Kwa dhuluma ambayo Jakaya Kikwete alimfanyia Mzee Lowassa, ataumaliza uzee wake bila amani

Kwa dhuluma ambayo Jakaya Kikwete alimfanyia Mzee Lowassa, ataumaliza uzee wake bila amani

Cha kushangaza hata kamati ya Bunge haikumpa shinikizo la kujiuzulu.
Kamati haikumuhoji, maana hakukuwa na ushahidi wa moja kwa moja wa kumtia hatiani.
Lowassa alijitakia mwenyewe kujiuzulu.

Hana wa kumlaumu.

Yani hata kama alilazimishwa kujiuzulu, kama aliona hajafanya kosa, alitakiwa kukataa kujiuzulu mpaka afukuzwe kazi tujue kafukuzwa.

Ukijiuzulu tu, umekubali makosa, usitarajie kurudi.

Kurudi hapo ni kufanyiwa hisani tu.

Sasa watu wanataka kulazimisha hisani?
 
Sipo upande wowote, lakini sioni dhulma yoyote hapa iliyofanywa na kikwete. Kikwete alikuwa na haki ya kuchagua kuwa anapendelea nani awe Raisi anayefuata, lakini haki hiyo haikuwa imefungwa kwa vigezo vya urafiki na Lowasa au kuwa kama mtu aliyeko kwenye Kifungo huru. Hakuwa na deni kwa Lowasa, hivyo ilikuwa ni haki yake kuchagua.

Mbali na hilo, kujiuzulu kwa Lowasa ulikuwa ni mpango uliolenga kuwapa masilahi wote wawili, na kama hujui Lowasa hakujiuzulu by surprise. Mchezo wote huu ulikuwa kwenye mpango na walijadiliana pamoja, wala haikuwa na tafsiri ya kuzungukana.

Sasa Basi, haijalishi ni mangapi Kikwete alifanya na Lowasa huko nyuma lakini yote hayo hayakuwa na kusudi la kumfanya yeye kufungwa katika kufanya machaguzi yake aliyoyapenda kwa moyo wake. Hakuna dhulma aliyoifanya kwa Lowasa.
Lowassa hata hakuhojiwa na kamati ya bunge kuhusu kashfa ya Richmond, hii peke yake ilionesha kutohusika kwake.. sasa Kikwete kukata jina la Lowassa lisiende kupigiwa kura ndio inayoitwa dhulma kwa wajumbe kukataliwa kumchagua mtu wanaemtaka na dhulma kwa Lowassa kwa kukataliwa nafasi ya kuweza kuchaguliwa!
 
Kama hivyo ndio ilivyokuwa Kikwete alikuwa na sababu gani kukata jina na Lowassa lisiende kupigiwa kura ? Roho ya korosho, halafu anakuja msibani bila haya anatamka kuwa marehemu bado alikuwa rafiki yake!! Jamaa ana roho ya kichawi kabisa.
Urafiki hauna uhusiano wa kupata madaraka ya uma.
Kila siku jamii inalalamika kuhusiana na jambo hilo bado kuna watu mnalilia kubebwa na marafiki.
Pambana mwenyewe kama una uwezo, acha kulilia watu.
 
JK kama mtu ana mapungufu yake, hawezi kukosa. Huwezi kuongoza mamilioni ya watu ukakosa matatizo.

Lakini, haya mambo mengi hatuna hata uhakika kama yametokea hivyo yanavyosemwa yalitokea, na kama yametokea kweli, ni JK aliyeamuru ama watu wa chini yake tu wamejipendekeza kufanya mambo bila amri.

Sitaki kuongea mengi, lakini nataka kusema kwamba ukiongea katika network za kifamilia, halafu ukisikiliza stories za kwenye magazeti na vijiweni, stories nyingi ni tofauti sana. Tatizo viongozi wa Bongo hawana uwazi. Mimi saa nyingine naongea na hao watoto wa kina Warioba na Lowassa, naona dah, kazi yetu kupata story straight ni kubwa sana.

Kuna mambo nashindwa hata kukubishia kwa sababu sitaki kutengeneza mzozo ambao hauwezi kuwa settled one way or another hapa.

Ukweli utabaki kuwa, kipindi cha JK ni kipindi ambacho watu walikuwa huru sana kusema. Kipindi pekee cha kukilinganisha na kipindi cha JK ni kipindi cha Mzee Mwinyi cha Ruksa.

Mambo mengine mtamlaumu JK wakati JK hahusiki moja kwa moja na wala hajaagiza mtu.

Nitakupa mfano mmoja ninaoujua binafsi unaoonesha mambo mengine mnaweza kumpa lawama JK kuwa kaamuru, wakati hata hakuamuru na in fact yupo against nayo.

Kipindi cha JK Jamiiforums ilikuwa moto sana. Kipindi hicho FMES (RIP) na wenzake waliokuwa serikalini walikuwa wanapata sana nondo za ndani ya serikali na kuzimwaga hapa, watu wakawa wanachambua mambo na kuinanga serikali kwa style ya "Kumkoma Nyani Giladi". Wakongwe wa JF watakumbuka.

Sasa, ikatokea Polisi fulani wakubwa wakawa wanataka sifa, wakamkamata mkuu Maxence Melo. Wakamfunga.

Kusikia hivyo, tukalianzisha bonge la timbwili kimataifa. Tukawatafuta "The Committe to Protect Jouranalists" www.cpj.org , tukawatafura Human Rights Watch, wakalianzisha timbwili kwenye vyombo vya habari vya kimataifa. Shout out to Mimi Mwanakijiji kwa kazi kubwa aliyoifanya.

Tanzania ikawa ina trend vibaya kwamba inaminya uhuru wa habari.

JK kusikia hivyo, akasema kwa nini mnawasumbua hawa vijana wa dotcom ambao hawana hata impact kwenye utawala wangu? Waachieni tu, msiwabugudhi. Msinichafulie jina la nchi yangu bila sababu.

Mara moja Max akaachiwa.

Sasa, kwa mtu ambaye hakuwa karibu na ile story, angeweza kujua kuwa JK aliamuru Max ashikwe, halafu ikaonekana issue imeleta negative press kimataifa, akaamuru Max aachiwe.

Kumbe, Max alivyoshikwa hata JK hakujua.

Mambo mengine tunaweza kumlaumu JK kwa sababu watu wa chini wamejipendekeza tu. JK mwenyewe hata hakuyapenda.
Kama hakuyapenda angeyalaani, sio kukaa kimya kama alivyofanya.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Sipo upande wowote, lakini sioni dhulma yoyote hapa iliyofanywa na kikwete. Kikwete alikuwa na haki ya kuchagua kuwa anapendelea nani awe Raisi anayefuata, lakini haki hiyo haikuwa imefungwa kwa vigezo vya urafiki na Lowasa au kuwa kama mtu aliyeko kwenye Kifungo huru. Hakuwa na deni kwa Lowasa, hivyo ilikuwa ni haki yake kuchagua.

Mbali na hilo, kujiuzulu kwa Lowasa ulikuwa ni mpango uliolenga kuwapa masilahi wote wawili, na kama hujui Lowasa hakujiuzulu by surprise. Mchezo wote huu ulikuwa kwenye mpango na walijadiliana pamoja, wala haikuwa na tafsiri ya kuzungukana.

Sasa Basi, haijalishi ni mangapi Kikwete alifanya na Lowasa huko nyuma lakini yote hayo hayakuwa na kusudi la kumfanya yeye kufungwa katika kufanya machaguzi yake aliyoyapenda kwa moyo wake. Hakuna dhulma aliyoifanya kwa Lowasa.
Dhuluma ya kwanza kumtosa Richmond wakati ishu ilikua ya kwake.
Kutumia madaraka yake kuhakikisha lowasa hawi rais
 
Sasa hivi kuna kulaumu fulani kwa chuki na ushabiki tu. Sio kwamba hakuna kulaumu objectively, lakini kuna watu wanalaumu kwa fashion.

Yani mimi kuna mengi sana namlaumu Kikwete, lakini ukitaka kujua mtu anayelaumu objectively, angalia kama hata siku moja kamtetea Kikwete.

Ukikuta mtu kila kitu, kila siku anamponda tu Kikwete, kila siku, kila kitu, anaponda tu, ujue hapo hakuna objectivity, ni kulaumu kwa mkumbo, kwa ushabiki.

Kikwete hawezi kuwa amepatia kila kitu, lakini pia, hawezi kuwa amekosea kila kitu, sasa inakuwa vipi ukose kizuri chochote cha kusema hata siku moja moja?

Mimi naweza kumlaumu Kikwete leo kwenye jambo moja, kesho likaja jambo lingine nikamtetea.

Kwa sababu, najikita kwenye jambo zaidi, hoja, si kumuangalia mtu.

Kikwete mini sina shobo naye, nilikuwa naitwa kwenda kujutana naye nyumbani kwa balozi New York City, natoa udhuru tu kwa heshima ya balozi kusema ningependa kwenda, lakini nitakuwa kazini.

Kwa sababu nilikuwa naogopa naweza kwenda halafu nikamkaba rais, halafu balozi akaonekana hana maana kakaribisha wahuni waende kula na rais.

Lakini, hilo halina maana hakuna nilipoona Kikwete yuko sawa.

Kuna mtu kanukuu post yangu ya kitambo leo kuhusu kumtetea Kikwete.

From February 26 2011.

Post in thread 'Kikwete alivyoondoka Monduli chuo cha Jeshi kwa misukosuko' Kikwete alivyoondoka Monduli chuo cha Jeshi kwa misukosuko
Hutaki mabaya ya Kikwete yasemwe sijui kwa nini, na kila napozidi kukusoma nakuona unavyojigeuza kuwa msemaji wake, kumtetea mpaka kwa maneno yanayoonesha dhahiri umejitungia mwenyewe.

Unaposema Kikwete alikuwa na mazuri na mabaya yake, kisha hapo hapo ukaanza kumtetea kwa kumuita alikuwa "mzee wa Saigon kwenye vijiwe vya kahawa" na "mtu wa kuacha upepo upite" unajichanganya mwenyewe.

Kwasababu nilipokuonesha hayo mabaya ya wakati wa utawala wake, naona unahamishia lawama kwa wasaidizi wake, sio tena mzee wa kuacha upepo upite, unadai yeye hakutoa ruhusa, jambo ambalo ninaamini kabisa huna uhakika nalo, ni mawazo yako binafsi, na huku ndiko kujigeuza msemaji wake nakokwambia.

Na mara nyingi kufahamiana na mtu kwa karibu, automatically kunakufanya kisaikolojia uwe upande wake kumtetea bila kujua, ndicho unachofanya hapa.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Kwamba Lowassa 'Urais ulikuwa ni Haki yake kutoka Kwa Mungu' kwahiyo kadhulumiwa?

Cha ajabu wanaolia Lia na hili ni Chadema...kama Lowassa aliona Ccm wamemdhulumu why alirudi CCM?
Kama alisamehe why Chadema inawauma sana?
Lowassa hii Haki ya kuwa Rais ilitoka wapi?si na Kambona nae watoto wake watadai Nyerere alimdhulumu Urais?watoto wa Sokoine je waseme Baba Yao aliuwawa ili asiwe Rais?

Mijitu mizima inalialia na consipiracy theory za kitoto kabisa
🤔💭🔭📝
 
Sasa, kama Lowassa alimwambia Kikwete anataka kujiuzulu, Kikwete akakataa, lakini Lowassa akalazimisha kujiuzulu, huoni Lowassa kajitakia mwenyewe kupigwa chini kwa kulazimisha kujiuzulu?

Ulitegemea vipi Kikwete aendelee ku support mbio za Urais za Lowassa baada ya Lowassa mwenyewe kulazimisha kujiuzulu kutokana na kashfa ya Richmond?

Yani ulitaka Kikwete ampigie kampeni ya urais Lowassa aliyeshindwa Uwaziri Mkuu kwa kashfa?

Huoni kwamba Lowassa ndiye aliyemsaliti Kikwete hapo kwa kulazimisha kujiuzulu na kumuachia manyanga Kikwete, wakati labda alihitajika kupambana akiwa upande wa serikali?

Mtu aliyejiuzulu Uwaziri Mkuu kutokana na msukosuko wa kashfa, unajuaje akipata urais na kupata msukosuko wa kashfa hatajiuzulu tena?

Lowassa alipewa mtihani wa uongozi, akashindwa. Kikwete akaona huyu kashindwa, twende na wengine.

Hata mimi ningemshangaa sana Kikwete kama angempigia kampeni Lowassa kwa sababu ni rafiki yake tu.
🤔🤝📝
 
It's not necessarily lazima ni JK!, sometimes wahafidhina wana nguvu kuliko rais!, ila mkubwa ni jalala!.

Ni kweli kwasababu by that JK alikuwa bado ni mjamaa, na EL alikuwa tayari ni bepari!, sasa wote ni mabepari!.

Sina uhakaki kama makubaliano haya yalikuwepo!, ila kunafanyika vitu vingi ambavyo sio, mfano kutoa fomu moja, kugombea kwa msesereko, kupokezana Mkristo na Muislam.

Sii kweli, jina la Lowassa lilichinjiwa baharini hata kwenye CC halikujadiliwa, ila akina sisi tuliisha muandaa kisaikolojia Elections 2015 - Licha ya kukubalika, Jina la Lowassa halitafika hata CC!

Sii kweli, jina la EL halikutoka hata CC, hivyo halikuingia hata NEC, ule wimbo wa "Tunaimani..." ni uliimbwa NEC! Elections 2015 - Edward Lowassa sio lazima yeye tu ndiye awe Rais wetu 2015, Rais wetu wa 2015 ni...

Sii kweli!, wanaoamua nani awe ngombea wa CCM, sio wana CCM, ni kitu kinachoitwa "the inner circle" angalia tarehe ya bandiko hili Elections 2015 - Mgombea wa Urais Kwa tiketi ya CCM, 2015 "Could Be" John Pombe Magufuli

Sii kweli!, kura zote mpaka za urais zimehesabiwa vituoni na kila msimamizi alipewa copy ya matokeo!, TV Program Alert: Msidanywe na Wanasiasa Kuhusu Uchaguzi Mkuu: Ulikuwa Huru na wa Haki!. Shuhudia! ila kwa upande wa Zanzibar, kule ndio kweli EL alimbwaga JPM Elections 2015 - Imethibitishwa pasi na shaka kuwa ni kweli kabisa, Zanzibar, Maalim Seif na CUF ndio walioshinda

Hii sii kweli, Elections 2015 - Kama Hii ni Kweli, Then, Serikali Yetu ni Serikali Dhalimu?, Haramu?. Hukumu ya Karma ii Juu Yake! makarateka yalifanywa uchaguzi wa 2020!.

Sii kweli, ni wahafidhina!, kwa siasa za Zanzibar, ni lazima CCM ishinde for the sake of Muungano!, ukisikia Muungano tutaulinda kwa gharama yoyote, ushindi wa lazima wa CCM Zanzibar ni moja ya gharama hizo. Iwapo CCM itashindwa Zanzibar, Nini Majaaliwa ya Muungano?

ukitenda wema mwingi kuliko ubaya karma inarekebisha "The Power of 'Karma'- Ndio Hukumu Pekee ya Haki Kamili Hapa Duniani!, Unahukumiwa kwa Matendo Yako!

Baada ya ushauri huu, Ushauri wa bure kwa Rais Kikwete, muombe msamaha Lowassa kabla ya October 25!

Amen
🗼🙏🆒
 
With RESPECT kwako, inaonekana wewe unaishi kule LALA LAND, kama hujui why Lowassa (MHSRIP)alirudi ccm, nikuache tu,kweli mkuu hujui kuwa alilazimishwa kwa kunyimwa haki yake kwa serikali ya ccm kutumia vyombo vya dola,basi wewe ni kenges
Ndugu sio lazima umtukane mwenzio, ukiwekwa hoja yako kuonyesha na kuthibitisha hoja yako inatosha kama alivyofanya wenzako! hajatukana popote!

Mahaba yasitupofushe!

Msiba utaisha, maisha yataendelea, kujukwaanika utaendelea Mkuu!
 
Hizo ni minutiae za nuance ambayo big picture optics haijali.

Kwa nini Lowassa alikubali kujiuzulu? Kwa nini alishindwa kusimamia Wizara ya Madini kama PM?

Wananchi wachache sana wanaweza kuchambua mambo hivyo.

Lowassa alivyojiuzulu, Rais George Bush aliipongeza serikali ya Tanzania kwa kuliondoa jizi hilo Lowassa. Alisema kitu kuipongeza Tanzania "for getting rid of that crook".

Ndivyo ilivyoeleweka hata kimataifa huko. Ndivyo wananchi wengi walivyoelewa, Lowassa fisadi kajiuzulu.

Sasa Tanzania ingeonekana vipi ikiwa "that crook" anarudi kuwa rais na Kikwete anampigia kampeni?

Ingeonekana kumbe haya yote maigizo ya Pwagu na Pwaguzi, hawa wote majambazi tu yanatuchezea akili.

Ndicho Kikwete alichokataa hicho.

Kwenye siasa, hata kama umejiuzulu kwa sababu wewe kiongozi tu, hukushiriki moja kwa moja, optics, imagery matters.
Mwinyi alijiuzulu kwa kashfa ya polisi kuua raia.
 
Nakunukuu

"""Cha ajabu wanaolia Lia na hili na Chadema...kama Lowassa aliona Ccm wamemdhulumu why alirudi CCM?
Kama alisamehe why Chadema unawajua sana?""""


Vita alivyo pigana JPM ndio vita vilivyo kua vya wana mabadiliko na for sure JOHN POMBE MAGUFULI alimuheshimu sana tena sana EDWARD LOWASSA na hakuwai toa shombo Wala shit zozote Kwa EL

Kama una clip tuwekee hapa

Na ndio maana LOWASSA alipo rudi CCM alisema maneno mawili NIMERUDI NYUMBANI

CCM YA JPM haikua na matatizo na EDWARD LOWASSA

MAGUFULI akiwa raisi aliwai kumkimbilia kumsalimia kaka yake EDWARD LOWASSA na hata kumpa mialiko ya ikulu....
Mkuu,

Uliwahi kujua tafsiri ya push up za Magufuli jukwaani????

Umesahau kesi ya mwanaye Lowasa?

Je, stahiki zake kama waziri mkuu zilishitishwa na nani?

Aliyesema hawezi kumpa mkono mpinzani ni nani?

Aliyewafukuza kina Sofia simba uanachama ni nani?

Usitete unafiki Mkuu, tulia, acha watu waomboleze kwa amani!
 
Hatari sana, kwahiyo mlitaka JK amsaidie EL kushinda Urais? Eti kwakuwa walikuwa marafiki? Kwahiyo tunaunga mkono Urais kugawiwa kwa minajili ya urafiki?.

EL alikuwa CCM na tabia hizi tunazomsema nazo JK ndio hizi hizi wana CCM wote wanazo, EL aliondoka CCM baada ya kukatwa pale Dodoma, kama alikuwa mwema alipaswa kuikacha CCM toka 1995 na sio kusubiri maslahi yalipokoma.

EL na JK wanajuana kuliko Mimi na wewe tunavyowajua, unapokwenda kumlaumu JK huku humjui EL kiundani nawewe itabidi tukuite mnafiki au mmbeya.

Mwenyezi Mungu ndiye anapanga kifo cha kila mtu na namna gani kitokee.
🤝📝🆒
 
Sasa kama kashfa haikuwa ya Lowassa, ilikuwa ya serikali nzima, Lowassa kutaka kujiuzulu yeye ni kimbelembele.

Na mtu kimbelembele anaweza kuleta matatizo katika uongozi.

Ni hivi, ingekuwa Kikwete kamtuma Lowassa ajiuzulu, kamwambia "Edward, haya maji ni marefu, inabidi tumtoe mtu hapa ili kuinusuru serikali, tena mtu mzito, nakuomba kama rafiki yangu ujiuzulu ili kuinusuru serikali, halafu hapo baadaye mambo yakipoa, tutakurudisha ugombee urais nikimaliza mimi".

Halafu Lowassa akasema "Kweli? Serikali inaweza kuanguka? Na mimi kujiuzulu kwangu ndiko kutainusuru? Mnanitaka nijiuzulu halafu nitakuwa rais baada yako? Hapo hakuna shida, najiuzulu"

Halafu Lowassa akajiuzulu.

Halafu baadaye, alipotaka kuwa rais, Kikwete akamruka. Akamkata.

Hapo sawa, ungeweza kusema Kikwete mtu jahili na laghai, kamuhadaa mwenzake ajiuzulu, kwa ahadi kuwa atamfanya awe rais, mwenzake akajiuzulu, na urais akamkata.

Lakini mambo hayakuwa hivyo. Kwa maelezo yako, Kikwete hakutaka Lowassa ajiuzulu. Hata Lowassa alivyotaka kujiuzulu, Kikwete alikataa, Lowassa akalazimisha kujiuzulu.

Sasa hapo mpango wa Kikwete wa Lowassa kuendelea kuwa Waziri Mkuu umekataliwa na Lowassa.

Aliyemsaliti mwenzake kati ya Kikwete na Lowassa ni nani hapo?

Na kama Lowassa alikataa mpango wa Kikwete kuendelea kuwa Waziri Mkuu, kwa nini unafikiri ni sawa Kikwete kukubali mpango wa Lowassa kuja kuwa rais?
🤝📝🆒
 
Hutaki mabaya ya Kikwete yasemwe sijui kwa nini, na kila napozidi kukusoma nakuona unavyojigeuza kuwa msemaji wake, kumtetea mpaka kwa maneno yanayoonesha dhahiri umejitungia mwenyewe.

Unaposema Kikwete alikuwa na mazuri na mabaya yake, kisha hapo hapo ukaanza kumtetea kwa kumuita alikuwa "mzee wa Saigon kwenye vijiwe vya kahawa" na "mtu wa kuacha upepo upite" unajichanganya mwenyewe.

Kwasababu nilipokuonesha hayo mabaya ya wakati wa utawala wake, naona unahamishia lawama kwa wasaidizi wake, sio tena mzee wa kuacha upepo upite, unadai yeye hakutoa ruhusa, jambo ambalo ninaamini kabisa huna uhakika nalo, ni mawazo yako binafsi, na huku ndiko kujigeuza msemaji wake nakokwambia.

Na mara nyingi kufahamiana na mtu kwa karibu, automatically kunakufanya kisaikolojia uwe upande wake kumtetea bila kujua, ndicho unachofanya hapa.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Mkuu Denoo rudia kupitia andiko la Kiranga upya utaona anachosema. Hasemi Kikwete alikuwa malaika wala shetwani.

Anamaanisha Kikwete alikuwa na mazuri yake na mabaya yake! Naye Kiranga anasema kwenye zuri atasema na kwenye baya atasema, na ndivyo alivyo!

Sio kwa Kikwete tu hata kwa watu wengine, kwa kweli yupo objective kwenye hoja zake, na mara nyingi hana biasness!

Tujadili bila mahaba, tutajifunza mengi!
 
Kwamba Lowassa 'Urais ulikuwa ni Haki yake kutoka Kwa Mungu' kwahiyo kadhulumiwa?

Cha ajabu wanaolia Lia na hili ni Chadema...kama Lowassa aliona Ccm wamemdhulumu why alirudi CCM?
Kama alisamehe why Chadema inawauma sana?
Lowassa hii Haki ya kuwa Rais ilitoka wapi?si na Kambona nae watoto wake watadai Nyerere alimdhulumu Urais?watoto wa Sokoine je waseme Baba Yao aliuwawa ili asiwe Rais?

Mijitu mizima inalialia na consipiracy theory za kitoto kabisa
Hii nchi ina viazi wengi Sana , walitaka uraisi wa kupeana kishikaji , ?? Hii ni nchi siyo Mali ya mtu , alaf unajiuzuru Kwa makosa ya wengine , Kwa nn usiache kila mtu akapambana na Hali yake na ukweli ukajulikana , unalinda uovu wa mtu ili aje akulipe wema , duh
 
Back
Top Bottom