Kwa dhuluma ambayo Jakaya Kikwete alimfanyia Mzee Lowassa, ataumaliza uzee wake bila amani

Kwa dhuluma ambayo Jakaya Kikwete alimfanyia Mzee Lowassa, ataumaliza uzee wake bila amani

JK kama mtu ana mapungufu yake, hawezi kukosa. Huwezi kuongoza mamilioni ya watu ukakosa matatizo.

Lakini, haya mambo mengi hatuna hata uhakika kama yametokea hivyo yanavyosemwa yalitokea, na kama yametokea kweli, ni JK aliyeamuru ama watu wa chini yake tu wamejipendekeza kufanya mambo bila amri.

Sitaki kuongea mengi, lakini nataka kusema kwamba ukiongea katika network za kifamilia, halafu ukisikiliza stories za kwenye magazeti na vijiweni, stories nyingi ni tofauti sana. Tatizo viongozi wa Bongo hawana uwazi. Mimi saa nyingine naongea na hao watoto wa kina Warioba na Lowassa, naona dah, kazi yetu kupata story straight ni kubwa sana.

Kuna mambo nashindwa hata kukubishia kwa sababu sitaki kutengeneza mzozo ambao hauwezi kuwa settled one way or another hapa.

Ukweli utabaki kuwa, kipindi cha JK ni kipindi ambacho watu walikuwa huru sana kusema. Kipindi pekee cha kukilinganisha na kipindi cha JK ni kipindi cha Mzee Mwinyi cha Ruksa.

Mambo mengine mtamlaumu JK wakati JK hahusiki moja kwa moja na wala hajaagiza mtu.

Nitakupa mfano mmoja ninaoujua binafsi unaoonesha mambo mengine mnaweza kumpa lawama JK kuwa kaamuru, wakati hata hakuamuru na in fact yupo against nayo.

Kipindi cha JK Jamiiforums ilikuwa moto sana. Kipindi hicho FMES (RIP) na wenzake waliokuwa serikalini walikuwa wanapata sana nondo za ndani ya serikali na kuzimwaga hapa, watu wakawa wanachambua mambo na kuinanga serikali kwa style ya "Kumkoma Nyani Giladi". Wakongwe wa JF watakumbuka.

Sasa, ikatokea Polisi fulani wakubwa wakawa wanataka sifa, wakamkamata mkuu Maxence Melo. Wakamfunga.

Kusikia hivyo, tukalianzisha bonge la timbwili kimataifa. Tukawatafuta "The Committe to Protect Jouranalists" www.cpj.org , tukawatafura Human Rights Watch, wakalianzisha timbwili kwenye vyombo vya habari vya kimataifa. Shout out to Mimi Mwanakijiji kwa kazi kubwa aliyoifanya.

Tanzania ikawa ina trend vibaya kwamba inaminya uhuru wa habari.

JK kusikia hivyo, akasema kwa nini mnawasumbua hawa vijana wa dotcom ambao hawana hata impact kwenye utawala wangu? Waachieni tu, msiwabugudhi. Msinichafulie jina la nchi yangu bila sababu.

Mara moja Max akaachiwa.

Sasa, kwa mtu ambaye hakuwa karibu na ile story, angeweza kujua kuwa JK aliamuru Max ashikwe, halafu ikaonekana issue imeleta negative press kimataifa, akaamuru Max aachiwe.

Kumbe, Max alivyoshikwa hata JK hakujua.

Mambo mengine tunaweza kumlaumu JK kwa sababu watu wa chini wamejipendekeza tu. JK mwenyewe hata hakuyapenda.
Mkuu ni nadra sana au hakuna mahali popote duniani Rais au mtawala mkuu wa nchi anaweza kuthibitika kutenda mambo yoyote yaliyo mabaya zaidi sana kwenye nchi ambayo katiba imempa madaraka makubwa mno Rais na kumfanya kutowajibika au kuweza kuwajibishwa na chombo chochote.

Ni vigumu kuona popote Hitler akisema au akitoa amri ya Wayahudi kuuwawa, ni vigumu sana hata kwa madikteta wakatili sana kupata ushahidi popote wakiamuru mateso kwa wapinzani na wakosoaji wao, mara zote huwa ni watu "wanaojipendekeza". Ila kama mtawala hataki mambo fulani ni wajibu wake kuonyesha kwa kauli zisizo na kificho hataki hayo mambo na kuwaondoa kabisa wanaojipendekeza wanaoweza kufanya hayo mambo asiyokubaliana nayo.
 
Halafu inaendeshwa kwa karata tatu.

Cheusi umeliwa wewe, chekundu nimekula mimi 🤣🤣🤣.

😂 😂 😂 😂 😂 😂 Kama wana majuto wajijutie wenyewe...kama wana machozi wajililie wenyewe. Huwezi kufikiria nchi yenye watu Mil 60 ni mali ya watu wachache. Waigawane wanavyotaka.

Ni ujinga uliojificha kwenye usomi.
 
Lazima umtetee huyo bwege wenu anaewalisha nyie maboya!

Hapana...Marehemu aliigizwa cha kike..ila alidhani yeye ni mtoto wa mujini haikumuhusu. Mnagawanaje nchi kama vile ni mali yenu binafsi? Ni utopolo uliopitiliza
 
Mkuu ni nadra sana au hakuna mahali popote duniani Rais au mtawala mkuu wa nchi anaweza kuthibitika kutenda mambo yoyote yaliyo mabaya zaidi sana kwenye nchi ambayo katiba imempa madaraka makubwa mno Rais na kumfanya kutowajibika au kuweza kuwajibishwa na chombo chochote.

Ni vigumu kuona popote Hitler akisema au akitoa amri ya Wayahudi kuuwawa, ni vigumu sana hata kwa madikteta wakatili sana kupata ushahidi popote wakiamuru mateso kwa wapinzani na wakosoaji wao, mara zote huwa ni watu "wanaojipendekeza". Ila kama mtawala hataki mambo fulani kuonyesha kwa kauli zisizo na kificho hataki hayo mambo na kuwaondoa kabisa wanaojipendekeza wanaoweza kufanya hayo mambo asiyokubaliana nayo.
Sawa,

Na JK alikuwa anaangalia "political expediency". Alikuwa mtu wa mahesabu.

Alikemea pale alipoona kuwa watu wanaonewa wakati hata wasipoonewa hakuna impact kwenye serikali yake.

Lakini pia, kuna mengi hakuamuru, ila yalifanyika na hakukemea, kwa sababu yalimpa political advantage.

Ndiyo maana hata polisi walikuwa wanabahatisha bahatisha wanakamata kamata hawajui wapi mzee atafurahia na kuwaacha tu, na wapi ataona hapafai na kuwakaripia.

Kwa hayo siwezi kumtetea.

Lakini, kwenye la Lowassa, Lowassa kukubali kujiuzulu tu alijiangusha mwenyewe.

Kuna jamaa mmoja anaitwa Preet Bharara. Mmarekani mwenye asili ya India. Alikuwa US District Attorney for The Southern District of New York. Hapo ndipo kwenye ma deal yote machafu ya Wall St. Majambazi ya dunia ya wizi wa kalamu kwenye New York Stock Exchange , NASDAQ etc yalikuwa chini ya jurisdiction yake, ma boss yote ya Mafia ya New York City yalikuwa kwake. Hicho kiti alikalia Rudolph Giuliani kabla hajawa meya wa New York City.

Sasa, Trump alivyoingia kuwa rais alimkuta huyu Preet Bharara. Trump alijua kuwa ana madudu mengi sana hapo New York City. Akawa anataka kukutana na Preet Bharara ampange. Trump huwa ana ujinga fulani wa kuleta u Mafia kwenye kazi za serikali. Yani anawaambia wale wateule wa rais waape kiapo cha kuwa watiifu kwake personally, si kwa rais wa US.

Sasa huyo jamaa Preet Baharara anajua kazi yake vizuri, yani kazi yake haimruhusu hata kukutana kutana na rais ovyo. Kwa sababu kazi yake inamtaka awe huru na ana mipaka mpaka ya kuweza kumchunguza rais. Sasa Trump akawa anataka kukutana na Preet Bharara. Preet anauliza sababu, anataka justification kisheria na kikazi. Trump akawa hawezi kutoa sababu. Preet Baharara akawa anampotezea.

Trump akamwambia Preet Bharara, Preet, usiringe kukutana na mimi, ninaweza kukutoa kwenye hiyo kazi. Preet Bharara akaendelea kukataa kukutana na Trump.

Trump akamwambia Preet Bharara, naona hatutaendana, nakutaka ujiuzulu nichague mtu mwingine akalie hicho kiti.

Preet Bharara akamwambia Trump, over my dead body, sijiuzulu ng'o. Kama unataka, nifukuze kazi dunia nzima ijue umenifukuza kazi. Nijiuzulu kwa sababu gani wakati sijakosea kitu?

Trump akaona hakuna jinsi. Akamfukuza kazi Preet Bharara.

Politico waliandika hii habari hapa.


Sasa, huyu Muhindi Mmarekani mimi namuheshimu sana.

Kwa sababu, ni mtu ambaye alijiona hana kosa, akaombwa kujiuzulu kisiasa, akakataa, ikabidi afukuzwe kazi dunia nzima ijue katoka kazini kwa kufukuzwa, si kwa kujiuzulu.

Sasa, mtu kama huyu Preet Bharara akiniambia kuwa yeye hakufanya lolote baya, ndiyo maana hakujiuzulu, amefukuzwa kazi kwa sababu za kisiasa, naweza kumsikiliza.

Si Lowassa, mtu aliyekubali kuandika barua ya kujiuzulu mwenyewe.

Ukishaandika barua ya kujiuzulu umekubali makosa.

Watu wakikuchinjia baharini kisiasa baada ya hapo ni sawasawa tu.
 
Kwamba Lowassa 'Urais ulikuwa ni Haki yake kutoka Kwa Mungu' kwahiyo kadhulumiwa?

Cha ajabu wanaolia Lia na hili ni Chadema...kama Lowassa aliona Ccm wamemdhulumu why alirudi CCM?
Kama alisamehe why Chadema inawauma sana?
Lowassa hii Haki ya kuwa Rais ilitoka wapi?si na Kambona nae watoto wake watadai Nyerere alimdhulumu Urais?watoto wa Sokoine je waseme Baba Yao aliuwawa ili asiwe Rais?

Mijitu mizima inalialia na consipiracy theory za kitoto kabisa
Wajinga wenzako wame like,eti wewe una akili [emoji3064][emoji3064][emoji3064]
 
Wote hawakuwa wema kwa watanzania, walilinda maslahi yao binafsi na watu wao, mwananchi akaachwa ajipambanie katika mazingira magumu.

Huu utamaduni mpaka sasa unaendelea.

Labda kama ita make sense kuwa JK alikuwa na huruma kidogo kwa kuwaza huyu akiingia kwa ushauri ambao huwa ananipa, hata hayo mazingira magumu, yatakuwa magumu zaidi.

Ndio maana wakatuacha tena kwa mtu alieamua kutubatiza na jina kabisa "wananchi wanyonge", nae akaendelea na mambo yale yale, akayapaka rangi tu na maigizo mengi.

Rais wa kujali maendeleo ya Tanzania kiujumla hawezi kutoka CCM, labda kile chama kipasuke na kufuta tamaduni mbovu zilizopo katika masuala ya kiuongozi.

Lowasa(R.I.P) alidhulumiwa au hakudhulumiwa, alikuwa anacheza timu ambayo huo ni utamaduni wao.
 
Waswahili wa Pwani sio watu wakuwaamini.


Lowasa alifanya kosa kubwa kumuamini mswahili
Lowassa alikataliwa na Julius Nyerere 1995

Lowassa akakataliwa na Bunge 2007

Lowassa akakataliwa na Chadema akawekwa kwny orodha ya wahalifu wakubwa wa Taifa
Lowassa akakataliwa na Dr Wilbroad Slaa

Jakaya pamoja na tofauti zake na Lowassa hakuhujumu miundombinu ya kiuchumi ya Lowassa hata mmoja

lakini baada ya Jk kustaafu Lowassa kishapelekwa polisi na kuanza mbinyo wa kiuchumi hadi akarudi chamani
 
hata mimi naona kuna jitu linaenda kuishi maisha ya wasiwasi sana hadi pale Mungu atakalichukua..maana lilitenda dhurma na uongo mwingi kwa wengine. pole yake
 
Tena mainly wanaomlaumu ni Chadema followers...hapo ndo inazidi kushangaza
Sio kweli kuwa wengi wanaomlaumu Kikwete ni wa Chadema; Lowassa alikuwa na following kubwa ccm kuliko alipoingia Chadema !!
It was his overwhelming following in ccm which catapulted Magufuli to be the ccm presidential flag bearer and ultimately the Tanzania President!
 
Tena mainly wanaomlaumu ni Chadema followers...hapo ndo inazidi kushangaza
Sasa hivi kuna kulaumu fulani kwa chuki na ushabiki tu. Sio kwamba hakuna kulaumu objectively, lakini kuna watu wanalaumu kwa fashion.

Yani mimi kuna mengi sana namlaumu Kikwete, lakini ukitaka kujua mtu anayelaumu objectively, angalia kama hata siku moja kamtetea Kikwete.

Ukikuta mtu kila kitu, kila siku anamponda tu Kikwete, kila siku, kila kitu, anaponda tu, ujue hapo hakuna objectivity, ni kulaumu kwa mkumbo, kwa ushabiki.

Kikwete hawezi kuwa amepatia kila kitu, lakini pia, hawezi kuwa amekosea kila kitu, sasa inakuwa vipi ukose kizuri chochote cha kusema hata siku moja moja?

Mimi naweza kumlaumu Kikwete leo kwenye jambo moja, kesho likaja jambo lingine nikamtetea.

Kwa sababu, najikita kwenye jambo zaidi, hoja, si kumuangalia mtu.

Kikwete mini sina shobo naye, nilikuwa naitwa kwenda kujutana naye nyumbani kwa balozi New York City, natoa udhuru tu kwa heshima ya balozi kusema ningependa kwenda, lakini nitakuwa kazini.

Kwa sababu nilikuwa naogopa naweza kwenda halafu nikamkaba rais, halafu balozi akaonekana hana maana kakaribisha wahuni waende kula na rais.

Lakini, hilo halina maana hakuna nilipoona Kikwete yuko sawa.

Kuna mtu kanukuu post yangu ya kitambo leo kuhusu kumtetea Kikwete.

From February 26 2011.

Post in thread 'Kikwete alivyoondoka Monduli chuo cha Jeshi kwa misukosuko' Kikwete alivyoondoka Monduli chuo cha Jeshi kwa misukosuko
 
Madaraka makubwa, usipokuwa na hekima, hasa hekima ya Mungu, yanalevya. Na ukikosa hekima unaweza kudhania kuwa wewe ni kila kitu, kwa sababu hakuna wa kukuhoji wala kukuadhibu.

Mathalani madaraka ya Rais wa Tanzania, anaweza kuyatumia vyovyote apendavyo, hata kuua, akitaka, na asihojiwe wala kushtakiwa mahali popote Duniani.

Lakini hawa watawala, kwa kukosa hekima huwa wanaamini kuwa hawawezi kuhojiwa Duniani, ahera wala hata na nafsi zao.

Marehemu Lowasa, aliuishi uaminifu kwa urafiki wake na Kikwete, lakini Kikwete alimsaliti na kumdhulumu rafiki yake.

Lowasa alijitoa kwa nguvu na moyo wake wote katika kuhakikisha Kikwete anakuwa Rais. Hata ndege iliyompeleka Kikwete Dodoma wakati anautafuta Urais, naambiwa iligharamiwa na Lowasa.

Serikali ya Kikwete ipopata msukosuko kutokana na kashfa ya Richmond, huku Msabaha akitamka wazi kuwa zigo la Richmond halikuwa lake kama waziri, kwa sababu wakati wote aliwasiliana na Serikali kupitia Waziri Mkuu, na hivyo kama kuna makosa, basi ni makosa ya Serikali nzima, Lowasa alimwendea Kikwete kumweleza kuwa yeye ameamua kujiuzulu ili kuilinda Serikali. Kikwete alikataa ombi la Lowasa kujiuzulu, lakini marehemu alishikilia msimamo wake, akiamini ndiyo njia ya kuiokoa Serikali ya Kikwete isidondoke, na pengine ipate imani ya aina fulani toka kwaWabunge.

Katikati ya safari yao, tofauti na makubaliano yao ya awali kuwa yeye marehemu amsaidie Kikwete kuwa Rais 2005, halafu Kikwete amsaidie marehemu kuutafuta Urais mwaka 2015, Kikwete alimtosa rafiki yake na kutaka Urais uende kwa mdogo wake.

Kikwete akifahamu wazi kuwa hakukuwa na mgombea yeyote ndani ya CCM na hata nje, wa kumzidi marehemu, akatumia madaraka yake, kuliondoa jina la Lowasa, lisipelekwe kwenye mkutano mkuu wa CCM.

Huku zaidi ya wajumbe 2,000 wa mkutano mkuu wa CCM wakiwa wamejiandaa kumpigia kura Lowasa RIP, kwa mshangao mkubwa wakaambiwa jina la Lowasa halipo.

Wajumbe wa mkutano mkuu, baada ya kuujua ukweli namna Kikwete alivyodhulumu haki ya rafiki yake wa awali ili Urais uende kwa mdogo wake, wakaitana nje, wakaambizana kuwa wale wote waliokuwa wamejiandaa kumchagua Lowasa, kura zao wampe mgombea aliyeonekana dhaifu kuliko wote, na ambaye amewekwa na Kikwete kama chambo. Ndipo ushindi ulipomwangukia Magufuli RIP.

Lowasa hakukata tamaa, aliamua kugombea nafasi ile ile kupitia CHADEMA. Sote tunayakumbuka mafuriko ya Lowasa. Lakini Kikwete akiwa amefunga mkataba wa kudumu wa kumdhulumu marehemu, huku majumuisho ya kura kutoka vituoni yakionesha wazi kuwa Lowasa alikuwa anaongoza kwa kura nyingi, aliwatuma Polisi kwenda kuvamia kituo cha ujumlishaji kura za Lowasa, wakapora computers zote, na kuwaweka mahabusu wajumlishaji wa kura.

Watanzania, nyakati hizi, tunaombeleza msiba wa Edward Lowasa, ambaye kiuhalisia ndiye aliyechaguliwa na wananchi kuwa Rais wa JMT mwaka 2015.

Lakini ni Kikwete pia, ndiye aliyemdhulumu ushindi wa Urais wa Zanzibar, Maalim Seif RIP.

Dhuluma ya Kikwete kwa marehemu hawa, itaitafuna nafsi yake mpaka siku yake ya mwisho. Madaraka yalimlevya, akaisahau haki. Akasahau kuwa madaraka ni kitu cha kuja na kupita, lakini haki huamua maisha yako ya leo na ya umilele.

Nina hakika, hata wakati huu wamsiba, watu watamtazama Kikwete kwa kujiuliza maswali mengi sana. Je, anaupenda sana na kuisikitikia mwili wa marehemu kuliko nafsi ya marehemu ilipokuwa hai?

Ndugu zangu, tutendeni haki ili tuwe na amani hadi siku za uzee wetu.

Kwa heri Lowasa, mtu uliyependwa na Watanzania walio wengi, ukadhulumiwa na wachache.

Mungu wa rehema, tunakuomba umtuze mja wako kwa raha ya milele kwani aliyathamini uhai wa wengine kuliko madaraka yake binafsi.
Sipo upande wowote, lakini sioni dhulma yoyote hapa iliyofanywa na kikwete. Kikwete alikuwa na haki ya kuchagua kuwa anapendelea nani awe Raisi anayefuata, lakini haki hiyo haikuwa imefungwa kwa vigezo vya urafiki na Lowasa au kuwa kama mtu aliyeko kwenye Kifungo huru. Hakuwa na deni kwa Lowasa, hivyo ilikuwa ni haki yake kuchagua.

Mbali na hilo, kujiuzulu kwa Lowasa ulikuwa ni mpango uliolenga kuwapa masilahi wote wawili, na kama hujui Lowasa hakujiuzulu by surprise. Mchezo wote huu ulikuwa kwenye mpango na walijadiliana pamoja, wala haikuwa na tafsiri ya kuzungukana.

Sasa Basi, haijalishi ni mangapi Kikwete alifanya na Lowasa huko nyuma lakini yote hayo hayakuwa na kusudi la kumfanya yeye kufungwa katika kufanya machaguzi yake aliyoyapenda kwa moyo wake. Hakuna dhulma aliyoifanya kwa Lowasa.
 
Cha kushangaza hata kamati ya Bunge haikumpa shinikizo la kujiuzulu.
Kamati haikumuhoji, maana hakukuwa na ushahidi wa moja kwa moja wa kumtia hatiani.
Kama hivyo ndio ilivyokuwa Kikwete alikuwa na sababu gani kukata jina na Lowassa lisiende kupigiwa kura ? Roho ya korosho, halafu anakuja msibani bila haya anatamka kuwa marehemu bado alikuwa rafiki yake!! Jamaa ana roho ya kichawi kabisa.
 
Back
Top Bottom