa Kikwete kamtuma Lowassa ajiuzulu, kamwambia "Edward, haya maji ni marefu, inabidi tumtoe mtu hapa ili kuinusuru serikali, tena mtu mzito, nakuomba kama rafiki yangu ujiuzulu ili kuinusuru serikali, halafu hapo baadaye mambo yakipoa, tutakurudisha ugombee urais nikimaliza mimi".

Halafu Lowassa akasema "Kweli? Serikali inaweza kuanguka? Na mimi kujiuzulu kwangu ndiko kutainusuru? Mnanitaka nijiuzulu halafu nitakuwa rais baada yako? Hapo hakuna shida, najiuzulu"

Halafu Lowassa akajiuzulu.

Halafu baadaye, alipotaka kuwa rais, Kikwete akamruka. Akamkata.

Hapo sawa, ungeweza kusema Kikwete mtu jahili na laghai, kamuhadaa mwenzake ajiuzulu, kwa ahadi kuwa atamfanya awe rais, mwenzake akajiuzulu, na urais akamkata.

Lakini mambo hayakuwa hivyo. Kwa maelezo yako, Kikwete hakutaka Lowassa ajiuzulu. Hata Lowassa alivyotaka kujiuzulu, Kikwete alikataa, Lowassa akalazimisha kujiuzulu.

Sasa hapo mpango wa Kikwete wa Lowassa kuendelea kuwa Waziri Mkuu umekataliwa na Lowassa.

Aliyemsaliti mwenzake kati ya Kikwete na Lowassa ni nani hapo?

Na kama Lowassa alikataa mpango wa Kikwete kuendelea kuwa Waziri Mkuu, kwa nini unafikiri ni sawa Kikwete kukubali mpango wa Lowassa kuja kuwa rais?

Hawa watu walikuwa wanafanya biashara ya upatu 😂 😂 😂 😂 😂 😂 😂 😂
 
Tatizo haya mnayaongea ninyi mkifikiri kila mtu anatumia namna kama zenu ku handle life dissapointents.
Mzee unaweza kuta anaishi happy tu.
 
Nimesoma kidogo lakini kubwa nimeona umbea umetamalaki,mara ndege alikodi Lowasa,mara Membe mdogo wake Kikwete! Membe mmwera kwa baba na mama wakati Kikwete ni mkwere kwa baba na mama! Huu ujinga unaopeana kwenye vijiwe vya kahawa muuache hukohuko jamani.
Hahaha hahaha halafu sasa watu wanataka tuamini wale wanayoamini wao, ukiwapa story za Kitaa za upande mwingine hawataki wakati zote ni "hearsay" tu za vijiweni

Humu kuna mtu anaweza hata kukublock eti kisa umembishia Jambo fulani ambalo hata ushahidi nao Hana.
 
Back
Top Bottom