Kwa dhuluma ambayo Jakaya Kikwete alimfanyia Mzee Lowassa, ataumaliza uzee wake bila amani

Kwa dhuluma ambayo Jakaya Kikwete alimfanyia Mzee Lowassa, ataumaliza uzee wake bila amani

Kwamba Lowassa 'Urais ulikuwa ni Haki yake kutoka Kwa Mungu' kwahiyo kadhulumiwa?

Cha ajabu wanaolia Lia na hili ni Chadema...kama Lowassa aliona Ccm wamemdhulumu why alirudi CCM?
Kama alisamehe why Chadema inawauma sana?
Lowassa hii Haki ya kuwa Rais ilitoka wapi?si na Kambona nae watoto wake watadai Nyerere alimdhulumu Urais?watoto wa Sokoine je waseme Baba Yao aliuwawa ili asiwe Rais?

Mijitu mizima inalialia na consipiracy theory za kitoto kabisa
Tunazungumzia urafiki mungu kaingiaje hapo .kikwete hakukata jina ssbabu et hafai sasa alimpaje uwaziri mkuu ? Ni roho ya kiburi na wivu kuwa lowasa anakubalika kumzidi.
 
Ypu do not get my point.

Hapa tunaongelea dhuluma, siyo kumsaidia.

Kikwete alimdhulumu Lowasa haki ya kupigiwa kura na wajumbe, tena wengi waliokuwa wakimtaka awe mgombea kupitia CCM.

Lowasa akaondoka CCM, akagombea kupitia CHADEMA, akashinda katika kupata uwingi wa kura, Kikwete tena akamdhulumu kwa kutumia madaraka yake.
Lowasa alikuwa mgonjwa kila mtu alikuwa anajua
 
Kutokuwa dhaifu na kuwa na nguvu hata Hitler ana sifa hizo. That does not mean Hitler was good for Germany or the world.

Sokoine alikuwa na maamuzi sana lakini alikuwa na papara. Kuna siku Nyerere alitania tu akisema barabara zetu hususan vijijini ni mbovu sana, inaonekana kama tutahitaji wakuu wa wilaya wajifunze kupanda farasi ili kufikia wananchi.

Kesho yake Sokoine akaanza maongezi ya kuagiza farasi. Balozi Raphael Lukindo akatoa tahadhari, jamani farasi wanataka maandalizi, wanataka mipango, mkiwaleta kwa pupa watakufa tu. Sokoine akatumia turufu ya Uwaziri Mkuu kunyamazisha hoja za balozi Raphael Lukindo, akaagiza farasi tu kutoka Argentina. Mwishowe farasi wale wakafa kama alivyotabiri balozi Raphael Lukindo.

So much for being a strong lrader.

Whether Lowassa ni kiongozi mzuri au si kiongozi mzuri is debatable, what is not debatable, ni kwamba, Lowassa kujiuzulu, against Kikwete's advice per Bams, ilikuwa fatal mistake, ilikuwa shooting oneself in the foot before starting a marathon, and hoping to win.

Na kumtegemea Kikwete am support Lowassa baada ya Lowassa kujiuzulu kwa scandal, against Kikwete's wishes, is pure naivette.
📝🤝👍👏
 
Hutaki mabaya ya Kikwete yasemwe sijui kwa nini, na kila napozidi kukusoma nakuona unavyojigeuza kuwa msemaji wake, kumtetea mpaka kwa maneno yanayoonesha dhahiri umejitungia mwenyewe.

Unaposema Kikwete alikuwa na mazuri na mabaya yake, kisha hapo hapo ukaanza kumtetea kwa kumuita alikuwa "mzee wa Saigon kwenye vijiwe vya kahawa" na "mtu wa kuacha upepo upite" unajichanganya mwenyewe.

Kwasababu nilipokuonesha hayo mabaya ya wakati wa utawala wake, naona unahamishia lawama kwa wasaidizi wake, sio tena mzee wa kuacha upepo upite, unadai yeye hakutoa ruhusa, jambo ambalo ninaamini kabisa huna uhakika nalo, ni mawazo yako binafsi, na huku ndiko kujigeuza msemaji wake nakokwambia.

Na mara nyingi kufahamiana na mtu kwa karibu, automatically kunakufanya kisaikolojia uwe upande wake kumtetea bila kujua, ndicho unachofanya hapa.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
1. Mabaya ya Kikwete tumeyasema mengi sana. Ukibisha nitakuwekea hapa ushahidi. Mimi namsema Kikwete vibaya au vizuri kulingana na hoja. Mimi si mtu wa kusema kwa fashion au mkumbo.

Kikwete tumemsema kuanzia udhaifu wake, matumizi yake mabaya ya fedha za umma mpaka safari zake zisizo idadi. Tangu kabla hajawa rais enzi za "Kumkoma Nyani Giladi" mpaka kesho tutamsema. What are you talking about?

2. Kusema Kikwete alikuwa mtu wa Saigon ni kumtetea? Kivipi? Kusema Kikwete alikuwa mtu ambaye akipata scandal anasema "huu ni upepo, utapita tu" ni kumtetea? Kivipi? Kiongozi anayesema "huu ni upepo tu, utapita" baada ya scandal ni indifferent. Mimi kumuita kiongozi indifferent naona si sifa nzuri. Ni sifa mbaya, kwamba huyu kiongozi hajali. Anaziba masikio kwenye scandal. Sasa kumuita kiongozi hajali, anaziba masikio kwenye scandal ni mumtetea?Mbona tunaona jambo lilelile tofauti sana?

Unajenga hoja kwa mantiki au unalalamika kwa hisia tu?

Unasoma ninachoandika au unachotaka wewe niwe nimeandika?

3. Nimetoa mfano wa case moja ambayo Kikwete hakuijua ya Maxence Melo alivyoshikwa. Hii case naijua kwa sababu niliishughulikia kampeni yake ya kinataifa. Na Kikwete ndiye aliyeamuru Max aachiwe. Nikasema kutakuwa na nyingine nyingi kama hizo. Pia sikumtetea Kikwete moja kwa moja nikasema kuna cases nyingine Kikwete anapata political expediency na advantage anazifumbia macho, na kwa hizo siwezi kumtetea. Hapo napo nimemtetea Kikwete?

4. Kikwete nafahamiana naye kwa karibu? Wapi? Kivipi? Kikwete kawa rais mimi nishaondoka Tanzania. Wakati niko Tanzania Kikwete was mostly a nobody. Mpaka 95 anakuja kugombea urais tukashangaa, hata huyu naye anataka kuwa rais? Wakati kawa rais anakuja New York City mambo ya UN nilikuwa naitwa sana kwa balozi kukaa naye Kikweye, jinsi nisivyomfagilia wala kutaka kuwa karibu naye nilikataa mara zote kwenda. Nilikataa nafasi zote za kukutana na Kikwete. Sasa ningekuwa shabiki wa Kikwete u avyoni paint hivyo, ningekataa kukutana naye? Kikwete nimemjulia wapi mimi?
 
JK inawezekana ana matatizo yake, mengi tu.

Lakini, kwenye hili la Lowassa.

Mimi sielewi kwa nini JK analaumiwa kwenye hili.
Mkuu watu hawapendi watu makini, smart na calculative. Kosa walilolifanya Lowassa na Magufuli ni kutafsiri upole na ucheshi wa Kikwete for weakness, a very fatal mistake!
 
Na JK kutoikataa hiyo barua, ndio hofu kwake ikaanza akiamini kama Lowassa angekuwa Rais, basi angekuja kulipa kisasi.

Pia, uchafu wa Ridhiwani wakati wa utawala wa baba yake, JK akaamua kumtosa Lowassa, ndio maana Ridhiwani akaropoka "Rais hatatoka Kaskazini", kwasababu ya hofu ya kisasi.

Walijua angekuwa Membe ili awalinde, bahati mbaya mambo yakatibuka bahati ikamuangukia Magufuli, hapo tena ikabidi waliokuwa na dili chafu waanze kujisalimisha kwa Magufuli, akiwemo Home Shopping Centre na GSM.

Makubaliano yao yaliitwa; Gentleman's Agreement.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Mkuu Lowassa alijiuzulu mwenyewe kweupe bungeni akisema, namnukuu "najua shida ni uwaziri mkuu"

Kikwete anaingiaje hapo??

Alikuwa anataka uwaziri mkuu wakati alikuwa Rais?

Kukurupuka kwake na hasira zilimponza! Ukweli ni kwamba hakuna anaye mfahamu Lowassa kuliko Kikwete mwenyewe!
 
Mwinyi alijiuzulu kwa kashfa ya polisi kuua raia.
Ni hivi.

Kujiuzulu si jambo baya. Linaweza kuonesha character.

Lakini, ukijiuzulu, umekubali makosa ama kwa kitu ulichofanya wewe mwenyewe moja kwa moja, ama kwa kitu ambacho ulitakiwa kusimamia kama kiongozi lakini hukusimamia vizuri.

Umekubali makosa.

Sasa, ukishakubaki makosa, hilo halina maana ni lazima watu watakutupa tu.

Lakini pia halina maana watu watakupetesha tu bila kujali kuwa ulijiuzulu.

Siasa ina mambo mengi. Unaweza kuibuka kidedea hata kama a compromise candidate.

Lakini, unakuwa unewaachia watu wengine waamue fate yako, you leave so much to chance, you taint your resume.

Watu wakikufanyia hisani kukuruhusu uwe rais, ni sawa na vizuri.

Lakini, kimsingi, unakuwa umeshawapa watu sababu ya kusema "huyu alishaharibu, tusimpe nafasi, ataharibu tena".

Siasa za kipindi cha Nyerere zilikuwa tofauti sana, zilikuwa more forgiving. Chama kimoja. Uteuzi uko wa siri sana. Rais mwenyewe mnamchagua mmoja kwa kura ya Ndiyo au Siyo. Mwinyi alipewa grace hiyo.

Tanzania ike ni tofauti sana na Tanzania ya vyama vingi.

Siasa za kipindi cha Kikwete zilikuwa za ushindani zaidi. Zilikuwa za one mistake one goal, saa nyingine unatengenezewa tu goal bika mistake kama Salim Ahmed Salim. Figisu tu.

Sasa, dunia ya figisu tupu, ukishajiuzulu ndiyo umewapa watu msemo kwamba huyu hafai, alijiuzulu.

Sasa hapo Lowassa kakubali kujiuzulu, kajipiga rusasi ya mguu mwenyewe kabla ya kuanza marathon, mlitegemea na yeye aturudishe nyuma kwenye siasa za enzi ya Nyerere kweli?
 
Hiyo stori ya Sokoine na kuleta farasi inaonyesha jinsi gani alikuwa kiongozi anayejali hali za raia wa chini, kama mpango wake huo wa kuwapa wakuu wa Wilaya farasi ungefanikiwa( na kama pia haukuhujimiwa ukizingatia farasi ni mmojawapo ya wanyama wanaovumilia mazingira magumu sana) huenda viongozi wangejibidiisha na leo hii vijiji vyote vingekuwa na lami kuepuka kuendelea kutembelea farasi.

Hiki pia ndicho Lowassa alikuwa akikipigia kelele, kwamba watu wafanye maamuzi katika nafasi badala ya kujizungusha zungusha tu. Akiwa waziri alisimama kidete kwamba tutatumia maji ya Ziwa Victoria kupelekea raia maji safi potelea pote na leo hii maji ya Ziwa Victoria yanatumiwa na mamilioni ya raia.
Mkuu farsasi anavumilia kuliko punda???? 🤣 🤣 🤣
 
Wewe unasema nafsi yake ndiyo itakayomhukumu wakati wengine hata hawaamini kwamba wana nafsi.

Hapa naona dua za kuku nyingi ambazo hazimpati mwewe.

Kama unaona JK ana makosa sana, mfungulie mashtaka, mvizie mtandike kofi, fanya kitu.

Ukisubiri nafsi yake imhukumu wakati mwenzako anajua kula bata tu kwenda mbele, tena kwa kutumia kodi yako, utasubiri sana.
🤣🤣🤣🎤🔊
 
Madaraka makubwa, usipokuwa na hekima, hasa hekima ya Mungu, yanalevya. Na ukikosa hekima unaweza kudhania kuwa wewe ni kila kitu, kwa sababu hakuna wa kukuhoji wala kukuadhibu.

Mathalani madaraka ya Rais wa Tanzania, anaweza kuyatumia vyovyote apendavyo, hata kuua, akitaka, na asihojiwe wala kushtakiwa mahali popote Duniani.

Lakini hawa watawala, kwa kukosa hekima huwa wanaamini kuwa hawawezi kuhojiwa Duniani, ahera wala hata na nafsi zao.

Marehemu Lowasa, aliuishi uaminifu kwa urafiki wake na Kikwete, lakini Kikwete alimsaliti na kumdhulumu rafiki yake.

Lowasa alijitoa kwa nguvu na moyo wake wote katika kuhakikisha Kikwete anakuwa Rais. Hata ndege iliyompeleka Kikwete Dodoma wakati anautafuta Urais, naambiwa iligharamiwa na Lowasa.

Serikali ya Kikwete ipopata msukosuko kutokana na kashfa ya Richmond, huku Msabaha akitamka wazi kuwa zigo la Richmond halikuwa lake kama waziri, kwa sababu wakati wote aliwasiliana na Serikali kupitia Waziri Mkuu, na hivyo kama kuna makosa, basi ni makosa ya Serikali nzima, Lowasa alimwendea Kikwete kumweleza kuwa yeye ameamua kujiuzulu ili kuilinda Serikali. Kikwete alikataa ombi la Lowasa kujiuzulu, lakini marehemu alishikilia msimamo wake, akiamini ndiyo njia ya kuiokoa Serikali ya Kikwete isidondoke, na pengine ipate imani ya aina fulani toka kwaWabunge.

Katikati ya safari yao, tofauti na makubaliano yao ya awali kuwa yeye marehemu amsaidie Kikwete kuwa Rais 2005, halafu Kikwete amsaidie marehemu kuutafuta Urais mwaka 2015, Kikwete alimtosa rafiki yake na kutaka Urais uende kwa mdogo wake.

Kikwete akifahamu wazi kuwa hakukuwa na mgombea yeyote ndani ya CCM na hata nje, wa kumzidi marehemu, akatumia madaraka yake, kuliondoa jina la Lowasa, lisipelekwe kwenye mkutano mkuu wa CCM.

Huku zaidi ya wajumbe 2,000 wa mkutano mkuu wa CCM wakiwa wamejiandaa kumpigia kura Lowasa RIP, kwa mshangao mkubwa wakaambiwa jina la Lowasa halipo.

Wajumbe wa mkutano mkuu, baada ya kuujua ukweli namna Kikwete alivyodhulumu haki ya rafiki yake wa awali ili Urais uende kwa mdogo wake, wakaitana nje, wakaambizana kuwa wale wote waliokuwa wamejiandaa kumchagua Lowasa, kura zao wampe mgombea aliyeonekana dhaifu kuliko wote, na ambaye amewekwa na Kikwete kama chambo. Ndipo ushindi ulipomwangukia Magufuli RIP.

Lowasa hakukata tamaa, aliamua kugombea nafasi ile ile kupitia CHADEMA. Sote tunayakumbuka mafuriko ya Lowasa. Lakini Kikwete akiwa amefunga mkataba wa kudumu wa kumdhulumu marehemu, huku majumuisho ya kura kutoka vituoni yakionesha wazi kuwa Lowasa alikuwa anaongoza kwa kura nyingi, aliwatuma Polisi kwenda kuvamia kituo cha ujumlishaji kura za Lowasa, wakapora computers zote, na kuwaweka mahabusu wajumlishaji wa kura.

Watanzania, nyakati hizi, tunaombeleza msiba wa Edward Lowasa, ambaye kiuhalisia ndiye aliyechaguliwa na wananchi kuwa Rais wa JMT mwaka 2015.

Lakini ni Kikwete pia, ndiye aliyemdhulumu ushindi wa Urais wa Zanzibar, Maalim Seif RIP.

Dhuluma ya Kikwete kwa marehemu hawa, itaitafuna nafsi yake mpaka siku yake ya mwisho. Madaraka yalimlevya, akaisahau haki. Akasahau kuwa madaraka ni kitu cha kuja na kupita, lakini haki huamua maisha yako ya leo na ya umilele.

Nina hakika, hata wakati huu wamsiba, watu watamtazama Kikwete kwa kujiuliza maswali mengi sana. Je, anaupenda sana na kuisikitikia mwili wa marehemu kuliko nafsi ya marehemu ilipokuwa hai?

Ndugu zangu, tutendeni haki ili tuwe na amani hadi siku za uzee wetu.

Kwa heri Lowasa, mtu uliyependwa na Watanzania walio wengi, ukadhulumiwa na wachache.

Mungu wa rehema, tunakuomba umtuze mja wako kwa raha ya milele kwani aliyathamini uhai wa wengine kuliko madaraka yake binafsi.
Ujasusi ni kazi ngumu wewe laani wenzio wanakula Raha maana wanaishi kwa jina la jamuhuri.... So ilaani jamuhuri🇹🇿🤐
 
Mkuu Denoo rudia kupitia andiko la Kiranga upya utaona anachosema. Hasemi Kikwete alikuwa malaika wala shetwani.

Anamaanisha Kikwete alikuwa na mazuri yake na mabaya yake! Naye Kiranga anasema kwenye zuri atasema na kwenye baya atasema, na ndivyo alivyo!

Sio kwa Kikwete tu hata kwa watu wengine, kwa kweli yupo objective kwenye hoja zake, na mara nyingi hana biasness!

Tujadili bila mahaba, tutajifunza mengi!
Hii kazi uliyojipa ya kuwajibia wengine unaamini utaiweza kweli?!

Mimi nimemjibu Kiranga kwa kujumuisha hoja zake wakati nikijadiliana nae, sijamjibu kwa kutumia post yake moja kama ulivyo copy wewe.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
1. Mabaya ya Kikwete tumeyasema mengi sana. Ukibisha nitakuwekea hapa ushahidi. Mimi namsema Kikwete vibaya au vizuri kulingana na hoja. Mimi si mtu wa kusema kwa fashion au mkumbo.

Kikwete tumemsema kuanzia udhaifu wake, matumizi yake mabaya ya fedha za umma mpaka safari zake zisizo idadi. Tangu kabla hajawa rais enzi za "Kumkoma Nyani Giladi" mpaka kesho tutamsema. What are you talking about?

2. Kusema Kikwete alikuwa mtu wa Saigon ni kumtetea? Kivipi? Kusema Kikwete alikuwa mtu ambaye akipata scandal anasema "huu ni upepo, utapita tu" ni kumtetea? Kivipi? Kiongozi anayesema "huu ni upepo tu, utapita" baada ya scandal ni indifferent. Mimi kumuita kiongozi indifferent naona si sifa nzuri. Ni sifa mbaya, kwamba huyu kiongozi hajali. Anaziba masikio kwenye scandal. Sasa kumuita kiongozi hajali, anaziba masikio kwenye scandal ni mumtetea?Mbona tunaona jambo lilelile tofauti sana?

Unajenga hoja kwa mantiki au unalalamika kwa hisia tu?

Unasoma ninachoandika au unachotaka wewe niwe nimeandika?

3. Nimetoa mfano wa case moja ambayo Kikwete hakuijua ya Maxence Melo alivyoshikwa. Hii case naijua kwa sababu niliishughulikia kampeni yake ya kinataifa. Na Kikwete ndiye aliyeamuru Max aachiwe. Nikasema kutakuwa na nyingine nyingi kama hizo. Pia sikumtetea Kikwete moja kwa moja nikasema kuna cases nyingine Kikwete anapata political expediency na advantage anazifumbia macho, na kwa hizo siwezi kumtetea. Hapo napo nimemtetea Kikwete?

4. Kikwete nafahamiana naye kwa karibu? Wapi? Kivipi? Kikwete kawa rais mimi nishaondoka Tanzania. Wakati niko Tanzania Kikwete was mostly a nobody. Mpaka 95 anakuja kugombea urais tukashangaa, hata huyu naye anataka kuwa rais? Wakati kawa rais anakuja New York City mambo ya UN nilikuwa naitwa sana kwa balozi kukaa naye Kikweye, jinsi nisivyomfagilia wala kutaka kuwa karibu naye nilikataa mara zote kwenda. Nilikataa nafasi zote za kukutana na Kikwete. Sasa ningekuwa shabiki wa Kikwete u avyoni paint hivyo, ningekataa kukutana naye? Kikwete nimemjulia wapi mimi?
- Kinachojadiliwa hapa kumhusu Kikwete ni issue yake na Lowassa, hayo ya zamani wachana nayo. Nikitazama majibu yako kwa hii issue, ndio nimekwambia nakuona umejigeuza msemaji wake kwasababu majibu yako ni kama unatuaminisha kwamba Kikwete hakuwa mtu wa visasi, yeye anaujua na kuupenda utani wa vijiweni.

Wakati kiuhalisia nimekuwekea yaliyotokea enzi za utawala wake, ukabadilika, ukahamishia lawama kwa wasaidizi wake, nikakuuliza tena, kama hakuwa mtu mbaya kwanini hakujitokeza kuwakemea hao wasaidizi wake wakati wa awamu yake, sikuona jibu lako.

- Nashangaa hapa unaniuliza swali dogo namna hiyo!, kwamba hukujua uliposema Kikwete alikuwa mtu wa "Saigon" na "kuacha upepo upite" hukuwa unamtetea?, hukujua kama kwa kusema kwako hivyo, ulituonesha tabia za Kikwete kwamba ni mtu asiyejali maneno ya watu? mpaka pale nilipokuonesha vile maneno ya wengine yalivyomkera akawaumiza wakati wa utawala wake?!

Hata kama ulitoa mfano mmoja wa case ya Melo, lakini nami nikakujibu kwa kukupa mifano yangu inayoonesha Kikwete alikuwa tofauti, hakuwa mtu wa kupuuza maneno kama unavyotuaminisha hapa, wakati mwingine alikuwa akijibu kwa vitendo.

-Hili la wewe mara zote ulipoitwa kwa balozi ukaonane na Kikwete ulikataa, ukweli unaujua mwenyewe, lakini haufiti wala kufubaza yote niliyokuandikia hapo juu. I rest my case.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Hii kazi uliyojipa ya kuwajibia wengine unaamini utaiweza kweli?!

Mimi nimemjibu Kiranga kwa kujumuisha hoja zake wakati nikijadiliana nae, sijamjibu kwa kutumia post yake moja kama ulivyo copy wewe.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Usijali sana nani kaandika, jibu hoja tu.

Ukianza kuangalia sana nani kaandika ndiyo mwanzo wa kufanya logical fallacy ya ad hominem.

Yani ndiyo mwanzo wa kuacha kujadili hoja iliyoletwa na kumjadili mtoa hoja kwa personal attacks.

Hoja ni kwamba umeambiwa Kikwete anazungumzwa pande zote, mabaya na mazuri yake.

Ubaya wa Watanzania wengi ni watu wa falsafa ya "all or nothing at all". No nuance.

Yani, wakimpenda mtu, wanampa mahaba yoote, hakuna kibaya watakachokiona kwake, wanamtetea kama ushabiki wa Simba na Yanga.

Na wakimchukia, wanamchukia moja kwa moja. Bila breki.

Ukiwapa watu mtihani wa kuorodhedha mazuri na mabaya ya Paul Makonda hapa, wengi wataweka mazuri tu au mabaya tu, kuweka mizani ni kitu kigumu sana kwa wengi.

Sasa tunapokuja wengine ambao tunaweza kuongea kwa nizani, siku moja Kikwete tukimtetea, siku nyingine tukimponda, kulingana na hoja, wasiompenda wengine wakiona tumemtetea wanaona huu ni ushabiki wao wa Simba na Yanga wa kila siku.

Come on man.

Some of us are more evolved than that.
 
Hoja ni kwaajili ya wenye akili timamu, siyo wewe.

Hakuna mahali iliposemwa kuwa Urais ilikuwa ni haki yake Lowasa bali kama umechaguliwa na wananchi, ni haki ya wananchi kuongozwa na mtu waliyemchagua.

Juzi umemsikia Prof. Tibaijuka akisema kwamba alimwambia Lowasa kuwa akigombea kuoitia chama kingine tofauti na CCM kwa mifumo ya nchi ilivyo, hatatangazwa kuwa Rais. Na ndicho alichokifanya Kikwete.
Watu wa kaskazini wote walitaka Lowasa awe raisi haijalishi kupitia CCM au CDM.
 
Ni hivi.
Kujiuzulu si jambo baya. Linaweza kuonesha character.
Lakini, ukijiuzulu, umekubali makosa ama kwa kitu ulichofanya wewe mwenyewe moja kwa moja, ama kwa kitu ambacho ulitakiwa kusimamia kama kiongozi lakini hukusimamia vizuri.
Na pia kuna kujiuzulu ili kumnusuru Bosi na maswahiba!
Umekubali makosa.
Sasa, ukishakubaki makosa, hilo halina maana ni lazima watu watakutupa tu.

Lakini pia halina maana watu watakupetesha tu bila kujali kuwa ulijiuzulu.
Siasa ina mambo mengi. Unaweza kuibuka kidedea hata kama a compromise candidate.

Lakini, unakuwa unewaachia watu wengine waamue fate yako, you leave so much to chance, you taint your resume.
Watu wakikufanyia hisani kukuruhusu uwe rais, ni sawa na vizuri.

Lakini, kimsingi, unakuwa umeshawapa watu sababu ya kusema "huyu alishaharibu, tusimpe nafasi, ataharibu tena".

Sasa, dunia ya figisu tupu, ukishajiuzulu ndiyo umewapa watu msemo kwamba huyu hafai, alijiuzulu.
Rais H.A. Mwinyi wa Zanzibar ameeleza, alimwandikia Rais Kikwete barua ya kujiuzulu uwaziri wa Ulinzi kutokana na milipuko ya Mabomu, na ilitokea mara mbili. Rais Kikwete alimkatalia kujiuzulu.

Kuhusu ENLowassa
Rais Kikwete alikuwa na uwezo wa kuita 'caucus' ya Chama chake kulijadili suala
Kikwete alikuwa na option ya kutishia kulivunja au kulivunja Bunge kama litamwandama Waziri mkuu wake
Rais Kikwete akiwa sehemu ya Bunge angeomba kwenda kulihutubia Bunge kwa kadhia hiyo.

Rais Kikwete hakufanya jitihada zozote na kumwacha ENL akikaangwa na Bunge.

Hapa simaanishi kwamba kulikuwa na makosa kumkaanga, la hasha lakini ni ukweli kwamba 'rafiki yake ' hakumsaidia. Pengine Kikwete alijua huo ndio utakuwa mwisho wa ushawishi wa ENL katika siasa za Tanzania

Lowassa alibaki na machaguo mawili, kwanza, akomae kutojiuzulu, Bunge limpigie kura ya kutokuwa na imani.
Kuondolewa kwa 'vote of no confidence' kungehitimisha ndoto na safari yake kisiasa once and for all

Pili, ajiuzulu kama sehemu ya kuwajibika na kuinusuru serikali ili apate nafasi mbele ya safari.
Hii ilikuwa '' viable option'' na tumeona ilimsaidia kurudia katika ulingo kwa mara nyingine akiwa na nguvu kubwa.

Kwanini Kikwete analaumiwa? Si kwasababu hakumpa mshirika wake Urais.

JK analaumiwa kwa mambo mawili, kwanza kumtosha ENL wakati alijua mafisadi walivyosaidia mtandao uliomweka madarakani. Kama Rais wa nchi , JK alijua mauza uza ya Richmond na walioko nyuma yake! alijua!

Pili, ENL alijijenga tena baada ya anguko la Uwaziri mkuu. Utaratibu wa chama ni majina kupitiwa na lenye kura nyingi linasonga mbele kwa mchujo zaidi. JK alijua ushawishi wa Lowassa.

Kwa kujua Lowassa hana Kikwakzo na ameshinda kwa uhalali na kwa kujua mbinu za kumzuia kwa kumuanguasha u-P,M zimeshindwa, JK akakata jina la Lowassa si kwa kushindwa bali kwa hiyana tena kinyuma na taratibu za upatikanaji wa mgombea.


Kikwete hakumdhulum Urais , alimdhulumu Lowassa kwa kuvunja taratibu zilizokuwa zinapeleka jina na Lowassa mbele. Alikata jina, Lowassa hakushindwa! hiyo ni dhuluma inayoongelewa
 
Back
Top Bottom